Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 118,415
- 219,851
Mungu akuongezee palipopungua mkuu.Safi sana, nachangia sasa hivi na naomba na huku kwetu Rock City tufanye mambo ili haya mashetwani maccm yakafie mbele
Mungu akuongezee palipopungua mkuu.Safi sana, nachangia sasa hivi na naomba na huku kwetu Rock City tufanye mambo ili haya mashetwani maccm yakafie mbele
mjomba nimejikuta tu nachukua simu yangu na kuchangia mihela , asante kwa picha nzuri hasa hiyo ya kwanza .
mjomba nimejikuta tu nachukua simu yangu na kuchangia mihela , asante kwa picha nzuri hasa hiyo ya kwanza .
Dhamira njema husukuma mambo mema kutokea. Dhamira njema huungwa mkono na wote wenye nia njema. Dhamira njema husababisha mtu kutenda kwa ubunifu na udhati wenye kumaanisha bila kukata tamaa kwa yale yaliyo katika mipango kufikia uhalisia. Dhamira njema haizuiliwi. Dhamira njema ni wazo la Mungu na ndio mpango halisi wa Mungu.
CHADEMA Kanda ya Kaskazini ni dhamira yetu kushinda UCHAGUZI MKUU MWAKA 2015.. Mwaka 2015, ni mwaka wa Kazi.. Tumedhamiria kushinda.. Hatutazuiliwa.. Hatutaki Fedha wala jambo lolote liwe kikwazo cha Dhamira hii njema ambayo Watanzania wanaisubiria ili 1 Novemba 2015 Watanzania wapate sherehe mpya ya Uhuru wa Tanzania..
Tunakuomba ICHANGIE CHADEMA KANDA YA KASKAZINI, ili tufikie dhamira hii. Changia kiasi chochote kuanzia Tshs 500, Tshs 1,000, Tshs 2,000, Tshs 5,000, Tshs 10,000 na kuendelea ambayo utaitoa kila MWEZI HADI KUFIKA OKTOBA 2015 au kila muda (WIKI MOJA au WIKI MBILI) ambao Dhamira yako njema ya kuchangia itakusukuma. Kwa wingi wetu tutaweza kufanya mambo makubwa kwa udhati wenye kumaanisha bila kukata tamaa.
Kwa uhakika, kila mchangiaji atapata fursa ya kujua kile alichochangia kimefanya nini na matokeo yake nini..
Asante kwa Sadaka yako ya Ukombozi....!!
Amani Golugwa
Katibu - CHADEMA KANDA YA KASKAZINI
golugwa@gmail.com
+255 784 343 275
Arusha.
www.chademakandakaskazini.blogspot.com
***************************************************************************************
Jinsi ya kuchangia Chadema Kanda ya Kaskazini
Kwa M-Pesa
1. Piga *150*00#
2. Chagua Kipengele 4-Lipa kwa Mpesa
3. Chagua Namba 4
4. Ingiza namba ya kampuni (213040)
5. Ingiza namba ya kumbukumbu (KAS)
6. Ingiza kiasi Tshs XXXX
7. Ingiza namba ya SIRI XXXX
8. Bonyeza 1 kuhakiki
9. Utapokea ujumbe wa SMS Imethibitishwa kiasi XXX.
imetumwa kwa PAYLINKSYSTEMLIMITED
kwenye akaunti namba KAS
Kwa maelezo zaidi piga 0759 282850 (Katibu wa Kanda)
Fedha za Sabodo zimeliwa tena mnaanzisha njia nyingine ya kuwaibia watanzania , sasa tumechoka , nendeni mkawadanganye huko msituni hatutaki.
CHADEMA kila wakati michango lakini manufaa ya michango ni kuwanufaisha wachache sasa tumestuka tafuteni chaka jingine hapa hakuna nini wala nini ni wizi mtupu.
hiyo kitu ingekaa kitaifa ingekuwa vizuri sana kuliko hivyo mlivyoweka. na mwisho wa siku mkubali kukaguliwa matumizi ya hizo fedha kwa manufaa ya chama na umma
Pesa inaingia moja kwa moja kwa katibu wa kanda....unategemea nini hapo?
Kila siku cdm inachangisha. Hizo niharakati gani za kuchangisha miaka 22 bado mnachangisha au mmepata poli munajenga nchi yenu?
mjomba nimejikuta tu nachukua simu yangu na kuchangia mihela , asante kwa picha nzuri hasa hiyo ya kwanza .
Wew acha ushamba yaan kutoka kyela huko unataka kuchangia Saccos .ya wachaga unaniangusha eryth...
Acheni usanii nyie watu wameishawashtukia.