Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
CCM imekuwa chama chenye nguvu kwa sababu ya pesa walizo nazo au wanazo-control, kuiba (kama vile EPA) na michango ya mabilioni kupitia wafanyabiashara ambao baadhi yao hupata mwanya ya kufanya wizi na ufisadi mwingine bila hofu kubwa ya kuchukuliwa hatua.
Sasa ukiondoa pesa basi CCM hakuna kitu. Baada ya uchaguzi, mgao wa CCM wa ruzuku kutoka serikalini umepungua kwa zaidi ya Sh milioni 200 kila mwezi na tayari tumeona hilo limeanza kuwawewesesha.
CCM wanazo taarifa kwamba CDM wanapata fedha nyingine nyingi ukiachilia mbali ruzuku ya serikali. Hili linawatia wasiwasi mkubwa. Taarifa hizo ni kwamba kuna baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wameanza kukichangia CDM kama kinga kwamba kutokana na dalili zinazoonekana waziwazi wa kupungua umaarufu wa CCM, huenda CDM ikachukua nchi 2015.
Hawa wafanyabiashara (Waesia na Waafrika) wajanja sana, wanachangia CDM kimya kimya, (ukiuachia huyo Sabodo) tena mabilioni mengi. Wameona upepo jinsi unavyovuma.
Sasa hilo ndilo linaipa CCM kiwewe kikubwa na ndiyo maana wanatoa kauli kwamba CDM inapata hela kutoka nje "kufanya machafuko". Wanajua kwamba wakisema wanapata kutoka ndani, haitakuwa na element ya "crime" ndani yake kwani nao CCM si wanapata pesa kutoka ndani?
Lakini hizi ndizo siasa -- na ninasema hivi -- CCM iko tayari kutumia kila mbinu katika uwezo wake, za halali na haramu, iko hata tayari kumwagika damu kuliko kuachia madaraka kwa chama kingine kwa njia halali za kidemokrasia. Dalili hizo ziko na baadhi yake na kama hili la kuwasingizia CDM wanapata hela kutoka nje.
Sasa ukiondoa pesa basi CCM hakuna kitu. Baada ya uchaguzi, mgao wa CCM wa ruzuku kutoka serikalini umepungua kwa zaidi ya Sh milioni 200 kila mwezi na tayari tumeona hilo limeanza kuwawewesesha.
CCM wanazo taarifa kwamba CDM wanapata fedha nyingine nyingi ukiachilia mbali ruzuku ya serikali. Hili linawatia wasiwasi mkubwa. Taarifa hizo ni kwamba kuna baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wameanza kukichangia CDM kama kinga kwamba kutokana na dalili zinazoonekana waziwazi wa kupungua umaarufu wa CCM, huenda CDM ikachukua nchi 2015.
Hawa wafanyabiashara (Waesia na Waafrika) wajanja sana, wanachangia CDM kimya kimya, (ukiuachia huyo Sabodo) tena mabilioni mengi. Wameona upepo jinsi unavyovuma.
Sasa hilo ndilo linaipa CCM kiwewe kikubwa na ndiyo maana wanatoa kauli kwamba CDM inapata hela kutoka nje "kufanya machafuko". Wanajua kwamba wakisema wanapata kutoka ndani, haitakuwa na element ya "crime" ndani yake kwani nao CCM si wanapata pesa kutoka ndani?
Lakini hizi ndizo siasa -- na ninasema hivi -- CCM iko tayari kutumia kila mbinu katika uwezo wake, za halali na haramu, iko hata tayari kumwagika damu kuliko kuachia madaraka kwa chama kingine kwa njia halali za kidemokrasia. Dalili hizo ziko na baadhi yake na kama hili la kuwasingizia CDM wanapata hela kutoka nje.