Habari mbaya kwa walaji wa Kitimoto: Huenda wengi wao wakaja kupata kifafa!

Nguruwe ambapo katika mwili wake hukusanyika jumla ya vijiumbe maradhi visivyoondoka kwa kuoshwa

Mdomo ni maficho ya vijidudu, bakteria na virusi vinavyokwenda kwa binadamu na wanyama.


Baadhi yake vinamhusu nguruwe, mfano wa kidudu kiitwacho Trchinella, nywelenywele ziitwazo

Balantidium Dysentery, wadudu wa tumbo (Taenia Solium) na mchango wa nguruwe (Spiralis).

Baadhi yake huingizwa kwenye maradhi mengi ya pamoja baina ya binadamu ( Cysticercosis & Influenza) na wanyama.


Minyoo (Ascaris na Fasciolopsis Buski) hupatikana kwa wingi nchini China.

Maradhi ya Balantidiasis hupatikana kwa wachunga nguruwe na wenye kuchanganyika nao, na

yanaweza kuenea kwa sura ya mlipuko kama ilivyotokea katika moja ya visiwa vya bahari ya Pacific

baada ya kimbunga. Maradhi yanakuwepo panapokuwepo nguruwe katika nchi zilizoendelea

kiviwanda kinyume na madai ya uwezekano wa kuushinda uchafu wake kwa kutumia teknolojia

mpya zinazoharamisha kula nyama bila ya kibali, hasa nchini Ujerumani, Ufaransa, Philippines na Venezuela.

Kwa kula minofu ya nyama ya nguruwe, (Trichinellosis) hupatwa na ugonjwa wa Balantidium

Dysentery. Kwani mke hubungua kuta za matumbo kwa ajili ya kuweka mayai ambayo yanafikia

kiasi cha 10,000. Mayai hayo huingia kwenye misuli kupitia damu na kugeuka kuwa ni vijiyai vyenye kuambukiza.

Ama kupata maradhi kupitia mchango wa nguruwe, ni kuwa hiyo hupatikana baada ya kula minofu ya nguruwe mwenye ugonjwa.

Minyoo hukua kwenye mchango wa binadamu na urefu wake unaweza kufikia meta saba, na

unakuwa na kichwa chenye miba inayosababisha kukwaruzika kwa kuta za michango na mchupo

mkubwa wa damu, na ana mirija minne na shingo. Aina za mke huzaliwa kama kwamba ni

wanyama pekee na hufikia maelfu. Na katika kila mmoja kati ya mnyama, huzaliwa zaidi ya mayai

elfu moja iwapo utakula Cysticercosis.

Kupatwa na ugonjwa wa minyoo ya tumbo la binadamu, hutokana na kula chakula kilichoingia

mayai na kutoa lava, na huingia katika damu kupitia kiungo chochote. Na hatari yake hukisiwa kwa

mujibu wa umuhimu wake.

Maradhi haya hayatokei kabisa kutokana na kupatwa na mchango usio na miba katika kichwa na

wenye madhara madogo


kabisa Taenia Saginata ya ng'ombe. Chanzo.MziziMkavu



KIIMANI
kwa upande wa Quran
"Yeye Amekuharimishieni mzoga tu na damu na nyama ya nguruwe na kilichotajiwa, katika kuchinjwa kwake, jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu" (2: 173).


KWA UPANDE WA BIBILIA
"Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu ni najisi. Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao" wala msiguse mizoga yao (Walawi 11: 7 – 8).

mkuu naona umeorodhesha magonjwa mengi kwelikweli hadi umenipeleka kwenye somo la medincine na macrobiology, kitu nachoweza kusema ni kuwa nguruwe ana nyama tamu sana, hili si jambo la siri. pia ina ubora kiafya kwa kuwa ni aina ya whitemeat kama unavyojua white meat iko safe na mambo ya cholesterol na mengineyo, na zaidi ya yote hata kwa tathmini yako binafsi maeneo yanayofuga nguruwe hayo magonjwa uliyoorodhesha hayajaonyesha athari za kufikia hatua ya kuacha ulaji ama kuweka quarantine, kiasi kwamba kuna watakaosoma hapa hasa malaymen na kuona kilichoandikwa ni hadithi na si kweli japo kuna ukweli wake. umeandika magonjwa mengi ya nguruwe lakini jua kuna magonjwa mengi ya wanyama wengine pia. kitu nachotaka kusisitiza hapa ni kuwa ulaji wa nyamakwa ujumla una madhara kuliko ulaji wa mimea/majani. mfano nyama maarufu ya kondoo inatatizo la kupelekea matatizo kwenye magoti (gauti) tena kuliko mbuzi!! kwanini basi hawakuiona ni nyama haramu? i dont know?

