jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,323
Nimewajibika kuwaandikia enyi mjuao kiswahili, ya kwamba si mtu, kundi la watu, taasisi binafsi au za serikali, nchi, wala bara lolote linalomiliki "UFAHAMU" niwakumbushe, wanasayansi wa awali, kwa UFAHAMU wao walikubaliana kusema umbo la dunia ni kama meza kubwa, wakatengeneza na sheri kuwa ni marufuku kusema au hufundisha vinginevyo, kanuni za adhabu kwa kosa hilo ikawa ni kunyongwa ikithibitishwa umehubiri kinyume na "UFAHAMU" ule. Kwa wajuao, akatokea miongoni mwao kupata UFAHAMU tofauti ya kuwa dunia haiko kama meza, bali dunia ni duara, jopo la wanasayansi walipothibitisha mwenzao amepingana na UFAHAMU wao walimnyonga, hatimaye walikuja kubaliana na ufahamu wa marehemu kuwa dunia ina umbo la duara, yapimeni maelezo haya myaweke kwenye mizania ya mchungaji msataafu wa Loliondo. Mwenye hoja aweke jamvini.