josias
Member
- Jan 7, 2014
- 47
- 34
Anaandika Sam Ruhuza kukosoa mfumo wa Teuzi kuwatenga Wananchi wa Wilaya ya Ngara.
Ndugu zangu Wanangara!
Nimetafakari sana hizi teuzi serikalini, kuna sehemu sizielewi, mnisaidie!
Ngara kuna watu ccm kwelikweli na vijana wengi wasomi tu, lakini kwenye teuzi, hauwaoni, lakini wanavyojifanya ni ccm damdam hadi unashangaa vipi hawaonekani, lakini maeneo ya wapinzani ndipo teuzi kila kukicha!!
Kigoma walipoamua kura zao kuwapa wapinzani hasa NCCR- Mageuzi majimbo yote, ccm wakashtuka, kila kitu wamepeleka kigoma! Mlezi wa Mkoa ni waziri mkuu, Makamu wa Rais, Waziri, wakuu wa Mikoa, Gavana Benki Kuu, yaani hauwezi kukuta teuzi yoyote hakuna mtu wa Kigoma, Barabara, Maji, umeme na bado kwenye uchaguzi ccm hawana uhakika wa kura za kigoma!
Angalia Kilimanjaro, Arusha na Mara walipoamua kuwapa Chadema! Teuzi na miradi kibao ni maeneo hayo!
Tuje kwenye ziara za viongozi wa serikali, hayo maeneo kila siku wanapishana, lakini Ngara walipoamua wenyewe kuipenda ccm, aibu hata kusema!!
Yaani kuna wakati naona wanangara wanajipendekeza ccm wakati yenyewe hata haiwapendi na ukijifanya kutambua haki yako, wanakuita Mrundi, Mnyarwanda kukukata spidi!!
Angalia hata teuzi za Mbunge wa Ngara, katika historia Ngara hatujawahi kuwa na Waziri kamili, tumeishia kwa Naibu Waziri Afya Mh Sebabii Gwassa 1975 tena nafikiri miaka miwili sikumbuki vizuri na Naibu Waziri Ujenzi na Mawasiliano Mh Gachocha 1985-90 kama sikosei na hao wote ni teuzi za kipindi chao cha kwanza cha uchaguzi, lakini kuanzia hapo hakuna teuzi tena Naibu wala Waziri!
Tumekuwa na Wabunge wasomi kwelikweli, wazoefu wakubwa Serikalini, lakini teuzi hakuna!!
Yaani Ngara ni sahihi sana kusema watu wanajipendekeza ccm wakati wenye chama chao hawawapendi!!
Nimeamua kuandika hili humu, japo wengine watalichukua kisiasa na kuwa na maono tofauti na mengine wanajua wao, lakini naangalia zaidi Maslahi ya Ngara na sitoshangaa baada ya andiko hili, ukaanza kuona teuzi zijazo mtu wa Ngara yumo kwasababu natambua nguvu ya maandiko yangu!
Binafsi Sihitaji uteuzi wowote ule, ila Ngara ni walipa kodi kama wananchi wengine, nitafurahi sana kuona jina la Mwananchi wa Ngara akipata uteuzi wowote angalau ashiriki kwenye kamati za maamuzi!
Naomba nieleweke Hii ni kwa maslahi ya Wanangara wote na kwa vizazi vyote pasipo kujali misimamo yao kisiasa zaidi ya uwezo wao kiuongozi, bila sisi wenyewe kuiongelea Ngara yetu na wananchi wake, hakuna mwingine wa kuongea na kusikika!
Naomba tu kutahadhalisha Ndugu zangu wa Ngara kuepuka haka kaugonjwa ka uchawa maana naona kameanza kuingia Ngara, sio asili yetu huo, tutawatenga Machawa wote ili mpone kwanza na muelewe uchawa ni udhalilishaji wako binafsi na ndio maana mnasababishana hata teuzi ziwapite wengine!!
