Hivi mradi wa DARTS aliubuni nani? Was it the best/cheaper option

siku zote huwa nasikitishwa sanaa na watanzania kwa kuwa na majibu mepesi kwa critical issues. Nyumba ya Maskini huwa haiishi kujengwa. hata Mradi haujaisha tayari tumelalamika haijatolewa tathmini ya kitaalamu tayari tumejitwika utaalamu na ujuaji kibaooo jamani hebu muwaache wataalamu wamalize kazi yao ndio tuje tuanze kuwaambia kasoro kutokana na output yao. inasikitisha project iko at 55% watu tushalalamika sana na kinachosikitisha hizi barabara hata miaka 3 hazijamaliza ila ukizitazama ni kama za miaka 5 uchafu matofali kubomoka yaani ili mradi tu yote hii ni sababu ya kukosa ustaarabu tu. hata tujenge flyovers tuweke reli nzuri na kila kizuri kama hatutokuwa wastaarabu sisi wenyewe matatizo yetu hayatoisha. sote mashahidi uvunjanji wa taratibu za undeshaji vyombo vya moto unavyochangia foleni tena kiasi kikubwa ila tunaona udogo wa barabara kama a big issue. tumejengewa uwanja mzuriiii lakini watu wanavunja viti wanaharibu miundombinu mwisho wa siku watakuja wanalalamika hapa uwanja hauna ubora. hebu hata hivi vidogo tulivyonavyo tuvitumie kwa utaratibu na ustaarabu. tusipo badirika wenyewe hata ijengwe flyovers sijui treni ya Umeme hamna kituu. na tujifunze kuwa wavumilivu subili kitu kikamilike then uliza wataalamu ni kwanini output imekuwa tofauti na ulivyotegemea
Katika project management mradi una fail hata kabla haujaanza. Muda ule unapoisha inakuwa ni kujidhihirisha tu. Ile barabara iliyokuwepo haijamaliza miaka 20 inakwanguliwa na kuwekwa nyingine yenye mapungufu mengi tu ni failure mbaya na hasara kwa taifa. Walipashwa kujenga fly overs , kuchimba chini na kuweka madaraja kwenye junctions. Mfano ubungo, mwenge, tazara, fire, magomeni-flyovers. Tabata, buguruni, akiba, Kamata na kwingineko kwenye ukorofi upande mmoja ukachimbwa magari yapite chini na upande mwingine liwepo daraja magari yapite juu. Hili nalo limetushinda baada ya kujitawala kwa zaidi ya miaka 50!🙈
 
Mradi huu haujakava njia zote za jiji. watakaofaidika ni wale tu wanaotumia njia hizo kama Kimara - Kivukoni, Morocco - Magomeni. Na ni waletu watakaotumia huo usafiri,

Wengine wote watendelea na msoto wa foleni.
 
Nimekuwa nikitafakari namna ambavyo nchi yangu inaendeshwa naomba kuwashirikisha GT wenzangu juu ya potential white elephant iliyotengenezwa kwenye DARTS.
- Je ni kweli DARTS ilikuwa ndiyo best option (in terms of cost, efficiency and priority)ya kupunguza msongamano Dar?
- Je hizi nyumba za kusubiria wasafiri zilikuwa zina ulazima wa kujengwa kwa gharama kama ilivyofanyika sasa
- Je namna ambayo barabara zimejengwa itapunguza foleni kweli?

Kwa maoni yangu (I stand to be corrected), DARTS haitapunguza msongamano na huenda ikaongeza, na kama kweli mradi huu ulijadiliwa kwa mapana yanayostahili then kuna umuhimu wa watu waliodhani huu ndio mwarobaini wa msongamano wa magari Dar(ni muhimu kuwafahamu ili tuweze kujiridhisha na weledi wao, au hata IQ zao)

Kama ningekuwa mimi ningeanza na kujenga fly overs kwanza, then barabara za pembezoni kwanza na kama pesa bado ipo ningeimalisha usafiri wa reli ndani ya jiji la Dar pamoja na kuimalisha uchukuzi wa mizigo kutokea bandari ya Dar kwa kuweka dry port kubwa Ruvu au Mlandizi.
Ukiziwekea lami barabara za Kinyerezi-Mbezi Lousi, Makongo Juu-Goba, Tangi Bovu-Morogoro Rd, Mbagala-Kipawa/Banana/Ukonga utapunguza msongamano kwenye barabara ndani ya jiji la Dar kwa kiwango kikubwa na kwa gharama ndogo kuliko huu wendawazimu wa DARTS.

