kuku dume
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 414
- 62
Ebu 'just imagine' wewe ni kijana wa umri wa kati ambaye hujaoa au kuolewa. Una Girlfriend/Boyfriend na katika mazungumzo yenu mna kundi la damu linalofanana. Pamoja na huyu wa ukweli una 'vidumu' kadhaa na kuna stori kitaa kwamba moja kati ya wale uliowahi kujihusisha nao ni HIV+; jambo lililokufanya kuapa kutokupima ukihofia kwamba nawe umekwesha potisivika. Inatokea Boyfriend/Girlfriend wako ana shida ya damu na msaada wako ni wa MUHIMU SANA KUNUSURU MAISHA YAKE. Je, utajitosa kwenda kutoa damu potelea mbali lolote litakalotokea kudhihirisha mapenzi yako kwake au utamkimbia ama kulumbikiza vijisababu?? Wanaojua kupenda naomba munifungue akili.