Hivi Mungu alikosa njia nyingine ya kufikisha ujumbe tofauti na Vitabu?

February Makamba

JF-Expert Member
Jan 31, 2020
2,115
2,822
Venezuela!

Mungu anatumia vitabu/maandishi kufikisha ujumbe wake, iwe kupitia biblia au Quran.

Tatizo la hii njia ni kuwa inategemea utafsiri/enterpretation ya binadamu.

Tatizo la binadamu ni kuwa tunatofautiana uelewa na uwezo wa kutafsiri.

Unaweza kuchukua wanazuoni wawili wote wenye elimu kubwa ya dini, ukawapa kifungu kimoja na kila mtu akatoka na maana tofauti kulingana na uelewa wake.

Hii imesababisha kuwepo madhehebu lukuki, utasikia mara kuna wasabato, waluteri, walokole, wasunni, washia, wayahudi, wapentekoste nk. Nk.

Wengine wameenda mbali mpaka wanaitana wenyewe kwa wenyewe wapagani, makafiri, waliopotea nk. Nk.

Hii imepelekea mpaka vita kwa baadhi ya sehemu kisa tu utofauti wa kutafsiri vifungu vya Mungu.

Wengine wanasema Nguruwe kula ni ruksa na wengine wanasema alaye nguruwe anatenda dhambi na haendi mbinguni.

Sasa Mungu atachukua watu gani? Wanaokula au ambao hawali?

Kama atachukua ambao hawali, je hawa wanaokula kwasababu ya kutafsiri vibaya maandiko yake kutokana na upeo wa kibinadamu wana kosa gani?

Mungu anayejua kila kitu, hakuona kuwa akitumia vitabu atawapotosha binadamu wengi kulingana na utofauti wa upeo wao wa kutafsiri mambo?

Kwanini asingetumia njia bora zaidi kufikisha ujumbe wake? Au hajui hiyo njia? Au hana huo uwezo?

Au hakujua kuwa binadamu watatofautiana kutafsiri?

Na sasa kuna dini na amadhehebu zaidi ya 50, 000 duniani na kila moja linajiona lenyewe ndio lipi sahihi.
Sasa sijui Mungu atachukua lipi, au atachukua yote?

Atachukua wanaoamini Kutunza sabato ya jumamosi tu na wengine wote kuchomwa moto? Au atachukua wanaoamini kunena kwa Lugha na wengine wote kuchomwa moto?
 
Mkuu ingekuwa hivyo kungekuwa na madhehebu laki na ushee yanayokinzana?
Madhehebu hayo ni biashara za wajanja!

Nikupe rejea! Ukimkuta mtu shambani mwako Kang'oa muhogo anatafuna Utajua njaa Jee Ukimkuta kang'oa mihogo kajaza kwenye kiroba huyo ni ni njaa au mwizi?

Utahitaji mtu wa dhehebu akufundishe nani ni mwizi kati ya watu hao wawili??
 
Yote ni kwa mapenzi yake kwa kuwa yeye ndie muweza wa yote

Hata kama angeamua injili ije kwa lugha ya alama na wasio elewa wachomwe ni sawa tu

Wewe fikra zako ndo zimependekeza hivyo kutokana na uionavyo dunia na watu wake. Lakini swali je wajua yeye anaionaje hii dunia na hao watu wake na kusudio hasa la kuiacha dunia iwe kama ilivyo nini,

Hivyo usijisumbue kumshauri kwa kuwa huwezi kumuelewa kwa sababu yeye mwenyewe hajajiweka wazi. Na hayo yote ni kwa mapenzi yake.
 
Mans knowledge is limited. What we don't is beyond our knowledge.

Kuna baadhi ya mambo huwa tunapoteza muda na nguvu kuyahoji.

Tambua hakuna mwanadamu anaefahamu uwezo au utashi wa Mungu Kwamba kwanini alifanya kile na kwanini hakufanya hiki.

Vitabu vya dini hasa Biblia vimejaribu kumuelezea Mungu lakini ile ni "summary" tu ya machache kuhusu.Vitabu vya dini sio mwisho wa kila kitu kumuhusu Mungu.

Mungu ni zaidi ya tunavyodhani na tulivyofundishwa. Km kikiandikwa kitabu kumuelezea Mungu basi h kitabu hicho kitakuwa hakina mwisho na hakuna mwanadamu atakaeweza kukimaliza kukisoma.
 
Mungu anayejua kila kitu, hakuona kuwa akitumia vitabu atawapotosha binadamu wengi kulingana na utofauti wa upeo wao wa kutafsiri mambo?
Kwanini asingetumia njia bora zaidi kufikisha ujumbe wake? Au hajui hiyo njia? Au hana huo uwezo?
Au hakujua kuwa binadamu watatofautiana kutafsiri?
Njia bora kama ipi??
Watu wengine mna mambo ya ajabu sana

Kuna njia gani nyingine ya maana kufikisha elimu isipokuwa maandishi??
 
