Hamtaki kujiingiza kwenye Siasa basi acheni waliojiingiza huko wale na Watoto wao

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
HAMTAKI KUJIINGIZA KWENYE SIASA BASI ACHENI WALIOJIINGIZA WALE WAO NA WATOTO WAO

Na, Robert Heriel

Waacheni warithishane madaraka, waacheni wapeane vyeo. Mlitaka wafanyaje? Wao ni wanasiasa na watawala mlitaka wawape watoto wao nini kama sio mambo hayo.

Haiwezekani watu wahangaike na siasa kutwa kuchwa, miaka nenda Rudi ninyi mnawatazama tuu. Wengine Baba zao wamekufa, wengine wamefanywa vilema, wengine walionja joto la jiwe, alafu wakifanikiwa na kuanza Kula matunda Yao mnaanza kupiga makelele, come on motherfantashiru. Tuweni serious kidogo.

Hivi Kwa mfano mtu Kama Tundu Lisu, au kina mbowe, au kina Mdude Chadema na kambi Yao. Wachukue nchi alafu wakianza Kula matunda ya jasho lao na kuwarithisha watoto wao Madaraka au vyeo watokee watu wanapiga kelele kuwa wanajipendelea. Mlitaka wafanyaje?

Wakati wakipigana mliwaachia au mlikuwa nyumanyuma Kwa Hofu au wengine hamkuwa upande wao. Leo wamepata mnajifaraguza Kama ajuza asiye na tumaini. Pumbavu!

Kama unataka Madaraka au utawala ingia kwenye Siasa. Utakula vya Siasani, utawapa watoto matunda ya Siasa.
Lakini kama utajiingiza kwenye biashara utakula vya kwenye biashara na kuwarithisha watoto wako mambo ya biashara.

Kuna watu wanapenda vitu vya burebure.
Wengine watoe jasho alafu Yao Yale tuu. Upuuzi tuu!

Wana-CCM wataendelea kurithishana matunda ya Siasa Kwa sababu ndio haki Yao. Hakuna haja ya kulaumiana hapa.

Wakati unawaza Kwa nini viongozi wa nchi wanarithishana Madaraka na utawala jiulize Baba yako alikuwa anafanya nini hapo Kabla, isijekuwa Baba au Babu yako ndio Wale wenzao walipokuwa wakiitisha maandamano kupigania maslahi ya nchi au chama cha Siasa wao walikuwa nyumanyuma kama Mfuko wa suruali ya kabwela.
Jiulize hao Watoto wa viongozi wanaopewa vyeo na kurithishwa Madaraka Baba au Babu zao walifanya nini.

Hata hao CHADEMA au ACT au chama chochote kitakachoanzishwa watakaopigania Dola wakafanikiwa kupata hiyo Dola elewa watakaokula Mema ya nchi ni Wale wa Kule juu tuu.

Alafu mwisho ujiulize wewe unayohaki hiyo Kwa misingi ipi?
Umefanya nini upewe Cheo au Madaraka.
Sio utake kuvuna mahali usipopanda.

Kwenye Siasa kuna mambo hatari mno.
Kuna kupoteza maisha,
Kuna kujeruhiwa na kufanywa kilema,
Kuna kuwekwa Jela,
Kuna kufilisiwa,
Kuna kuvurugiwa familia,
Kuna kubakwa
Kuna kuharibiwa jina,
Sasa wewe upewe Cheo au Madaraka bila kutoa kafara fulani, uliona wapi mambo Kama hayo ndugu yangu.

Hata Daudi kabla hajawa Mfalme Ali-risk maisha yake Kwa Goliath, yaani ilikuwa Do or Die. Yaani pata potea.
Daudi alishanusurika mara kadhaa kuuawa na Mfalme Sauli, unafikiri Mpaka Daudi anakuwa Mfalme alipewa burebure kama pesa ahongwavyo Demu.
Hivyo Suleiman kurithishwa ufalme ni kutokana na jasho la Baba yake Daudi,

Ninachotaka kusema ni kuwa, hakuna mambo ya burebure hapa, Kama ulitaka mambo ya burebure muombe Mungu uzaliwe wakati mwingine mwanamke, tena hata ungezaliwa mwanamke lazima kuna mambo ulipie ndipo uyapate.

