255Texter
Senior Member
- Aug 31, 2007
- 150
- 8
Ndugu zangu Watanzania wenye mapenzi ya kweli kwa Taifa letu, naandika maneno haya huku moyo wangu ukuwa mzito sana kutokana na mauaji ya kila siku yanayoendeshwa na chombo tulichokikabidhi ridhaa ya kulinda usalama wetu.
Jeshi la Polisi ni chombo muhimu katika jamii ambacho katika jamii huru na zenye kufuata utawala wa sheria, ni chombo kinachoaminiwa na kupendwa na raia.
Kwetu Tanzania, ni dhahiri kwamba jeshi la Polisi limepoteza uhalali wa kuwa chombo cha kulinda amani na usalama wa raia na mali zao.
Sababu ya kwanza ya jeshi hili kupoteza uhalali wake, ni mfumo mzima wa uongozi wake ambao kama ilivyo kwa vyombo vingine vya dola (TAKUKURU nk), unatokana na uteuzi wa Raisi na unatumikia matakwa ya Raisi na chama chake. Hivyo, uongozi wa chombo cha kuhakikisha usalama wa raia wote(wana-CCM na wasio wana-CCM) unafanya kazi yake si kwa misingi ya uadilifu wa "Profession" ya upolisi, bali kwa kufuata maagizo na matakwa ya wanasiasa.
Sababu ya Pili ambayo inahusiana na hiyo ya kwanza, ni ukiukwaji wa maadali na utaratibu mbovu katika kusaili, kuchagua na kuajiri waTanzania wenye sifa za kujiunga na Jeshi hilo. Si ajabu siku hizi kuona watu wenye rekodi za uhalifu na kuwahi kushitakiwa na/au kutiwa hatiani kwa uhalifu, ndio wanaajiriwa kuwa mapolisi. Pia, kupotea kwa maadili hayo katika mfumo wa ajira ya Polisi inapelekea watu wenye vyeti vya kughushi kuwa na ujasiri wa kuwasilisha vyeti hivyo katika maombi ya ajira ndani ya Polisi. Hiki ni kipimo cha jinsi gani Jeshi la Polisi limeshindwa wajibu wake wa msingi, kwani ni moja ya majukumu ya Jeshi hilo kutafiti, kugundua na kufichua cyeti au kielelezo chochote ambacho ni cha kughushi.
Ingawa matatizo ni mengi yanayowakabili askari Polisi, ikiwemo ujira mdogo, ukosekanaji wa vitendea kazi nk, lakini sababu hizo mbili nilizoanisha hapo juu ndio msingi wa kuporomoka kwa utendaji ndani ya jeshi hilo na kulifanya lipoteze uhalali wake wa kuendelea kuwepo kama chombo cha ulinzi wa usalama wa raia na mali zao. Ni kutokana na sababu hizo za msingi, ndio maana tunasikia askari Polisi wakihusishwa na ujambazi na vitendo vingine vingi vya uhalifu. Uongozi mbovu uliotokana na ajira zisizofuata taratibu madhubuti, ndio kiini cha kuwa na viongozi wa Polisi ambao wanaagiza askari wao kuleta "mshiko" pale askari hao wanapopangiwa kufanya doria. Si ajabu basi, kwa uongozi wa aina hiyo kuwaagiza askari wao kufanya mauaji ama kwa nia ya kuficha ushahidi (Ref. URT vs Zombe) au kutekeleza maagizo ya mabosi wao wa kisiasa. Kwa kifupi hakuna maadili ya Kipolisi kwa kuwa mfumo mzima umekufa.
Kwa sababu hiyo basi, hatuna budi sisi kama wananchi, kuweka shinikizo la kutaka Jeshi hilo livunjwe na kuundwa upya. Uvunjwaji wa Jeshi hilo ufuate mpangilio maalum, kama ifuatanyo:
1) Iundwe Tume/Kamati Huru chini ya moja ya Majaji waliostaafu (e.g. Jaji Augustino Ramadhani)
2) Uongozi wote wa Juu wa Jeshi (IGP pamoja na Makamishna wote) katika makao makuu waondolewe/wastaafishwe na nafasi zao kukasimiwa na Tume. MaRPC wote pia waondolewe.
3) Tume ifanye mpango wa kuajiri kwa mkataba maalum, maafisa wa Polisi kutoka nchi za jumuiya ya madola (Ghana, Nigeria, Uganda) ili kuchukua madaraka ya uongozi katika Makao Makuu. Pia kupata ushauri wa kitaalam kutoka nchi marafiki (e.g. Schotland Yark-UK)
4) Tume ifanye usaili na uhakiki wa maafisa wa Polisi kuanzia cheo cha Inspector kwa msaada wa wataalamu hao kutoka nchi za nje, ili kuweza kupata wachache wenye uadilifu wa hali ya Juu na rekodi safi, ili wakaimishwe madaraka ya u-RPC.
5) Tume kwa kushirikiana na uongozi mpya wa juu katika Jeshi, lianze usaili na uhakiki wa askari wote, ili kuthibitisha vyeti vyao, historia zao kimaisha na rekodi zao za kazi. Wale watakaothibitika kuwa sio safi, waondolewe mara moja na ikibidi kushtakiwa kama watagunduliwa kughushi vyeti au historia zao za maisha.
Tume ipewe muda wa miaka mitano wa kulisafisha Jeshi la Polisi na baada ya kipindi hicho cha mpito, iundwe Tume ya Kudumu ya Usimamizi wa Jeshi la Polisi, ambayo itaundwa na Bunge na kutoa ripoti yake kwa Kamati ya Bunge inayosimamia Wizara ya Mambo ya Ndani. Hii itakuwa ni mwisho wa ukiritimba wa viongozi wa CCM wa kulitumia Jeshi la Polisi kwa manufaa yao kisiasa.
