Hoja ya Sam Ruhuza kuhusu teuzi inatafakarisha

josias

Member
Jan 7, 2014
47
34
Anaandika Sam Ruhuza kukosoa mfumo wa Teuzi kuwatenga Wananchi wa Wilaya ya Ngara.

Ndugu zangu Wanangara!

Nimetafakari sana hizi teuzi serikalini, kuna sehemu sizielewi, mnisaidie!

Ngara kuna watu ccm kwelikweli na vijana wengi wasomi tu, lakini kwenye teuzi, hauwaoni, lakini wanavyojifanya ni ccm damdam hadi unashangaa vipi hawaonekani, lakini maeneo ya wapinzani ndipo teuzi kila kukicha!!

Kigoma walipoamua kura zao kuwapa wapinzani hasa NCCR- Mageuzi majimbo yote, ccm wakashtuka, kila kitu wamepeleka kigoma! Mlezi wa Mkoa ni waziri mkuu, Makamu wa Rais, Waziri, wakuu wa Mikoa, Gavana Benki Kuu, yaani hauwezi kukuta teuzi yoyote hakuna mtu wa Kigoma, Barabara, Maji, umeme na bado kwenye uchaguzi ccm hawana uhakika wa kura za kigoma!
Angalia Kilimanjaro, Arusha na Mara walipoamua kuwapa Chadema! Teuzi na miradi kibao ni maeneo hayo!

Tuje kwenye ziara za viongozi wa serikali, hayo maeneo kila siku wanapishana, lakini Ngara walipoamua wenyewe kuipenda ccm, aibu hata kusema!!

Yaani kuna wakati naona wanangara wanajipendekeza ccm wakati yenyewe hata haiwapendi na ukijifanya kutambua haki yako, wanakuita Mrundi, Mnyarwanda kukukata spidi!!

Angalia hata teuzi za Mbunge wa Ngara, katika historia Ngara hatujawahi kuwa na Waziri kamili, tumeishia kwa Naibu Waziri Afya Mh Sebabii Gwassa 1975 tena nafikiri miaka miwili sikumbuki vizuri na Naibu Waziri Ujenzi na Mawasiliano Mh Gachocha 1985-90 kama sikosei na hao wote ni teuzi za kipindi chao cha kwanza cha uchaguzi, lakini kuanzia hapo hakuna teuzi tena Naibu wala Waziri!

Tumekuwa na Wabunge wasomi kwelikweli, wazoefu wakubwa Serikalini, lakini teuzi hakuna!!
Yaani Ngara ni sahihi sana kusema watu wanajipendekeza ccm wakati wenye chama chao hawawapendi!!

Nimeamua kuandika hili humu, japo wengine watalichukua kisiasa na kuwa na maono tofauti na mengine wanajua wao, lakini naangalia zaidi Maslahi ya Ngara na sitoshangaa baada ya andiko hili, ukaanza kuona teuzi zijazo mtu wa Ngara yumo kwasababu natambua nguvu ya maandiko yangu!

Binafsi Sihitaji uteuzi wowote ule, ila Ngara ni walipa kodi kama wananchi wengine, nitafurahi sana kuona jina la Mwananchi wa Ngara akipata uteuzi wowote angalau ashiriki kwenye kamati za maamuzi!
Naomba nieleweke Hii ni kwa maslahi ya Wanangara wote na kwa vizazi vyote pasipo kujali misimamo yao kisiasa zaidi ya uwezo wao kiuongozi, bila sisi wenyewe kuiongelea Ngara yetu na wananchi wake, hakuna mwingine wa kuongea na kusikika!
Naomba tu kutahadhalisha Ndugu zangu wa Ngara kuepuka haka kaugonjwa ka uchawa maana naona kameanza kuingia Ngara, sio asili yetu huo, tutawatenga Machawa wote ili mpone kwanza na muelewe uchawa ni udhalilishaji wako binafsi na ndio maana mnasababishana hata teuzi ziwapite wengine!!

