sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Hali ya nchi ni tete,ni tete kwa kuwa tu mhimili wa bunge umeshindwa kuisimamia serikali kama katiba inavyozungumza kwenye ibara ya 63 (2) inayosema bunge ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka,kwa niaba ya wananchi,kuisimamia na kuishauri serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu ya katiba hii. Leo hii bunge hili lililopewa meno kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano linakiuka kwa makusudi majukumu yake kwa kuwa tu kiongozi wa bunge ambaye ni Spika ana toka chama tawala cha CCM.Bunge hili limekuwa chombo cha kukandamiza demokrasia kwa vyama vyenye wabunge wachache bungeni. Ukiwa na bunge kama hili,ufisadi ndani ya serikali hutamalaki na bunge kugeuzwa sehemu ya mipasho ama kupoteza dira na mwelekeo wa bunge.Tumeona mambo mengi yanayotokea ndani ya mjengo huo kiasi cha kupelekea serikali kuwasahau wapiga kura wake kwa kuwa tu kuna watu wamejazana ndani ya bunge kwa maslahi ya kupitisha bajeti za kifisadi na mambo ovyo ovyo yasiyo na tija kwa wananchi. Kuna tofauti gani kati ya bunge letu na ze comedy,japokuwa ze comedy kazi yao ni kutufurahisha na kutuburudisha.Inawezekanaje kwa bunge makini na wabunge wake kuunga hoja asilimia mia moja,lakini ndani ya mchango wake unaikataa bajeti.Ukifika wakati wa kupiga kura kupitisha bajeti hiyo kinachongaliwa maslahi ya chama. Niliwahi kusema ni bora wananchi tutafute kanuni ambayo itatuwezesha kupiga kura ya kutokuwa na imani na bunge hili kwa kushindwa kutuwakilisha vema kwa maslahi ya taifa letu.Leo hii waziri mkuu ana thubutu kusema wameshazungumza na mihimili mingine,mahakama na bunge.Nini maana ya mazungumzo hayokama si serikali kutoa maagizo na kuingilia madaraka ya mihimili inayojitegemea . Hali kama hii inaleta picha halisi ni jinsi gani serikali inatumia mihimili hii katika kubaka demokrasia.Uzembe unaonyeshwa na bunge ni chanzo kikubwa cha kuwa na serikali dhaifu isiyo jali hali za wananchi wake.Hali hii imesababisha serikali kutokuwa makini pamoja na interejensia yake kupitia vyombo vyake vya usalama kushindwa kudhibiti matukio ya uvunjifu wa amani ndani ya taifa letu. Tusitegemee hata siku moja bunge hili la CCM litakuja kusimamisha shilingi kwa maslahi ya wananchi na bunge kuvunjwa ili kuitisha uchaguzi.Hali kama hii ndiyo inapelekea wabunge toka CCM kuwa mavuvuzela ndani ya bunge kwa kuhofia kutokurudi au kushughulikiana ndani ya chama. Ukweli utabaki kuwa ukweli,ila cha msingi tusifanye makosa kewnye kutoa maoni yatakayo pelekea kupata katiba yenye meno na itayotanguliza Tanzania na wananchi wake kwanza.Bunge hili chofu linaingia kwenye Guinness book of record kwa kuwa bunge lililoshindwa kuisimamia serikali na linaloridhia uuzwaji wa taifa letu kwa gharama ya bure.Ni heri na Sultani Mangungo amabye hakuwa na elimu kuliko bunge letu lilivyo kwa sasa. Napenda kuwakaribisha wana JF tushirikiane kuangalia ni sheria ipi au kanuni itakayo tuwezesha kupiga kura ya kutokuwa na imani na bunge hili.Mungu inusuru Tanzania yetu.