Wanasiasa, viongozi wa nchi, watawala endeleeni kula nchi kadiri muwezavyo, rithishane peaneni vyeo na Madaraka muwezavyo Hilo ndio Fungu Lenu. Msione haya Kwa kufanya hivyo. Ni Haki yenu. Hiyo ni halali yenu.
Kama kuna mtu anaona sio halali basi aingie kwenye Ligi au ringi na ninyi akishinda Fresh asiposhinda basi aache lawama.

Kila kazi inanamna yake ya kuifanya. Hivyo ndivyo hata kwenye Siasa zina namna yake.

Katika ngazi ya familia, unakuta Kijana wakati ana- hustle kutafuta maisha mazuri ndugu na marafiki wanakuwa mbali naye. Lakini akishapata tuu kelele ndio zinaanza,
Ooh! Anatumia pesa vibaya,
Anavaa nguo za gharama alafu hasaidii ndugu zake,
Ananunua magari na majumba makubwa wakati ndugu zake ni choka mbaya,
Anasomesha watoto wake shule za gharama ilhali watoto wa ndugu zake wanashindwa kulipa Ada za Shule za bei nafuu.
Oooh! Anampendelea mkewe alafu site ndugu zake ametusahau.
Hivi hiyo ni Akili Kweli. Acheni uzombi!

Ukitaka kitu kizuri fanya mwenyewe, kitafute mwenyewe sio usubiri wengine wakutafutie au wakutanyie. Huo ni upuuzi.

Au unakuta mtu kuanzisha Kampuni yake anaajiri ndugu zake au kabila lake alafu unasikia wapuuzi wanapiga kelele oooh! Wanaukabila, oooh! Wanaubaguzi! Oooh! Hivi ninyi Mbuzi meee mtakuwa na akili Lini?
Kwa nini nanyi msianzishe Kampuni au biashara zenu ili mfanye kama mnavyopenda?
Mnachojua ni kupangia watu chakufanya huku mkishindwa kujipangia wenyewe chakufanya. Acheni upuuzi.

Yaani mtu aache kuajiri ndugu yake akuajiri wewe ili asionekane ati ni mkabila au mbaguzi, labda awe hamnazo. Mambo ya hivyo wanafanyaga watu wajinga wasiojielewa, wanaopenda sifa za kijinga.

Ninachotaka kusema ni kuwa; Kula mtu awajibike Kwa kile anachokitaka katika maisha yake. Ukiona changamoto pambana sio uanze kulalamika
Kanuni kuu inasema; Usitamani Mali ya jirani yako.
Kumaanisha usiwe na kijicho, wivu mbaya.
Kama wanarithishana nawe fanya kazi upate cha kurithisha watoto wako. Hakuna atakayekuonea wivu.

Kama unapenda Madaraka au utawala kanuni za kiulimwengu zipo wazi Kabisa. Weka mikakati, pambana kufa na kupona upate hayo Madaraka.
Sio umuombe mwenye Madaraka au utawala akupe Madaraka au utawala wake. Tumia hata akili, Hilo Jambo haliwezekaniki.
Usituletee mambo ya umama hapa.
Na lazima ujue kuwa kwenye mapambano yoyote hasa ya Kisiasa lolote linaweza kutokea. Hivyo ujipange haswa sio ujipange kulialia kama Mbuzi Bali jipange haswa

Taikon nimemaliza mwenye swali anaweza kuuliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Hata kama tutajiingiza wote huko, bado wataendelea kula wao na watoto wao, kwani hata sasa sio wote wanaokula kwasababu wako kwenye siasa.

Halafu mifano uliyoitoa haiendani na mada yako, kampuni inaweza kuwa ni mali binafsi ya mtu, lakini chama cha siasa, ni cha wote, japo kwenye kula ndio wanakula wachache.
 
Umekosea Sana kutolea mfano wa Tundu Lissu, Mdude, sjui Mbowe , huo ni mfano mfu hauna uhalisia wowote , hao wataendelea kuteseka tuu na kuranda Randa huku na kule ,....!! Huwez kutofautisha CCM na vyombo vyote vya usalama ....!!
 
