Haya ndo mapokezi ya Rais Kikwete USA

Wote wanaoonekana kwenye picha ni wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani

Samahani kwa lugha hii lakini ina maana nikisema pole zake kwa "nyani asiyeweza kuona manyoya yaliyvonyonyoka makalioni mwake." Binafsi huwa nasikia aibu kubisha hodi kila siku nyumbani kwa mtu, wengine kama akina kikwete haya zimewatoka.

Kuchokwa ndio huko ambapo unaona hata tu gavana wa jimbo haendi kumpokea ila analakiwa na watanzania. Uzururuaji mwingine ni aibu na atakapomaliza muda wake tutasikia mengi kwa hawa wamarekani. Wamarekani si wa kudeka nao ipo siku watayaanika madudu yake kama walivyomwanika kuhongwa suti huko Uingereza.

Sina shaka kama Kikwete passport yake anahitaji kubadilishiwa kila mwaka maana inajaa haraka kwani makazi yake ni kuzunguka zaidi duniani badala ya kuwatumikia watanzania.
FaizaFoxy anajua maana ndiye anayemwandalia masurufu ya safarini.


 
Baba moja mama moja, hakuna ubishi haupo.....Dah! wanafanana mpaka masikio!

attachment.php

ha ha ha hakuna ubishi hapo.
 
Bibie vipi? Matatizo ya umeme yamemalizika? Kikwete aliahidi kufikia December 2007 mgao wa umeme utakuwa historia.
Mkuu Jasusi, Mwaka 2006 miezi minne tu toka aukwae Uraisi, Col. Dr. Al Haj Jakaya Mrisho Kikwete alitoa ahadi na malengo kadha wa kadha na kuahidi kuyatimiza kwa ari, kasi na nguvu mpya. Akiongea kwenye hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbali mbali wa nje na ndani pamoja na wawekezaji, aliwaahidi wananchi kuwa chini ya miaka mitatu tatizo la umeme lingeshughulikiwa na kubaki historia. Haya hapa ni maneno yake aliyoyatoa kwa lugha ya Kiingereza kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika;
Kikwete said:
We have been grappling with this problem for quite some time now – but only with ad hoc measures.The recent power problems have afforded us the opportunity to rethink our energy strategy in holistic terms. We have learnt that ad hoc measures are costly in the long run and have their own limits. As we grapple with our energy problem, we are witnessing an upsurge of interest for investments in power generation in Tanzania. We are confident that in two years time, we will be on course to realize reliable power supply in Tanzania.
Leo inakaribia miaka kumi toka atoe ahadi yake hiyo, matatizo ya umeme aliyoyakuta yako pale pale, mgao unaendelea kama kawa na kama Katiba itaheshimiwa mwakani tutampata Raisi mpya. Wakati hali halisi ndiyo hiyo, Watanzania walio ugenini nchini kwa watu DMV tunaambiwa wamemtunuku tuzo ya usimamizi na uongozi bora. Surely wonders will never cease!
 
Wadau tusaidiane,hivi kweli sahihi kwa rais kutembelea nchi nyingine na akapokelewa na wananchi wake wanaoishi huko tu?



dc2.jpg

Huu ni upotoshaji. Umejuaje haya yalikuwa ni mapokezi ya rais baada ya kuzuru USA? Je kama ilikuwa ni function fulani ya wa-Tz utajuaje? Pia umejuaje kuwa hao wote ni wa -tz? Au na wewe ulikuwapo huko? Haujaweka sources za ku-support maelezo yako.
 
Huu ni upotoshaji. Umejuaje haya yalikuwa ni mapokezi ya rais baada ya kuzuru USA? Je kama ilikuwa ni function fulani ya wa-Tz utajuaje? Pia umejuaje kuwa hao wote ni wa -tz? Au na wewe ulikuwapo huko? Haujaweka sources za ku-support maelezo yako.

Siurse; CCM BLOG
 
Huu ni upotoshaji. Umejuaje haya yalikuwa ni mapokezi ya rais baada ya kuzuru USA? Je kama ilikuwa ni function fulani ya wa-Tz utajuaje? Pia umejuaje kuwa hao wote ni wa -tz? Au na wewe ulikuwapo huko? Haujaweka sources za ku-support maelezo yako.
Kwani kiongozi mkubwa kama raisi akienda kwenye hiyo unaita function fulani hapati MAPOKEZI? Akienda ofisi ya ubalozi hapati MAPOKEZI? Nyie wenzetu mnalielewaje neno mapokezi?
 
Kwani wewe ni Salary Slip? Nimemwambia yeye kwa vile najua hana kazi yoyote zaidi ya kujipendekeza kwa akina Mbowe

wewe jamaa alivyokwambia kuwa IQ yako ni ndogo, ni ndogo kweli! humu JF ni mawazo huru, unaweza kusoma mawazo ya mtu yeyote na ukatoa maoni yako! yaani wewe ni sawa na Hawa ghasia, asiyejua umuhimu wa elimu!
 
Mkuu, kama ni hivyo mbona wakati wa maraisi Nyerere, Mwinyi na Mkapa hatukuyaona hayo. Umejitahidi tu mkuu kutetea, na kupongeza kwa hilo, chongo kuiita kengeza.

Hapakuwa na Nguvu ya mawasiliano Kama Leo .....katia mguu tu wamedaka clip whatsapp wamerushaa
 
Acheni kupotosha nyie Mburulaz. Hapo Rais Kikwete alikuwa kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na hao anaosalimiana nao ni maafisa ubalozi. Nye mlitaka afuatane na Obama kwenye ubalozi huo?

Wewe ndiyo unapotosha!Obama HAWEZI mpokea JK ANAYEKUJA hapa kila mwezi tena anakaa weeks 2!Yaani nani ana muda wa kupoteza kushinda JFK kumsubiri mtu ambaye USA kama ndiyo nyumbani kwake!

Msafara wake pale AVENUE haukuwa hata na king'ora!dani ya miezi miwili ya siku 60 kaka USA siku 33!!!Rais gani huyu?Anakuja USA siku 12 kabla ya siku yake ya kuhutubia UN!
 
Lakini hizo picha haziwezi kutoa ushahidi wa kuamini kwamba hayo ndio mapokezi. Jamani kuweni wagumu kidogo kuamini mambo kirahisi rahisi hasa kunapokuwa hakuna ushahidi wa kutosha kutoka kwa mtoa habari. Huyu mtoa mada angalau angeleezea kuwa yeye alikuwepo uwanja wa ndege tokea rais anaingia au alielezwa na mtu wa kuaminika, kwamba rais ametua 'airport', hapakuwa na kiongozi yeyote wa USA (hapo picha ingeweza ku-support) ila watanzania wanaoishi huko. Hizo picha alizoweka sio kwamba alishapokelewa, na tayari amesha achana na waliompokea yupo sehemu nyingine?
 
Back
Top Bottom