Hali ya chemba za majitaka Kariakoo ni mbaya, Utapishaji Vyoo unafanyika kiholela

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120

Nimepita Kariakoo leo kwakweli hali ya Miundombinu zikiwemo Barabara za Mitaa na Chemba za Majitaka ni mbaya inatia kinyaa na Mamlaka zinaendelea kukusanya Kodi pale kama hazioni.

Mbaya zaidi Chemba zimepasuka katika maeneo ambayo watu wanalazimika kutembea kwenye uchafu unaotoka katika mitaro iliyopo chini ya Barabara.

Cha ajabu Mamlaka zinapita katika njia hizo kila wakati na hakuna hatua zinazochukuliwa ukizingatia wakat huu kuna mvua zinazoendelea kunyesha hali inayoweza kusababisha Mgaonjwa ya Mlipuko ikiwemo homa za matumbo.

Waziri wa Afya Wizara ya Afya Tanzania inapaswa kufika na kuangalia jinsi hali ya usalama wa afya za Watanzania ikiwa hatarini.
 
Watu wanayakanyaga tu

Na syo kariako hata City Centre wanafanya hivyo

Kipindi cha mvua tena wanayaachia

Ova
 
Kuna mda kariakoo na posta kote Kuna Nuka mavi ,uozo , mbwa aliyekufa, samaki waliooza, na Kila aina ya harufu hasa mvua ikinyesha
 
Back
Top Bottom