Tanzania ni yetu SOTE ikiwamo NGARA!

samruhuza
 
Je kwanini Idara ya Uhamiaji ya Tanzania ina sababu za msingi kuwafanyia uchunguzi wa ziada wenyeji wa Kigoma, Tabora na Kagera juu ya uraia wao ?

Case study: The Protocol Signed at Kigoma, on 5 August 1924,​

Ni hatari sana, sababu hata Ubelgiji na Uingereza walipoingia mkataba baada ya Ubelgiji kuikalia mikoa ya Kigoma , Biharamulo, Tabora yote ikiwa mji wa Tabora nchini Tanganyika ndiyo makao makuu ya Majeshi ya Belgium.

Ni baada ya kumfurusha Mjerumani Tanganyika, washirika hawa wakoloni wa Belgiji na Uingereza mara tu baada ya vita kuu ya pili ya dunia 1914 - 1919 iliyopiganwa Tanganyika pia, mataifa ya kikoloni yaliyoshinda Tanganyika ya Ujerumani (German East Africa) yaani Ubelgiji na Uingereza yalingia Treaty /mkataba / makubaliano/ IGA


Le gènèral Tombeur et Bataille de Tabora

From February 23, 1915 to September 19, 1916, Charles Tombeur was commander-in-chief of the Force Publique in the Congo and this mandate ended following the capture of the town of Tabora by his troops. After this victory, he was knighted and would henceforth be called Tombeur de Tabora. Some monuments were subsequently erected in his memory and for the soldiers of the Public Force. What was the role of Charles Tombeur in the first Belgian offensive campaign and the capture of Tabora and how is he remembered? This research is divided into three chapters: the first takes stock of the diplomatic and military situation in the Belgian Congo before the war and explains the progress of Tombeur's African campaign. The second chapter analyzes the particular difficulties of fighting in Africa and the role of Tombeur in overcoming them. Finally, the last chapter focuses on how to commemorate and remember Tombeur, the African campaign and the soldiers who fell during these battles. Source : Charles Tombeur et la victoire de Tabora : souvenir d’un général hier et aujourd’hui | Mémoire UCL

22. Exchange of notes accepting the protocol signed at Kigoma, on 5 august 1924, relative to the Tanganyika-Ruanda-Urundi frontier. Brussels, 17 May 192646,47​

(46League of Nations, Treaty Series, vol. 54, p. 239.)

(47See also the Agreement between the United Kingdom and Belgiun regarding Water Rights on the Boundary between Tanganyika and Ruanda-Urundi, London, 22 November 1934, in Legislative Texts and Treaty Provisions concerning the Utilization of International Rivers for Other Purposes than Navigation (United Nations publication, Sales No. 63.V.4), p. 97.)

No. 1 - The British Ambassador at Brussels to the Belgian Minister for Foreign Affairs

Brussels, 17 May 1926

Monsieur le Ministre,

I have the honour, under instructions from His Majesty's Principal Secretary of State for Foreign Affairs, to convey to Your Excellency by the present note the formal acceptance by His Majesty's Government of the Protocol signed at Kigoma on 5 August 1924, with its accompanying maps, as defining the boundary between Tanganyika territory and the Belgian mandated territory of Ruanda-Urundi.

I am at the same time instructed to draw the attention of the Belgian Government to paragraph 51 of the Protocol in question and to invite them to agree that, notwithstanding the new boundary in Lake Tanganyika which is defined by the said paragraph, all customary rights of fishing and passage exercised by natives living on either side of it should be preserved, but that, at the same time, even with regard to the rights of fishing and passage, the respective Governments should preserve their common law rights and should not, for instance, be debarred from levying a fishing tax on all persons alike who use their territorial waters.

I should be grateful if Your Excellency would be good enough to confirm to me that the Belgian Government is in agreement with His Majesty's Government with regard to the arrangements indicated in the preceding paragraph.

I avail myself of this opportunity, etc.