tukija kwenye upande wa bibilia ni vizuri tukifahamu kuwa namna ya kusomaji na kuielewa bibilia si kama inavyosomwa quran na kuitafsiri. kuna madai nisiyoweza kuthibitisha kuwa kuran inatasfsiriwa kama ilivyoandikwa, kama ni hivyo pengine neno la petro kuotesha kushushuiwa nguruwe kwenye ndoto na akaambiwa ale lakina akakataa akasema hawezi kula najisi na sauti ya mungu ikamjibu kuwa alichokiumba mungu usikitie unajisi lingetosha kabisa kuwafanya wakristo walitumie kutetea ulaji wa nyama ya nguruwe.

kuna neno kwenye baibo linasema kuhusu: ki=umuua mzinzi, kutokufanya kazi siku ya sabato, ulaji najisi.
tukianza na;
mafarisayo walimpelekea yesu mwanamke wakimwambia sheria ya musa inatutaka tumpige mawe tumwuue, lakini mpaka mwisho wa siku yesu hakumuua na waliomuhukumu waliondoka zao bila kumgusa, kama ni kulinganisha tungeanza na kujiuliza je waislamu mwanamke mzinzi anahukumiwaje?

pia kuna matendo yaliyofanyika yalioonekana yakivunja sabato lakini yesu akasema yeye ni bwana wa sabato(kama kula mashuke, kubeba kitanda).

pia kuna swala la kutoa talaka kwa mke yesu alionyesha kulipinga.je waislamu wanamtazamo sawa kuhusu talaka?,
vilevile swala la kuoa wake wengi(ndoa za mitaala, je yesu alisemaje kuhusu idadi ya wanawake wa kuoa na je waislamu wnachukuliaje idadi ya wanawake wa kuoa?

na ukiongezea na hili la ulaji wa nguruwe ukiweka neno la yesu aliposema si kimwingiacho mtu kinamtia unajisi bali kimtokacho kwani kile kimtokacho hupita na kwenda chooni...najua umeshasema kuwa unampenda yesu kwakuwa wewe ni mwislamu,na wakristo wanafuata alichofanya yesu na si kile tu wayahudi walikichukua katika mapokeo yao paradoxically yesu alisoma elimu ya kiyahudi pia. napata picha kuwa namna bibilia inavyotafsiriwa si vile kuran inatafsiriwa na ndio maana wakristo wengi wanakula nguruwe bila kujali andiko hilo linalodaiwa kukataza ulaji huu wa nyama ya nguruwe. naheshimu imani yako lakini najaribu kueleza kwanini wakristo hawajali hilo andiko na wanaendelea kula nguruwe kila kikicha.
wakristo wanamtumia yesu kama role model wao, ambapo yalioandikwa kwenye torati na sheria za musa alionesha kutofautiana nazo, na bibilia imezionyesha sheria zote na ajabu ni pale yesu aliposema hakuja kutangua torati bali kuitimiliza. na hapa ndipo tafsir inapoanzia kwani


mkuu lengo langu hapa ni kuonyesha kuwa namna ya kuitafsiri kuran ni tofauti na ile inayotumika kwenye bibilia. thats it.

yohana 10:34
34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu? 37 Kama sizitendi kazi za Baba yangu, msiniamini; 38 lakini nikizitenda, ijapokuwa hamniamini mimi, ziaminini zile kazi; mpate kujua na kufahamu ya kuwa Baba yu ndani yangu, nami ni ndani ya Baba.
 
Nimepata swali. Yani kinyesi cha mtu kina tegu. Nguruwe akila kinyesi anaambukizwa tegu. Mtu akimla nguruwe aliyepata tegu toka kwa mtu, anaambukizwa tegu ambao wanasababisha kifafa. Kwa nini mtu asijiambukize kifafa hadi amsubiri nguruwe?
 
Hapa inatakiwa ujuwe vizuri mzunguko wa maisha ya tegu(life cycle of Taenia sodium). Hapo utapata jibu la swali lako. Nikiwa na muda nitaandika zaidi.
 
hizi zote ni propanda za ki-neoliberal ambazo zinataka kuonesha kila kinachozalishwa Africa ni substandard, kwanini nguruwe wa Mbeya na sio wa Marekani au kwingineko?
 
Haina maana kuwa ni nguruwe wa mbeya tu. Tumetoa mfano tu wa aina ya ufugaji unaweza kupelekea uenezwaji. Haha maharashtra kwingine kwokote wanakofuga nguruwe kwa utaratibu usiofaa nguruwe wanaweza kuwa na ugonjwa huu. Na si nguruwe wote wa Mbe
 
wa Mbeya. Tafiti zimefanyika pia Nigeria za watt kupata kifafa kinachotoka na tegu
 


Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimehadharisha walaji wa nyama ya nguruwe nchini, kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa.

