Hoja binafsi kuhusu umri wa wabunge

kwa mujibu wa katiba ya yetu ya mwaka 77, ili mtanzania agombee ubunge, anapaswa kuwa na umri usiopungua miaka 22. ruhusa huu umefanya bunge letu liwe na wabunge wengi vijana. ni jambo zuri! tatizo langu liko kwenye mwenendo na tabia ya vijana kwa ujumla. wabunge wengi vijana akina zitto, kafulila, mnyika, sugu. mkosamali, mdee, magige, bulaya.... nk..... hawajaoa au kuolewa. pana umuhimu kwao kuoa au kuolewa



NDOA HUJENGA AKILI NA NA HULETA HESHIMA

nasisitiza wakaoe au wakaolewe kwa sababu uwezo wa kufanya hivyo wanao. ndoa humfanya mtu ajiheshimu na pia aheshmike. jamii humuona alieoa kama mtu aliekamilika.



UJANA UNAWASUMBUA WABUNGE VIJANA

umri wa mtu aghalabu kuathiri upeo wake wa kufikiri na kujieleza. kitendo cha mnyika kumtukana mh Rais bungeni na kumuita dhaifu ni kinyume cha kanuni za bunge na ni kinyume na desturi zetu watanzania. la kushangaza alichokua anazungumzia hakimhusu Rais moja kwa moja! kusema hadharani bungeni kuwa "rais kikwete ni dhaifu" ni kauli ya kumdhalilisha mh rais. mnyika licha ya kuwa na shahada ya chuo kikuu, damu ya ujana inamsumbua. aliombwa na naibu spika kufuta kauli yake lakini akakaidi kufanya hivyo! mchango ambao angeutoa kuwawakilisha wana ubungo kuhusu bajeti hakuweza kuutoa baada ya kutolewa nje ya ukumbi wa bunge na naibu spika ndugai



NINI KIFANYIKE?



kwa nia njema nashauri katika maoni ya katiba mpya, tupendekeze umri wa mbunge uanze miaka 30. umri huu mtu anakuwa keshapitia mikiki mingi ya maisha. anajua la kusema kama mtu mzima aliekamilika. naomba kuwasilisha!!!!!!

livingstone lusinde kibajaji ameoa,ana watoto(wala sio mtoto) na ana miaka zaidi ya 30..kwa maana hii,kwa vipimo vyako vya busara..huna hoja.

Halafu watanzania mtaacha lini uoga??lini hasa??rais mmemchagua wenyewe,kama amekuwa dhaifu asiambiwe jamani??kwani amekuwa nani?mfalme?yesu?mohammad?au malaika?Nadhani kama tumempa kazi na ameshindwa kuifanya kwa mkono hodari..yeye ni DHAIFU!
 
Hivi kusema 'dhaifu' na kusema 'mnafiki' kipi ni tusi?
Kwa maneno haya lazma una umri wa 80+ na hauelewi nini kinaendelea duniani!
 
watu wanafikiri mtu akishakuwa raisi amekuwa mungu wa pili hapa duniani asiguswe wala asisemwe no raisi ni kama wewe anaenda chooni kama kawaida na mahitaji yote kama yako kinachobadilika hapo ni hiyo status tu kwa hiyo na yeye ni binadamu anaweza kukosea na kukosolewa vile vile jamani mbona haya maneno huwa tunayatumia sana maofisini kwa kuwa leo kasema bungeni limekuwa bango?? nahisi hawa wanaopinga hili jambo ni kile kizazi cha TANU. zamani baba akisema jambo kwenye familia hata kama lina madhara kuanzia mke, mtoto wote wanagwaya ila leo ukisema kama umekosea mtoto anakuambia kabisa baba ni hivi na hivi tufanye hivi ili mambo yaende sawa na unaambiwa kabisa hapo umekosea so mkubali mabadiliko la kundi hili la vijana. vijana hatuishi kwa unafiki tunakuchana hapo hapo. ila kesho tumesahau tunasonga mbele. mi sioni kama kuna tatizo kabisa basi kwenye mkutano ujao nahisi VUVUZELA nape atalishikia pango la Udhaifu utasikia alivyo kichwa maji huyo.
 
kwa mujibu wa katiba ya yetu ya mwaka 77, ili mtanzania agombee ubunge, anapaswa kuwa na umri usiopungua miaka 22. ruhusa huu umefanya bunge letu liwe na wabunge wengi vijana. ni jambo zuri! tatizo langu liko kwenye mwenendo na tabia ya vijana kwa ujumla. wabunge wengi vijana akina zitto, kafulila, mnyika, sugu. mkosamali, mdee, magige, bulaya.... nk..... hawajaoa au kuolewa. pana umuhimu kwao kuoa au kuolewa



NDOA HUJENGA AKILI NA NA HULETA HESHIMA

nasisitiza wakaoe au wakaolewe kwa sababu uwezo wa kufanya hivyo wanao. ndoa humfanya mtu ajiheshimu na pia aheshmike. jamii humuona alieoa kama mtu aliekamilika.



