Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Hii imenipa moyo kwamba sasa Chadema imeanza kuelewa siasa ,kwani siasa sio vita ni mbinu na mikakati iliyokomaa kimipango,hili la kutoelekea mahakamani ni mwanzo wa kuonyesha kutokuwa na imani na mahakama zetu hapa Tanzania.
"...........Mala ambaye ni Diwani wa Kimandolu, alisema baada ya kukaa na viongozi wa ngazi za juu wa Chadema, wameona hakuna sababu ya kufanya hivyo kwani wanachojua wao ni kwamba nafasi ya Meya wa Jiji hilo bado iko wazi kwani kikao kilichomchagua Meya ni batili.Alisema hawataenda mahakamani kwani wamebaini kuwa wakifanya hivyo watakuwa wamejimaliza.
Uzoefu unaonyesha kuwa kukimbilia mahakamani sio tija kwani kesi inaweza kupigwa danadana hata zaidi ya miaka mitano. Sisi bado tuna hatua nyingi tunazoweza kuzichukua kudai haki yetu, hatuna wasiwasi kwani tunaamini kuwa tunatetea haki ya wananchi walio wengi, alisema Mala.
Kuhusu msimamo wao wa kumtambua ama kutomtambua Meya aliyechaguliwa, alisema sio tu kuwa hawamtambu Meya huyo, Gaudence Lymo, bali hawautambui hata mkutano wa Baraza la Madiwani uliomchagua kwani ulikuwa wa upande wa chama kimoja cha CCM..."
"...........Mala ambaye ni Diwani wa Kimandolu, alisema baada ya kukaa na viongozi wa ngazi za juu wa Chadema, wameona hakuna sababu ya kufanya hivyo kwani wanachojua wao ni kwamba nafasi ya Meya wa Jiji hilo bado iko wazi kwani kikao kilichomchagua Meya ni batili.Alisema hawataenda mahakamani kwani wamebaini kuwa wakifanya hivyo watakuwa wamejimaliza.
Uzoefu unaonyesha kuwa kukimbilia mahakamani sio tija kwani kesi inaweza kupigwa danadana hata zaidi ya miaka mitano. Sisi bado tuna hatua nyingi tunazoweza kuzichukua kudai haki yetu, hatuna wasiwasi kwani tunaamini kuwa tunatetea haki ya wananchi walio wengi, alisema Mala.
Kuhusu msimamo wao wa kumtambua ama kutomtambua Meya aliyechaguliwa, alisema sio tu kuwa hawamtambu Meya huyo, Gaudence Lymo, bali hawautambui hata mkutano wa Baraza la Madiwani uliomchagua kwani ulikuwa wa upande wa chama kimoja cha CCM..."