No. 2 - The Belgian Minister for Foreign Affairs to the British Ambassador at Brussels

Brussels, 17 May 1926

Your Excellency,

I have the honour to acknowledge receipt of your letter of today's date, in which you are good enough to inform the Royal Government that His Britannic Majesty's Government accepts the Protocol signed at Kigoma on August 5, 1924, with its accompanying maps, as defining the boundary between Tanganyika Territory and the Belgian mandated territory of Ruanda-Urundi.

The Belgian Government also approves these documents.

At the same time you draw the attention of the Belgian Government to paragraph 51 of the Protocol in question and invite them to agree that, notwithstanding the new boundary in Lake Tanganyika which is defined by the said paragraph, all customary rights of fishing and passage exercised by natives living on either side of it should be preserved, but that at the same time, even with regard to the rights of fishing and passage, the respective Governments should preserve their common law rights and should not, for instance, be debarred from levying a fishing tax on all persons alike who use their territorial waters.

The Belgian Government has the honour to confirm to Your Excellency that they are in agreement with His Britannic Majesty's Government with regard to these arrangements.

................................................................
9 December 2020

Rais Magufuli aingilia kati, aeleza sababu ya somo la Historia kuwa la lazima ili ndugu zetu wa magharibi mwa Tanganyika wasibaguliwe​


Magufuli : Historia ya kweli ifundishwe, vijana lazima waifahamu historia yetu tumetoka wapi. Haiwezekani watoto wetu wafahamu historia ya Mansa Mussa wa huko Afrika ya Magharibi lakini hata ya "kwetu" hawaifahamu. ( Kigoma iliyokuwa ndani ya Ruanda-Urundi mpaka 1924 chini ya utawala wa Ubeljii) hawaifahamu.....

100 YEARS BELBASES

A FORGOTTEN PAGE OF BELGIAN COLONIALISM IN AFRICA

Belgian bases in East Africa​



The Belgian colonial period ended with the independence of Burundi and Rwanda on July 1, 1962, but there is still a vestige of our colonial past: the Belbases in Tanzania.

In 1919, during the negotiation of the Treaty of Versailles, Great Britain was able to seize almost all the German colonies in East Africa. Rwanda and Burundi became Belgian mandate areas.

But Belgium, which had also participated in the war effort in East Africa, was not satisfied, protesting strongly. She received in 1921 from the British a commercial gesture as a consolation, the so-called Belbases (from "Belgian Bases"), sites in two ports of Tanganyika: Kigoma on Lake Tanganyika, and Dar es Salaam on the Indian Ocean , with free transit on the railway between these two ports.

This agreement was signed 100 years ago, on March 15, 1921.

Belgium leased the concession for a symbolic franc per year, where it could build docks and warehouses, initially in perpetuity, from 1956. for 99 years.
Goods to and from the Belgian colonies in Central Africa could pass tax-free via the railway. The Belgian government entrusted the operation to a private company, the Belgian East African Agency, which later became the International Maritime Agency (AMI).
In 1956, the Belbases were transferred to the colonial government, which now funded the infrastructure. After the independence of Congo, Burundi and Rwanda, the Belbases became the joint property of the former colonies.

The transit zone gradually lost its economic importance and, certainly after the riots of 1991 (Congo) and 1994 (Rwanda), traffic from Central Africa stopped. Between 1994 and 1995 the AMI began discussions on an "honorable end" to the management agreement, in 1996 Tanzania took over the sites.

Even if they have not been used for 25 years, in theory these Belbases still exist, because the four countries (Tanzania, Burundi, Congo and Rwanda) have not yet been able to agree on compensation for the takeover of the installations.

 
Watu wa ngaramujini mna matatizo.

Wahangaza na washubi ni wachache lakini Wana roho mbaya sana.

Wanyangara mnapaswa kutawaliwa tu,

Wanyangara watata sana, mkiwapa urais watajaza Ndg zao warundi na watusi.
 
