Hizi ni dalili kuwa Rais Magufuli ana mapungufu ya uongozi?

Kuna watu humu hawapendi kabisa kusikia neno Escrow. ........!! Magufuli astick tu kwenye ahadi yake ya mahakama ya Mafisadi ili tujue ukweli nani ni fisadi nchi hii!!
 
Kopo ndiyo nani? wewe mwenyewe unaishi kwa shemeji yako huna uhakika na maisha yako unawaita wasio na njaa kopo? Je? Ukipata pesa hata ukamiliki pikipiki utawaita nini? Hivi kopo ndilo lilibeba mapesa ya Escrow? Kopo ndilo lilinunua kivuko kibovu cha mwaka 1978 kwa billion 8 ? Hilo kopo ndilo liliuza nyumba za Serikali na zingine kuzigawa kwa michepuko na wadogo zake? au zile billion 250 walizolipwa makandarasi hewa ziliingizwa kwenye hilo kopo?
Hapo ndio unadhihirisha kuwa wengiwenu mpompo tu, akili yako inaishia kumdhania mtu, umekalili mambo kimazoea, nalishwa na shemeji!!! shida yoote mlikunywa maji yali kwisha kuogwa na Mbowe, Narudia Magufuli alikuwa na mpinzani KOPO sasa mlitegemea tupeleke ikulu KOPO? Hahaha hakuna hilo Tumesha wazoea ZUZU wenu Mbowe akiamka na ajenda ya MWIZI KUWA MTAKATIFU VICHAA WAKE WOOTE JF MNAJIACHIA
 
Binadamu bwana! Haweshi maneno. Fungeni hakuli zenu. Jpm ana miaka mitano. Ndo kwanza ana siku 30 mshaanza vijineno. Afu pilipili usoila yakuwashiani? Hata asipofanya mtakavyo ndo tumemchagua ajenge barabara sio kukamata mafisadi. Kwani mamvi wenu hatopona
 
CCM ni ile ile Ohoo ni ile ile !!!!!, Kikwete ni yule yule Ohoo ni yule yule!!!!!, na Magufuli ni yule yule Ohoo!!!! ni yule yule!!!!!!!

Watanzania wanashindwa kuelewa kuwa nchi haiongozwi kwa matukio kwa maana ya kwa matukio yakiisha hakuna jipya
 
Tuliompa kura na kumpigia kampeni tumelizika..na tunajua anaendelea kukaza uzi
 
Rais Magufuli - mapungufu ya uongozi

Sijaridhika wala kukubaliana na utumbuaji wa majipu wa huyu Mheshimiwa Magufuli, ambaye ni Rais wa Jamhuri yetu ya Muungano.

Jambo la kwanza alilonikosesha nisimwamini kwa asilimia kubwa niusanii namna alivyokwepesha kashfa ya watu binafsi waliojimilikisha UDA na kuikosesha serikali mapato kwa kukwepa kodi. Suala la UDA limefukiwafukiwa hadi sasa linaonekana kutopewa uzito stahiki.

Uteuzi wa baraza la mawaziri umedhihirisha hana jipya zaidi ya kuwanyanyapalia dagaa huku wahusika wakuu wa kashfa bandarini, Escrow na TRA waliokuwa mawaziri na makatibu wakuu wa serikali ya Kikwete akiwatunukia uwaziri tena na kuendelea Ukatibu Mkuu licha ya kashfa nzito zilizoibuliwa na bunge hadi kuachia ngazi.

Kushindwa kushughulikia mgogoro wa Uchaguzi Mkuu Zanzibar dalili tosha Rais Magufuli kadiri ya msimamo wa CCM hana ubavu kwa chama chake, bali kukipigia magoti tu. Hana nguvu alina nayo kikatiba ila kutii matakwa ya chama chake.

Dhahiri alichoanza Rais Magufuli ni nguvu za soda, hatimaye yatakayojilia ni kukata tamaa na kuendelea na mazoea bora liende muhula uishe.

Ndio mjue nchi haiongozwi kwa matukio
 
Jpm ameanza kwa kilipa kisasi kwa jk. Anawatema wateule wake wote. Na aliolazimishwa kuwateua kama Jmakamba na Nape kawaficha kama yeye alivyoundiwa wizara ya vitoweo
 
Ccm ni ile ile oooh ni ile ileee....Mliopiga kura kwa Ccm poleni...ndg zangu...Ccm wengine hatuna uchungu wengine wowote...kwanza kura yangu sikuipa Ccm....Moyo wangu safi...bila majuto yoyote...!!!! .....(kiuzalendo)JPM Ana nia nzuri lakini...lkn tatizo chama chake CCM...poleni ndg zangu..Hamna jipya hapo...CCM ni ile ile ooh ni ile ileeee hata mkivimba ...mkilia ni ileee ileee...Mmeipenda wenyewe...ohhhh ni ileee ileeee......
 
Hata mwenyezi Mungu alifanya kazi kwa siku Saba na ndio ana nguvu zote sembuse binadamu. Hebu mwacheni afanye kazi yake. Sisi watu wa kawaida tunafurahia sana poleni zenu msubiri tu zamu yenu!!!! Na kama unaamini ni nguvu ya soda basi wewe endelea tu kuisoma namba!
 
Ni mapema sana kusema hili limemshinda katika busara za kawaida kabisa huwezi kufanya kila kitu kwa wakati mmoja. Ameanza na Bandari na TRA ambapo ni muhimili mkubwa wa Mapato ya nchi. Nchi ya Singaple imeendelea sana kwa sababu ya bandari tu. Mwacheni afanye kazi tuache mahaba ya LOWASA pembeni kwa sasa.
 
Mkuu majipu yapo kibao mengine yapo kule kule ofisini alipokuwa Magufuli yaani wizara ya Ujenzi ambapo zilipotea billion 250 kwa kulipwa makandarasi hewa huku kivuko kibovu chakavu cha mwaka 1978 kikinunuliwa kwa billion 8 wakati bei harisi ni million 400 tu, haya majipu Magufuli hayawezi hata Jipu la Mwakyembe kaliogopa mabehewa mabovu aliyonunua yatatumika hakuna wa kuthubutu kumuuliza tena hata zile pesa za Ukarabati wa Reli hakuna wa 10% uwanja wa ndege anazitafuna kwa raha zake, jipu la chenji ya Rada chenji bunge la katiba na chenji nyinginezo kibao zinazoliwa na wajanja pasipo jipu kutumbuliwa, Magufuli atathubutu kidogo kidogo sana lakini majipu makubwa hataweza kuyatumbua milele.

Naona wewe unayajua! itakuwa vema ukagombea ili uyatumbue
 
Majembe ya kuchimbia chini hela za uma.Sina imani tena na Magufuli?

ahh! nyinyi si mlikuwa mkiimba " tunaimaaaaani na lowassa oya! oyaa!"....

sishangai hunaimani na magufuli ....
 
No comment! Tulitarajia yanayojiri same or same or movie na iendelee
 
Back
Top Bottom