Haya magazeti yanamuonea Magufuli au ndivyo ilivyo

Kama kuna ushahidi kwamba kweli walibaka watoto wa umri wa miaka sita na nane hilo halisahemeki, labda siku ya hukumu ya Mungu lakini sio ya hapa duniani. Yaani hao ni wa kuozea kwenye jela mpaka wafe. Japo nimesema kama kuna ushahidi, isije kuwa kulikua na kizungumkuti cha kuwaonea hao jamaa. Labda jamaa hawakufanya hicho kitu, iwe kuna mtu aliwacheza na kuwambambikizia, maana nategemea hadi rais afikie kuwapa msamaha lazima usalama wa taifa walichunguza kwa kina.

Kuna makosa ya kusamehe, hata wauaji husamehewa, lakini walawiti wa watoto wadogo, bora ufie jela.
Ukweli kwamba mahakama iliwakuta na hatia ya kubaka hauwezi kupingika wala kubadilishwa. Na ukweli kuwa rais aliwaachia kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na katiba pia hauwezi kubadilishwa. Lakini tukio hili linaunganishwa na ile amri yake ya kufukuza wanafunzi wanaopata ujauzito wakiwa shule. Hapo ndo watetezi wa masuala ya watoto na haki za binadamu wanapima mzani, kumwachia mtu aliyehukumiwa kuwa kabaka halafu unamfukuza shule aliyepata ujauzito; pengine kwa kubakwa pia. Hapa panahitaji busara kweli kweli. Ndiyo maana vyombo vya habari ambavyo huwa sio vya kishilawadu hadi vya ulaya viliandika kuhusu utata huo wa matukio hayo mawili. Kuna chombo kimoja cha kuaminika kutoka huko ulaya niliona wakiandika kuwa MAGUFULI AWAACHIA HURU WABAKAJI WA WATOTO HUKU AKIAMURU WASICHANA WANAOPEWA UJAUZITO WAKIWA SHULE WAFUKUZWE.

Ukiiangalia kauli hii huwezi kulaumu chombo hicho cha habari wala kukiita cha kishilawadu, maana ni kweli aliamuru wasichana wajawazito wafukuzwe shule, babu seya aliachiwa kwa mujibu wa sheria na mahakama ilimuona na hiyo hatia.

Lakini kama ulivyouliza kuhusu ukweli wa kutokea tukio hilo la ubakaji. Naweza kusema babu seya mwenyewe, wanawe na wale watoto wanaodaiwa kubakwa ndio wanaojua ukweli halisi wa hili tukio. Sisi wengine tunaweza kuwa tunasukimwa na emotions tu!

Shida kubwa ni kuwa suala hili linagusa maslahi ya wengi kijamii, kisiasa n.k. Wengi wanadai babu seya alionewa na alisingiziwa kwa sababu binafsi. Ilifikia hatua wakati wa kampeni za uchaguzi 2015 baadhi ya wagombea wakinadi sera zao kupitia suala hili kuwa wakichaguliwa watawaachia huru akina babu seya.


Kutokana na hayo maneno ndo maana mitazamo iko tofauti, na rais naamini kupitia washauri wake na watu wa usalama wamelifanyia kazi suala hilo. Ndo maana hata baada ya hawa jamaa kuachiwa watu wengi walipongeza hatua hiyo, maana wengi ni kama walikuwa wakiisubiri kwa hamu.
 
cha maneno ya unazi, unadhani wazazi wa watoto wanajisikiaje? Angelibakwa mtoto wako, mama yako, dada yako, shangazi ungelijisikiaje? Tafakari pande zote
Kumshukuru Rais aliyewasamehe kifungo mi naona haitoshi, waende kuwaomba msamaha watoto waliowabaka na familia zao. Vinginevyo masononeko yao yataongezeka na sasa watamlilia Mungu, ambapo ni mbaya sana.
 
Uongo mtupu hawana kosa lolote hao hakuna asiyejua viking alikua anatoka na hawara ya mkwere eti familia nzima mpaka katoto cha under 18 kabake mxiiiiuuuu
Una uhakika HAKUNA ASIYEJUA..???? Una hakika hata bibi yangu kijijini alikuwa anajua..???
 