Utafiti wa kisayansi uliofanywa na SUA, umebaini kuwa baadhi ya nguruwe wana minyoo aina ya tegu ambao nyama yao
ikiliwa bila kuiva vizuri, mlaji atapata minyoo hiyo ambayo huingia kichwani na kusababisha kifafa.

Akizungumza na mwandishi hivi karibuni, Mhadhiri na Mtafiti wa Idara ya Sayansi ya Wanyama na Uzalishaji ya SUA, Profesa Faustine Lekule, alisema sampuli za utafiti huo kutoka Mbeya, zimebaini nguruwe wengi wakiwamo wanaosafirishwa katika miji mikubwa wameathirika na minyoo hiyo.

Kwa mujibu wa Profesa Lekule, wataalamu wa SUA wanaosimamia Mradi wa Utafiti wa Kuboresha Ufugaji wa nguruwe kwa mkoa wa Mbeya ili kuinua pato la kaya, unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA), walibaini hatari hiyo baada ya kuchukua sampuli ya nyama ya nguruwe kwa ajili ya vipimo.

"Majibu ya sampuli ambazo wataalamu wamezichukua kutoka kwa nguruwe wa wafugaji kwenye baadhi ya vijiji, wamebainika kukumbwa na hatari hii.

"Lazima jitihada za makusudi zichukuliwe katika kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili kati ya watafiti na Serikali," alisema Profesa Lekule.

Alisema maambukizi ya tegu au minyoo ya nguruwe yanatokana na tabia za baadhi ya wafugaji kutozingatia ufugaji bora kwa kuwaacha kujitafutia chakula na maji mitaani na kula kinyesi cha binadamu.

Kwa mujibu wa Profesa Lekule, baadhi ya wafugaji wamekuwa wakijisaidia vichakani na kuwaacha nguruwe kutafuta malisho katika vichaka na kula kinyesi chao, hali inayochangia ongezeko la maambukizi ya minyoo ya tegu hao.

Baada ya kula kinyesi minyoo humwingia mwilini na kumdhoofisha na baadaye binadamu anapokula nyama ambayo haijaiva vizuri, minyoo hiyo humwingia na kusababisha kifafa baada ya kuingia kichwani.

Alisema athari za kuenea kwa maambuziki hayo inaweza kutokea katika miji mikubwa ikiwamo Dar es Salaam kwa kuwa nguruwe wa Mbeya husafirishwa na kuuzwa maeneo hayo.

"Hatua hii inaweza kusababisha kusambaa kwa ugonjwa huu, hivyo ushirikiano kati ya wafugaji, wafanyabiashara, Serikali na wataalamu wa afya katika kufikia hatua ya kumaliza changamoto hii unahitajika," alibainisha Profesa Lekule



Sifikirii kabisa kwamba habari hii ni mbaya kama ilivyopewa kichwa cha habari hapo juu. habari ina maneno mengiiii ambayo ni ya kishabiki tu. Kwa mtazamo wangu hii habari yote ingefupishwa kwa maneno machache ya ushauri kuwa: watu wale nyama ya nguruwe iliyoiva vizuri kutokana na kuweza kuwepo kwa minyoo ya Tegu ambayo inaweza sababisha kifafa, simple. Kwasababu sidhani mpaka sasa kama kuna watu ambao wanakula nyama hii ikiwa mbichi.

 
Watu wengi hawajui madhara ya kula kitimoto ambacho hakijaiva vizuri. kitimoto unatikiwa ukipike mwenyewe nyumbani ili kiive vizuri ili kuua hao minyoo hatari.
 
tangu Adamu na mkewe watende dhambi pale Eden,maeneo ya Iraq,hakuna kilichofaa kwa maisha ya binadamu,Biblia inasemaa vyoote vikalaaniwa.Hakuna kilicho salama hapa Duniani,tunaishi kwa neema za Mungu tu
 
Nipo sinza hapa twende hapo dagadagaa kitu kitamu sana ati

dagaadagaa kwa kitimoto cha kila aina ni kama kwa baresa na bidhaa za unga tatizo mvua mkuu ila hap ukiingia tazama wanapochomea kwa mkono wa kulia unaweza ukala hadi ukaomba poo tatizo ukija hapo wanakupokea juu juu hivyo uwezi juawapi wanatengeza poa,ila sasa hii mvua huo uwanja haujaa jaa maji,pana muinuko kidogo lakini je utakaa wapi sasa
 
Back
Top Bottom