UJANA UNAWASUMBUA WABUNGE VIJANA

umri wa mtu aghalabu kuathiri upeo wake wa kufikiri na kujieleza. kitendo cha mnyika kumtukana mh Rais bungeni na kumuita dhaifu ni kinyume cha kanuni za bunge na ni kinyume na desturi zetu watanzania. la kushangaza alichokua anazungumzia hakimhusu Rais moja kwa moja! kusema hadharani bungeni kuwa "rais kikwete ni dhaifu" ni kauli ya kumdhalilisha mh rais. mnyika licha ya kuwa na shahada ya chuo kikuu, damu ya ujana inamsumbua. aliombwa na naibu spika kufuta kauli yake lakini akakaidi kufanya hivyo! mchango ambao angeutoa kuwawakilisha wana ubungo kuhusu bajeti hakuweza kuutoa baada ya kutolewa nje ya ukumbi wa bunge na naibu spika ndugai



NINI KIFANYIKE?



kwa nia njema nashauri katika maoni ya katiba mpya, tupendekeze umri wa mbunge uanze miaka 30. umri huu mtu anakuwa keshapitia mikiki mingi ya maisha. anajua la kusema kama mtu mzima aliekamilika. naomba kuwasilisha!!!!!!

Mada yako ni nzuri ila tatizo tu namna ulivyoileta umeonyesha kwamba kuoa ni muhimu kuliko umri huo hapo ndipo udhaifu wa mada yako ulipo, vinginevyo kuoa hata kijana wa miaka 18 anaruhusuwa kisheria lakini je amekomaa kuwa kiongozi? Ungejaribu kubuni namna ya kuwasilisha ujumbe wako na kuhusu kuona ingekuwa moja ya maoni yako ambayo unaona yanasaidia kijana kutulia na hata kuwa na mwenzi wa kumpa ushauri, vinginevyo vijembe hivyo usingevipata.

Naweza kuisahihisha hoja yako kama ifuatavyo:

Vijana ni wazungumzaji wazuri na pengine hata kupanga hoja nzuri, tatizo hoja zao zinakosa hekima na busara. Hii inatokana na ukweli wa kibaoloiia kwamba binadamu hukua hatu kwa hatu hadi kukomaa kimwili na kiakili. Vijana wengi chini ya umri wa miaka 30 na kabisa umri huo wa 22 ni kipindi ametoka kwenye hatua ya
teenage ambayo ni kila mmoja anajua umri ambao vijana hawaambiliki wala kusikia wakiangalishwa, hali kadhalika ni kipindi kijana anapojiona anaweza kila kitu wakati si hivyo kutokana na kupevuka maungo lakini bongo huwa halijatulia.

Umri mdogo huo wa vijana huwa wanafikiri kwamba wanaweza kila kitu, lakini wakishaanza kufikisha umri wa miaka 30 huanza kujiona hawawezi kila kitu na ni ukweli wanajisikia kuna wanachopungukiwa na hivyo hitaji la kushirikiana na wengine kufanikisha huibuka. Huo ndio umri ambao vijana wengi tupo tunadai haki za kushika madaraka wakati mwili na akili havijakomaa vizuri ila tu ni makuzi. Vijana wengi wa siku hizi sababu ya lishe nzuri kuanzia miaka 13-14 wanaonekana wakubwa kwa umbo lakini je kiakili wamekua?

Kuna lugha nyingi ambazo zinaleta mkanganyiko kutoka kwa vijana, tatizo ni busara na hekima ya kuchagua maneno na nafasi gani unaongelea na kwa watu wa aina gani na katika nazingira gani. Nini watu wanatazamia uongee? Ukiona wengi wanashtuka na kauli hata kama maudhui yake ni nzuri lakini lugha si nzuri, maana yake umeteleza. Hata kama utakuwa umejaribu kujenga hoja baadaye ya kutetea jambo hilo ni shauri ya kujitetea tu ila kuna kitu kimekosekana ambacho kimezoeleka kama
diplomatic language. Hata hivyo inatemegea sana na umri kwani umri wa ujana kama alivyosema Mbowe ni hali ya ujana kulipuka kama moto wa gas.

Mapokeo na utamaduni wetu vijana wanatakiwa kufundwa na wazee katika mambo mengi iwe katika maisha na uongozi, sababu si za kuzunguka ila tu ni wazee kutulia kiakili na kutoa neno lenye kupima kwa subira kutokana na uzoefu wa maisha kuangalia nini adhari za pande zote na kuchagua lile ambalo halitaleta mkanganyiko mkubwa.

Yaliyotokea Bungeni leo wengu tunashangilia, lakini kwangu naona kuna kitu kimepungua katika kauli ya Mnyika kwa kukosa kutoa kauli hiyo nzito kwa maneno laini (diplomatic language). Watanzania wengi hata wenye nafasi kubwa huwa hatuelewi tunaopongea mikutanoni au hawa wa mataifa makubwa wanapotuambia kitu, tunafikiria kusifiwa kumbe tumesemwa na kudharaurika kwa sababu ya kutoelewa utumiaji wa
diplomatic language. Wenzetu wanaweza kukusema sana na hata kukudharau lakini usipojua utafikiria anakupongeza na mkabaki mnacheka na kuendelea na yaliyojilia ni sababu ya matumizi ya lugha.

