Hili la maiti kulipishwa madeni Hospitali za Serikali limekaaje?

Poleni kwa msiba. Huduma zinalipiwa kulingana na matumizi ya mteja husika. Pia laki 7 ni ndogo sana ukilinganisha na gharama halisi, ujue hiyo laki saba ni baada ya kulipiwa na ruzuku ya serikali, bila ruzuku mteja angedaiwa hata milioni kadhaa kwa shida aliyokuwa nayo na matumizi yake. Kifo ni mapenzi ya mungu hakihalalishi kuondolewa deni. Niulize swali hivi ukinunua sukari dukani wakati unapokea ikamwagika unamwambia muuzaji kuwa nipe sukari nyingine kwa malipo yaleyale? au unalipia tena. Kumbuka siku si nyingi Raisi wetu alilazimika kumlipia mama mmoja hapa Muhimbili shilingi milioni 5 ili achukue mwili wa mama yake. Huu ulikuwa ni mfano tosha kuwa nini kinastahili .Kwa maana hiyo basi ni haki kulipia huduma. Kumbuka usipozichangia huduma iko siku utazikosa kwani zitakuwa zimeisha

Huduma zikosekane serikali ikiwa wapi, watu kila siku wanalipa kodi.

..........Laki saba ni gharama ndogo? Hivi unajua kuna mtu hawezi hata kupata Milo mitatu kwa siku na akiumwa anatakiwa apate matibabu mtu wa aina hiyo ataweza kulipa laki saba kweli?
 
Hakika mkuu suluhisho pekee ni bima. Ukishindwa NHIF, AAR, Strategies, Jubilee na kampuni zingine wafuate hata tiGO wana bima pia. Tatizo tunapenda sana kudharau hivi vitu.

Umeziona taratibu mpya za kujiunga na BIMA (NHIF)..?

Labda hizo bima zingine, lakini hata kabla ya hii mpya.... 1.5M kwa mwaka sio wengi waliweza ukiacha watumishi ambao hukatwa juu kwa juu.
 
Huduma zikosekane serikali ikiwa wapi, watu kila siku wanalipa kodi.

..........Laki saba ni gharama ndogo? Hivi unajua kuna mtu hawezi hata kupata Milo mitatu kwa siku na akiumwa anatakiwa apate matibabu mtu wa aina hiyo ataweza kulipa laki saba kweli?

Huyo jamaa anayejitujisha itakuwa ni mtumishi anayekatwa moja kwa moja, laki SABA sio kiasi kidogo kukomboa MAITI.... kuna haja ya kuwajibisha hizi hospitali inapotokea KIFO sio tu wajifiche kwenye “mapenzi ya Mungu” hata kama ilikuwa uzembe wao huku wao wakinufaika.

Cc MANILABHONA
 
Mloganzila ni jipu kwa kila kitu. Ilipoanza walikuwa hadi wanatoa diaper kwa wagonjwa mahututi siku hizi walaaa washaacha na gharama ni zilezile kubwa. Mbali na hapo umakini hakuna wagonjwa wanakufa Kama kuku. Yani wodi moja ya cardiac kufa watu 6 kwa siku ni kitu cha kawaida. Sijui tutaponea wapi
kutakuwa na shida na hao madaktari hapo, operation ya hernia kuondoa mtu ni ngumu sana napata mashaka na wataalamu wa hapo.
 
Wakati akiwa hai bila shaka anakuwa alitumia services. Hizo lazima irudishwe
Lakini pia anapokuwepo mortuary lazima anatumia services za hapo lazima zilipiwe ili ziendelee kutolewa. Otherwise siku mtakuta marehemu wenu wameanza kuoza napo mtaanza kulalamika tena. Hizi ni cost sharing. Ni among of the policy
Habarini wapendwa,

Wiki hii mzee wetu alikuwa anaumwa Hernia, tarehe 07/11/2019 tukampeleka Mloganzila hospital akitokea hospitali ya Bagamoyo, kufika kule usiku akafanyiwa upasuaji, saa kumi alfajiri akafariki. Sasa tarehe 08/11/2019 tukaenda ili kuchukua mwili wa marehemu akazikwe.

Kufika pale tunaambiwa marehemu anadaiwa jumla ni Tsh 775,000/= tukalalamika mbona hela nyingi hivyo, wakatuambia nendeni ustawi wa jamii labda wanaweza kuwasaidia mkilalamika kuwa hamna uwezo, kwenda kule tukaambiwa kuwa hata iko kiasi mlichotajiwa kapewa punguzo sababu katokea hospitali ya Serikali kuja hapa, kukosa hivyo ingekuwa mara mbili yake.