Ukweli kwamba mahakama iliwakuta na hatia ya kubaka hauwezi kupingika wala kubadilishwa. Na ukweli kuwa rais aliwaachia kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na katiba pia hauwezi kubadilishwa. Lakini tukio hili linaunganishwa na ile amri yake ya kufukuza wanafunzi wanaopata ujauzito wakiwa shule. Hapo ndo watetezi wa masuala ya watoto na haki za binadamu wanapima mzani, kumwachia mtu aliyehukumiwa kuwa kabaka halafu unamfukuza shule aliyepata ujauzito; pengine kwa kubakwa pia. Hapa panahitaji busara kweli kweli. Ndiyo maana vyombo vya habari ambavyo huwa sio vya kishilawadu hadi vya ulaya viliandika kuhusu utata huo wa matukio hayo mawili. Kuna chombo kimoja cha kuaminika kutoka huko ulaya niliona wakiandika kuwa MAGUFULI AWAACHIA HURU WABAKAJI WA WATOTO HUKU AKIAMURU WASICHANA WANAOPEWA UJAUZITO WAKIWA SHULE WAFUKUZWE.

Ukiiangalia kauli hii huwezi kulaumu chombo hicho cha habari wala kukiita cha kishilawadu, maana ni kweli aliamuru wasichana wajawazito wafukuzwe shule, babu seya aliachiwa kwa mujibu wa sheria na mahakama ilimuona na hiyo hatia.

Lakini kama ulivyouliza kuhusu ukweli wa kutokea tukio hilo la ubakaji. Naweza kusema babu seya mwenyewe, wanawe na wale watoto wanaodaiwa kubakwa ndio wanaojua ukweli halisi wa hili tukio. Sisi wengine tunaweza kuwa tunasukimwa na emotions tu!

Shida kubwa ni kuwa suala hili linagusa maslahi ya wengi kijamii, kisiasa n.k. Wengi wanadai babu seya alionewa na alisingiziwa kwa sababu binafsi. Ilifikia hatua wakati wa kampeni za uchaguzi 2015 baadhi ya wagombea wakinadi sera zao kupitia suala hili kuwa wakichaguliwa watawaachia huru akina babu seya.


Kutokana na hayo maneno ndo maana mitazamo iko tofauti, na rais naamini kupitia washauri wake na watu wa usalama wamelifanyia kazi suala hilo. Ndo maana hata baada ya hawa jamaa kuachiwa watu wengi walipongeza hatua hiyo, maana wengi ni kama walikuwa wakiisubiri kwa hamu.
Mimi ningependa kujikita katika hili jambo la wanafunzi wanaopata uja uzito wakiwa shuleni, sheria na sera za nchi hii tangu enzi za mwalimu Nyerere ni kwamba mwanafunzi wa kike akipata ujauzito, huo ndiyo mwisho wake, aliyempa ujauzito anapelekwa mahakamani, magufuli anachokifanya ni kuisimamia na kuipo msukumo zaidi, watu wengi wanadhani ameitunga au ameianzisha Magufuli, sio kweli hata kidogo.

Mashirika mbalimbali yanayotetea haki za watoto wa kike ambayo yanaona sheria hii haifai au imepitwa na wakati, yanapaswa kuanza kufanya lobbying ili iweze kubadilishwa badala ya kumlaumu Magufuli anayesimamia sheria tuliojiwekea sisi wenyewe.

Mjadala huu ulifika Bungeni na walio wengi walikataa kuwaruhusu wajawazito kuendelea na masomo katika shule za serikali, ila wanaweza kupitia njia mbadala ya kujiendeleza waweze kufikia azma yao hiyo, jambo ambalo kwakweli hata mimi ninaliunga mkono.

Sent from my MediaPad T1 8.0 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo serikali ya jk iliamua kuukaa kimya wakati ule uvumi wa uongo ukienea na kujikita vichwani mwa watu,
kumbe watu wenyewe wamefungwa kabla jk hajawa rais,

lakini katiba inampa mamlaka rais ya kumsamehe yeyote,
amesukumwa na nini kusamehe ndo swali kubwa la kujiuliza,maana ishu ya kubaka watoto ndo dhambi kubwa hasa maana maisha ya wale watoto yalishaharibiwa
 
..kama wameonewa basi kuachiwa tu haitoshi, wanastahili KULIPWA.

