Hii ndiyo CV ya Idd Azzan

Mtu aliyezaliwa 1965 akisema fursa ya vyuo ilikuwa haipo ni kwa sababu alikuwa kilaza tena hakukuwa na ufisadi na kusoma ilikuwa bureee bwerere tena yeye akiwa palepale jikoni enzi za analogue alikuwa na advantage. Lakini sasa yaonekana alikuwa mtoto wa kijiweni kupata stori za Yanga na Simba hivyo book haikuwa saana. Lakini jihadharini watu wa namna hiyo huwa pia ni TISS maana kipindi wanapotea wanaenda mazoezi wakirudi wanaibukia kwenye makampuni binafsi na mipira kama Azan

Sio 1966 tu hata waliosoma miaka 1990s pia fursa ilikuwepo wabunge wa design hii wanasoma kwa sababu hata ukiangalia CV yake utaona amemaliza primary school 1979 lakini ajabu secondari amekumbuka kujiendeleza miaka ya 2000, hii inainyesha moja kwa moja kuna kitu alikuwa anatafuta nacho si kingine ni uongozi. Kama mtu alikosa fursa ya kwenda sekondari kulikuwa na fursa nyingine ya kusoma masomo ya jioni.
 
Hapo kwenye wakuu wa wilaya ndugu MchunguZI ndio inaniuma maana wanateuliwa watu ambao hata experience ya uongozi hawana, maana kazi ya mkuu wa wilaya ni kusimamia utekelezaji wa halmashauri alafu unamtoa mtu from nowhere tena msela with zero experience of local government kwenda kushika u-DC hapa unategemea nini hapa kama sio kufanya kampeni za chama tawala na vitu vingine vya kichama. Hizi poat zinatakiwa mtu ambae amekuwa katika utumishi wa umma kwa muda mrefu ili iwe rahisi kutekeleza shughuli na ndio maana unakuta DC anaingia vijijini na kuwafukuza kazi watendaji wa kata na vijiji/mitaa wakati hiyo si kazi yake (sema nchi hii ndio hivyo wananchi wake wengi ni kubali yaishe otherwise siku wananchi watakapojitambua nadhani watu wakigombea ubunge kipindi kimoja hawatachukua fomu kipindi kingine)
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tunaomba pia cv za wabunge wa chadema tulinganishe na hii.Ingekuwa ni vizuri mno

Inaelekea CDM mnaigopa maana alietoa hii thread hajajitambulisha kama CDM, kwanini zikija thread zinazoonyesha mambo tata ya CCM huwa mnakimbilia CDM kufanya comparison, why not other party?
 
hilo nalo neno ndo maana wanaishia kuomba rushwa.mie naomba kiingereza kipitishwe wawe wanaongea bungeni wengine kila siku watakuwa wagonjwa.

Hata kisipopitishwa kiingereza bado tatizo lipo pale pale hata kama ni kwa kiswahili kama mtu hana nondo za kutosha kuhusu mada flani hata umpe fursa ya kuuzungumza kisukuma bado hawezi kwa kuwa maarifa ya agenda husika na madogo. Ni kama tulivyokuwa primary school tunafundishwa kwa kiswahili lakini bado vilaza walikuwepo, elimu ni ufunguo wa maisha hata kama amesoma kijapani, kichina etc
 
DAR ES SALAAM ndo tulitegemea ingekuwa kitovu cha mabadiliko ktk hii nyanja ya democrasia lkn matokeo yake hovyo kabsa watu mna chuo kikuu cha kwanza TZ lkn ni wavivu wa kufikiri wanabaki kuwasufia wabunge wa upinzani kutoka vijijini jaman badilikeni wana daresalaama
 
Wapendwa huyo ndugu cv yake ni nzuri ukilinganisha na wabunge wengine wa ccm kama akina Lusinde wa mtera, au ngonyani wa korogwe na wengine kwa kweli ni shida kubwa. tatizo lingine linaloletelea haya yote ni kwamba mkwanja unatumika sana kwenye chaguzi zetu na kufanya wenye fedha kuingia kwa wingi kwenye chombo hiki nyeti cha maamuzi ya nchi yetu.
 
