collezione
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 352
- 178
Leo naomba tujadili usalama wa maisha yetu.
1)Tuseme Umepanda basi unaelekea mwanza. Huko Barabarani hakuna sheria za uendeshaji high_way (na kama zipo hazifuatwi). Uko kwenye basi na dereva anakimbiza vibaya mno... Wakati huo huo tunajua mabasi mengi yanatumia matairi ya kichina ambayo sio imara (tanzania hakuna chombo kinachokagua, wamiliki wa mabasi watumie matairi gani, kwa usalama wa raia)... Punde basi likipinduka, watu wakafa. Hayo ni mapenzi ya Mungu????
2)Unaumwa tumbo. unaenda pharmacy kununua pain killers. Huko dukani pamejaa madawa feki na mengine yame-expire. Baada ya miaka michache unagundulika na cancer... Hayo ni mapenzi ya Mungu???
3) Wana_reseach wameandika, magari mabaovu Ndio chanzo cha magonjwa mengi yatokanayo na mfumo wa hewa. Kutokana na uchakavu wa injini. Moshi wa magari chakavu ni hatari kwa maisha ya binadamu.... Haya Unaishi Tanzania nchi ambayo haina sheria ya magari chakavu. Foleni ziko kila kona ya jiji la dar-es-Salaam... Hivi baada ya miaka kadhaa ukakutwa na cancer ya mapafu. Hayo ni mapenzi ya Mungu??
Hivi ndugu hatujiulizi kwa nini wazungu average wanaishi miaka mingi kuliko wa-Afrika????
Ukijiuliza hilo, utajua kwamba vifo vingi sisi waafrica tunaweza kuviepuka. Ila tatizo hakuna sheria, na mikakati ya kupunguza hivi vifo.
Wahisani, wanaleta misaada ya Malaria na ukimwi. Wajanja wanakula. Leo hii kila baada ya dakika Africa mtoto anakufa kwa Malaria. Hii nayo ni mipango ya Mungu????
1)Tuseme Umepanda basi unaelekea mwanza. Huko Barabarani hakuna sheria za uendeshaji high_way (na kama zipo hazifuatwi). Uko kwenye basi na dereva anakimbiza vibaya mno... Wakati huo huo tunajua mabasi mengi yanatumia matairi ya kichina ambayo sio imara (tanzania hakuna chombo kinachokagua, wamiliki wa mabasi watumie matairi gani, kwa usalama wa raia)... Punde basi likipinduka, watu wakafa. Hayo ni mapenzi ya Mungu????
2)Unaumwa tumbo. unaenda pharmacy kununua pain killers. Huko dukani pamejaa madawa feki na mengine yame-expire. Baada ya miaka michache unagundulika na cancer... Hayo ni mapenzi ya Mungu???
3) Wana_reseach wameandika, magari mabaovu Ndio chanzo cha magonjwa mengi yatokanayo na mfumo wa hewa. Kutokana na uchakavu wa injini. Moshi wa magari chakavu ni hatari kwa maisha ya binadamu.... Haya Unaishi Tanzania nchi ambayo haina sheria ya magari chakavu. Foleni ziko kila kona ya jiji la dar-es-Salaam... Hivi baada ya miaka kadhaa ukakutwa na cancer ya mapafu. Hayo ni mapenzi ya Mungu??
Hivi ndugu hatujiulizi kwa nini wazungu average wanaishi miaka mingi kuliko wa-Afrika????
Ukijiuliza hilo, utajua kwamba vifo vingi sisi waafrica tunaweza kuviepuka. Ila tatizo hakuna sheria, na mikakati ya kupunguza hivi vifo.
Wahisani, wanaleta misaada ya Malaria na ukimwi. Wajanja wanakula. Leo hii kila baada ya dakika Africa mtoto anakufa kwa Malaria. Hii nayo ni mipango ya Mungu????