Vyama vya siasi na uongozi wa Uma ni taasisi/kazi za Watu wote bila kujali upendeleo wowote ule ndio maana anatoka huyu anaingia mwngn

Mambo ya upendeleo wa waziwazi Lisa baba Yako alisoata Basi wewe unastahili zaidi hapana unatupotosha bwana Taikon, la sivyo waongoze familia zao , lazima yakemewe vikali

Umasikini unazidi, njaa, ajira vinaumiza Watu miaka nenda uje Watu hawajali

Watu wapo wengi wanaofaa kuwa viongozi kwanini wachache waote mizizi kisa tu watangulizi wao walisota hakuna uongozi wa kifalme Mkuu?

Kwa hili unatupotosha Sana
 
Hata kama tutajiingiza wote huko, bado wataendelea kula wao na watoto wao, kwani hata sasa sio wote wanaokula kwasababu wako kwenye siasa.

Halafu mifano uliyoitoa haiendani na mada yako, kampuni inaweza kuwa ni mali binafsi ya mtu, lakini chama cha siasa, ni cha wote, japo kwenye kula ndio wanakula wachache.

Hata nchi ni Mali ya watu.
Walioipigania ndio wenye haki ya kuila.

Kadiri watu wanavyoipigania nchi Yao ndivyo uwezekano WA kuila unavyokuwa Mkubwa.
Tafsiri yake ni kuwa Waafrika wengi wameshindwa kupigania nchi zao. Kama wangeweza kufanya hivyo basi kila mtu angeweza kupata gawio lake kulingana na Mchango wake.

Sasa Kama mtu Hana Mchango wowote ndani ya nchi ulitegemea achangiwe nini?
 
Vyama vya siasi na uongozi wa Uma ni taasisi/kazi za Watu wote bila kujali upendeleo wowote ule ndio maana anatoka huyu anaingia mwngn
Mambo ya upendeleo wa waziwazi Lisa baba Yako alisoata Basi wewe unastahili zaidi hapana unatupotosha bwana Taikon, la sivyo waongoze familia zao , lazima yakemewe vikali
Umasikini unazidi, njaa, ajira vinaumiza Watu miaka nenda uje Watu hawajali
Watu wapo wengi wanaofaa kuwa viongozi kwanini wachache waote mizizi kisa tu watangulizi wao walisota hakuna uongozi wa kifalme Mkuu????
Kwa hili unatupotosha Sana

Sijapotosha kitu hapo MKUU.

Ukiona nchi Fulani kuna kundi Fulani linakula zaidi ya kundi jingine lazima ujiulize swali Kwa nini iwe hivyo.
Ninachoandika ni kile nilichokifanyia tathmini na haya ninayoandika ni matokeo tuu ya kile nilichokiona.

Nataka nikuambie, nchi hii na zingine za Afrika haziendelei Kwa sababu kuna kutegeana miongoni mwa watu katika kuikomboa Nchi.

Haiwezekani wategaji walingane Sawa na waliokuwa mstari wa mbele Hilo haliwezekaniki.

Hata Waisrael waliokuwa wanakula Mema ya nchi ni WALAWI kutokana na kuwa Waliokuwa Fronti kukomboa Waisrael kutoka Misri utumwani ni Musa na Haruni ambao ni kabila la Lawi.

Kama watu wanataka wale Mema ya nchi lazima wawe mstari wa mbele kuikomboa nchi.
Kwa Mali zao
Kwa jasho Lao
Kwa damu zao
Kwa akili Yao
Kwa karama zao
Kwa vipaji vyao.

Haiwezekani wengine wakiendelea kukomboa nchi wakiwa mstari wa mbele alafu kuna wengine wanakuwa nyumanyuma kanakwamba sio kundi moja linaloelekea sehemu moja.
Wanakuwa sehemu ya kutoa lawama na changamoto za ndani ya nchi.
 
Ni sawa tu hata wakiamua kurithishana na kuifanya serikali iwe monarchy sisi tunachotaka ni maendeleo yaonekane basi
 
Umekosea Sana kutolea mfano wa Tundu Lissu, Mdude, sjui Mbowe , huo ni mfano mfu hauna uhalisia wowote , hao wataendelea kuteseka tuu na kuranda Randa huku na kule ,....!! Huwez kutofautisha CCM na vyombo vyote vya usalama ....!!


Utatofautishaje sasa wakati HAO ndio waliounda nchi?
Hivyo ni vitengo tuu.

