Sherehe za CCM Dodoma Zaingia doa, Wang'oa bendera ya CHADEMA, Aden Rage ashuhudia

othorong'ong'o

Senior Member
Jan 20, 2011
103
19
Nimepata taarifa sasa hivi kwamba sherehe za CCM zilizokua zikiendelea DODOMA eneo la Mwanga Bar imeahirishwa. Hii ni baada ya WanaCCM kung'oa bendera ya CHADEMA lililokua eneo hilo ili kupisha sherehe yao. Naomba walioko karibu watupe updates zaidi
aden_rage.jpg


Source: DODOMA FM

============
UPDATE:
============

Kutoka Mwananchi - Januari 04, 2013

CHADEMA, CCM wazichapa Dodoma

vuruguccm.jpg


SHEREHE za miaka 36 za kuzaliwa kwa CCM jana ziliingia dosari, baada ya kuibuka vurugu kubwa kati ya wafuasi wa chama hicho na Chadema mkoani Dodoma wakati wakigombea eneo na mti wa kutundika bendera za vyama vyao.

Vurugu hizo zilizotulizwa na Polisi wa Kutuliza Ghasia (FFU), zilitokea jana mchana katika uwanja huo uliopo karibu na Baa ya Mwanga, baada ya CCM kung'oa bendera ya Chadema iliyokuwepo uwanjani hapo, ili waweke bendera zao kwa ajili ya mkutano ambao ulikuwa sehemu ya maadhimisho hayo.

Vurugu zilizuka baada ya wafuasi wa Chadema kuwataka wenzao wa CCM waendelee na mkutano katika eneo hilo kwa sharti la kurejeshwa kwa bendera iliyong'olewa. Wafuasi wa vyama hivyo wakiwamo wabunge wa CCM walionekana wakivutana kunyang'anyana mti wa bendera.

"Baada ya CCM kugoma, Chadema walijaribu kurudisha bendera hiyo kwa nguvu, jambo ambalo lilifanya wafuasi wa CCM waanze kuokota mawe na kuwarushia wapinzani wao hao, huku Chadema nao walianza kujibu mapigo," alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.

Baadhi ya wabunge wa CCM walioshiriki katika vurugu hizo na majimbo yao kwenye mabano ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Nyambari Nyangwine (Tarime), Seleman Jafo (Kisarawe), Said Mtanda (Mchinga) na Mary Chatanda (Viti Maalumu).

Baadhi ya wafuasi wa CCM walionekana wakibeba mawe na kuwapiga wenzao wa Chadema na kusababisha tafrani kubwa katika eneo hilo la mkutano.

Katibu wa Chadema Wilaya ya Dodoma Mjini, Jellah Mambo alisema kuwa tukio hilo limetokana na wafuasi wa CCM kung'oa bendera ya Chadema iliyokuwa ikipepea eneo la Mwanga Baa kulikofanyika sherehe za chama chao (CCM).

"Kwanza wamechukua bendera yetu. Halafu tumeshangazwa na CCM kuruhusiwa kufanya maadhimisho yao wakati kuna agizo la Mkuu wa Mkoa na polisi kukataza mikusanyiko ya kisiasa wakati wa Bunge.

"Kwa nini sisi (Chadema) tuzuiwe mikutano yetu wakati wenzetu wanafanya? Huku si kutenda haki....Tulikuwa na mikutano ya kuimarisha chama katika kata kuanzia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili, lakini tumezuiwa na tukaheshimu mamlaka," alisema katibu huyo.

Pia tulikuwa tufanye mkutano na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, lakini tukazuiwa na tuliheshimu amri hiyo, alisema.

Mambo alisema katika vurugu hizo wafuasi wawili wa Chadema; Idd Kizota na Anord Swai waliumizwa na kushonwa nyuzi saba usoni.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Ezekiel Mpuya alisema hana taarifa za majeruhi hao

"Ni vigumu kujua, unless (isipokuwa) wafike hospitalini wakisindikizwa na kundi la wafuasi wenzao waliokuwa kwenye sare. Kama walikuja kama wagonjwa wengine sio rahisi sana kwangu kujua," alisema Dk Mpuya.