From own experience from somewhere in this world. Flyovers can be a major traffic jammer due to bottle necks if cross roads are insufficient to handle heavy traffic.
 
Mradi wa DART ni kwa ajiri ya kuboresha usafili (publictransport). Daladala zitaondelewa katika barabara zile kubwa km kutoka kimaraau Morocco kwenda kivukoni, au kariakoo nk . kutakuwa na mabasi makubwa ambayoyataendeswa kwa ratiba maalumu. Kuhusu foleni ni kwamba kama daladalazitaondolewa ndiyo usumbufu wake utapungua. Mfano ni pale manzese huwa kunakuwana foleni kwa sababu daladala zinaziba njia.
Watakaonufaika hasa ni watumiaji mabasi hayo, kama utaonakwa gari binafsi kuna foleni then kunakuwa na option ya kufika mjini kwa wakatikwa kutumia basi. Hii haipo kwa sasa

hyo DART ndo imekuwa kadhia kwa wengine wanaotumia hyo barabara, bora tungebaki na daladala zetu ila sio hii mirija tunayoitumia kupishana na malori
 
Watu ni mazezeta kweli wakufikiri....inamaana magari ya mwendo kasi yanahitajika moro road tu. Mbagala hakuna foleni? Gongo la mboto je? Tegeta posta?

Toeni hoja zenu kwa kuwaza hali halisi...acheni kuwaza kiitikadi.

Ntemi ameelezea vizuri sana hapo mwanzo. Kuwa feeder roads zilitakiwa ziwe tayari kabla ya huo uchafu hapo moro.

Kwa akili ndogo tu..mtu unapaswa kujiuliza magari ya mwendo kasi yatapunguzaje foleni? Kwanza ni kwamba hayatasimama hovyo kama ilivyo kwa dalax2 za sasa ila hebu jiulize....hizo bus zikifika ubungo na shekilango etc hayatasubiria taa?? au yatakuwa na kipaombele? Nakama yatakua na kipaombele...je ni fair kwa magari ya pande nyingine za taa?

Huo mradi hauwezi kuwa na maana kama taa zitaendelea kutumika period.

Huu mradi ni chaka...ambaye haoni hilo basi atakua analaje jambo...au itikadi
 
ile barabara mbona ilishawaaibisha kusubiri iishe ndo useme wafanye hiki au kile hio sio akili kwa mfano mwanzoni walitenganisha njia ya kwenda na kurudi kwa uzio kwa maana ya kupita basi moja kwa wakati jamaa wa kawaida tu wakauliza sa ikitokea basi moja limekwama mengine ya nyuma yatapita wapi? manake magari yanaweza kukwama hata yale ya ikulu yaliwahi kuzima magufuli akabaki ametoa macho 🙉🙉🙉😨😨😨😨😨 sasaiv ule mkanda wameukata angalia kutoka kimara mwisho nadhan mpaka temboni na kigamboni kuna alama nyeusi. swala kutokua wastaarabu inaletwa na loyality watu wakipiga kura mnawaibia wakikataa mnawapiga wakitumia wawakilishi bungeni mnawazomea na kuwafokea kama nyie ndo miungu unategemea nn?
 
DART sio kwa ajili ya kupunguza msongamono, soma kwanza kirefu chake ndio utajua ipo kwa ajili gani.
 
Mleta mada asante sana. Ni kweli huu mradi umeanguka kabla haujaisha. Mosi ni wembamba wa barabara na ujenzi unaobana magari kama ngombe wanapita kwenye josho, yaani ukibugi mambo Kimara kutoka nje au kugeuza ni mpaka Ubungo mataa. Jee gari zilizoopata ajali au zilizoharibika zitatolewaje?? Pili kuna maeneo ambayo mradi huu umeyatayarisha kuwa ya mauaji, mfano ule mwingiliano wa barabara pale Magomeni kwa Sheikh Yahya, mambo ni zig zag. Tatu ili kona yenye herufi S pale kimara mwisho kuelekea Mbezi, malori mengi yatajibwaga kule bondeni. Ziada ya hayo, eneo lote kuanzia junction ya NSSF pale Technical College hadi Posta ya Zamani hadi Ferry ni mchanganyiko maalumu. In conclusion, mradi huu ulianzia kwenye jibu (percent ya rushwa) kurudi kinyume nyume kwenda kwenye swali (Gharama ziweje). Tanzania ni zaidi ya uijuavyo!!
 