Angekuja yeye mwenyewe ? ,Watu wangemtukana, unless angekuja kwa muonekano wa malaika asiguse ardhi

Angekuja kwa umbo la binadamu waroma wangemuweka jera
Nshu ni kwmb kuna umuhimu gan wa kumuacha shetani atake over dunian unless km mbinguni ni padogo ko mungu anataka raia wachache tu km sio ivo mungu atakua hana upendo wa kweli kwetu atakua anatuombea njaa ama uskute huwa anamuongezea nguvu shetani ili aendelee kutukusanya km njugu
 
Nshu ni kwmb kuna umuhimu gan wa kumuacha shetani atake over dunian unless km mbinguni ni padogo ko mungu anataka raia wachache tu km sio ivo mungu atakua hana upendo wa kweli kwetu atakua anatuombea njaa ama uskute huwa anamuongezea nguvu shetani ili aendelee kutukusanya km njugu
Kwa mujibu wa maandiko Binadamu anateseka sababu alifanya makosa ya kula hilo Tunda so Mungu inaoneka a alitaka sote twende Mbinguni

Lakini hata hivo Mungu haeleweki kwa kutumia akili bali imani,hata mimi huwa najiuliza mengi tu
 
Yote ni kwa mapenzi yake kwa kuwa yeye ndie muweza wa yote

Hata kama angeamua injili ije kwa lugha ya alama na wasio elewa wachomwe ni sawa tu

Wewe fikra zako ndo zimependekeza hivyo kutokana na uionavyo dunia na watu wake. Lakini swali je wajua yeye anaionaje hii dunia na hao watu wake na kusudio hasa la kuiacha dunia iwe kama ilivyo nini,

Hivyo usijisumbue kumshauri kwa kuwa huwezi kumuelewa kwa sababu yeye mwenyewe hajajiweka wazi. Na hayo yote ni kwa mapenzi yake.
Kutokana na watu kutofautiana kutafsiri maandiko imepelekea mpaka vita za kidini na mamilioni ya watu wamefariki, huku kulikuwa na vita kati ya waroma na protestants, waroma na wayahudi, kule kuna vita kati ya Shia na Sunnis, sunnis na Ahmadiya nk. Nk.

Sasa Mungu kupitia maandiko yake amesababisha vita na watu wengi kufa, kubaguliwa, kutengwa kisa utofautiano wa kuelewa maandiko.
Je ulikuwa ni mpango wa Mungu hayo yote yatokee? Yani ametuchanganya makusudi? Mungu wa uchafuzi? Yani ametutenganisha binadamu makusudi? Tulitegemea Mungu angependa kutuunganisha katika upendo.


Kama unasema ndiyo eti hayo ni mapenzi yake

Basi inabidi sisi tujirekebishe kidogo. Au turekebishe maandiko yake kidogo. Maana tunaamini kuwa
1.Mungu anaweza yote
2.Mungu ni pendo/God is full of mercy
3.Mungu anajua kila kitu

Kwasababu kama ana upendo au amejaa rehema asingeruhusu hayo yote yatokee..
Lakini labda anao upendo ila hakujua kama akitumia maandiko yake atapandikiza chuki kwa binadamu, na kama ni hivi basi kumbe hajui kila kitu.
Au alijua ila alikosa njia bora zaidi ya kufikisha ujumbe? Basi kumbe hawezi kila kitu.

Mwisho wa siku hakuna option nyingine, lazima kuna mahala atafeli.
Either hawezi kila kitu, au hajui kila kitu, au sio pendo/hana huruma wala rehema. Au hayupo kabisa
 
Mans knowledge is limited.What we don't is beyond our knowledge.

Kuna baadhi ya mambo huwa tunapoteza muda na nguvu kuyahoji. Tambua hakuna mwanadamu anaefahamu uwezo au utashi wa Mungu Kwamba kwanini alifanya kile na kwanini hakufanya hiki. Vitabu vya dini hasa Biblia vimejaribu kumuelezea Mungu lakini ile ni "summary" tu ya machache kuhusu.Vitabu vya dini sio mwisho wa kila kitu kumuhusu Mungu. Mungu ni zaidi ya tunavyodhani na tulivyofundishwa. Km kikiandikwa kitabu kumuelezea Mungu basi h kitabu hicho kitakuwa hakina mwisho na hakuna mwanadamu atakaeweza kukimaliza kukisoma.
Sawa, em fikiria kwa engo hii, kama mungu anaweza kila kitu kwanini anashindwa kumfanya binadamu amuelewe?

Kwasababu kushindwa kumuelewa ndio kunamfanya binadamu aende kinyume naye.
Mpaka sasa sijui kama nguruwe kula ni dhambi au la, Huku wasabato wanasema ni dhambi, kule walokole wanasema iliruhusiwa, kule waislam wanasema ni haram.

Mfano Kama nguruwe ni haram kweli, Siku akija Mungu atawalaumu walokole na waRC na waluteri kwa kutoelewa maandiko yake? Atawaadhibu kwa kosa lake mwenyewe la kushindwa kutumia mbinu bora zaidi kufikisha ujumbe?

Kama hatawalaumu atawasamehe, then kuna umuhimu gani wa kuleta haya maandiko?

Kila engo ukiliangalia hili hatoki.
 
Tangu kuzaliwa binadamu anajua jambo baya na Zuri haitaji kitabu kumweleza , chukulia mtoto mchanga mkunjie sura ya kumtisha atalia kwamba ni ubaya , ila mwonyeshe tabasamu atafurahi kwamba ni jema . Hivyo vitabu ni ujanja wa wachache tu kutawala imani za watu japo kuna mazuri mengi kwenye vitabu tunakumbushwa tu.
 
Back
Top Bottom