Hili la vijana kuvuta petrol pamoja na gundi

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,252
Arusha.

Petroli na gundi inapogeuka kuwa dili kwa vijana.

Kutokana na ugumu wa maisha, kukosa ajira, kazi ngumu imewalazimu vijana wengi kuingia kwenye makundi ya ajabu na yanayofanya mambo ya kushangaza katika jamii, mojawapo ni hii aina mpya ya uvutaji wa petrol pamoja na gundi kama njia mojawapo ya kilevi.

Vijana wengi waliokwisha kuingia kwenye uraibu huo wanadai kuwa ni kutokana na upatikanaji wake na urahisi wa bei ya bidhaa husika.

Baadhi ya vijana hao wameoneka wakiwa wanafanya hivyo katika maeneo ya stand zote kubwa na ndogo, mitaani Na hata majumbani. Huku wakioneka ni vijana waliokwisha kata tamaa ya maisha.

Screenshot_20240313-150716.png


Vijana hao ni wenye umri kuanzia miaka 13 hadi 45 na Kati ya vijana hao wengi wao hawana makazi. Na. Pia Wamekuwa tishio kwa jamii.
 
Kuhusu petrol ni zamani sana unatumika labda tu ww ndo ulichelewa kujua....gundi naskiaga tu sijawahi ona mtu akitumia
 
Mungu awasaidie Vijana wetu kujitambua na kuwa na hofu ya Kimungu ndani yao

Yaani Matumizi ya madawa ya Kulevya wao
Bangi wao
Shisha wao
Mirungi wao
Pombe wao
Ushoga wao
Umalaya wao
........wao
........wao 🙌
 
Back
Top Bottom