Mradi huu haujakava njia zote za jiji. watakaofaidika ni wale tu wanaotumia njia hizo kama Kimara - Kivukoni, Morocco - Magomeni. Na ni waletu watakaotumia huo usafiri,

Wengine wote watendelea na msoto wa foleni.

hii ni phase one. phase two kilwa road na nyerere road,,,phase three ali hassan mwinyi.

 
Watu ni mazezeta kweli wakufikiri....inamaana magari ya mwendo kasi yanahitajika moro road tu. Mbagala hakuna foleni? Gongo la mboto je? Tegeta posta?

Toeni hoja zenu kwa kuwaza hali halisi...acheni kuwaza kiitikadi.

Ntemi ameelezea vizuri sana hapo mwanzo. Kuwa feeder roads zilitakiwa ziwe tayari kabla ya huo uchafu hapo moro.

Kwa akili ndogo tu..mtu unapaswa kujiuliza magari ya mwendo kasi yatapunguzaje foleni? Kwanza ni kwamba hayatasimama hovyo kama ilivyo kwa dalax2 za sasa ila hebu jiulize....hizo bus zikifika ubungo na shekilango etc hayatasubiria taa?? au yatakuwa na kipaombele? Nakama yatakua na kipaombele...je ni fair kwa magari ya pande nyingine za taa?

Huo mradi hauwezi kuwa na maana kama taa zitaendelea kutumika period.

Huu mradi ni chaka...ambaye haoni hilo basi atakua analaje jambo...au itikadi

1. hii ni phase one...phase two ni kilwa road/nyerere road then wanamalizia phase three ali hassan mwinyi road
2.magari ya mwendokasi yatapunguza foleni kwasababu yatakuwa na hadhi na usafi utakaofanya watu wengi waache magari nyumbani na kutumia usafiri huu,watu hawapendi kuendesha kila siku kwasababu ya gharama lakini hawana option kwa sababu ya karaha za daladala
3.yatasubiri taa,kwani taa inakaa muda gani hadi icheleweshe??taa haisimamishi zaidi ya dk tatu pia kuna sensor zinaweza kuwekwa na yakapewa kipaumbele.

4.nimetembea nchi nyingi zina mabarabara makubwa na flyover nyingi mno lakini foleni ipo. foleni haimalizwi kwa kupanua barabara na kujenga flyover kwasababu kila siku watu wananunua magari,kupanua barabara na flyover kuna mwisho. foleni inapunguzwa kwa kuimarisha public transport na kuwafanya watu wasipende kutumia magari binafsi na ndio DART itakachofanya,it wont happen overnight it will take time lakini matunda yake mtayaona.
 
mcfm40, unaponda DART kwamba how come milori, mibasi, private cars humo humo! mbona unajikanganya? Lengo la DART ni kwamba usafiri wa jumla utumie barabara zinayojitegemea! ukitumia private car ndo kagombane na malori kwenye common roads! Frm Mbezi kuja Ubungo nd V/S, abiria watatumia DART buses mediam size ambazo ni kubwa zaidi kuliko Coaster! kimsingi, unafuu utakuwa kwa wale wanaotumia public transport ambao ndio wengi na wanaotumia private watakachoepukana nacho ni fujo za daladala, basi!

Nasdaz, Unafikiri foleni dar inasababishwa na daladala au magari binafsi? Hizo barabara unavyoona wewe malori mawili yanweza "yakaovertakiana". huoni kwamba ni nyembamba sana? Unafikiri kwa nini watu wanatumia magari binafsi? Unafikri nitaacha gari langu binafsi Mbezi niapnde ya DART nifike ubungo nikagombanie daladala za mwenge au tegeta? Au Gongo la mboto na Mbagala? Tunachosema sema hapa what was supposed to come last came first, and vice versa! Bara za pembezoni zilitakiwa zijengwe kwanza. Mfano Mbezi -Kinyerezi; Mbezi Tegeta automatically foleni ingepungua. Lakini hata hiyo mibasi ikianza kufanya kazi hakutakuwa na unafuu wa foleni kwa sababu watu wanaoenda maeneo ya tegeta na wanaoenda maeneo ya Mbagala, Airport, gombo la mboto n.k kutokea maeneo ya mbezi lazima waende kwanza ubungo. Kumbukua morogro road ndiyo lango kuu la kuingilia dar lakini eti double road imeishia kimara! What a joke?
 
