Hili tatizo la ardhi linaumiza akili mno na linachanganya

D Metakelfin

JF-Expert Member
Mar 23, 2017
3,160
3,259
Habari wanajamvi,

Siku ya juzi tarehe 19 september 2023 tumeletewa notisi ya malipo ya kodi ya ardhi (nimeambatanisha) ikiamrisha tulipe kodi ya ardhi jumla ya shilingi 244,700/=tshs

Kodi ya mwaka huu ni 7,500/=tshs

Baada ya kuulizia afisa mtendaji yeye anadai jumla ya hilo deni ni tangu mwaka 1996.

UTATA ULIPO (na ndipo nahitaji msaada wa wanasheria na wataalamu)

1: hili eneo marehemu baba yangu alinunua pagale na kulikarabati na kuwa nyumba kamili ya kuishi mwaka 2005 lakini jina la kwenye hii notisi sio la marehemu baba yangu aliyekuwa mmiliki wa eneo hili wala sio la mtu aliyemuuzia(baba yangu aliuziwa hili eneo) yaani jina silitambui

2: Karatasi ya kuandikishana mauziano ya hilo pagale nayo kwa bahati kwa bahati mbaya ilipotea.

3: Kuhusu kodi ya jengo tushalipia sana tu ila kwa sasa wanakata kwenye umeme(japo hata risiti za zamani pia hamna )

4: Gharama walizoandika NI :-

TOZO YA MWAKA 2023/2024 7,500/=

MALIMBIKIZO 150,210/=

TOZO 144,450/=

hapo kiuhalisia jumla ni 302,160/= Lakini wameandika Jumla ni 244,700/=

Wamefika wakamkabidhi mtoto mimi sikuwepo.

Je msaada wa wataalamu ni upi hapo maana nimechanganyikiwa na sina hata pa kutoa hizo fedha kwa sasa pili sielewi kama hicho kiwanja ni hiki kweli au vipi kutokana na majina kutoyatambua

Msaada wa haraka tafadhali

IMG-20230921-WA0005.jpg
 
Kafanye search ya hicho kiwanja ilikuwa ujue
Nani mmiliki
Tangu lini
Namba ya hatimiliki.

Baada ya hapo, sehemu nzuri ya kuwabana ni kwenye survey.
Nani ali-survey?
Majirani walisaini form SF 92?
Kwanini wewe hukuhusishwa?
Beacon numbers and their certificates? Nani aliomba na kuchukua? Je, zipo kwenye kiwanja chako?
Coordinates zinafanana?

Anza na manispaa, especially survey and mapping division ndiyo chanzo cha migogoro. Na huyo Hamza aitwe (wataangalia namba ya NIDA).
Anzia hapo Kwanza.
 
Kafanye search ya hicho kiwanja ilikuwa ujue
Nani mmiliki
Tangu lini
Namba ya hatimiliki.

Baada ya hapo, sehemu nzuri ya kuwabana ni kwenye survey.
Nani ali-survey?
Majirani walisaini form SF 92?
Kwanini wewe hukuhusishwa?
Beacon numbers and their certificates? Nani aliomba na kuchukua? Je, zipo kwenye kiwanja chako?
Coordinates zinafanana?

Anza na manispaa, especially survey and mapping division ndiyo chanzo cha migogoro. Na huyo Hamza aitwe (wataangalia namba ya NIDA).
Anzia hapo Kwanza.
Huyo hamza hata wao hawamjui lakini wanadai ndie mmiliki wa kiwanja lakini kiuhalisia hapa tulinunua jengo ambalo halijaisha na mmiliki hakua huyu mmiliki aliyetuuzia anaitwa benjamin Lupala mwaka 2005
 
Kafanye search ya hicho kiwanja ilikuwa ujue
Nani mmiliki
Tangu lini
Namba ya hatimiliki.

Baada ya hapo, sehemu nzuri ya kuwabana ni kwenye survey.
Nani ali-survey?
Majirani walisaini form SF 92?
Kwanini wewe hukuhusishwa?
Beacon numbers and their certificates? Nani aliomba na kuchukua? Je, zipo kwenye kiwanja chako?
Coordinates zinafanana?

Anza na manispaa, especially survey and mapping division ndiyo chanzo cha migogoro. Na huyo Hamza aitwe (wataangalia namba ya NIDA).
Anzia hapo Kwanza.
Mmiliki aliyetuuzia anaitwa benjamin lupala
Tangu mwaka 2005
Tuliuziana kwa barua document alikuwa anatunza Marehemu baba yangu alipokufa ilipotea
Hakuna aliyesurvey
Majirani hawajasaini form yeyote
Sina document yeyote kwa sasa zaidi ya zile za umeme na maji kwenye nyumba japo naishi hapa tangu tulivyonunua mwaka 2005 na hakuna migogoro wowote shida ni hiyo notisi tu iliyoletwa.
 
Mmiliki aliyetuuzia anaitwa benjamin lupala
Tangu mwaka 2005
Tuliuziana kwa barua document alikuwa anatunza Marehemu baba yangu alipokufa ilipotea
Hakuna aliyesurvey
Majirani hawajasaini form yeyote
Sina document yeyote kwa sasa zaidi ya zile za umeme na maji kwenye nyumba japo naishi hapa tangu tulivyonunua mwaka 2005 na hakuna migogoro wowote shida ni hiyo notisi tu iliyoletwa.
Hicho kiwanja kina number na number ya kitalu.
Kwa hiyo kipo surveyed.
Nenda kafanye search ya hicho kiwanja, ni 40,000/-.
Hakikisha unalipia kwa kutumia control number.
Utaipata majibu ya umiliki wake.
Pili, mtafute surveyor achukue coordinates za hapo, akuambie hiyo nyumba IPO kwenye kiwanja namba ngapi, na kitalu namba ngapi.
Then fananisha. Unaweza Kujua haya in a week.
 
Hicho kiwanja kina number na number ya kitalu.
Kwa hiyo kipo surveyed.
Nenda kafanye search ya hicho kiwanja, ni 40,000/-.
Hakikisha unalipia kwa kutumia control number.
Utaipata majibu ya umiliki wake.
Pili, mtafute surveyor achukue coordinates za hapo, akuambie hiyo nyumba IPO kwenye kiwanja namba ngapi, na kitalu namba ngapi.
Then fananisha. Unaweza Kujua haya in a week.
Hii naona itakuwa nzuri sana.
Ahsante
 
Pole sana mkuu,naona mpka kichwa kimeuma umeamua upige na panadol kabisa ili mambo yaende vizuri.Nje ya mada,hivi hakuna option kwenye mitandao ya simu kulipia kodi ya ardhi kwa kiasi-installment mpaka umalize maana yangu imeshagonga lk2,nataka nipunguze kidogo kidogo mpaka iishe...
 
Nashauri wizara ya Ardhi angepewa January Makamba. Huyu mwamba angeiweza sana
 
Back
Top Bottom