..Lakini kama walilawiti watoto na hukumu yao ni ya haki, basi hawakustahili kuachiwa baada ya kutumikia kifungo kwa miaka 13 tu.

..swali ninalojiuliza ni kwanini watawala WANAWAFARIJI na KUWAHURUMIA wahukumiwa wa ubakaji kuliko victims wao?

..Kwenye nchi za wenzetu ktk majira ya sikukuu kama hizi head of state huonana na watu wenye shida mfano watoto yatima, wenye ulemavu, etc. Siyo kuonana na watu waliopatikana na hatia ya kulawiti watoto.

..Kwa maoni yangu hii ni AIBU kwa nchi yetu. This is not something I would feel comfortable to tell my friends who are overseas about my country.

Cc MK254
 
Kutokana na kesi ilivyoenda na baadae rufaa ilivyosikilizwa, inaonyesha kweli hawa watu walitenda kosa, kwani hata Mabere Marandu ambaye ndiye aliyekuwa wakili wao alionyesha kwamba kesi iliamuliwa kwa halali kabisa.

Katiba ya Tanzania, inampa madaraka rais kumsamehe mtu yeyote aliyefanya kosa lolote lile, kwa jinsi busara zake zinavyomuelekeza, haya ni madaraka makubwa sana kumuachia mtu mmoja awe nayo, katika vipengele ambavyo ningependa siku moja kirekebishwa ni hiki, japo kianze na neno"kwa kushauriana, au kwa kuwadhirikisha.....".

Kwamba kuwasamehe wabaki ni mbaya zaidi kuliko mtu aliyeua mtu au watu kwa makusudi, hilo sikubaliani nalo, japo kubaka ni kubaya, lakini kukatisha uhai wa mtu ni jambo baya zaidi mtu unaweza kumtendea, kwa mfano ikitolewa option gerezani kwa wafungwa waliohukumiwa kifo wachague kati ya kunyongwa au wabakwe na kunajisiwa na kisha kuachiliwa huru, unahisi wengi watachagua lipi?, naomba kuwakilisha
Mkuu Rais ni taasisi wala si mtu mmoja!! Ukisikia wanasema Rais elewa ni taasisi wala si mtu mmoja!!
 
Ukweli kwamba mahakama iliwakuta na hatia ya kubaka hauwezi kupingika wala kubadilishwa. Na ukweli kuwa rais aliwaachia kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na katiba pia hauwezi kubadilishwa. Lakini tukio hili linaunganishwa na ile amri yake ya kufukuza wanafunzi wanaopata ujauzito wakiwa shule. Hapo ndo watetezi wa masuala ya watoto na haki za binadamu wanapima mzani, kumwachia mtu aliyehukumiwa kuwa kabaka halafu unamfukuza shule aliyepata ujauzito; pengine kwa kubakwa pia. Hapa panahitaji busara kweli kweli. Ndiyo maana vyombo vya habari ambavyo huwa sio vya kishilawadu hadi vya ulaya viliandika kuhusu utata huo wa matukio hayo mawili. Kuna chombo kimoja cha kuaminika kutoka huko ulaya niliona wakiandika kuwa MAGUFULI AWAACHIA HURU WABAKAJI WA WATOTO HUKU AKIAMURU WASICHANA WANAOPEWA UJAUZITO WAKIWA SHULE WAFUKUZWE.

Ukiiangalia kauli hii huwezi kulaumu chombo hicho cha habari wala kukiita cha kishilawadu, maana ni kweli aliamuru wasichana wajawazito wafukuzwe shule, babu seya aliachiwa kwa mujibu wa sheria na mahakama ilimuona na hiyo hatia.

Lakini kama ulivyouliza kuhusu ukweli wa kutokea tukio hilo la ubakaji. Naweza kusema babu seya mwenyewe, wanawe na wale watoto wanaodaiwa kubakwa ndio wanaojua ukweli halisi wa hili tukio. Sisi wengine tunaweza kuwa tunasukimwa na emotions tu!

Shida kubwa ni kuwa suala hili linagusa maslahi ya wengi kijamii, kisiasa n.k. Wengi wanadai babu seya alionewa na alisingiziwa kwa sababu binafsi. Ilifikia hatua wakati wa kampeni za uchaguzi 2015 baadhi ya wagombea wakinadi sera zao kupitia suala hili kuwa wakichaguliwa watawaachia huru akina babu seya.


Kutokana na hayo maneno ndo maana mitazamo iko tofauti, na rais naamini kupitia washauri wake na watu wa usalama wamelifanyia kazi suala hilo. Ndo maana hata baada ya hawa jamaa kuachiwa watu wengi walipongeza hatua hiyo, maana wengi ni kama walikuwa wakiisubiri kwa hamu.

Ulivyoiweka inakaa PR lakini pia umeiacha kiaina, kwanza neno mnalotumia la 'kubaka' hilo ni PR, maana kosa lilikua la kulawiti watoto. Ambalo ni mbovu sana hata zaidi ya kuua mtu, maana hao watoto kuanzia hapo waliishi maisha ya kizombi ni kama waliouawa tu.

Kuna jinsi mnaizungusha ili ionekane kama ni kosa la kubaka (rape) ya watu waliobalehe ambalo halina uzito kama kulawiti watoto wa miaka sita na nane.
Anayway kuna kitu kimoja nakubaliana na wewe, kwa rais kufikia uamuzi wa kuwaachia huru hawa, lazima kuna uchunguzi wa maafisa wa usalama walihusika pakubwa na kupata ukweli kindani ndani. Maana sioni jinsi rais anaweza kujitoa ufahamu na kuwaachia huru walawiti wa watoto waliohukumuwa na mahakama baada ya ushahidi kudhihirisha matendo yao.
 
Gazeti limeandika na kuanika kwenye kichwa cha habari kwamba Magufuli akutana ikulu na wabakaji wa watoto walioachiwa kutoka kwenye magereza. Hivi hawa jamaa walibaka hao watoto wa umri wa miaka sita au ilikua uonevu, na kama kweli walibaka, nini kilipelekea hadi wakapewa msamaha wa rais na kualikwa ikulu.

Taarifa kama hizi ningezipuuza kama zingeangazwa na yale magazeti ya Kishilawadu, lakini hili la The East African huwa naliheshimu, sijaelewa mbona watumiea maneno makali hivi kumuanika rais wa Tanzania.
----------------------------------------------------------------------

NGUZA.jpg


The Nguzas and President John Magufuli (centre) at State House Dar es Salaam on January 2, 2018. PHOTO | NMG

Tanzania’s President John Magufuli on Tuesday met with two musicians, who had been serving life sentences for raping girls, at State House in Dar es Salaam.

Viking Nguza and his son Johnson Nguza had paid a call to the President to thank him for granting them clemency.

The two singers were among 61 convicts who were pardoned by the President during Tanzania’s Independence day fete on December 9, 2017.

They had spent 13 years behind bars for raping 10 primary school girls, aged between six and eight years, in 2003. Viking, popularly known as Babu Seya and Johnson (Papii Kocha) were convicted of the crimes in June 25, 2004 and sentenced to life in jail.

While visiting with President Magufuli, the Nguzas pledged to be good citizens.

"Since we were released we wanted to meet you so that we could thank you in person and today it is a dream come true," Babu Seya told the President.

“I thank you so much for forgiveness and now I am ready to work hard,” he added.

On his part, the President thanked the Nguza family for paying him a visit. The two had been accompanied by two other family members, Francis Nguza and Nguza Mbangu.
“You shouldn’t thank me rather you should thank God, who is the only one with the power to forgive,” the President told them.
“Now you have to work hard and follow God,” he said.

The release of the Nguzas has been condemned by children rights activists.

Magufuli meets pardoned child rapists
Mtoa mada mbona hueleweki? Huamini kama walibaka? Au huziamini mahakama zetu? Au ulitaka gazeti liandikeje?
 
..kama wameonewa basi kuachiwa tu haitoshi, wanastahili KULIPWA.

..Lakini kama walilawiti watoto na hukumu yao ni ya haki, basi hawakustahili kuachiwa baada ya kutumikia kifungo kwa miaka 13 tu.

..swali ninalojiuliza ni kwanini watawala WANAWAFARIJI na KUWAHURUMIA wahukumiwa wa ubakaji kuliko victims wao?