Kwahiyo wasitishe mradi? Binadamu kweli huwezi kumridhisha! hata ufanyeje,utalaumiwa tu..
 
Watu ni mazezeta kweli wakufikiri....inamaana magari ya mwendo kasi yanahitajika moro road tu. Mbagala hakuna foleni? Gongo la mboto je? Tegeta posta?

Toeni hoja zenu kwa kuwaza hali halisi...acheni kuwaza kiitikadi.

Ntemi ameelezea vizuri sana hapo mwanzo. Kuwa feeder roads zilitakiwa ziwe tayari kabla ya huo uchafu hapo moro.

Kwa akili ndogo tu..mtu unapaswa kujiuliza magari ya mwendo kasi yatapunguzaje foleni? Kwanza ni kwamba hayatasimama hovyo kama ilivyo kwa dalax2 za sasa ila hebu jiulize....hizo bus zikifika ubungo na shekilango etc hayatasubiria taa?? au yatakuwa na kipaombele? Nakama yatakua na kipaombele...je ni fair kwa magari ya pande nyingine za taa?

Huo mradi hauwezi kuwa na maana kama taa zitaendelea kutumika period.

Huu mradi ni chaka...ambaye haoni hilo basi atakua analaje jambo...au itikadi

Usiwe mjuzi wa kila kitu hasa yale mambo ambayo huyaelewi....tuliza ball uone ni Morogoro road tu au??? kwa taarifa yako hiyo unayoiona ni Phase ya mwanzo tu barabara zote kubwa ulizozitaja kwa kadri uwezo utakavyoruhusu zitafuata taratibu....La msingi ningependa ujue ni kuwa hizi options zote watu wanazisema sio kwamba hazifahamiki ... zinafahamika zote na kila moja inafaa katika kupunguza foleni na adha ya usafiri jijini ila kinachoangaliwa ni kipi kianze na kipi kifuate... serikali imeanza na utaratibu wa Dart ili kusaidia wakazi wa jiji wa kipato cha chini na kati ambao wengi wanatumia usafiri wa Daladala wawe na uhakika na uharaka wa kufika mjini kwenye shughuli zao,,,ww mwenye gari lako la kubeba abiria watano mipango yako itafuata baadae ..... Tuwe na uzalendo wa kukubali kidogo nchi inatupatia
 
Nasdaz, Unafikiri foleni dar inasababishwa na daladala au magari binafsi? Hizo barabara unavyoona wewe malori mawili yanweza "yakaovertakiana". huoni kwamba ni nyembamba sana? Unafikiri kwa nini watu wanatumia magari binafsi? Unafikri nitaacha gari langu binafsi Mbezi niapnde ya DART nifike ubungo nikagombanie daladala za mwenge au tegeta? Au Gongo la mboto na Mbagala? Tunachosema sema hapa what was supposed to come last came first, and vice versa! Bara za pembezoni zilitakiwa zijengwe kwanza. Mfano Mbezi -Kinyerezi; Mbezi Tegeta automatically foleni ingepungua. Lakini hata hiyo mibasi ikianza kufanya kazi hakutakuwa na unafuu wa foleni kwa sababu watu wanaoenda maeneo ya tegeta na wanaoenda maeneo ya Mbagala, Airport, gombo la mboto n.k kutokea maeneo ya mbezi lazima waende kwanza ubungo. Kumbukua morogro road ndiyo lango kuu la kuingilia dar lakini eti double road imeishia kimara! What a joke?
Kwanza ni barabara zipi unazosema ni nyembamba kiasi kwamba malori hayawezi kupishana? Kama unazungumzia za DART, ni kwamba kwenye zile barabara hakuna gari zingine ambazo zitaruhusiwa kupita zaidi ya mabasi ya DARTs yenyewe! Na hata hayo ya DART, huwa hayapishani na ndio maana barabara zimefanywa kuwa nyembamba!!!

