Joshua Bukuru
Member
- Apr 16, 2011
- 76
- 95
Ndugu wana-jamiiforums, tukubali au tusikubali hali ya muundo wa muungano tulionao haibebeki tena. Huu muungano wa serikali 2 hauna nafasi tena katika dunia ya utandawazi. Nayesema haya kwa sababu nimewasikiliza wanzibar katika makongamano yao, juu ya elimu ya uraia na jitihada mpya za tume katika kukusanya maoni ya katiba mpya. Wameapa kuwa liwalo na liwe kwa maana kuwa tusipokubali (watanganyika) muundo wa serikali 3 basi na muungano uvunjike. Hizi ni kauli zao. Japokuwa Mwl Nyerere alitahadharisha hili, yeyete atakayekuwa wa kwanza kujitenga, basi upande wa pili utabaki salama.Na nje ya muungano, hatuna zanzibar bali tuna Unguja na Pemba. Na hii inaweza kuwa kwa sababu ya ujinga au ulevi wa madaraka wa viongozi wao. Sasa wameanza na si kwamba kuwa watanganyika nao wanafurahishwa na muundo huu...
Pia nimesoma magazeti kuwa Rais wa Zanzibar Shain naye ameapa kuulinda muungano kwa gharama zote, kisa ni kwamba sera ya CCM ni kulinda muungano na si kuvunja muungano. Kama kweli kasema hivyo basi, mimi najiuliza maswali yafuatayo:?
1. Je, yuko tayari kulinda maslahi ya CCM kuliko ya wananchi wa Zanzibar waliomwanjiri katika nafasi hiyo aliyonayo? Ukweli ni kwamba if they voted for him, they can also devote for him. Haki hiyo wanzanzibar wanayo na asiwapuuze katika maoni yao.
2.Rais Shain hazungumzi auhatamki ni sababu zipi zitamfanya apuuze madai ya wazanzibar ambao ndiyo wengi kuliko hizo sera za CCM zisizobadirika. Kuitwa kiongozi ni kutanguliza maslahi ya watu wako unaowaongoza. Au ni ule woga na fadhila za kutowaudhi viongozi wa Tanganyika waliompa nafasi hiyo ya urais, maana zanzibar imekuwa ikichaguliwa viongozi na CCM-tanganyika.
Sasa basi, tuanze kuwaza serikali 3 au 1 maana 2 haiwezekani tena. Nina wasiwasi hizi serikali 2 zinaweza kutufikisha kwenye serikali sifuri(0). Tukiwa nazo tatu basi na mfumo wa mahakama zetu itabidi ubadilishwe, na hapa chini nimeambatanisha mfumo wa mahakama zetu unavyotakiwa kuonekana. Ni maoni yangu tu na napenda tujadili kama watanzania. Sasa nasema karibuni sana...
Pia nimesoma magazeti kuwa Rais wa Zanzibar Shain naye ameapa kuulinda muungano kwa gharama zote, kisa ni kwamba sera ya CCM ni kulinda muungano na si kuvunja muungano. Kama kweli kasema hivyo basi, mimi najiuliza maswali yafuatayo:?
1. Je, yuko tayari kulinda maslahi ya CCM kuliko ya wananchi wa Zanzibar waliomwanjiri katika nafasi hiyo aliyonayo? Ukweli ni kwamba if they voted for him, they can also devote for him. Haki hiyo wanzanzibar wanayo na asiwapuuze katika maoni yao.
2.Rais Shain hazungumzi auhatamki ni sababu zipi zitamfanya apuuze madai ya wazanzibar ambao ndiyo wengi kuliko hizo sera za CCM zisizobadirika. Kuitwa kiongozi ni kutanguliza maslahi ya watu wako unaowaongoza. Au ni ule woga na fadhila za kutowaudhi viongozi wa Tanganyika waliompa nafasi hiyo ya urais, maana zanzibar imekuwa ikichaguliwa viongozi na CCM-tanganyika.
Sasa basi, tuanze kuwaza serikali 3 au 1 maana 2 haiwezekani tena. Nina wasiwasi hizi serikali 2 zinaweza kutufikisha kwenye serikali sifuri(0). Tukiwa nazo tatu basi na mfumo wa mahakama zetu itabidi ubadilishwe, na hapa chini nimeambatanisha mfumo wa mahakama zetu unavyotakiwa kuonekana. Ni maoni yangu tu na napenda tujadili kama watanzania. Sasa nasema karibuni sana...