Tanzania ni yetu SOTE ikiwamo NGARA!
samruhuza
Ndugu zangu Wanangara!
Nimetafakari sana hizi teuzi serikalini, kuna sehemu sizielewi, mnisaidie!
Ngara kuna watu ccm kwelikweli na vijana wengi wasomi tu, lakini kwenye teuzi, hauwaoni, lakini wanavyojifanya ni ccm damdam hadi unashangaa vipi hawaonekani, lakini maeneo ya wapinzani ndipo teuzi kila kukicha!!
Kigoma walipoamua kura zao kuwapa wapinzani hasa NCCR- Mageuzi majimbo yote, ccm wakashtuka, kila kitu wamepeleka kigoma! Mlezi wa Mkoa ni waziri mkuu, Makamu wa Rais, Waziri, wakuu wa Mikoa, Gavana Benki Kuu, yaani hauwezi kukuta teuzi yoyote hakuna mtu wa Kigoma, Barabara, Maji, umeme na bado kwenye uchaguzi ccm hawana uhakika wa kura za kigoma!
Angalia Kilimanjaro, Arusha na Mara walipoamua kuwapa Chadema! Teuzi na miradi kibao ni maeneo hayo!
Tuje kwenye ziara za viongozi wa serikali, hayo maeneo kila siku wanapishana, lakini Ngara walipoamua wenyewe kuipenda ccm, aibu hata kusema!!
Yaani kuna wakati naona wanangara wanajipendekeza ccm wakati yenyewe hata haiwapendi na ukijifanya kutambua haki yako, wanakuita Mrundi, Mnyarwanda kukukata spidi!!
Angalia hata teuzi za Mbunge wa Ngara, katika historia Ngara hatujawahi kuwa na Waziri kamili, tumeishia kwa Naibu Waziri Afya Mh Sebabii Gwassa 1975 tena nafikiri miaka miwili sikumbuki vizuri na Naibu Waziri Ujenzi na Mawasiliano Mh Gachocha 1985-90 kama sikosei na hao wote ni teuzi za kipindi chao cha kwanza cha uchaguzi, lakini kuanzia hapo hakuna teuzi tena Naibu wala Waziri!
Tumekuwa na Wabunge wasomi kwelikweli, wazoefu wakubwa Serikalini, lakini teuzi hakuna!!
Yaani Ngara ni sahihi sana kusema watu wanajipendekeza ccm wakati wenye chama chao hawawapendi!!
Nimeamua kuandika hili humu, japo wengine watalichukua kisiasa na kuwa na maono tofauti na mengine wanajua wao, lakini naangalia zaidi Maslahi ya Ngara na sitoshangaa baada ya andiko hili, ukaanza kuona teuzi zijazo mtu wa Ngara yumo kwasababu natambua nguvu ya maandiko yangu!
Binafsi Sihitaji uteuzi wowote ule, ila Ngara ni walipa kodi kama wananchi wengine, nitafurahi sana kuona jina la Mwananchi wa Ngara akipata uteuzi wowote angalau ashiriki kwenye kamati za maamuzi!
Naomba nieleweke Hii ni kwa maslahi ya Wanangara wote na kwa vizazi vyote pasipo kujali misimamo yao kisiasa zaidi ya uwezo wao kiuongozi, bila sisi wenyewe kuiongelea Ngara yetu na wananchi wake, hakuna mwingine wa kuongea na kusikika!
Naomba tu kutahadhalisha Ndugu zangu wa Ngara kuepuka haka kaugonjwa ka uchawa maana naona kameanza kuingia Ngara, sio asili yetu huo, tutawatenga Machawa wote ili mpone kwanza na muelewe uchawa ni udhalilishaji wako binafsi na ndio maana mnasababishana hata teuzi ziwapite wengine!!
Tanzania ni yetu SOTE ikiwamo NGARA!
samruhuza