Hii ni Morogoro au Kibera!!!??

Coza Mhando

Senior Member
Dec 14, 2010
194
7
Habari wana JF,nadhani ni bukheri kabisa wa afya!.
Kwa kweli kwa umaarufu wa huu mji ktk historia ya bongo hii nyanja yoyote ile huwezi kuamini ukifika tu hapa mjini morogoro. Mji umekithiri kwa uchafu ukianzia tu pale kituo cha mabasi yanayoenda mikoani hapatamaniki.
Njoo huku mjini pembezoni mwa barabara ni mifuko ya plastiki iliyotumika,chupa za maji na taka nyingine chungu zima. Mitaani huku uswahilini kama mafiga,k'ndege,mawenzi,mafisa,kilakala,kikundi ,kihonda,manzese,sultani,chamwino ndio hapatamaniki,
Utafikiri ni ile kibera ya kenya.
Sijui mamlaka husika zinafanya nini!,waende wakajifunze kule moshi na mwanza,
wana morogoro vp au mmeridhika na huu "uvundo"
"turudisheni zile enzi zetu za maji yatiririka toka milimani morogoro"
Aaaaagrrrr!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom