Hawamnyoshei Kidole Kikwete? - Alichoahidi Hotuba ya kwanza Bungeni 2005

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Hotuba yake kwa Wabunge wale wale ambao miaka sita baadaye wameamua kumgeukia Ngeleja; Wabunge wanaosahau kuwa Kikwete huyo huyo ndiye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini na hawakumkoromea hivi.. well.. kama kweli watu wamekasirishwa na tatizo la umeme mtu sahihi siyo Waziri Mkuu wala Waziri wa Nishati ni Rais.. na chama chake...

Nishati
Mheshimiwa Spika:
Nishati ni sawa na chembe za damu mwilini. Tutapanua wigo na aina ya vyanzo vya umeme na nishati kwa jumla ili kuwa na nishati ya kutosha na yenye gharama nafuu kukidhi mahitaji ya uzalishaji viwandani, utoaji wa huduma za kijamii, na matumizi ya nyumbani.

Tutayashughulikia kwa kipaumbele cha juu matatizo ya sasa yahusuyo upatikanaji wa umeme nchini.

Mheshimiwa Spika:
Ilani ya CCM ya Uchaguzi wa Oktoba 2005 inasema wazi kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itaharakisha mradi wa kupata umeme kutoka makaa ya mawe ya Mchuchuma.

Na hivyo ndivyo tutakavyofanya. Aidha, Serikali ya Awamu ya Nne itafufua mipango ya umeme wa Mto Rusumo na Stigler's Gorge.

Vile vile tutaharakisha upatikanaji wa umeme kutoka gesi asilia ya Mnazi Bay.

Mheshimiwa Spika:
Lengo la Serikali ya Awamu ya Nne pia ni kuendeleza kazi ya kufikisha umeme katika miji mikuu ya wilaya isiyo na umeme hivi sasa, kuongeza kasi ya kupeleka umeme vijijini kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini, na kuiunganisha Mikoa ya Kigoma na Ruvuma katika gridi ya Taifa.
 
Nakunga mkono M. Mwanakijiji, haiwezekeni amfuko atoboe mwenye nguo halafu alaumiwe alie azimwa nguo. Jk ndio wa kusulubiwa si Ngeleja, Ngeleja amewekwa hapo kwa faida ya wachache ikiwemo aliyemrudisha hapo kwa vipindi 2 mfululuzo.
 
thnks MMJ

stori zinakuwa zilezile na mibunge yetu sijui ikoje kazi yao kuunga mkono mkona agrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Magwanda wanashangaza kweli kweli, hivi nyinyi kimewashinda nini kuonesha mfano? wakati sasa ni soko huru? na mnao mafariki wanaowatembelea kama kile chama cha kikristo cha ujerumani, hivi mnashindwa kuongea nao wawakopeshe majenereta ya umeme muoneshe mfano?
 
Hotuba yake kwa Wabunge wale wale ambao miaka sita baadaye wameamua kumgeukia Ngeleja; Wabunge wanaosahau kuwa Kikwete huyo huyo ndiye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini na hawakumkoromea hivi.. well.. kama kweli watu wamekasirishwa na tatizo la umeme mtu sahihi siyo Waziri Mkuu wala Waziri wa Nishati ni Rais.. na chama chake...
Umefunga mjadala wooote. Mwenye macho haambiwi tazama...
 
Back
Top Bottom