Boban kuikosa Yanga, atimkia Sweden
Clara Alphonce
KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi 'Boban' kwa mara ya kwanza anaikosa mechi ya Yanga baada ya kuondoka jana kwenda Sweden kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutokea Nairobi Boban alisema kuwa anaenda kwenye majaribio Sweden kwa mwezi mmoja katika klabu ya Dakurd.
"Niko Nairobi hapa napumzika safari inaendelea tena jioni kwenda Sweden ndio hivyo bwana naikosa mechi hiyo da sina jinsi," alisema Boban.
Alisema kuwa anasikitika sana kuikosa mechi hiyo kwani alikuwa na hamu nayo kwani safari hii tumepania kuwafunga baada ya kushindwa kuwafunga katika msimu uliyopita.
Pamoja na hayo Boban alisema kuwa bado anaimani kubwa na kikosi cha Simba msimu huu na anaamini kuwa watashinda katika mechi hiyo ambayo inasubiliwa na mashabiki wa pande zate mbili.
Hata hivyo alisema kuwa kwa sasa ameamua kuelekeza akili yake katika majaribio hayo iliaweze kufanya vizuri na kupata timu huo ya kuchezea.
KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi 'Boban' kwa mara ya kwanza anaikosa mechi ya Yanga baada ya kuondoka jana kwenda Sweden kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutokea Nairobi Boban alisema kuwa anaenda kwenye majaribio Sweden kwa mwezi mmoja katika klabu ya Dakurd.
"Niko Nairobi hapa napumzika safari inaendelea tena jioni kwenda Sweden ndio hivyo bwana naikosa mechi hiyo da sina jinsi," alisema Boban.
Alisema kuwa anasikitika sana kuikosa mechi hiyo kwani alikuwa na hamu nayo kwani safari hii tumepania kuwafunga baada ya kushindwa kuwafunga katika msimu uliyopita.
Pamoja na hayo Boban alisema kuwa bado anaimani kubwa na kikosi cha Simba msimu huu na anaamini kuwa watashinda katika mechi hiyo ambayo inasubiliwa na mashabiki wa pande zate mbili.
Hata hivyo alisema kuwa kwa sasa ameamua kuelekeza akili yake katika majaribio hayo iliaweze kufanya vizuri na kupata timu huo ya kuchezea.