singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,532
Ubadhirifu wa fedha chadema mpaka sabodo kawakimbia
Ubadhirifu wa fedha chadema mpaka sabodo kawakimbia
Mwongozo: nataka kuchanga ila ikifika hatua ya namba ya kumbukumbu mfano KAS au VIC simu hainipi erufi hizo badala yake inanipa namba. Mmoja akasema badilisha chip kwenda simu isiyo smart phone...lakini tatizo limeendelea. Tafadhari msaada.
Mutakyamirwa.. Piga namba 0759 28 28 50 upate msaada wa maelekezo wa namna ya kuchangia iwapo umekwama. Asante kwa Sadaka yako ya Ukombozi.
Wizi mtupu
Nyinyi si mlifukuza Zitto baada ya kuwashtaki?
Wajinga ndio waliwao, Mimi nimeshaichangia CHADEMA mara mbili lakini matumizi ya michango ile yanaishia kuwanufaisha Viongozi waandamizi wa CHADEMA huku mashina yao mikoani yakiwa katika hali mbali. Acheni wizi wa kijinga.
Tunaomba udhibitisho wa mchango wako iyo mara mbili na kama hauna naona unyamaze ivo ivo milele make hauko kwenye mstari walioko wazalendo wengine
Hongera kanda ya kaskazini very creative nimeshatuma mchango wangu kila mwezi 5000
piga kazi vijana ila hzo pesa msisahau kujenga ofisi iliyo nzur na ya kisasa kila wiliya nami ntawapa wangu....
Kwani pesa ya ruzuku inafanya kazi gani?tangu muanze kutuchangisha kwenye mikutano mbona hatujaambiwa matumizi??CDM mpo kibiashara zaidi..iyo jero c bora ninunue fungu la dagaa kuliko kuchangia wazandiki
Dhamira njema husukuma mambo mema kutokea. Dhamira njema huungwa mkono na wote wenye nia njema. Dhamira njema husababisha mtu kutenda kwa ubunifu na udhati wenye kumaanisha bila kukata tamaa kwa yale yaliyo katika mipango kufikia uhalisia. Dhamira njema haizuiliwi. Dhamira njema ni wazo la Mungu na ndio mpango halisi wa Mungu.
CHADEMA Kanda ya Kaskazini ni dhamira yetu kushinda UCHAGUZI MKUU MWAKA 2015.. Mwaka 2015, ni mwaka wa Kazi.. Tumedhamiria kushinda.. Hatutazuiliwa.. Hatutaki Fedha wala jambo lolote liwe kikwazo cha Dhamira hii njema ambayo Watanzania wanaisubiria ili 1 Novemba 2015 Watanzania wapate sherehe mpya ya Uhuru wa Tanzania..
Tunakuomba ICHANGIE CHADEMA KANDA YA KASKAZINI, ili tufikie dhamira hii. Changia kiasi chochote kuanzia Tshs 500, Tshs 1,000, Tshs 2,000, Tshs 5,000, Tshs 10,000 na kuendelea ambayo utaitoa kila MWEZI HADI KUFIKA OKTOBA 2015 au kila muda (WIKI MOJA au WIKI MBILI) ambao Dhamira yako njema ya kuchangia itakusukuma. Kwa wingi wetu tutaweza kufanya mambo makubwa kwa udhati wenye kumaanisha bila kukata tamaa.
Kwa uhakika, kila mchangiaji atapata fursa ya kujua kile alichochangia kimefanya nini na matokeo yake nini..
Asante kwa Sadaka yako ya Ukombozi....!!
Amani Golugwa
Katibu - CHADEMA KANDA YA KASKAZINI
golugwa@gmail.com
+255 784 343 275
Arusha.
www.chademakandakaskazini.blogspot.com
***************************************************************************************
Jinsi ya kuchangia Chadema Kanda ya Kaskazini
Kwa M-Pesa
1. Piga *150*00#
2. Chagua Kipengele 4-Lipa kwa Mpesa
3. Chagua Namba 4
4. Ingiza namba ya kampuni (213040)
5. Ingiza namba ya kumbukumbu (KAS)
6. Ingiza kiasi Tshs XXXX
7. Ingiza namba ya SIRI XXXX
8. Bonyeza 1 kuhakiki
9. Utapokea ujumbe wa SMS Imethibitishwa kiasi XXX.
imetumwa kwa PAYLINKSYSTEMLIMITED
kwenye akaunti namba KAS
Kwa maelezo zaidi piga 0759 282850 (Katibu wa Kanda)
Poa we mchangie Mbowe akale bata na Nkya Dubai.