Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,493
- 30,187
Tulimsikia alipokuwa kwenye mkutano wa kampeni, huko Bariadi akimuahidi Mzee Andrew Chenge, ambaye alishinda kura za maoni jimboni kwake, kuwa atampa nafasi "nzuri" ya uteuzi, miongoni ya nafasi zake nyingi za uteuzi, kwa sharti tu la kumuunga mkono mgombea "wao" wa vikao vya juu vya Central Committee!
Aliamua kumuahidi nafasi hiyo ya uteuzi, kama afanyavyo Mwalimu anapoamua kumzawadia pipi, mtoto wa shule ya chekechea!
Alifanya vivyo hivyo alipofika Shinyanga Mjini, ambapo alimuahidi Stephen Masele, nafasi ya uteuzi, kwa kuwa amegundua kuwa Jimbo hilo, kuna hatari kubwa sana, ya kulipoteza na kwenda upinzani, baada ya vikao vya juu vya chama cha CCM "kupindua" maamuzi ya wajumbe, kwa kumteua Petrobas Katambi, ambaye aliachwa mbali sana, katika kura hizo za maoni.
Wananchi wamekuwa wakijiuliza, ikiwa Rais Magufuli anaamini kuwa ana nafasi nyingi za uteuzi, ni kwanini asitumie nafasi hizo, kumteua "kipenzi" chake Katambi?
Vivyo vivyo alipofika Biharamulo, akamuahidi Anna Tibaijuka, ambaye alitangaza mwenyewe kuwa kutokana na umri wake kuwa mkubwa, anastaafu siasa, na kuamua kuanza kula pensheni yake.
Lakini cha ajabu Rais Magufuli akaamua "kumlazimisha" huyo mama wa "vijisenti vya mboga" kuwa eti bado a anamuhitaji, kwa hiyo ataendelea kumtumia kwenye nafasi nyingine.
Kwanza nimweleze Rais Magufuli kuwa hivi sasa yeye ni mgombea, kama walivyo wagombea wengine, kwa hiyo siyo vyema kuamua kuahidi kutoa vyeo wakati akijua yupo kwenye kinyang'anyiro cha Uchaguzi, ambapo anaweza kushinda, lakini vile vile wananchi wanaweza wasimpe kura za kutosha na hivyo anaweza kung'olewa kwenye nafasi hiyo ya Urais, na asiwe Rais wa awamu ya sita na atakuwa Rais Mstaafu.
Hivi nimuulize Rais Magufuli, hivi akishindwa kwenye Uchaguzi huu wa mwaka huu, hivyo vyeo anavyowaahidi hao "wakereketwa" wa chama chake, atawazawadia akiwa Chato kwake, akiwa Rais Mstaafu?
Kwa vile huu ni Uchaguzi, kuna kushinda na kushindwa, iweje yeye akiwa mgombea kama walivyo wagombea wengine, akina Tundu Lissu, ajihakikishie uhakika wa asilimia 100, wa kushinda Uchaguzi huu?
Au yeye Rais Magufuli anaamini kuwa ni lazima atashinda, hata kama kura hazitatosha, kwa kuwa Tume ya Uchaguzi itakayotangaza matokeo hayo ni "yake" aliyoiteua?
Vile vile kuna hoja nyingine kubwa, kama yeye Rais Magufuli anafahamu kuwa idadi ya vijana wanaomaliza vyuo vikuu na kupata degree zao ni kwa maelfu, ambao hawana kazi, iweje sasa, awaahidi nafasi za kuteuliwa hao "wazee" waliostaafu na kuanza kula pensheni zao, wakati akiwaacha "solemba" vijana hao, ambao kutwa kucha wanazunguka na CV zao bila mafanikio yoyote?
Hivi unawezaje kumhakikishia nafasi ya uteuzi Mzee Andrew Chenge, ambaye amekuwa akifanya kazi, tokea enzi za utawala wa awamu ya kwanza ya Mwalimu Nyerere, wakati kuna vijana wengi kwa maelfu."wakisota" wakiwa hawana ajira zozote?