Kumi mbaroni

Vurugu hizo zilizosababisha watu wawili kuumizwa vibaya, zililazimisha Jeshi la Polisi kuwatia mbaroni watu kumi wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chadema

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alikiri kutokea vurugu hizo, lakini akasema bado anafanyia kazi suala hilo.

Kamanda Misime alikiri Serikali mkoani Dodoma kuzuia mikutano ya kisiasa wakati wa Bunge, lakini akasema kwa CCM ni tofauti kwa kuwa hizo ni sherehe zao za kuzaliwa kwa chama.

"Ninasoma hapa magazeti yenu, mmeandika wenyewe maadhimisho ya miaka 36. Sasa hawa wanaadhimisha hiyo miaka 36 na siyo mkutano wa kisiasa...Tulichokataza ni maandamano, misafara ya pikipiki na kufanya mikutano ya siasa," alisema Misime.

Akihutubia katika mkutano huo baada ya hali kutulia mgeni rasmi, Mbunge wa Jimbo la Tarime, Nyangwine aliwakandia wapinzani na kusema kuwa wanachokifanya ni kuendeleza vurugu nchini na hawana sera ya maendeleo.

"Hivi jamani, hii leo hawa jamaa watasema nini? Kama suala la barabara, leo hii unaweza kutoka Mtwara hadi Mwanza kwa baiskeli, kama maji, michakato inafanyika, kama umeme ndiyo usiseme, hivi wanataka nini?

"Hawa jamaa wamezoea kufanya vurugu...Si mmeona wenyewe hapa, hawana lolote zaidi ya kufikiria vuru, wananchi msikubali kuhadaiwa,"alisema.

JK akemea mifarakano

Akizungumza mkoani Kigoma kulikofanyika maadhimisho hayo kitaifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, alikemea siasa za makundi ndani ya chama, akisema tabia hiyo haijengi.

"Mifarakano ndani ya chama inayopaliliwa na viongozi ndani ya chama, inakibomoa chama na ndiyo maana tumepoteza majimbo matano katika uchaguzi uliopita," alisema.

Aliendelea:"Ninasoneneka sana kuona viongozi wetu wanajiingiza katika makundi, tabia hii haijengi, turejee katika maazimio yaliyopitishwa katika mkutano mkuu uliopita, ambayo yalisisitiza kuwapo kwa umoja na mshikamano."

Rais Kikwete alisema angetamani umoja na mshikamano wa chama hicho ungeendelea kudumu, ili amalize muda wake akikiacha chama kikiwa imara na kuendelea kushika dola.

"Mimi sasa ninaelekea kwenye ungwe ya mwisho ya uongozi, nataka nikabidhi kijiti kwa mwana-CCM…Nataka niondoke nikiwa nimeicha CCM imara " alisema Rais Kikwete .

Katika hotuba hiyo Rais Kikwete pia aligusia maendeleo yaliyofikiwa katika kipindi cha utawala wake akitaja maeneo kama ujenzi wa barabara, madaraja na uimarishaji sekta ya maji kuwa ni baadhi ya maeneo yaliyopiga hatua.

Alisema atapondoka madarakani jambo kubwa ambalo angependa Watanzania wakumbukuke kwalo ni kuitwa bwana maendeleo na hivyo sasa anaendelea kuisimamia vyema ilani ya chama chake ili kuendelea kukamilisha miradi iliyobaki.

Mapema Rais Kikwete aliongoza mamia ya wakazi wa Mji wa Kigoma katika matembezi ya mshikamano ikiwa ni ishara ya kuhimiza umoja na mshikamano kwa Watanzania.

Kikwete aliungana na viongozi wenzake Makamu Mwenyekiti CCM Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa chama hicho Abdulrahman Kinana, lakini katika hali isiyo ya kawaida baadhi ya viongozi wa chama hicho hawakushiriki, akiwemo wenyeviti wastaafu, Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi.