Umri wa miaka 22 si umri mzuri wa kuwa viongozi kwa umma, bali ni umri wa kuandaliwa kuwa kiongozi, ndio maana kuandaa mabaraza ya vijana waanze kukomaa huko na kisha wapewe madaraka wakishahitimu huko katika kujizoesha, kutoka huko unaweza kupata vijana wengi wazuri sana katika kuongoza nchi. La sivyo tunaruka hatua muhimu ambayo inaweza kusababisha hamasa ya viongozi vijana kuitumbukiza nchi katika matatizo makubwa hadi machafuko.

Mtoa mada ametoa mada nzuri, ila tu hakutoa hoja zenye kujenga ukweli wa hoja zake na hivyo hoja yake kuonekana dhaifu kwa kufikiria kukomaa kwa mtu ni kuwa katika maisha ya famili (ndoa) wakati kuna mambo mengine ya msingi ambayo kijana anatakiwa kupitia hadi kufikia wakati mzuri ambao anaweza kujiamini na kuona kasoro zake huo ndio ubora wa uongozi.
 
watu wanafikiri mtu akishakuwa raisi amekuwa mungu wa pili hapa duniani asiguswe wala asisemwe no raisi ni kama wewe anaenda chooni kama kawaida na mahitaji yote kama yako kinachobadilika hapo ni hiyo status tu kwa hiyo na yeye ni binadamu anaweza kukosea na kukosolewa vile vile jamani mbona haya maneno huwa tunayatumia sana maofisini kwa kuwa leo kasema bungeni limekuwa bango?? nahisi hawa wanaopinga hili jambo ni kile kizazi cha TANU. zamani baba akisema jambo kwenye familia hata kama lina madhara kuanzia mke, mtoto wote wanagwaya ila leo ukisema kama umekosea mtoto anakuambia kabisa baba ni hivi na hivi tufanye hivi ili mambo yaende sawa na unaambiwa kabisa hapo umekosea so mkubali mabadiliko la kundi hili la vijana. vijana hatuishi kwa unafiki tunakuchana hapo hapo. ila kesho tumesahau tunasonga mbele. mi sioni kama kuna tatizo kabisa basi kwenye mkutano ujao nahisi VUVUZELA nape atalishikia pango la Udhaifu utasikia alivyo kichwa maji huyo.

Ni ukweli mtupu tunakosa kuelewa hilo kwamba Rais ni binadamu anayekosea kama wengi tunavyofanya ndio maana ana wengi waliomzunguka katika kumsaidia kuongoza na kabisa kumshauri namna bora ya kuongoza nchi. Lakini ukweli unabaki hata wewe ukiwa na kitu cha kumshauri baba yako unachagua lugha gani ambayo baba yako atabaki na heshima yake kwako na pia atajisikia kijana unaakili ya kutoa jambo zuri la kumshauri baba. Si mradi kuropoka tu bila kuchagua maneno ya kuongea katika nafasi uliyo nayo.
 
Ni ukweli mtupu tunakosa kuelewa hilo kwamba Rais ni binadamu anayekosea kama wengi tunavyofanya ndio maana ana wengi waliomzunguka katika kumsaidia kuongoza na kabisa kumshauri namna bora ya kuongoza nchi. Lakini ukweli unabaki hata wewe ukiwa na kitu cha kumshauri baba yako unachagua lugha gani ambayo baba yako atabaki na heshima yake kwako na pia atajisikia kijana unaakili ya kutoa jambo zuri la kumshauri baba. Si mradi kuropoka tu bila kuchagua maneno ya kuongea katika nafasi uliyo nayo.

sawa mkuu kwa mfano nikimuambia baba yangu hivi " baba hapo umefanya udhaifu kabisa fanya hivi" nitakuwa nimemkosea baba yangu heshima?? naomba unieleweshe hapo please.
 
sawa mkuu kwa mfano nikimuambia baba yangu hivi " baba hapo umefanya udhaifu kabisa fanya hivi" nitakuwa nimemkosea baba yangu heshima?? naomba unieleweshe hapo please.


Hutakuwa umefanya vibaya ile lugha hiyo ni kali utakuwa unaonekana si mahiri wa kuchagua lugha ambayo itakujengea heshima kwako na kwako.
 
Hutakuwa umefanya vibaya ile lugha hiyo ni kali utakuwa unaonekana si mahiri wa kuchagua lugha ambayo itakujengea heshima kwako na kwako.

Kwa hiyo JEMBE MNYIKA (JM) jana alitolewa nje kwa sababu sio mahili wa kuchagua lugha? Naomba mwongozo wako mkuu
 
Back
Top Bottom