Leo hii nimehitimu mafunzo yangu ya shahada ya kwanza hakika nina nafasi ya kuwa mkurugenzi ikiwa hawa watu wasiokuwa na sifa wataondolewa wote. taifa linaloamini katika giza linafanya vitu kigizagiza pia.
 
Hizo Diploma zina utata sidhani kama TCU wanazitambua incase unataka kuingia university ila tusimlamu maana tatizo ni wananchi wenyewe ambao wengi wana link kipaji cha mtu / umaarufu na uwezo wa kuongoza pia tatizo lingine ni tume ya uchaguzi/katiba inahitaji sifa moja kuu ambayo ni kujua kusoma na kuandika (in most cases ukiwa STD 7) mengine ni sifa za ziada.

Unaweza kuja Kimbunga na CV yako nzuri tena ukiwa na practical experience nzuri ila kwa kuwa jina lako sio kubwa itakuwia ngumu kupata kura kwa siasa zetu za Tanzania na ndio maana unakuta watu wanaanza kwenye vyama vidogo vidogo na wakati mwingine wanaanzisha mashindano ya mpira na kuyaita kombe la Kimbunga ili mradi jina lake liwemo midomoni mwa watu.

Ifike mahala vyama viangalie uwezo binafsi wa uongozi bila kujali anakubalika vipi kwa jamii ndio maana miaka ya nyuma mtu alikuwa anashinda katika ngazi ya mkoa jina likienda taifa wanaliengua na wakiweka mtu mwingine wanaweka mtu makini.

STD & si hoja ila anatakiwa awe jembe hasa kwa lugha ya sasa maana kuna wengine wanajua issues na mbinu za ku-network na wasomi mbalimbali. (CONCLUSION: Tunatakiwa tubadilishe kipengele cha sifa za mgombea ubunge ili tuwafanye watu wanaokimbilia kwenye siasa wa-activate vichwa vyao kwa kwenda shule vinginevyo mijadala mikubwa ya kisheria na mingine ambayo inatumia general knowledge kama mtu huna shule ya kueleweka itakuwa tabu.

Mkuu nilikuwa na mpango wa kuanzisha kombe la Mbuzi naona sasa nianzishe tu kombe la Kimbunga kutangaza jina ili 2015 nami nijikumbushe siasa.

Mkuu juzi juzi Kenya walijaribu kubadili sifa hasa za kielimu ili wabunge wawe wenye degree lakini kulikuwa na upinzani sijui uliishaje. Unapokuwa na watunga sheria wengi ambao wana sifa za chini usitegemee mabadiliko ya kuwaengua yapate njia nyepesi.
 
Mkuu nilikuwa na mpango wa kuanzisha kombe la Mbuzi naona sasa nianzishe tu kombe la Kimbunga kutangaza jina ili 2015 nami nijikumbushe siasa.

Mkuu juzi juzi Kenya walijaribu kubadili sifa hasa za kielimu ili wabunge wawe wenye degree lakini kulikuwa na upinzani sijui uliishaje. Unapokuwa na watunga sheria wengi ambao wana sifa za chini usitegemee mabadiliko ya kuwaengua yapate njia nyepesi.

Ni kweli Kimbunga maana kuna mijadala kiukweli hata ukiwa umeenda shule bado inahitaji uwe mahiri katika maeneo flani sembuse mtu ambae shuleless. Kuna siku mbunge wa Mbozi (Godfrey Zambi) alikuwa anachangia akasema tatizo mambo mengi yanaandikwa kwa kiingereza lakini tunayajadili kwa kiswahili sijui lini yataandikwa kwa kiswahili, akatoa hoja yake kulikuwa kuna maneno hayaeleweki vizuri, waziri katika kujibu si akawa na kigugumizi kujibu na kusema pamekosewa,ndipo nilipogundua wakti wengine wabunge wanapitisha hoja bila kupingwa bila kuangalia kiundani
 
