Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wananajamvi nauliza:
Hivi amani huombewa (au huombwa), kuihimiza au kuijenga? Nifafanue kidogo: Hapa nina maana kipi kinakuja cha msingi zaidi kuliko kingine: kuomba tu na kuhimiza kuwepo amani nchini au kuijenga amani hiyo katika misingi iliyo imara na ya haki? Kipi katika vitu viwili hivi kinaweza kuiokoa nchi katika farakano (na hata vita ya wenyewe kwa wenyewe) huko mbeleni?
Ninaanzisha mada hii kwa sababu sasa hivi naona watu wengi katika jamii, wanasiasa na viongozi wa dini pia wanahimiza na kuwataka watu waombe kuwepo kwa amani -- badala ya kuhimiza viongozi wa nchi na serikali kujenga misingi imara na ya haki katika jamii na kuendesha nchi katika misingi hiyo.
Nawasilisha.
Hivi amani huombewa (au huombwa), kuihimiza au kuijenga? Nifafanue kidogo: Hapa nina maana kipi kinakuja cha msingi zaidi kuliko kingine: kuomba tu na kuhimiza kuwepo amani nchini au kuijenga amani hiyo katika misingi iliyo imara na ya haki? Kipi katika vitu viwili hivi kinaweza kuiokoa nchi katika farakano (na hata vita ya wenyewe kwa wenyewe) huko mbeleni?
Ninaanzisha mada hii kwa sababu sasa hivi naona watu wengi katika jamii, wanasiasa na viongozi wa dini pia wanahimiza na kuwataka watu waombe kuwepo kwa amani -- badala ya kuhimiza viongozi wa nchi na serikali kujenga misingi imara na ya haki katika jamii na kuendesha nchi katika misingi hiyo.
Nawasilisha.