Hili ndilo kombora la x -22 lililotumika na Russia kushambulia jengo refu katika mji wa Dnieper

Urusi inachofanya huko Ukraine ni ugaidi na uhalifu wa kivita.
USA vs Iraq
USA vs talaban
Usa vs Vietnam.
NATO vs Yugoslavia.
USA in Syria.
USA in Korea.
USA in somalia.
USA in Panama.
USA in Granada.
USA in Libya.
USA in middle east.
Need I say more?
Yaani mnampenda USA na mambo yake yote.
Anataka Dunia nzima wanaume kwa wanaume tuingiliane kinyume na maumbile watu wanamuunga mkono.akishambulia nchi nyingine ni sawa akisogeza majeshi jirani na Urusi Urusi Hana haki ya kupinga.
 
USA vs Iraq
USA vs talaban
Usa vs Vietnam.
NATO vs Yugoslavia.
USA in Syria.
USA in Korea.
USA in somalia.
USA in Panama.
USA in Granada.
USA in Libya.
USA in middle east.
Need I say more?
Yaani mnampenda USA na mambo yake yote.
Anataka Dunia nzima wanaume kwa wanaume tuingiliane kinyume na maumbile watu wanamuunga mkono.akishambulia nchi nyingine ni sawa akisogeza majeshi jirani na Urusi Urusi Hana haki ya kupinga.
Marekani akifanya uovu ni haki kwa Urusi kufanya pia ?....uovu ni uovu tu haijalishi katenda nani.
 
Mnamo tarehe 14 Januari , jeshi la Ukraine liliripoti kwamba Urusi ilipiga jengo refu katika Dnipro kwa kutumia kombora la aina ya X-22 lililofyatuliwa kutoka kwenye kifyatuzi cha bomu Tu-22m3 juu ya Kursk lililopo karibu na mpaka na Ukraine.

Kombora la aina hii , kulingana na kamanda wa kikosi cha Air Force, katika kipindi cha dakika 30 lilipiga jengo refu lililopo katika mtaa wa Naberezhna Peremohy na kuwauwa watu wapatao 20 katika shambulio hilo. Bado Urusi haijatoa kauli yoyote kuhusina na shambulio hilo

"Urefu, na kasi ya kombora na eneo lilipofyatuliwa viliweza kutambuliwa kwa njia ya mtambo wa rada. Bila shaka lilikuwa ni kombora la Kh-22 ," ilisema Air Force.

Katika msimu wa majira ya kiangazi kombora la aina hii lilipiga jumba la maduma ya bidhaa mbali mbali (mall) katika eneo la Kremenchuk na kuwauwa watu makumi kadhaa.

Katika taarifa maalumu kamanda wa Air Force Luteni Jenerali Mykola Oleschuk alisema kwamba vikosi havina silaha zenye uwezo wa kudungua aina hii ya kombora.

Alisisistiza kuwa ni mifumo ambayo inaweza kudungua ndege pekee, ambayo inaweza kutolewa kwa Ukraine na washirika wake wa kigeni katika siku zijazo (tunazungumzia kuhusu mifumo ya aina hiyo kama vile Patriot PAC-3 or SAMP-T), ndio yenye uwezo wa kuzuia mashambulio yaliyolengwa na makombora haya ya anga.

Alitoa wito wa kutoaminiwa kwa taarifa ambazo zinapinga taarfa hizi.

[https://ichef]

CHANZO CHA PICHA,TYMOSHENKO. OFFICE OF THE PRESIDENT

"Tangu kuanza kwa uvamizi wa jeshi la Urusi nchini Ukraine, zaidi ya makombora ya aina hii 120 yamekuwa yakifyatuliwa ndani ya eneo la Ukraine. Hakuna hata moja lililodunguliwa kwa njia ya ulinzi wa anga ," alisisistiza kamanda.

Kulingana naye, uzito wa wa mfuniko wa kombora hili ni Kh-22 ambao ni sawa na kilogramu 950 , na umbali wa eneo linaloweza kupiga ni kiloita hadi 600.

Oleschuk alisema kuwa linapoyatuliwa kutoka maeneo ya mbali, linaweza kukwepa eneo lililolengwa kwa umbali wa mita mamia kadhaa.

Wakati huo huo, mwezi Mei 2022, Kamanda wa Air Force aliripoti kuangushwa kwa kombora la masafa la Kh-22.

Hatahivyo baadaye alitilia shaka hilo na kusema kuwa

"Taaarifa iliyotolea na vyanzo rasmi ni ya kuaminika kwa ujumla, lakini kuna baadahi ya taarifa zisizao za kuaminika zilizochapishwa kuhusu "kudunguliwa " kwa Kh-22s, hilo ni ukweli ," alikiri.

Ni roketi ya zamani ya Usotieti

X-22 ni silaha mojawapo kati ya makombora yaluyobuniwa katika enzi ya Muungano wa Usovieti ( USSR) katika miaka ya 1960.

Makombora haya yalitengenezwa kwa vilipuzi vya Tu-22 na baadaye yalirekebishwa na kuboreshwa zaidi, kombora hili likiwemo.

Kombora hili lililoboreshwa katika miaka ya 1970, lilikuwa na kasi ya kufurahisha ya mwendo wa kilomita 4,000 kwa saa . Lilikuwa na uwezo mkuwa wa kivita.