..Kwenye nchi za wenzetu ktk majira ya sikukuu kama hizi head of state huonana na watu wenye shida mfano watoto yatima, wenye ulemavu, etc. Siyo kuonana na watu waliopatikana na hatia ya kulawiti watoto.

..Kwa maoni yangu hii ni AIBU kwa nchi yetu. This is not something I would feel comfortable to tell my friends who are overseas about my country.

Cc MK254
Mkuu siyo kila kitu tutakuwa sawa duniani kote ndiyo maana huko wazungu wanaruhusu ndoa za jinsi moja wakati huku ni aibu kubwa kwenye familia. Kuna uwezekano huko hawasamehi wafungwa kama unavyodai lakini sisi tunasamehe hata kwenye vitabu vya Mungu vimeandikwa tusamehe! Hapo hapo vitabu vya Mungu vinakataza ndoa za jinsia moja lakini hao unao waamini wazungu wakafanya kinyume chake hivyo siyo kila wafanyacho wazungu tuige au ni kizuri sana!!
 
Daah hili jambo ni gumu sana. Upande mmoja unaangalia upande wa wazazi wa watoto, upande wa pili ni huruma kwa watuhumiwa ukizingatia walishasota 13 years japo walitakiwa wasote maisha. Upande wa tatu ni wafungwa wengine waliona hukumu kama ya vikings Et al lakini watafia jela
 
Gazeti limeandika na kuanika kwenye kichwa cha habari kwamba Magufuli akutana ikulu na wabakaji wa watoto walioachiwa kutoka kwenye magereza. Hivi hawa jamaa walibaka hao watoto wa umri wa miaka sita au ilikua uonevu, na kama kweli walibaka, nini kilipelekea hadi wakapewa msamaha wa rais na kualikwa ikulu.

Taarifa kama hizi ningezipuuza kama zingeangazwa na yale magazeti ya Kishilawadu, lakini hili la The East African huwa naliheshimu, sijaelewa mbona watumiea maneno makali hivi kumuanika rais wa Tanzania.
----------------------------------------------------------------------

NGUZA.jpg


The Nguzas and President John Magufuli (centre) at State House Dar es Salaam on January 2, 2018. PHOTO | NMG

Tanzania’s President John Magufuli on Tuesday met with two musicians, who had been serving life sentences for raping girls, at State House in Dar es Salaam.

Viking Nguza and his son Johnson Nguza had paid a call to the President to thank him for granting them clemency.

The two singers were among 61 convicts who were pardoned by the President during Tanzania’s Independence day fete on December 9, 2017.

They had spent 13 years behind bars for raping 10 primary school girls, aged between six and eight years, in 2003. Viking, popularly known as Babu Seya and Johnson (Papii Kocha) were convicted of the crimes in June 25, 2004 and sentenced to life in jail.

While visiting with President Magufuli, the Nguzas pledged to be good citizens.

"Since we were released we wanted to meet you so that we could thank you in person and today it is a dream come true," Babu Seya told the President.

“I thank you so much for forgiveness and now I am ready to work hard,” he added.

On his part, the President thanked the Nguza family for paying him a visit. The two had been accompanied by two other family members, Francis Nguza and Nguza Mbangu.
“You shouldn’t thank me rather you should thank God, who is the only one with the power to forgive,” the President told them.
“Now you have to work hard and follow God,” he said.

The release of the Nguzas has been condemned by children rights activists.

Magufuli meets pardoned child rapists
Ww mkenya angalia ya nchi yako,ya nchi yetu tuachie wenyewe hayakuhusu.
 
Hili jambo nimelitafakari mwisho wa siku nikajikuta naikumbuka hadithi moja ya kwenye bibilia

kwamba kuna bwana mmoja alikua akitafakari sana juu ya ufalme wa mbinguni huku akitembea kandokando mwa bahari....

mbeleni akakutana na mtoto amechimba shimo dogo alafu anachota maji kutoka baharini anayaweka kwenye hilo shimo

alipomuuliza unafanya nini...dogo akamjibu nataka nichote hayo maji yote niyaweke kwenye hili shimo....jamaa akapagawa.