Yaani ni Sawa wewe uanzishe taifa lako alafu uunde Serikali, alafu atokee mtu aone vyombo ulivyoviunda vinatofautiana na wewe huyo mtu atakuwa hajatumia akili yake vizuri.

Hao CHADEMA nimewatolea mfano katika kama sehemu ya kile wanachokifanya, yaani CHADEMA wachukue nchi miaka 20 ijayo alafu iwe ajabu mtoto wa Tundu Lisu kupewa Cheo. Huyo mtu atakayeshangaa hivyo lazima awe hamnazo.
 
Ni sawa tu hata wakiamua kurithishana na kuifanya serikali iwe monarchy sisi tunachotaka ni maendeleo yaonekane basi

😂😂😂😂
Maendeleo yanaonekana Kwa muono wao sio wa watu Baki.
Sio ajabu viongozi wa nchi wakaona nchi hii imeendelea Kwa sababu wao hakuna wanachokosa, 😀😀
Sijui Kama umepata Logic ya kile ninachoeleza hapa.

Watanzania Kama tunataka maendeleo lazima wote tuwe mstari wa mbele katika kushiriki shughuli za Kisiasa.
Siasa ndio maisha ya Sisi Wanadamu.

Unaona Wairan?
Yule mwanamke amefia mikononi mwa polisi huenda ni bahati mbaya au makusudi.
Lakini watu wote wanaungana kutetea haki za huyo mwanamke aliyeuawa. Bila kujali tofauti zao.
Ili nchi iendelee Kwa watu wote lazima ifike hatua ya namna hiyo.
Vinginevyo tutaendelea hivihivi.
 
Umetoa kuntu hapo mpaka na mimi naona haya. Sisi ndo wakosoaji wa wanasiasa lakini ukisikia mtu kaandika au katoa maoni, kimyaaa halafu akikamatwa tunaanza kelele.

Haiwezekani ukapenda haki bila kuhukumiwa. Mimi nakumbuka nilikuwa kati ya watu walioendesha baiskeli pale dodoma 1995.

Nilipata ruhusa ofisini nikafanya hivyo lakini mwisho wa siku Mrema kumbe alikuwa pandikizi na yule mama aliyeachia nadhani uwaziri au ubunge akawa kwenye UNCCR mageuzi jina namsahau.

Aliishia kupotea nakumbuka nilimtembelea kwake njia ya kwenda Mabwe pande wakati huo ilikuwa misitu na nyika. She was so nice but disappointed in politics of that time.
 
Umetoa kuntu hapo mpaka na mimi naona haya. Sisi ndo wakosoaji wa wanasiasa lakini ukisikia mtu kaandika au katoa maoni, kimyaaa halafu akikamatwa tunaanza kelele...

Wapo watu wanajitolea kutetea jamii lakini wakipata madhila au majanga jamii unakaa kimya. Huo ni upuuzi.
Jamii lazima ifundishwe kuwajibika na kuwawajibisha watu wasiofuata sheria.

Angalia tukio la mwanamke wa Iran, jinsi jamii za wenzetu wanavyojua kujitoa katika kupambania mambo mazuri/Haki. Lakini ingekuwa bongo ingekuwa tofauti Kabisa.

Kama tunataka maendeleo basi tusitegeane.
Ninauhakika Yule tunayemtegea ni lazima awe juu yetu na atupangie chakufanya, Kwa sababu yeye ndio katumia nguvu na gharama kubwa kuliko tuliokuwa nyumanyuma.

Hata kwenye familia au Kampuni mwenye hisa nyingi ndiye muamuzi WA mwisho na ndiye anayepata faida kubwa zaidi
 
Sijapotosha kitu hapo MKUU.

Ukiona nchi Fulani kuna kundi Fulani linakula zaidi ya kundi jingine lazima ujiulize swali Kwa nini iwe hivyo. Ninachoandika ni kile nilichokifanyia tathmini na haya ninayoandika ni matokeo tuu ya kile nilichokiona.
Ya nini kuwaaminisha watu juu ya kanuni za kidemokrasia Mambo ya uchaguzi huru, Mambo ya uwazi, vyama vingi kama wanajua fika hawapo Tayari kuwaachia wengine nao waingie.

Basi waifanye nchi iwe monarch tutaelewa kuliko kula wao kwa wao.

Sasa Kama kila MTU ana haki ya kuchaguliwa democracy IPO wapi Hapo??
 