Nawakilisha!
Jeshi la Polisi ni chombo muhimu katika jamii ambacho katika jamii huru na zenye kufuata utawala wa sheria, ni chombo kinachoaminiwa na kupendwa na raia.
Kwetu Tanzania, ni dhahiri kwamba jeshi la Polisi limepoteza uhalali wa kuwa chombo cha kulinda amani na usalama wa raia na mali zao.
Sababu ya kwanza ya jeshi hili kupoteza uhalali wake, ni mfumo mzima wa uongozi wake ambao kama ilivyo kwa vyombo vingine vya dola (TAKUKURU nk), unatokana na uteuzi wa Raisi na unatumikia matakwa ya Raisi na chama chake. Hivyo, uongozi wa chombo cha kuhakikisha usalama wa raia wote(wana-CCM na wasio wana-CCM) unafanya kazi yake si kwa misingi ya uadilifu wa "Profession" ya upolisi, bali kwa kufuata maagizo na matakwa ya wanasiasa.
Sababu ya Pili ambayo inahusiana na hiyo ya kwanza, ni ukiukwaji wa maadali na utaratibu mbovu katika kusaili, kuchagua na kuajiri waTanzania wenye sifa za kujiunga na Jeshi hilo. Si ajabu siku hizi kuona watu wenye rekodi za uhalifu na kuwahi kushitakiwa na/au kutiwa hatiani kwa uhalifu, ndio wanaajiriwa kuwa mapolisi. Pia, kupotea kwa maadili hayo katika mfumo wa ajira ya Polisi inapelekea watu wenye vyeti vya kughushi kuwa na ujasiri wa kuwasilisha vyeti hivyo katika maombi ya ajira ndani ya Polisi. Hiki ni kipimo cha jinsi gani Jeshi la Polisi limeshindwa wajibu wake wa msingi, kwani ni moja ya majukumu ya Jeshi hilo kutafiti, kugundua na kufichua cyeti au kielelezo chochote ambacho ni cha kughushi.
Ingawa matatizo ni mengi yanayowakabili askari Polisi, ikiwemo ujira mdogo, ukosekanaji wa vitendea kazi nk, lakini sababu hizo mbili nilizoanisha hapo juu ndio msingi wa kuporomoka kwa utendaji ndani ya jeshi hilo na kulifanya lipoteze uhalali wake wa kuendelea kuwepo kama chombo cha ulinzi wa usalama wa raia na mali zao. Ni kutokana na sababu hizo za msingi, ndio maana tunasikia askari Polisi wakihusishwa na ujambazi na vitendo vingine vingi vya uhalifu. Uongozi mbovu uliotokana na ajira zisizofuata taratibu madhubuti, ndio kiini cha kuwa na viongozi wa Polisi ambao wanaagiza askari wao kuleta "mshiko" pale askari hao wanapopangiwa kufanya doria. Si ajabu basi, kwa uongozi wa aina hiyo kuwaagiza askari wao kufanya mauaji ama kwa nia ya kuficha ushahidi (Ref. URT vs Zombe) au kutekeleza maagizo ya mabosi wao wa kisiasa. Kwa kifupi hakuna maadili ya Kipolisi kwa kuwa mfumo mzima umekufa.
Kwa sababu hiyo basi, hatuna budi sisi kama wananchi, kuweka shinikizo la kutaka Jeshi hilo livunjwe na kuundwa upya. Uvunjwaji wa Jeshi hilo ufuate mpangilio maalum, kama ifuatanyo:
1) Iundwe Tume/Kamati Huru chini ya moja ya Majaji waliostaafu (e.g. Jaji Augustino Ramadhani)
2) Uongozi wote wa Juu wa Jeshi (IGP pamoja na Makamishna wote) katika makao makuu waondolewe/wastaafishwe na nafasi zao kukasimiwa na Tume. MaRPC wote pia waondolewe.
3) Tume ifanye mpango wa kuajiri kwa mkataba maalum, maafisa wa Polisi kutoka nchi za jumuiya ya madola (Ghana, Nigeria, Uganda) ili kuchukua madaraka ya uongozi katika Makao Makuu. Pia kupata ushauri wa kitaalam kutoka nchi marafiki (e.g. Schotland Yark-UK)
4) Tume ifanye usaili na uhakiki wa maafisa wa Polisi kuanzia cheo cha Inspector kwa msaada wa wataalamu hao kutoka nchi za nje, ili kuweza kupata wachache wenye uadilifu wa hali ya Juu na rekodi safi, ili wakaimishwe madaraka ya u-RPC.
5) Tume kwa kushirikiana na uongozi mpya wa juu katika Jeshi, lianze usaili na uhakiki wa askari wote, ili kuthibitisha vyeti vyao, historia zao kimaisha na rekodi zao za kazi. Wale watakaothibitika kuwa sio safi, waondolewe mara moja na ikibidi kushtakiwa kama watagunduliwa kughushi vyeti au historia zao za maisha.
Tume ipewe muda wa miaka mitano wa kulisafisha Jeshi la Polisi na baada ya kipindi hicho cha mpito, iundwe Tume ya Kudumu ya Usimamizi wa Jeshi la Polisi, ambayo itaundwa na Bunge na kutoa ripoti yake kwa Kamati ya Bunge inayosimamia Wizara ya Mambo ya Ndani. Hii itakuwa ni mwisho wa ukiritimba wa viongozi wa CCM wa kulitumia Jeshi la Polisi kwa manufaa yao kisiasa.
Nawakilisha!