Kuhusu foleni zinasababishwa na nini ni mchanganyiko wa mambo angalau manne...barabara zenye few lanes, private cars nyingi ambazo haziendani na barabara zilizopo, daladala pamoja na kutozingatia sheria barabarani! Ni rahisi sana kusema tatizo kubwa ni barabara nyembamba... lakini lazima tukubali by the time zinajengwa hizi barabara ingekuwa ni ndoto kuwa (say) eight lanes, for from each side! So, ikiwa barabara zilizopo ndo hizo; what's the solution? Wengi tunakimbilia kutaja feeder roads. Hata mimi nakubali feeder roads zingekuw ni mkombozi mkubwa lakini town planning iliyopo haiweze ku-facilitate hilo zoezi na kuwa kama ilivyotarajiwa! Ni rahisi kuboresha feeders kwenye mji uliopangwa vizuri coz' tayari barabara zinakuwa zipo ila tu hazina ubora, so unapotaka kutengeneza feeders ni kwamba tu unaboresha barabara zilizopo! Lakini kwa Dar jinsi ilivyo, tunavyozungumza feeders ni kwamba, sehemu nyingi unatakiwa kujenga barabara from the scratch! Assume kutoka Ubungo kwenda Kimara... hizo feeders utazipitisha wapi kama si kwamba utalazimika kubomoa mamia ya nyumba ili kujenga barabara? Chukulia Kilwa Rd... from town to Mbagala and v/s, hizo feeders utazipitishia wapi kama si kwamba utalazimika kubomoa mamia ya nyumba na kujenga barabara from the scratches? Kwahiyo maeneo hayo, ikiwa hutaki BRT, ni ama ujenge flyovers along the existing roads or ufanye mass abolition of houses/buildings! Town planning ni tatizo kwa kuwa na feeders zitakazokuwa efficient.

Sasa basi, ili ku-serve both parties, mathalani kwa kupitia Morogoro Road, basi ilibidi nyumba zote, upande mmoja wa barabara zivunjwe kutoka Mbezi hadi Town, au angalau hadi Mapipa! Hilo lingefanyika, lingetoa nafasi kubwa ya kuongeza idadi ya lanes. If you were a decision maker, could you do it?

So WHY DART? Kilichoangaliwa pale ni interest ya majority! Wanaotumia private cars bado wataendelea kuchelewa makazini coz' magari kila siku yanaongezeka barabarani! Lakini wale wanaotumia public transport ambako DART inapita, wao wana uwezekano mkubwa sana tena sana wa kuwahi kuliko ilivyo sasa... WHY? There's limited possibility ya congestion along the DART lanes. Na kv wanaotumia private cars ni wachache sana as compared na wanaotumia public transport, then malengo yatakuwa yamefikiwa kwa kiwango kikubwa!

Kwamba wanaotoka Mbezi kwenda (say) Mbagala au Tegeta ni lazima kwanza wafike Ubongo then the all thing sounding like bullshit lazima ukumbuke kwamba BRT si kwa ajili ya kupunguza foleni barabarani... BRT ni maalumu kwa magari yanayotumia mfumo husika kufika mapema zaidi kule waendako kv barabara zao hazitumiki na other vehicles! So, huyo wa Mbezi kuja Ubungo, atafika mapema Ubungo than otherwise kwahiyo tatizo kwake litakuwa kuanzia Ubungo ikiwa anakoelekea bado DART haijafika... simple like that! Huyu anayetoka mjini kwenda Changanyikeni lakini anataka apitie kwanza Ubungo, ni kwamba atafika haraka zaidi Ubungo kwahiyo tatizo kwake litakuwa ni kuanzia Ubungo kwenda Changanyikeni assuming nako kuna magari mengi na no DART services!

REMEMBER barabara za DART zinapita katikati wakati hizi zingine zinapita pembeni ya DART. Hiyo imefanywa hivyo makusudi ili kuzuia uwezekano wa kuwa blocked kila mara na magari ya kawaida yanayoingia na kutoka barabarani!
 
1. hii ni phase one...phase two ni kilwa road/nyerere road then wanamalizia phase three ali hassan mwinyi road
2.magari ya mwendokasi yatapunguza foleni kwasababu yatakuwa na hadhi na usafi utakaofanya watu wengi waache magari nyumbani na kutumia usafiri huu,watu hawapendi kuendesha kila siku kwasababu ya gharama lakini hawana option kwa sababu ya karaha za daladala
3.yatasubiri taa,kwani taa inakaa muda gani hadi icheleweshe??taa haisimamishi zaidi ya dk tatu pia kuna sensor zinaweza kuwekwa na yakapewa kipaumbele.