Wengine ambao hawakuwepo katika matembezi hayo ni pamoja na makatibu wakuu wa zamani; Yusuph Makamba na Willison Mukama na wajumbe wote wa sekretarieti ya chama hicho iliyoteuliwa Novemba mwaka jana.

Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na viongozi wa vyama vya siasa vya PPRD cha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kile cha CNDD-FDD ambavyo vilisindikizwa na vikundi vya sanaa kutoka katika nchi hizo jirani.

 
Nyinyiem mnafanya nchi hii ni mali yenu siyo,tambueni wtz tumewachoka bado kuwapiga kiberiti mmoja mmoja.
 
Kama yule yule ncemba,ananikera anavyozuga anaipenda tz kwa kuvaa skafu ya bendera ya tz,kumbe la ,,.
 
mkutano unaoendelea mkoani kigoma hivi sasa watu wengi waliopo kwanye mkutano huo wanaonekana kwamba, ni wanahama wa vyama pinzani hasa chadema maana hawana furaha wala hawaitikii panaposemwa ccm oyeee!!!!!!angalieni kwenye ti star
 
bobovic, wamechoka sana maana wengine wametoka Kaliua, urambo, Kasulu, Kibondo
 
Kada wa CHADEMA mkoa wa Dodoma Arnold Swai akishambuliwa na wafuasi wa CCM jana kwa shinikizo la mbunge wa Tabora Mjini Ismail Aden Rage. Haya CCM wakifanya fujo haionekani..kunya anye kuku, akinya bata kaharisha! Katika picha ya pili anaonekana Aden Rage akimtoboa kada wa CHADEMA kwa kutumia mlingoti (ni mtu muuwaji sana huyu mtu, sijui ana roho gani)

KISA
Ni baada ya CCM kung'oa bendera ya CHADEMA iliyokuwepo (baa ya Mwanga) karibu na eneo ambalo sherehe za maadhimisho ya CCM zilikofanyikia... CHADEMA waliwataka CCM wafanye maadhimisho yao ila wahakikishe wanazirudisha bendera zilizong'olewa. Baada ya CCM kugoma, ndio CHADEMA wakiongozwa na Swai wakajaribu kuzirudisha wakakutana na huo mkasa!

===============
Updates

SHEREHE za miaka 36 za kuzaliwa kwa CCM jana ziliingia dosari, baada ya kuibuka vurugu kubwa kati ya wafuasi wa chama hicho na Chadema mkoani Dodoma wakati wakigombea eneo na mti wa kutundika bendera za vyama vyao.Vurugu hizo zilizotulizwa na Polisi wa Kutuliza Ghasia (FFU), zilitokea jana mchana katika uwanja huo uliopo karibu na Baa ya Mwanga, baada ya CCM kung'oa bendera ya Chadema iliyokuwepo uwanjani hapo, ili waweke bendera zao kwa ajili ya mkutano ambao ulikuwa sehemu ya maadhimisho hayo.

Vurugu zilizuka baada ya wafuasi wa Chadema kuwataka wenzao wa CCM waendelee na mkutano katika eneo hilo kwa sharti la kurejeshwa kwa bendera iliyong'olewa. Wafuasi wa vyama hivyo wakiwamo wabunge wa CCM walionekana wakivutana kunyang'anyana mti wa bendera.

"Baada ya CCM kugoma, Chadema walijaribu kurudisha bendera hiyo kwa nguvu, jambo ambalo lilifanya wafuasi wa CCM waanze kuokota mawe na kuwarushia wapinzani wao hao, huku Chadema nao walianza kujibu mapigo," alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.

Baadhi ya wabunge wa CCM walioshiriki katika vurugu hizo na majimbo yao kwenye mabano ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Nyambari Nyangwine (Tarime), Seleman Jafo (Kisarawe), Said Mtanda (Mchinga) na Mary Chatanda (Viti Maalumu).