Ya nini kuwaaminisha watu juu ya kanuni za kidemokrasia Mambo ya uchaguzi huru, Mambo ya uwazi, vyama vingi kama wanajua fika hawapo Tayari kuwaachia wengine nao waingie.
Basi waifanye nchi iwe monarch tutaelewa kuliko kula wao kwa wao
Sasa Kama kila MTU ana haki ya kuchaguliwa democracy IPO wapi Hapo??

Aliyekuambia nchi hii niya kidemokrasia ni Nani?
Ni lini demokrasia kwenye hii nchi ilipiganiwa?
Kitu pekee kilichopiganiwa kwenye hii nchi ni Uhuru huo mwaka 1961.

Mapambano ya demokrasia yameanza juzi hapa na bado hayajafika kiwango cha juu cha kuileta Demokrasia hapa nchini.

Nenda kasome Historia ya Demokrasia ya nchi za Ulaya utaelewa ninachokisema hapa.

Kila kitu lazima kipiiganiwe.

Au kasome Demokrasia ya Marekani ilianza kutamalaki lini tangu nchi hiyo ilipopata Uhuru mwaka 1776

Kitu kimoja uweke akilini ni kuwa, hao kina Lisu na mbowe ndio sasa wanahangaika kuileta demokrasia kwenye nchi hii.

Ndio maana watu wanataka Katiba Mpya,
 
"No sweet without sweat" ,"Asiye fanyakazi asile"Bible

Siku zote waoga hubaki duniani kuonesha makaburi ya mashujaa huimba sifa tele kwa watu walio jitoa kwa jasho na damu kupigania vitu muhimu,sababu ya uoga wao hushindwa hata kupigania haki zao wenyewe bali hutegemea mtu,watu au kundi fulani lifanye hivyo kwa niaba yao huu Ni ujinga uliona wapi mtu ana vuna sehemu ambayo haja panda ? Kanuni ya msingi ni Ile Ile "utakula uliko peleka mboga" hukujitoa kupigania Jambo kaa kimya ukiona walio jitoa wanakula jasho la sadaka zao.

Watu wanajitoa kupigana lengo kuu ni kutafuta nguvu sababu kuu ni moja nguvu ndio haki maana mwenye nguvu ndio anaye amua kipi ni haki na kipi sio haki hivyo aliye jitoa lazima ajipe haki yake Kwanza yeye kwa sadaka zake.
 
Aliyekuambia nchi hii niya kidemokrasia ni Nani?
Ni lini demokrasia kwenye hii nchi ilipiganiwa?
Kitu pekee kilichopiganiwa kwenye hii nchi ni Uhuru huo mwaka 1961.

Mapambano ya demokrasia yameanza juzi hapa na bado hayajafika kiwango cha juu cha kuileta Demokrasia hapa nchini.

Nenda kasome Historia ya Demokrasia ya nchi za Ulaya utaelewa ninachokisema hapa.

Kila kitu lazima kipiiganiwe.

Au kasome Demokrasia ya Marekani ilianza kutamalaki lini tangu nchi hiyo ilipopata Uhuru mwaka 1776

Kitu kimoja uweke akilini ni kuwa, hao kina Lisu na mbowe ndio sasa wanahangaika kuileta demokrasia kwenye nchi hii.

Ndio maana watu wanataka Katiba Mpya,
Mwl Nyerere alionyesha wazi kutopenda Mambo za kurithisha wanafamia wake Leo tunaona akina madaraka Ni Watu wa kawaida Kabisa
unadhani mwalimu asingeweza kuiweka nchi hii mfukoni mwake na kizazi chake kitawale Hadi Leo Kama sio dhana ya democracy ili mtawala mwalimu ni nini?
 
Umekosea Sana kutolea mfano wa Tundu Lissu, Mdude, sjui Mbowe , huo ni mfano mfu hauna uhalisia wowote , hao wataendelea kuteseka tuu na kuranda Randa huku na kule ,....!! Huwez kutofautisha CCM na vyombo vyote vya usalama ....!!
Akili yako ndogo, labda utakuwa siku moja utaelewa .
 
Viongozi wengi wa Sasa wamejawa na ubinafsi wa familia Zao
Refer familia ya mwl.Nyerere faninisha na sasa
 
Back
Top Bottom