Kwani mtu akiteuliwa kuwa mkuu wa mkoa, wilaya au waziri lina maslahi gani kwa watu wa jamii ikiwa vyeo hivyo ni vya kiutumishi tu na maslahi ya teuzi ni ya mhusika na si jamii yake.

Kwanza Ngara inatakiwa ipitishiwe operesheni kimbunga maana si desturi ya watanganyika kuhoji vitu vya hovyo kama hivyo.
 
Watu wa ngaramujini mna matatizo.

Wahangaza na washubi ni wachache lakini Wana roho mbaya sana.

Wanyangara mnapaswa kutawaliwa tu,

Wanyangara watata sana, mkiwapa urais watajaza Ndg zao warundi na watusi.
Huko wanatakiwa wachunguzwe uraia wao. Unampa uteuzi mtu halafu baada ya muda unasikia yuko kigali!
 
Anaandika Sam Ruhuza kukosoa mfumo wa Teuzi kuwatenga Wananchi wa Wilaya ya Ngara.

Ndugu zangu Wanangara!

Nimetafakari sana hizi teuzi serikalini, kuna sehemu sizielewi, mnisaidie!

Ngara kuna watu ccm kwelikweli na vijana wengi wasomi tu, lakini kwenye teuzi, hauwaoni, lakini wanavyojifanya ni ccm damdam hadi unashangaa vipi hawaonekani, lakini maeneo ya wapinzani ndipo teuzi kila kukicha!!

Kigoma walipoamua kura zao kuwapa wapinzani hasa NCCR- Mageuzi majimbo yote, ccm wakashtuka, kila kitu wamepeleka kigoma! Mlezi wa Mkoa ni waziri mkuu, Makamu wa Rais, Waziri, wakuu wa Mikoa, Gavana Benki Kuu, yaani hauwezi kukuta teuzi yoyote hakuna mtu wa Kigoma, Barabara, Maji, umeme na bado kwenye uchaguzi ccm hawana uhakika wa kura za kigoma!
Angalia Kilimanjaro, Arusha na Mara walipoamua kuwapa Chadema! Teuzi na miradi kibao ni maeneo hayo!

Tuje kwenye ziara za viongozi wa serikali, hayo maeneo kila siku wanapishana, lakini Ngara walipoamua wenyewe kuipenda ccm, aibu hata kusema!!

Yaani kuna wakati naona wanangara wanajipendekeza ccm wakati yenyewe hata haiwapendi na ukijifanya kutambua haki yako, wanakuita Mrundi, Mnyarwanda kukukata spidi!!

Angalia hata teuzi za Mbunge wa Ngara, katika historia Ngara hatujawahi kuwa na Waziri kamili, tumeishia kwa Naibu Waziri Afya Mh Sebabii Gwassa 1975 tena nafikiri miaka miwili sikumbuki vizuri na Naibu Waziri Ujenzi na Mawasiliano Mh Gachocha 1985-90 kama sikosei na hao wote ni teuzi za kipindi chao cha kwanza cha uchaguzi, lakini kuanzia hapo hakuna teuzi tena Naibu wala Waziri!

Tumekuwa na Wabunge wasomi kwelikweli, wazoefu wakubwa Serikalini, lakini teuzi hakuna!!
Yaani Ngara ni sahihi sana kusema watu wanajipendekeza ccm wakati wenye chama chao hawawapendi!!

Nimeamua kuandika hili humu, japo wengine watalichukua kisiasa na kuwa na maono tofauti na mengine wanajua wao, lakini naangalia zaidi Maslahi ya Ngara na sitoshangaa baada ya andiko hili, ukaanza kuona teuzi zijazo mtu wa Ngara yumo kwasababu natambua nguvu ya maandiko yangu!