Baadhi ya wafuasi wa CCM walionekana wakibeba mawe na kuwapiga wenzao wa Chadema na kusababisha tafrani kubwa katika eneo hilo la mkutano.

Katibu wa Chadema Wilaya ya Dodoma Mjini, Jellah Mambo alisema kuwa tukio hilo limetokana na wafuasi wa CCM kung'oa bendera ya Chadema iliyokuwa ikipepea eneo la Mwanga Baa kulikofanyika sherehe za chama chao (CCM).

"Kwanza wamechukua bendera yetu. Halafu tumeshangazwa na CCM kuruhusiwa kufanya maadhimisho yao wakati kuna agizo la Mkuu wa Mkoa na polisi kukataza mikusanyiko ya kisiasa wakati wa Bunge.

"Kwa nini sisi (Chadema) tuzuiwe mikutano yetu wakati wenzetu wanafanya? Huku si kutenda haki....Tulikuwa na mikutano ya kuimarisha chama katika kata kuanzia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili, lakini tumezuiwa na tukaheshimu mamlaka," alisema katibu huyo.

Pia tulikuwa tufanye mkutano na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, lakini tukazuiwa na tuliheshimu amri hiyo, alisema.

Mambo alisema katika vurugu hizo wafuasi wawili wa Chadema; Idd Kizota na Anord Swai waliumizwa na kushonwa nyuzi saba usoni.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Ezekiel Mpuya alisema hana taarifa za majeruhi hao.

attachment.php
attachment.php
 

Attachments

  • IMG00652-20130204-0245BBB.jpg
    IMG00652-20130204-0245BBB.jpg
    39 KB · Views: 3,317
  • BB2.jpg
    BB2.jpg
    33.4 KB · Views: 3,276
Naomba tafadhali sheria ichukue mkondo wake ili huyu msomali atambue hapa ni Tanzania na sio Somalia.Kwanza watu wa Tabora ni watu wa ajabu sana kwa nini wamemchagua mtu alie wahi kuwa convicted criminal

Mkuu huyu mtu sii mwema at all. Ni mtu mbaya sana..siasa sio vita. Nalaani kitendo cha kushambuliwa na kuumizwa vibaya kada wa chadema, mr anorld.
 
ukiangalia vizuri hiyo picha ya pili, Alhaj Ismail Aden Rage (Mb-CCM) anaonekana 'anabembea' kabisa anapimchoma Ndg Swai kwa mti. Yaani anashindilia haswa.

Ndg Swai na awawashitaki wote anaowajua pamoja na hao walioko katika picha zote.

Kando namwona kuna mpiga picha anachukua video, naye awasaidie kuwapa ushahidi kama ule wa kwa Mar Mwangosi.
 
ukiangalia vizuri hiyo picha ya pili, Alhaj Ismail Aden Rage (Mb-CCM) anaonekana 'anabembea' kabisa anapimchoma Ndg Swai kwa mti. Yaani anashindilia haswa.

Ndg Swai na awawashitaki wote anaowajua pamoja na hao walioko katika picha zote.

Kando namwona kuna mpiga picha anachukua video, naye awasaidie kuwapa ushahidi kama ule wa kwa Mar Mwangosi.

Kama kuna Vielelezo vya wazi namna hii sioni sababu kwa nini wanaharakati na wanasheria wa Chadema wasichukue hatia za kukomesha ushenzi huu.
 
Hebu mtujuze kwanza nini kiini cha hili songombingo! All in all Rage na wadhifa wote huo huwezi kufanya unachokifanya hapo!
 
huyu Mbulushi aliyeonekana na bastola leo anaonekana na mkuki akimchoma mwanachama wa Chadema sio? aangalie asije akahama nchi 2015
 
alikuwa wapi? wakati mwingne huwa tunakosea,kama aliwafuata kwenye mkusanyiko wao akiwa na sare za chadema lazima haya yatokee
 
huu ni uhuni na upumbavu! tofauti za kivyama na itikadi sio kigezo cha kutufanya watanzania tuchukiane hadi kufikia hali hii!
 
Back
Top Bottom