wanazuoni naomba mchango wenu. pamoja na nia yao pengine nzuri, sina uhakika ,CUF wameonyesha speed kubwa sana ya kudai katiba mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu. pamoja na yote wamekimbilia kumpelekea rasmu ya katiba mtu ambaye wote tunajua hana interest na katiba mpya(Celine dione) na wanadai serikali tatu. Swali hii hi-speed imetoka wapi mwaka huu? Ni kipi walichoona mwaka huu ambacho hawakukiona miaka mingine? Je ni CUF ipi inayodai serikali tatu? ya zanzibar au ya bara? kama ni ya zanzibar wao sera yao ni serikali moja, hilo liko wazi. kama ni ya bara ina maana kuna CUF 2 kwa sababu ya sera tofauti. Naomba CUF zote mbili wanijibu kupitia JF nia siyo mbaya ni kuelimishwa