4.nimetembea nchi nyingi zina mabarabara makubwa na flyover nyingi mno lakini foleni ipo. foleni haimalizwi kwa kupanua barabara na kujenga flyover kwasababu kila siku watu wananunua magari,kupanua barabara na flyover kuna mwisho. foleni inapunguzwa kwa kuimarisha public transport na kuwafanya watu wasipende kutumia magari binafsi na ndio DART itakachofanya,it wont happen overnight it will take time lakini matunda yake mtayaona
Hapo kwenye RED you're very right... magari kila siku yananunuliwa lakini uzuri wa BRT ni kwamba barabara zake zinatumia na magari yaendayo haraka peke yake unlike ordinary roads ambazo magari mengine yote yanapita huko! In short DART ni sawa ni sawa na usafiri wa kutumia treni mjini.
 
Usiwe mjuzi wa kila kitu hasa yale mambo ambayo huyaelewi....tuliza ball uone ni Morogoro road tu au??? kwa taarifa yako hiyo unayoiona ni Phase ya mwanzo tu barabara zote kubwa ulizozitaja kwa kadri uwezo utakavyoruhusu zitafuata taratibu....La msingi ningependa ujue ni kuwa hizi options zote watu wanazisema sio kwamba hazifahamiki ... zinafahamika zote na kila moja inafaa katika kupunguza foleni na adha ya usafiri jijini ila kinachoangaliwa ni kipi kianze na kipi kifuate... serikali imeanza na utaratibu wa Dart ili kusaidia wakazi wa jiji wa kipato cha chini na kati ambao wengi wanatumia usafiri wa Daladala wawe na uhakika na uharaka wa kufika mjini kwenye shughuli zao,,,ww mwenye gari lako la kubeba abiria watano mipango yako itafuata baadae ..... Tuwe na uzalendo wa kukubali kidogo nchi inatupatia

Uwezo gani kwani huu mradi tumeufanya kwa hela zetu?
 
Kwanza ni barabara zipi unazosema ni nyembamba kiasi kwamba malori hayawezi kupishana? Kama unazungumzia za DART, ni kwamba kwenye zile barabara hakuna gari zingine ambazo zitaruhusiwa kupita zaidi ya mabasi ya DARTs yenyewe! Na hata hayo ya DART, huwa hayapishani na ndio maana barabara zimefanywa kuwa nyembamba!!!

Kuhusu foleni zinasababishwa na nini ni mchanganyiko wa mambo angalau manne...barabara zenye few lanes, private cars nyingi ambazo haziendani na barabara zilizopo, daladala pamoja na kutozingatia sheria barabarani! Ni rahisi sana kusema tatizo kubwa ni barabara nyembamba... lakini lazima tukubali by the time zinajengwa hizi barabara ingekuwa ni ndoto kuwa (say) eight lanes, for from each side! So, ikiwa barabara zilizopo ndo hizo; what's the solution? Wengi tunakimbilia kutaja feeder roads. Hata mimi nakubali feeder roads zingekuw ni mkombozi mkubwa lakini town planning iliyopo haiweze ku-facilitate hilo zoezi na kuwa kama ilivyotarajiwa! Ni rahisi kuboresha feeders kwenye mji uliopangwa vizuri coz' tayari barabara zinakuwa zipo ila tu hazina ubora, so unapotaka kutengeneza feeders ni kwamba tu unaboresha barabara zilizopo! Lakini kwa Dar jinsi ilivyo, tunavyozungumza feeders ni kwamba, sehemu nyingi unatakiwa kujenga barabara from the scratch! Assume kutoka Ubungo kwenda Kimara... hizo feeders utazipitisha wapi kama si kwamba utalazimika kubomoa mamia ya nyumba ili kujenga barabara? Chukulia Kilwa Rd... from town to Mbagala and v/s, hizo feeders utazipitishia wapi kama si kwamba utalazimika kubomoa mamia ya nyumba na kujenga barabara from the scratches? Kwahiyo maeneo hayo, ikiwa hutaki BRT, ni ama ujenge flyovers along the existing roads or ufanye mass abolition of houses/buildings! Town planning ni tatizo kwa kuwa na feeders zitakazokuwa efficient.

Sasa basi, ili ku-serve both parties, mathalani kwa kupitia Morogoro Road, basi ilibidi nyumba zote, upande mmoja wa barabara zivunjwe kutoka Mbezi hadi Town, au angalau hadi Mapipa! Hilo lingefanyika, lingetoa nafasi kubwa ya kuongeza idadi ya lanes. If you were a decision maker, could you do it?