Binafsi Sihitaji uteuzi wowote ule, ila Ngara ni walipa kodi kama wananchi wengine, nitafurahi sana kuona jina la Mwananchi wa Ngara akipata uteuzi wowote angalau ashiriki kwenye kamati za maamuzi!
Naomba nieleweke Hii ni kwa maslahi ya Wanangara wote na kwa vizazi vyote pasipo kujali misimamo yao kisiasa zaidi ya uwezo wao kiuongozi, bila sisi wenyewe kuiongelea Ngara yetu na wananchi wake, hakuna mwingine wa kuongea na kusikika!
Naomba tu kutahadhalisha Ndugu zangu wa Ngara kuepuka haka kaugonjwa ka uchawa maana naona kameanza kuingia Ngara, sio asili yetu huo, tutawatenga Machawa wote ili mpone kwanza na muelewe uchawa ni udhalilishaji wako binafsi na ndio maana mnasababishana hata teuzi ziwapite wengine!!

Tanzania ni yetu SOTE ikiwamo NGARA!

samruhuza
NADHARIA MBILI KUHUSU KINACHOSABABISHA WANA NGARA WENGI WASIONEKANE KWENYE TEUZI

Nimepitia andiko la Sam Ruhuza, Moja ya Wanasiasa wakongwe, nguli na wabobezi kwenye siasa za Upinzani Nchini Tanzania toka kuanza kwa Mfumo wa Vyama vingi mnamo Mwaka 1992. Sam Ruhuza ni moja ya Viongozi wakubwa aliyehudumu kama Makamu Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi Taifa.

Nimeanza kwa kuelezea Uzito wa Mtoa hoja kabla ya Kuanza kuelezea Uzito wa Hoja yenyewe! !.

Katika chapisho lake la jana alitupia Jicho teuzi zilizofanyika jana katika nafasi za u DED, DC, RC na uhamisho uliofanyika.

Kama mzaliwa wa Ngara, Ndugu Sam Ruhuza alionyesha kusikitishwa kuona kuwa Teuzi nyingi ambazo zimekuwa zikifanyika Nchini toka Uhuru zimeiweka kando Wilaya ya Ngara pamoja na kuwa na Wasomi wengi tena Vijana. Hoja hii binafsi ninaona ina mashiko kwa kuangalia idadi ya Wana Ngara waliowahi kuteuliwa kushika nyadhifa za Ukurugenzi, Ukuu wa Wilaya, Ukuu wa Mkoa, Ukatibu Mkuu wa Wizara, Unaibu Waziri na Uwaziri. Kiukweli idadi ndogo Sana ya Wana Ngara imefanikiwa kuteuliwa katika Nyadhifa hizo.

Pamoja na Kuungana na Sam Ruhuza kuwa ni kweli ni Wana Ngara wachache wameteuliwa katika Nyadhifa mbalimbali ninaomba kupishana naye kuhusu hoja alizozitoa kuhusu kutoteuliwa kwa Vijana wa Ngara kushika nyadhifa mbalimbali Nchini.

Binafsi ninadhani Sio kweli kuwa wana Ngara hawateuliwi kwasababu wanaiunga Mkono Sana CCM. Katika hoja hii Ndugu Ruhuza alijaribu kuonyesha kuwa moja ya sababu za Wana Ngara hususani wana CCM kutoteuliwa ni kwasababu wanaiunga Mkono Sana CCM, huku akichagiza na Sentensi kuwa Wana Ngara wanajipendekeza kwa CCM, Hii ni hoja dhaifu Sana kwa sababu hakuna uthibitisho wa kisayansi kuwa Teuzi za Serikali zinalenga "kubembeleza" maeneo yaliyokuwa dominated na Upinzani.