Tukasema sawa, ndugu wakachangishana ikafika laki sita na ishirini, kuipeleka kule bado wakagoma, wakasema hadi hela itimie yote isipungue hata mia ndo maiti itatoka, basi tukapigia simu watu baki kuwakopa hela ikatimia tukaenda kupeleka tukapewa mwili wa marehemu. Sasa najiuliza hivi huu utaratibu wa kudai maiti ni haki kweli? Mtu amekufa bado mnamdai, sio laana kweli.

Kuna wapemba tumewakuta wanadaiwa milioni tatu za maiti wao, wameshauriana waende wakafanye kisomo cha kuswalia maiti pale hospitali, wakimaliza waondoke mwili wauache pale pale Mloganzila, wao wataisabu kama ndugu yao amekufia baharini na maiti haikupatikana kuliko kulipa hela hiyo.

Hii ni kweli jamani wala sio jambo la kutunga, marehemu katuachia madeni.

Zaidi, soma:


 
Kabla hajapatwa na umauti hospitali ilimhudumia bila kujali kuwa atakuwa na uwezo wa kulipa au la. Hicho ni kitendo cha uzalendo kwa hospitali husika ma kitendo cha utu kama walivyofundishwa medical school.
Hospitali za private haufanyiwi huduma mpaka ulipie kwanza.
Ningeshauri uwapongeze kwa kitendo cha kujitahidi kupambana na uhai wa ndugu yako mpaka pale iliposhindikana
Kuhusiana na kulipia gharama za matibabu aliyopewa kipindi alipokuwa hai, hilo halikwepeki.
Ni lazima zilipwe zote,ili hospitali iweze kuendesha shughuli mbalimbali za kutoa huduma kwa wengine watakaokuja.
Sera ya Afya ya Serikali kupitia wizara ya Afya inasema kuwa kila mtu atachangia huduma za Afya.
Kama amefariki ndugu zake watajichanga kulipia huduma hizo.
Hatalipia pale itakapothibitika kuwa huyo mtu hana uwezo.
Ni baada ya ofisi ya ustawi wa jamii ya hospitali kufanya detailed analysis na kujiridhisha kweli mgonjwa /marehemu hana uwezo. Jambo ambalo si rahisi.
 
Juzi tu hapa mtaani kuna jamaa kapata ajali akaenda kufia hapo wanaenda kufatilia mwili wanakuta deni laki tatu na usheee yaan ndani ya masaaa tu hapo nilichoka ...kwa kweli itafutwe namna ya kuwasaidia watu
 
Mloganzila ni mbaya kuliko popote duanian nilienda kufanya vipimo mwaka Jana hivi nikalipa gharama zote mwisho wakanishangaza kusomewa majibu hela nikamwambia nipen Basi ntajua mwenyewe mbele wakagoma mpaka nilipe na hapo nimesafir Kutoka katav mpaka hapo kwa matibabu tu nikaona isiwe kesi nikamwambia mhusika uzur hata wewe utaumwa na utakufa baki na majibu nikaondoka kurud katav Ila Mungu mwema sana sijawah tumia dawa yeyote Ila najihis nimepona kabisa maumivu hayapo kabisa
Ila I wish wenye kuweka hizo Sera sijui sheria wangekufa wote tu hapo tuqmze upya
Mloganzila ni kituo cha upigaji wafe na Sera zao
 
Hela za kulipa hospitali ndo hamna, ila hela za kupika wali, msibani, na kununua vitu vingine vihusivyo msiba inakuwepo? Au ishu mnaona shida kulipa hela ya matibabu wakati tayari mgonjwa kafariki? The thing ni kuwa gharam za kuuguza zilikuwa zimeshafanyika, kama ni ile panadol aliyotumia jana kabla hajafarii, lile drip, vyote vilinunuliwa kwa pesa, na inabid ipatikane pesa itakayo vinunua vingine ili wagonjwa wengine pia watumie, yule nesi aliemtibia hadi dakika ya mwisho, mwisho wa mwezi mshahara wake uko pale pale,