So WHY DART? Kilichoangaliwa pale ni interest ya majority! Wanaotumia private cars bado wataendelea kuchelewa makazini coz' magari kila siku yanaongezeka barabarani! Lakini wale wanaotumia public transport ambako DART inapita, wao wana uwezekano mkubwa sana tena sana wa kuwahi kuliko ilivyo sasa... WHY? There's limited possibility ya congestion along the DART lanes. Na kv wanaotumia private cars ni wachache sana as compared na wanaotumia public transport, then malengo yatakuwa yamefikiwa kwa kiwango kikubwa!

Kwamba wanaotoka Mbezi kwenda (say) Mbagala au Tegeta ni lazima kwanza wafike Ubongo then the all thing sounding like bullshit lazima ukumbuke kwamba BRT si kwa ajili ya kupunguza foleni barabarani... BRT ni maalumu kwa magari yanayotumia mfumo husika kufika mapema zaidi kule waendako kv barabara zao hazitumiki na other vehicles! So, huyo wa Mbezi kuja Ubungo, atafika mapema Ubungo than otherwise kwahiyo tatizo kwake litakuwa kuanzia Ubungo ikiwa anakoelekea bado DART haijafika... simple like that! Huyu anayetoka mjini kwenda Changanyikeni lakini anataka apitie kwanza Ubungo, ni kwamba atafika haraka zaidi Ubungo kwahiyo tatizo kwake litakuwa ni kuanzia Ubungo kwenda Changanyikeni assuming nako kuna magari mengi na no DART services!

REMEMBER barabara za DART zinapita katikati wakati hizi zingine zinapita pembeni ya DART. Hiyo imefanywa hivyo makusudi ili kuzuia uwezekano wa kuwa blocked kila mara na magari ya kawaida yanayoingia na kutoka barabarani!

Nasdaz, nini kinakufanya useme watu watafika mapema kazini au kwenye destinations zao? Unataka kuniambia mabasi ya DART yakifika kwenye makutano yataruhusiwa yapite kwanza magari mengine yasubirie? Umeshaelezwa mara nyingi kwamba tatizo la foleni Dar sio uwingi wa magari bali ufinyu wa barabara. Watu wanalazimika kutmia barabara moja pekee moro road kuingia mjini. Bara bara ya Mbezi- Tegeta mbona ipo tayari ni kuwekwa lami tu na hahitaji kubomoa nyumaba za watu? Ya mbezi kinyerzi mpka aiport mbona nayo ni lami tu! Ni ni hasa kimeifanya serikali mpka leo haijaona umuhimu wa kuborehs ahizo barabara? Kuhusu mjini kati km magomeni, karume, kifupi barabara zote ndani ya jiji zinatakiwa kuwa na fly ofer kwenye junctions. hakuna option nyingine.

Hii habari ya kusema DART lengo lake sio kupunguza foleni ni mbinu tu za kutaka kukwepa hoja. Hii la kusema lengo la dart sio kupunguza foleni limeanza kuzungumzwa baada ya watu kuhoji ni vipi huu mradi utakabiliana na kupunguza foleni kama junctions zitabaki zilivyo? Ukweli ni kwamba haya mbasi nayo yatajipanga kwenye foleni kusubiri trafiki aruhusu upande wao na sidhani kwamba kutakuwa na upendeleo! Feeder roads zipo nyingi tu ambazo ni mashimo tupu zingewekwa kwanza katika hali nzuri tatizo lingepungua kwa kiasi kikubwa. Unaposema kujenga feeder roads mpya ni gharama kwa sbabu inabidi watu wengi walipwe fidia ni kama unataka kusem huu mradi haukuhusisha watu kubomolewa nyumba zao na kulipwa fidia? Tatizo la huu mradi ni wa gharama kubwa ambao impact yake itakuwa ndogo. hayo mahela yangeweza kufanya kitu kizuri zaidi kukabiliana na taitizo la usafiri dar.
 
Nina wasiwasi kama watapunguza msongamano kwanza baadhi ya njia wamefunga mfano hapo akiba..zitaingia bus zao tu!watu na ofisi zilizopo hapo kati mtaa wa libya/morogoro wataingia vipi na magari yao?njia za kasi ni ferry kwenda kimara mwisho na magomeni to morroco!vipi kuhusu kwengineko msongamano uendelee?
 
Back
Top Bottom