Mwanzoni, kombora hili ambalo hutengenezwa kwenye ndege lilibuniwa kwa ajili ya mashambulizi dhidi ya vyombo vya majini, na iliangaliwa kama yenye ufanisi sana, iliogopwa katika nchi za Magharibi. Katika filamu "The Price of Fear" kuna sehemu maarufu zinazoonyesha vilipuzi hivi maarifu vikiipiga ndege ya Marekani ya abiria kwa makombora ya X-22.

Katika miaka ya 1970 na 80, lilikuwa ni kombora lenye ufanisi mkubwa la masafa marefu, lenye kasi ya juu zaidi na kifuniko chake kilikuwa ni dhabiti. Hatahibyo, ukweli kwamba asili yake liliundwa kwa ajili ya mashambulio ya majini, inatoa fursa ya kuamini kuwa halina ufanisi wa kufanya mashambulio ya ardhini.

[https://ichef]

CHANZO CHA PICHA,OFFICE OF THE PROSECUTOR GENERAL

Maelezo ya picha,

Kituo cha maduka kilichoharibiwa

Kombora lililobuniwa kwa ajili ya mashambulizi ya majini ni vigumu kuweza kutumiwa kfanya mashambulizi ya nch kavu – huongozwa na mtambo wa rada na eneo linalolengwa linapaswa kuonekana wazi – kwa mfano , kipande cha chuma ndani ya bahari.

Eneo linalolengwa ni vigumukuonekana kwenye uso wa dunia.

Roketi hizi zina mfumo wa kutafuta eneo linalolengwa, ambao huziongoza katika kulenga mashambulizi yake katika maeneo yaliyolengwa.

Hususan moja ya marekebisho yake ambapo- X-22NA -hukuruhusu tu kufyatua kombora kwenye maeneo yaliyolengwa, kwenye ardhi kulingana na jinsi yalivyopangwa " kwenye eno la ramani". Inaweza kupaa kwa kuzingatia eneo, lakini kwa ujumla liliundwa kujiongoza angani. Safari ya anga ya kituo kwa kituo.

Je ni ya kisasa na yana ufanisi upi?

Toleo la kwanza la kombora la X-22PSI lililoboreshwa lilikuwa na ufanisi wa kiwango cha chini – labda liliweza tu kuzingira eneo.

Ilikuwa ni kilomita mia moja, uwezo ambao sio mzuri sana kwa maeneo madogo yanayolengwa.

Baadaye, aina yake iliyoboreshwa, yenye kifuniko kipya ilitengenezwa.

Toleo la baadaye la mashambulio ya ardhini la kombora hili linafahamika kama Kh-22NA. Ni vigumu kusema lina uhanisi wa kiasi gani.

Lakini kwa vyovyote vile, wakati wa mashambulio yote ya Kremenchuk na Dnipro, yalijaribu kuongeza ufanisi. Kamanda wa Vikosi vya Ukraine aliripoti kuwa katika mashambulio yote mawili, vilipuzi vya , Tu-22M3 viliondoka kutoka katika uwanja wa ndege wa jimbo la Kaluga na yakapiga juu ya anga la Kursk.

Licha ya kuboreshwa, makombora ya Kh-22NA bado ni ya zamani, na kwa ujumla yanakabiliwa na hatari ya kudunguliwa na mifumo ya kukabiliana na mashambulio ya anga.

Ukiliyalinganisha na , "Caliber" kutoka katika Bahari nyeusi (Black Sea) yanapaa mbali zaidi na mbali kutoka kwenye maeneo yanayolengwa.

Kwa ujumla, kwa Kh-22NA, kadri inavyofyatuliwa kutoka mbali, ndivyo inavyokuwa vigumu kuyapiga kwa usahihi maeneo yanayolengwa.

Roketi hizi zina matatizo mengine – ni ngumu kuzitunza kutokana na utumiaji wake wa mafuta machafu yenye sumu. Kwa ujumla hizi ni silaha zilizopitwa na wakati, na kwa kawaida zilikuwa zikifyatuliwa katika masafa marefu wakati wa mazoezi ya mafunzo ya kijeshi.

Source: bbcnews swahili

View attachment 2484120
Putini anauliwa askari wake zaidi ya 400 yeye anajibu kwa kuua raia., poor putin..,
 
Urusi inachofanya huko Ukraine ni ugaidi na uhalifu wa kivita.
USA vs Iraq
USA vs talaban
Usa vs Vietnam.
NATO vs Yugoslavia.
USA in Syria.
USA in Korea.
USA in somalia.
USA in Panama.
USA in Granada.
USA in Libya.
USA in middle east.
Need I say more?
Yaani mnampenda USA na mambo yake yote.
 
Putin ni shetani kuliko hata shetani tunaemsikia!
Ila nawaambia mwisho wake ni mbaya sana sana!
Papa wa urusi kasema,,, nani wa kupinga
Screenshot_20230119-164625_RT News.jpg
 
Sasa kuwa raia wasio na silaha kwa makombora ni Ufala sana
Ndo waache kujificha kwa raia watoke wapambane wazi........hilo ghorofa wasingeweka mifumo ya kujilinda na makombora maeneo ya raia yasingewakuta hayo,,,,,zana ya kijeshi unaificha uraiani mwisho wa siku watu wakitandika mnapiga kelele wakati wao wenyewe wameshindwa kuwalinda raia wao
 
Back
Top Bottom