Suluhisho la kudumu hapa ni Universal Health Insurance coverage basi
 
Kabla hajapatwa na umauti hospitali ilimhudumia bila kujali kuwa atakuwa na uwezo wa kulipa au la. Hicho ni kitendo cha uzalendo kwa hospitali husika ma kitendo cha utu kama walivyofundishwa medical school.
Hospitali za private haufanyiwi huduma mpaka ulipie kwanza.
Ningeshauri uwapongeze kwa kitendo cha kujitahidi kupambana na uhai wa ndugu yako mpaka pale iliposhindikana
Kuhusiana na kulipia gharama za matibabu aliyopewa kipindi alipokuwa hai, hilo halikwepeki.
Ni lazima zilipwe zote,ili hospitali iweze kuendesha shughuli mbalimbali za kutoa huduma kwa wengine watakaokuja.
Sera ya Afya ya Serikali kupitia wizara ya Afya inasema kuwa kila mtu atachangia huduma za Afya.
Kama amefariki ndugu zake watajichanga kulipia huduma hizo.
Hatalipia pale itakapothibitika kuwa huyo mtu hana uwezo.
Ni baada ya ofisi ya ustawi wa jamii ya hospitali kufanya detailed analysis na kujiridhisha kweli mgonjwa /marehemu hana uwezo. Jambo ambalo si rahisi.
Huenda baba ako na mama yako Leo wapo na wanauwezo Ila ipo siku lutakukuta kubwa lako iman na utu vitakujia ndo utajifunza kuwa utu bora kuliko Mali na fedha
 
Watu wakiambiwa kateni Bima hawataki. Yakiwafika ndio yanakuwa yaleeee.

Hatuwezi fika kwa kulaumu kila siku.
Je kila mgonjwa akifa asilipe unadhani hospital zitajiendeshaje?

NB: Babu, Baba, Mama, Wadogo zangu na Watoto wangu wote na Mama Mkwe na Baba Mkwe na Mke wangu na Shemeji zangu na watoto wao wote wana Bima NHIF hivyo msinitusi
Shukuru Mungu kwa uwezo wenu Mungu amewapa akawanyima hao wengine
 
Ww acha hizo maana ya kulipa si kwamba mgonjwa apone mmeshindwa kumtibu mgonjwa kafa mnadai hela ya nn ww mfano umepeleka gari geleji limeshindwa kutengemaa utatoa pesa hata km fundi alitumia gharama ...Hapo tunaomba tu serikali iangalie namna ya kufanya maaana Afya ya watanzania ni muhim kwa taifa letu
Tatizo tunapenda lawama na kutafuta cheap popularity tu! Kabla ya kuwa Marehemu alikuwa mgonjwa na alihudumiwa kama mgonjwa na kupewa dawa. Kuna gharama zake. Alipofariki akawa Marehemu kuna gharama za kuhifadhi Marehemu. Jumla inakuwa laki 7. Je unataka kuniambia mgonjwa akifariki daktari alokuwa anamtibu asilipwe mshahara? Je akiwa Marehemu mortuary attendant, ajitolee bure, je umeme wa jokofu Tanesco wautoe bure? We need to be realistic na ndo maana bima ya Afya muhimu. Hakuna Huduma ya bure hapa TZ baada ya ujamaa ndugu yangu Mina cute
 
Ww acha hizo maana ya kulipa si kwamba mgonjwa apone mmeshindwa kumtibu mgonjwa kafa mnadai hela ya nn ww mfano umepeleka gari geleji limeshindwa kutengemaa utatoa pesa hata km fundi alitumia gharama ...Hapo tunaomba tu serikali iangalie namna ya kufanya maaana Afya ya watanzania ni muhim kwa taifa letu
Huo ni utoto sasa, kabla ya kuanza Kuandika kwanza soma kwa utulivu michango ya kabla. Ukikua utaelewa
 
Dah!umeongea kitu muhimu sana mkuu...maana hawa hawana cha kupoteza ufe usife chao kipo ila wakijua kua ukifa chao hakipo watapambana sana upone .
Kimantiki kabisa ilipaswa kama mgonjwa akifia hospital basi gharama zote zifutwe..

na hilo lingeongeza ufanisi wa matabibu ktk kumhudumia mgonjwa

kuhakikisha wanapigana kufa na kupona mgonjwa aishi na wapate malipo stahiki kwa haki

nawasilisha
 
Juzi tu hapa mtaani kuna jamaa kapata ajali akaenda kufia hapo wanaenda kufatilia mwili wanakuta deni laki tatu na usheee yaan ndani ya masaaa tu hapo nilichoka ...kwa kweli itafutwe namna ya kuwasaidia watu
hapafai pale, wapo kipesa zaidi,
 
Back
Top Bottom