Kama jk alikaa kimya, jpm kawasamehe....kuna jambo kubwa nyuma yake na sitegemei kama kizazi hiki tutakuja kujua labda vitukuu vyetu na wachache watakao kuwepo basi wawalishe matango madogo kwamba wanafahamu kilichotokea ilhali nao ni sehemu yetu humu tunao jitafutia majibu wenyewe lakini uhalisia unatushinda kujiaminisha.

Namuelewa sana jk anavyosema hakuna kazi ngumu kama uraisi....siamini kila maamuzi ni matakwa ya raisi ingawa zigo kasukumiwa yeye.
 
Kama kuna ushahidi kwamba kweli walibaka watoto wa umri wa miaka sita na nane hilo halisahemeki, labda siku ya hukumu ya Mungu lakini sio ya hapa duniani. Yaani hao ni wa kuozea kwenye jela mpaka wafe. Japo nimesema kama kuna ushahidi, isije kuwa kulikua na kizungumkuti cha kuwaonea hao jamaa. Labda jamaa hawakufanya hicho kitu, iwe kuna mtu aliwacheza na kuwambambikizia, maana nategemea hadi rais afikie kuwapa msamaha lazima usalama wa taifa walichunguza kwa kina.

Kuna makosa ya kusamehe, hata wauaji husamehewa, lakini walawiti wa watoto wadogo, bora ufie jela.
Mimi bado napingana na adhabu ya kifo na ya maisha jela. Mimi ni MTU wa kuangalia kisababishi cha MTU kutenda kosa,binadamu ubadilika kulingana na MTU na mazingira, anaweza Leo katenda kosa akahukumiwa,akijutia kosa La na kubadilika na kuwa MTU mwema ni vyema akasamehewa kwa kupunguziwa adhabu akifika level ya kuwa mwema zaidi,aachiwe haijalishi kapewa adhabu ipi. Ila akiachiwa akarudia kosa hilo hilo au lifananalo na hilo ni haki yake kupewa adhabu kubwa,maana inakua ni hulka.
 
Mimi ningependa kujikita katika hili jambo la wanafunzi wanaopata uja uzito wakiwa shuleni, sheria na sera za nchi hii tangu enzi za mwalimu Nyerere ni kwamba mwanafunzi wa kike akipata ujauzito, huo ndiyo mwisho wake, aliyempa ujauzito anapelekwa mahakamani, magufuli anachokifanya ni kuisimamia na kuipo msukumo zaidi, watu wengi wanadhani ameitunga au ameianzisha Magufuli, sio kweli hata kidogo.

Mashirika mbalimbali yanayotetea haki za watoto wa kike ambayo yanaona sheria hii haifai au imepitwa na wakati, yanapaswa kuanza kufanya lobbying ili iweze kubadilishwa badala ya kumlaumu Magufuli anayesimamia sheria tuliojiwekea sisi wenyewe.

Mjadala huu ulifika Bungeni na walio wengi walikataa kuwaruhusu wajawazito kuendelea na masomo katika shule za serikali, ila wanaweza kupitia njia mbadala ya kujiendeleza waweze kufikia azma yao hiyo, jambo ambalo kwakweli hata mimi ninaliunga mkono.

Sent from my MediaPad T1 8.0 using JamiiForums mobile app
Uko sahihi kabisa, na hili suala tumeliongelea sana kwenye jukwaa hili, uzi naona uko mbali nilitaka niuweke hapa.
 
Mkuu siyo kila kitu tutakuwa sawa duniani kote ndiyo maana huko wazungu wanaruhusu ndoa za jinsi moja wakati huku ni aibu kubwa kwenye familia. Kuna uwezekano huko hawasamehi wafungwa kama unavyodai lakini sisi tunasamehe hata kwenye vitabu vya Mungu vimeandikwa tusamehe! Hapo hapo vitabu vya Mungu vinakataza ndoa za jinsia moja lakini hao unao waamini wazungu wakafanya kinyume chake hivyo siyo kila wafanyacho wazungu tuige au ni kizuri sana!!

..sasa kwa kitendo hiki unaweza kusema kuwa Tz tunapinga mambo ya ulawiti?

..kama watu waliopatikana na hukumu ya kunajisi watoto wanakaribishwa eneo lenye heshima kuliko yote ktk nchi yetu tunajenga taswira gani?

..kwanini tunawahurumia, kuwafariji, na kuwatukuza watu hawa?

Cc MK254
 
Back
Top Bottom