X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Mirungi au kama inavyojulikana kama Qaat au Qaadka huko Somalia, na Yemen huitwa au Al-Qaat; ingawa kwa matamshi ya huko hutamkwa 'Gaat'.
Kadhalika Kenya kulingana na miji yake hujulikana kama; Miraa, Veve, Kijiti, Gomba n.k., na...
Tanzania ni maarufu kwa majina; Mirungi, Gomba, Gati, Miti, Majani, Miraa n.k.
Mirungi au (Catha edulis) Ni mmea au mti unaoota au kuoteshwa kwa wingi sana huko Ethiopia, Yemen na Kenya.
Jani hilo ambalo Wataalam wameeleza kuwa ni halifahi kutafuna kama tutakavyoona mbele ya makala hii, ni jani lenye madhara mengi katika siha ya mwanadam na lenye kusababisha mengi katika madhara na maangamizi ya kimaadili na kijamii.
Matumizi ya mmea huo ambao hakika kwa masikitiko makubwa, yameenea zaidi katika jamii zetu na haswa maeneo ya mijini na zaidi kwa wanaojulikana kama ‘Waswahili.'
Ingawa neno ‘Waswahili' asli yake ni neno la Kiarabu 'Saahil' pwani, mwambao na 'Saahiliy' -ya pwani, au mkaazi wa pwani au mwambao, ila neno hilo au jina hilo hivi sasa limegeuka kimatumizi na kuashiria zaidi kwa wale watu zaidi wa mtaani, wasiopenda kutumika; kufanya kazi, wasio wakweli, wapenda starehe, wasio na elimu, wazembe n.k.
Kwa wasio Waislam wao wanatumia jina hilo kuwaita nalo Waislam, na zaidi wakikusudia sifa hizo tulizozitaja hapo nyuma. Na kadhalika Waislam kadhaa huwaita wenzao hivyo wakimaanisha, wasio na ahadi, wasemao uongo, wasioaminika, wajanja wajanja, wajuaji, na wenye maneno mengi wasioshindika.
Mirungi inakusanya ndani yake alkaloid iitwayo cathinone, amphetamine kama kichangamsho (stimulant) ambayo inasemekana husababisha msisimko, uchangamfu, kuwa na aina ya furaha ya kuwazika –kuhandasika- na huondosha hamu ya kula na kusababisha ukosefu wa usingizi.
Mnamo mwaka 1980 WHO (Shirika la Afya Duniani) liliiweka Mirungi katika fungu la madawa ya kulevya ambayo inasababisha nafsi kutawaliwa nayo au kuwa na uraibu (addiction) kwa daraja ya kati hadi ile yenye nguvu.
Mti huo umekuwa ukiandamwa na mashirika yenye kupinga madawa ya kulevya kama shirika liitwalo DEA (Drug Enforcement Administration).
Shirika hilo katika mwaka 2006 Julai tarehe 26, shirika hilo katika operesheni iliyokuwa ikijulikana kama 'Somalia Express' ambayo katika upelelezi wake uliodumu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu ambao ulihusisha wanachama 44 wa kundi lililokuwa likisafirisha tani 25 za Mirungi ambazo zilikuwa na thamani ya Dola milioni 10 za Kimarekani kutoka Somalia kupelekwa Marekani. Shitaka (Kosa) hilo lilihusisha utoroshaji mkubwa kabisa wa Mirungi katika Historia ya Marekani.
Biashara hiyo ambayo imeshamiri nchi za Afrika Mashariki ambapo hivi sasa Tanzania imepigwa marufuku, na pia kuenea katika nchi za Ulaya na Marekani.
Kadhalika Kenya kulingana na miji yake hujulikana kama; Miraa, Veve, Kijiti, Gomba n.k., na...
Tanzania ni maarufu kwa majina; Mirungi, Gomba, Gati, Miti, Majani, Miraa n.k.
Mirungi au (Catha edulis) Ni mmea au mti unaoota au kuoteshwa kwa wingi sana huko Ethiopia, Yemen na Kenya.
Jani hilo ambalo Wataalam wameeleza kuwa ni halifahi kutafuna kama tutakavyoona mbele ya makala hii, ni jani lenye madhara mengi katika siha ya mwanadam na lenye kusababisha mengi katika madhara na maangamizi ya kimaadili na kijamii.
Matumizi ya mmea huo ambao hakika kwa masikitiko makubwa, yameenea zaidi katika jamii zetu na haswa maeneo ya mijini na zaidi kwa wanaojulikana kama ‘Waswahili.'
Ingawa neno ‘Waswahili' asli yake ni neno la Kiarabu 'Saahil' pwani, mwambao na 'Saahiliy' -ya pwani, au mkaazi wa pwani au mwambao, ila neno hilo au jina hilo hivi sasa limegeuka kimatumizi na kuashiria zaidi kwa wale watu zaidi wa mtaani, wasiopenda kutumika; kufanya kazi, wasio wakweli, wapenda starehe, wasio na elimu, wazembe n.k.
Kwa wasio Waislam wao wanatumia jina hilo kuwaita nalo Waislam, na zaidi wakikusudia sifa hizo tulizozitaja hapo nyuma. Na kadhalika Waislam kadhaa huwaita wenzao hivyo wakimaanisha, wasio na ahadi, wasemao uongo, wasioaminika, wajanja wajanja, wajuaji, na wenye maneno mengi wasioshindika.
Mirungi inakusanya ndani yake alkaloid iitwayo cathinone, amphetamine kama kichangamsho (stimulant) ambayo inasemekana husababisha msisimko, uchangamfu, kuwa na aina ya furaha ya kuwazika –kuhandasika- na huondosha hamu ya kula na kusababisha ukosefu wa usingizi.
Mnamo mwaka 1980 WHO (Shirika la Afya Duniani) liliiweka Mirungi katika fungu la madawa ya kulevya ambayo inasababisha nafsi kutawaliwa nayo au kuwa na uraibu (addiction) kwa daraja ya kati hadi ile yenye nguvu.
Mti huo umekuwa ukiandamwa na mashirika yenye kupinga madawa ya kulevya kama shirika liitwalo DEA (Drug Enforcement Administration).
Shirika hilo katika mwaka 2006 Julai tarehe 26, shirika hilo katika operesheni iliyokuwa ikijulikana kama 'Somalia Express' ambayo katika upelelezi wake uliodumu kwa muda wa mwaka mmoja na nusu ambao ulihusisha wanachama 44 wa kundi lililokuwa likisafirisha tani 25 za Mirungi ambazo zilikuwa na thamani ya Dola milioni 10 za Kimarekani kutoka Somalia kupelekwa Marekani. Shitaka (Kosa) hilo lilihusisha utoroshaji mkubwa kabisa wa Mirungi katika Historia ya Marekani.
Biashara hiyo ambayo imeshamiri nchi za Afrika Mashariki ambapo hivi sasa Tanzania imepigwa marufuku, na pia kuenea katika nchi za Ulaya na Marekani.