Binafsi ninaweza kutoa nadharia kuu mbili za Kutoteuliwa kwa Wana Ngara wengi kwenye nafasi za Uongozi kama ifuatavyo:-

1.Nadharia ya kwanza ni Historia Mbaya ya baadhi ya Waliowahi kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali. Hii inaweza kuwa moja ya sababu kubwa ya hiki tunachokishuhudia. Kuna uwezekano Mkubwa waliotangulia kuna namna waliacha doa kubwa kwenye "mifumo" hivyo kufanya wana Ngara kutoaminika sana. Nadharia hii inaweza kuthibitishwa na Hoja ya Kwamba, Baada ya Kustaafu ni Wana Ngara wangapi waliokuwa wakitumikia nafasi nyeti serikalini wameendelea kuaminiwa walau kuteuliwa kuwa Wenyeviti wa Bodi walau ya Mashirika ya Umma au Taasisi za Serikali? Binafsi Sina kumbukumbu sahihi, ni kama vile watumishi hao walikuwa wakisubiriwa kwa Hamu wastaafu wakae pembeni.

Nadharia ya Pili ni Ubinafsi, Chuki na Roho mbaya zetu wenyewe.
Kwenye nadharia hii ninajaribu kuzingatia ya Kwamba Mh. Rais anatumia Taasisi zake kufanya Vetting kupata watu wenye sifa kulingana na nafasi husika. Ufanisi wa Taasisi hizo unategemea Taarifa toka kwa Wananchi hususani wale wenye mamlaka na ushawishi kutoka katika eneo husika.
Kwa uwazi kabisa, ni Wana Ngara wachache sana wanaweza kutoa Positive Remarks kwa wana Ngara wenzao linapokuja suala la Fursa. Kwa kiasi kikubwa wana Ngara ambao tulitarajia watumie ushawishi wao kuwajenga na Kuwavuta wana Ngara wenzao kupanda juu wamekuwa mstari wa Mbele kuwadidimiza na kuwatengenezea ukuta mgumu wa Mafanikio. Tabia hii haijaanza juzi wala jana. Wakati fulani nilikuwa naongea na Wazee fulani wa Ngara, walikuwa wakinipa story kuhusu namna walivyokuwa wakijiita Waha ama Wahaya pale walipokutana na Wana Ngara wenzao kwenye Ofisi moja ili kulinda vibarua vyao. Walijua wazi kuwa wakijulikana tuu kuwa ni wana Ngara watapigwa Negative Comments na watapoteza nafasi zao.

Ili tupate Nguvu ya Kulalamikia Mfumo wa Uteuzi tunapaswa Kujikagua Sisi kwanza. Sisi ni mabingwa wa Kusagiana Kunguni sisi kwa Sisi. Moja ya wataalamu wa Kusagia wenzao Kunguni ni Mzee wangu Sam Ruhuza!!!
Kwenye andiko lake amemaliza kwa kuwasagia Watu Kunguni kuwa Wana Ngara hawateuliwi kwasababu ya Uchawa, hivi unatarajia Mzee Ruhuza akipata Fursa ya kutoa Comments kuhusu hao anaowaita Chawa atafanyaje?
Naomba nihitimishe kwa Kuwasemea Vizuri Vijana wenzangu wa Ngara:-

Ngara haijawahi kuwa na Vijana Chawa, wanaoitwa Chawa ni wale tuu wanaowasemea mazuri Viongozi wa Serikali kwa kazi nzuri wanazofanya. Vijana hao Wanaitwa Chawa na Kundi la Watu wenye Uchu wa madaraka ambao wanatamani kuona Viongozi walioko madarakani wakitukanwa na Kubagazwa kama vile hakuna walichofanya

Namalizia kwa Kushauri Viongozi wa Chama na Serikali kulichukua andiko la Sam Ruhuza katika namna Chanya. Vijana kama akina Lameck Jacton, Aneth Nyamziga, Hilali Ruhundwa, somebody Nchunda, Misigaro (Kijana wa Bukiriro kama sikosei, nilimfahamu kwa Hoja zake nzito kwenye uchaguzi wa 2015) na wengine wengi ninaowajua tumewasemea kwa kiwango gani ili mamlaka za Uteuzi ziwaone? Kwenye maeneo tunayohisi hawakidhi vigezo vya Uteuzi tumewatengeneza kwa kiasi gani ili wakidhi vigezo vya Uteuzi?

Josias Charles
 
Back
Top Bottom