Natumai wakuu mpo salama,
Kuna jambo limeanza kujitokeza nadhani linaweza kutishia mtaala wa elimu kwani limekuwa linakuwa kwakasi kubwa sana. Hili si jengine bali ni suala la tofauti baina ya Honorary Doctorate na PhD. Hebu tazameni taarifa hizi.
MH.MZINDAKAYA ATUNUKIWA PHD !!!Posted by Blog Team on July 12th, 2010
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samwel Sitta akimpongeza Mbunge wa Jimbo la Kwela Christant Mzindakaya jana mjini Dodoma mara baada ya kutununikiwa Shahada ya Uzamifu ya Heshima katika Filosofia ya Uongozi wa Biashara( Honorary Doctorate Degree of Philosophy in Business Administration) na Chuo Kikuu cha California State Christian cha nchini Marekani. Sherehe fupi za kumpongeza zilifanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini dodoma.
Mbunge Mbunge wa Jimbo la Kwela Christant Mzindakaya akiwashukuru wabunge wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania jana mjini Dodoma mara baada ya kutununikiwa Shahada ya Uzamifu ya Heshima katika Filosofia ya Uongozi wa Biashara( Honorary Doctorate Degree of Philosophy in Business Administration) na Chuo Kikuu cha California State Christian cha nchini Marekani. Sherehe fupi za kumpongeza zilifanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini dodoma. Picha na tiganya vincent-Dodoma.
Source: Mohammed Dewji
Nyengine hii
Dk Getrude Rwakatale atunukiwa tuzo na chuo kikuu cha marekani
Monday, July 12, 2010
Dk.Mchungaji Kiongozi wa kanisa la TAG Mikocheni B(Mlima wa Moto)Mh. Gertrude Rwakatare akionyesha Tuzo mbili ya Global Leadership Award na Tuzo ya Doctorate ya Divinity(Maswala ya Kiroho) alizotunukiwa na chuo Kikuu kilichopo Marekani kijulikanacho kama United Graduate College and Seminary University katika sherehe zilizofanyika Kanisani kwake jijini Dar es Salaam.
Source: Michuzi.
Hii sijui ni PhD au Honorary Doctorate? Na mama Rwakatare si alikuwa na PhD before au nimesahau jamani.
Pia kuna hii:
Hongera Mhe. John P. Magufuli kwa kupata PhD 11/28/2009
1 Comment(s)
Dr. Magufuli
Waziri wa Uvuvi na Mifugo, Dr. John Pombe Magufuri, akipongezana na Dr. John Stanslaus Nduguru ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma ya Ufundi katika Wizara ya Miundombinu, wakipongezana baada ya kuhitimu kozi ya PhD katika mahafali yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Magufuli tunajua amesomea UD PhD na amefanikiwa kuipata.
Wasiwasi kuongezeka huku kwa Honorary Doctorate kunaweza kuhatarisha taaluma za vyuo vikuu kwani tunashindwa kutafautisha Honorary Doctorate na Doctor of Philosophy. Au pengine sijui labda ziko sawa ndio maaana tuna Dr Kikwete, Dr Karume, Dr Salim, Dr. Shein, Dr. Mzindakaya, Dr Dr Dr Dr..... Je tutafika?
Kuna jambo limeanza kujitokeza nadhani linaweza kutishia mtaala wa elimu kwani limekuwa linakuwa kwakasi kubwa sana. Hili si jengine bali ni suala la tofauti baina ya Honorary Doctorate na PhD. Hebu tazameni taarifa hizi.
MH.MZINDAKAYA ATUNUKIWA PHD !!!Posted by Blog Team on July 12th, 2010
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samwel Sitta akimpongeza Mbunge wa Jimbo la Kwela Christant Mzindakaya jana mjini Dodoma mara baada ya kutununikiwa Shahada ya Uzamifu ya Heshima katika Filosofia ya Uongozi wa Biashara( Honorary Doctorate Degree of Philosophy in Business Administration) na Chuo Kikuu cha California State Christian cha nchini Marekani. Sherehe fupi za kumpongeza zilifanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini dodoma.
Mbunge Mbunge wa Jimbo la Kwela Christant Mzindakaya akiwashukuru wabunge wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania jana mjini Dodoma mara baada ya kutununikiwa Shahada ya Uzamifu ya Heshima katika Filosofia ya Uongozi wa Biashara( Honorary Doctorate Degree of Philosophy in Business Administration) na Chuo Kikuu cha California State Christian cha nchini Marekani. Sherehe fupi za kumpongeza zilifanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini dodoma. Picha na tiganya vincent-Dodoma.
Source: Mohammed Dewji
Nyengine hii
Dk Getrude Rwakatale atunukiwa tuzo na chuo kikuu cha marekani
Monday, July 12, 2010
Dk.Mchungaji Kiongozi wa kanisa la TAG Mikocheni B(Mlima wa Moto)Mh. Gertrude Rwakatare akionyesha Tuzo mbili ya Global Leadership Award na Tuzo ya Doctorate ya Divinity(Maswala ya Kiroho) alizotunukiwa na chuo Kikuu kilichopo Marekani kijulikanacho kama United Graduate College and Seminary University katika sherehe zilizofanyika Kanisani kwake jijini Dar es Salaam.
Source: Michuzi.
Hii sijui ni PhD au Honorary Doctorate? Na mama Rwakatare si alikuwa na PhD before au nimesahau jamani.
Pia kuna hii:
Hongera Mhe. John P. Magufuli kwa kupata PhD 11/28/2009
1 Comment(s)
Dr. Magufuli
Waziri wa Uvuvi na Mifugo, Dr. John Pombe Magufuri, akipongezana na Dr. John Stanslaus Nduguru ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma ya Ufundi katika Wizara ya Miundombinu, wakipongezana baada ya kuhitimu kozi ya PhD katika mahafali yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Magufuli tunajua amesomea UD PhD na amefanikiwa kuipata.
Wasiwasi kuongezeka huku kwa Honorary Doctorate kunaweza kuhatarisha taaluma za vyuo vikuu kwani tunashindwa kutafautisha Honorary Doctorate na Doctor of Philosophy. Au pengine sijui labda ziko sawa ndio maaana tuna Dr Kikwete, Dr Karume, Dr Salim, Dr. Shein, Dr. Mzindakaya, Dr Dr Dr Dr..... Je tutafika?