Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 750
- 1,800
Halmashauri ya jiji la Arusha imevuka malengo iliyojiwekea ya makusanyo ya mapato ya ndani ya shilingi Bilioni 15.6 na kufikia sh,bilioni 16.4 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 105.
Akiongea katika kikao cha mwisho wa mwaka cha baraza la madiwani wa jiji la Arusha,Mstahiki Meya wa jiji hilo, Kalisti Lazaro alisema mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo ,Dkt Maulid Madeni ambaye amefanikiwa kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.
Amesema halmashauri hiyo inavyanzo vingi vya mapato yakiwemo masoko na Mizani lakini yalikuwa yakipotea kutokana na baadhi ya watumishi wake wasiowaaminifu kushindwa kusimamia ipasavyo badala yake wamekuwa wakijinufaisha wenyewe,jambo ambalo kwa sasa limedhibitiwa.
"Baraza la madiwani linampongeza Mkurugenzi Dkt Madeni kwa kufanikiwa kuvuka malengo ya makusanyo ya mapato ya halmashauri na sisi kama madiwani tutatoa ushirikiano wa dhati kwake kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unazidi kuongezeka na hii inatokana na mfumo wake wabkuwapiga pingu walaji wa fedha za halmashauri" alisema Lazaro
Akiongelea suala la madawati amewataka watendaji kutofanya makosa ya mwaka Jana kwenda kununua madawati yasio na viwango wilayani Korogwe kwa bei kubwa ya sh,150,000 kila dawati badala yake kutumia vituo vya ndani ambapo thamani ya dawani moja haizidi sh, milioni 96.
Wakati huo huo Wakala wa barabara za mijini na vijijini Tarura katika jiji la Arusha amelalamikiwa kwa kutoa zabuni kwa kandarasi mmoja ambaye ameshindwa kukamilisha barabara za kiwango cha changarawe ndani ya muda aliopangiwa ndani ya kata za jiji hilo.
Amesema kuwa barabara za kata zimeshindwa kukamilika kwa visingizio vya kuharibika kwa greda jambo ambalo limewafanya wananchi kuanza kulalamika kwa ubovu wa barabara hizo ambazo hadi sasa hazijamalizika na kubaki vifusi vimelundikana kwa muda mrefu na kuwa kero kwa watumiaji wa barabara.
"Sijui ni vigezo gani mmechukuwa kumpata mkandarasi huyu moja ambaye ameshindwa kwenda na kasi ya ujenzi nawaomba mchukue hatua za haraka ili Kazi hiyo ya ujenzi iweze kukamilika ndani ya muda aliopangiwa" alisema Mstahiki Meya Lazaro.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa jiji la Arusha Dkt.Maulid Madeni ameitaka tarura jiji la Arusha kufanyakazi za wananchi kwa kufuata sheria na kuwajibika kwa jiji hilo kama sheria zinavyoelekeza na hatasita kuwachukulia hatua wale watakaohujumu juhudi za serikali kuwaletea wananchi maendeleo.
Ends.....
L
Akiongea katika kikao cha mwisho wa mwaka cha baraza la madiwani wa jiji la Arusha,Mstahiki Meya wa jiji hilo, Kalisti Lazaro alisema mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo ,Dkt Maulid Madeni ambaye amefanikiwa kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.
Amesema halmashauri hiyo inavyanzo vingi vya mapato yakiwemo masoko na Mizani lakini yalikuwa yakipotea kutokana na baadhi ya watumishi wake wasiowaaminifu kushindwa kusimamia ipasavyo badala yake wamekuwa wakijinufaisha wenyewe,jambo ambalo kwa sasa limedhibitiwa.
"Baraza la madiwani linampongeza Mkurugenzi Dkt Madeni kwa kufanikiwa kuvuka malengo ya makusanyo ya mapato ya halmashauri na sisi kama madiwani tutatoa ushirikiano wa dhati kwake kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unazidi kuongezeka na hii inatokana na mfumo wake wabkuwapiga pingu walaji wa fedha za halmashauri" alisema Lazaro
Akiongelea suala la madawati amewataka watendaji kutofanya makosa ya mwaka Jana kwenda kununua madawati yasio na viwango wilayani Korogwe kwa bei kubwa ya sh,150,000 kila dawati badala yake kutumia vituo vya ndani ambapo thamani ya dawani moja haizidi sh, milioni 96.
Wakati huo huo Wakala wa barabara za mijini na vijijini Tarura katika jiji la Arusha amelalamikiwa kwa kutoa zabuni kwa kandarasi mmoja ambaye ameshindwa kukamilisha barabara za kiwango cha changarawe ndani ya muda aliopangiwa ndani ya kata za jiji hilo.
Amesema kuwa barabara za kata zimeshindwa kukamilika kwa visingizio vya kuharibika kwa greda jambo ambalo limewafanya wananchi kuanza kulalamika kwa ubovu wa barabara hizo ambazo hadi sasa hazijamalizika na kubaki vifusi vimelundikana kwa muda mrefu na kuwa kero kwa watumiaji wa barabara.
"Sijui ni vigezo gani mmechukuwa kumpata mkandarasi huyu moja ambaye ameshindwa kwenda na kasi ya ujenzi nawaomba mchukue hatua za haraka ili Kazi hiyo ya ujenzi iweze kukamilika ndani ya muda aliopangiwa" alisema Mstahiki Meya Lazaro.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa jiji la Arusha Dkt.Maulid Madeni ameitaka tarura jiji la Arusha kufanyakazi za wananchi kwa kufuata sheria na kuwajibika kwa jiji hilo kama sheria zinavyoelekeza na hatasita kuwachukulia hatua wale watakaohujumu juhudi za serikali kuwaletea wananchi maendeleo.
Ends.....
L