Hivi hii hali ya Rais Magufuli, kuahidi kutoa nafasi ya kuwateua hao makada wa CCM, kama siyo mazingira ya utoaji rushwa wakati wa uchaguzi, tuiite nini?
Aliamua kumuahidi nafasi hiyo ya uteuzi, kama afanyavyo Mwalimu anapoamua kumzawadia pipi, mtoto wa shule ya chekechea!
Alifanya vivyo hivyo alipofika Shinyanga Mjini, ambapo alimuahidi Stephen Masele, nafasi ya uteuzi, kwa kuwa amegundua kuwa Jimbo hilo, kuna hatari kubwa sana, ya kulipoteza na kwenda upinzani, baada ya vikao vya juu vya chama cha CCM "kupindua" maamuzi ya wajumbe, kwa kumteua Petrobas Katambi, ambaye aliachwa mbali sana, katika kura hizo za maoni.
Wananchi wamekuwa wakijiuliza, ikiwa Rais Magufuli anaamini kuwa ana nafasi nyingi za uteuzi, ni kwanini asitumie nafasi hizo, kumteua "kipenzi" chake Katambi?
Vivyo vivyo alipofika Biharamulo, akamuahidi Anna Tibaijuka, ambaye alitangaza mwenyewe kuwa kutokana na umri wake kuwa mkubwa, anastaafu siasa, na kuamua kuanza kula pensheni yake.
Lakini cha ajabu Rais Magufuli akaamua "kumlazimisha" huyo mama wa "vijisenti vya mboga" kuwa eti bado a anamuhitaji, kwa hiyo ataendelea kumtumia kwenye nafasi nyingine.
Kwanza nimweleze Rais Magufuli kuwa hivi sasa yeye ni mgombea, kama walivyo wagombea wengine, kwa hiyo siyo vyema kuamua kuahidi kutoa vyeo wakati akijua yupo kwenye kinyang'anyiro cha Uchaguzi, ambapo anaweza kushinda, lakini vile vile wananchi wanaweza wasimpe kura za kutosha na hivyo anaweza kung'olewa kwenye nafasi hiyo ya Urais, na asiwe Rais wa awamu ya sita na atakuwa Rais Mstaafu.
Hivi nimuulize Rais Magufuli, hivi akishindwa kwenye Uchaguzi huu wa mwaka huu, hivyo vyeo anavyowaahidi hao "wakereketwa" wa chama chake, atawazawadia akiwa Chato kwake, akiwa Rais Mstaafu?
Kwa vile huu ni Uchaguzi, kuna kushinda na kushindwa, iweje yeye akiwa mgombea kama walivyo wagombea wengine, akina Tundu Lissu, ajihakikishie uhakika wa asilimia 100, wa kushinda Uchaguzi huu?
Au yeye Rais Magufuli anaamini kuwa ni lazima atashinda, hata kama kura hazitatosha, kwa kuwa Tume ya Uchaguzi itakayotangaza matokeo hayo ni "yake" aliyoiteua?
Vile vile kuna hoja nyingine kubwa, kama yeye Rais Magufuli anafahamu kuwa idadi ya vijana wanaomaliza vyuo vikuu na kupata degree zao ni kwa maelfu, ambao hawana kazi, iweje sasa, awaahidi nafasi za kuteuliwa hao "wazee" waliostaafu na kuanza kula pensheni zao, wakati akiwaacha "solemba" vijana hao, ambao kutwa kucha wanazunguka na CV zao bila mafanikio yoyote?
Hivi unawezaje kumhakikishia nafasi ya uteuzi Mzee Andrew Chenge, ambaye amekuwa akifanya kazi, tokea enzi za utawala wa awamu ya kwanza ya Mwalimu Nyerere, wakati kuna vijana wengi kwa maelfu."wakisota" wakiwa hawana ajira zozote?
Hivi hii hali ya Rais Magufuli, kuahidi kutoa nafasi ya kuwateua hao makada wa CCM, kama siyo mazingira ya utoaji rushwa wakati wa uchaguzi, tuiite nini?