Apollo
JF-Expert Member
- May 26, 2011
- 4,920
- 3,221
Mimi ninajiuliza sana, kwanini kuna watu wakiwa wanaanza mahusiano wanakuwa na jitihada na juhudi nyingi kunogesha mapenzi mfano kukupigia simu, kukupa kadi na zawadi na kuonyesha upendo alafu baada ya muda wanachoka. Yaani wanapunguza upendo sijui niseme wanachoka. Unakuta anapunguza muda wa kukupigia simu au ukimpigia anajifanya busy. Tena unakuta mwingine hana mpenzi pembeni wala hatoki nje ila anakuwa anapunguza upendo. Why? Ni kawaida kuwa mapenzi yananoga then yanapoa au ni mtu tu na tabia yake au hisia zake? Mbona kuna wengine wamedumu kwa miaka mingi ilia hawachokani? Msaada please!
NA SOLUTION YAKE NI NINI?
NA SOLUTION YAKE NI NINI?