Last edited by a moderator:
Nch
kwa mujibu wa kanuni za chaguzi za ccm, sifa ya elimu anayotakiwa kuwa nayo mbunge ni elimu ya darasa la saba. Nadhani mjadala ukielekea huko utakuwa na tija zaidi ili kama kuna haja ya kufanya marekebisho basi hoja zijengwe in that context. Vinginevyo kwa mujibu wa kanuni za chaguzi za ccm, mheshimiwa azzan ni mbunge halali kwani per kanuni za chama cha mapinduzi as of today, mgombea akiwa na kiwango cha elimu cha form four, form six, certificate, diploma, degree, n.k, hiyo inachukuliwa kama ni ziada tu na haipewi uzito na vikao vya kupitisha/kuchuja wagombea. Suala la elimu kwa sasa ni suala la wapiga kura mmoja kwa mmoja kuwa na uelewa tu kwamba je, itumike kama kigezo au lah.

Na mara nyingi ukiwa mgombea mwenye elimu kubwa, ni kawaida sana kujengewa fitina kwamba umechakachua au kampeni zako haziwatendei haki wagombea wasio na elimu, au kwamba peleka elimu yako kwingine ukajenge taifa, sio kwenye nafasi ya ubunge kwani mujibu wa kanuni ya ccm, darasa la saba linatosha, na wananchi hawana haja ya kuzingatia kiwango cha elimu kama ni kigezo cha kukuchagua kama mgombea/mbunge. Nadhani mjadala ungeelekezwa zaidi juu ya kanuni hii badala ya kumjadili mh azzan ambae katika mazingira haya, hana hatia na ni mwakilishi halali wa wananchi wa jimbo la kinondoni.
nchi hii haitapata kuendelea kama vilaza wanakaa mbele na wenye akili na ujuzi wanawekwa nyuma yao. Uzoefu wa miaka 50 hamsini umeonesha ni namna gani usawa wa binadamu hauwezi kuendekezwa katika kuendeleza nchi hii. Ni lazima tutoe nafasi wataalamu washike hatamu na watu wenye upeo wa kutosha kufanya maamuzi. Sasa nimeelewa ni kwanini ccm inafanya vituko. Tafsiri mbovu sana ya usawa wa binadamu. Livingstone, jah people, azzan na wengine hawana ubavu wa kupeleka mbele gurudumu la maendeleo ya nchi hii. Kuongoza sio kupiga kelele kuliko wengine au kuhimili kadamnasi . Ccm think twice, we are loosing at the expense of your bogus politics
 
Kilaza mwingine yuko mrogoro mjini. Vyuo vikuu viwili sua na muslim. Lakini abood kamtoa baruti prof wa sua. Sera mbovu za ccm hizi. Hawa umande wamaukimbia lakini wananga'ang'ania nafasi kubwa sijui tuwaeleweje?
 
NyinyiEM wengi ni vilaza wa Darasa la saba na form iv au kama ni prof basi ni wale aliwazungumzia Rev Peter(mb iringa)
akiri zao ni kama za huyu jamaa
 

Attachments

  • 6a0120a5c94e03970b015432ffa442970c-800wi[1].jpeg
    6a0120a5c94e03970b015432ffa442970c-800wi[1].jpeg
    23.1 KB · Views: 367
Watu kama hawa wakiwa bungeni watachangia kama ifuatavyo:
Asante sana mh. spika, kabla ya yote napenda kutoa shukurani zangu za dhati kabisa kwa Mh.W/M, mtukufu Rahisi, wabunge wote wa chama changu, Mwisho shukurani ziende kwa mke wangu, watoto wangu wa kike na wa kiume mmoja anaitwa Mh. Jingine yuke pale Juu hapa katika ukumbi wa Bunge

Baada ya kusema hayo hoja ya waziri ina mapungufu 1,2,3,3..... naunga mkono Hoja 100%.
 
Back
Top Bottom