Go Magufuli Go - Mabadiliko yana Gharama na Maumivu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
john-magufuli.jpg

Mwanzoni kabisa baada ya kuchaguliwa kwa Magufuli na kazi ilipoanza nilisema kitu ambacho sidhani kama watu wengi walielewa au walidhani nasema tu kwa sababu ya ushabiki. Nchi yetu ilipokuwa imefikia kiongozi yeyote ambaye alikuwa anakuja kuupokea uongozi uliopita jukumu lake la kwanza kabisa lilikuwa ni kusafisha; kuleta nidhamu na kubwa zaidi kupambana na ufisadi kama simba mbele swala. Sidhani kama watu walitegemea shock and awe ambayo inaendelea sasa nchini na labda inakwaza watu wengi.

Ni lazima tutambue kabisa kabla ya watu kupewa majumu sasa na bajeti mpya ya nini kinaenda kufanywa mwaka wa kwanza wa Magufuli ni lazima mianya yote izibwe kwanza, viongozi matatizo wachomolewe, na fedha ambazo zililiwa au kuchomolewa zirejeshwe. Ni lazima tuelewe kwanini kuna mkazo sana wa kuhakikisha fedha zinarudishwa kabla watu hawajapelekwa mahakamani. Ni rahisi zaidi kumpeleka mtu mahakamani kuliko kumfanya arudishe fedha!

Ni kweli itauma, ni kweli tutashangaa "duh" na wakati mwingine tunaweza hat akuhisi "eeh mbona anamgusa na huyu" lakini kama nilivyosema wakati ule "tengua tengua" bado ipo,, inakuja na hadi hivi sasa sidhani kama hata robo ya uchafu ulioharibu taifa letu umeshughulikiwa. Litagusa hata watu tunaowaheshimu au kuwapenda lakini tuliposhangilia aliposema "atatumbua majipu" tukumbuke hakusema majipu ya wengine tu! Au majipu ya maadui zetu tu. Yakianza kutumbuliwa ya nyumbani mwetu, marafiki zetu, jamaa zetu kama nilivyosema wakati ule tugune tu lakini ndiyo hivyo; "hakuna namna nyingine".

MMM
 
Mungu mwema na ktk hili ndiye anaefanya con faida kiukwel ya kufunga mtu wakat hela haijarud tunamambo mengi kwel hela zrud kwanza huko mahamani nbaadae
 
...hata sioni jipya kwenye ulichoandika,kwani huu sio muda wa kubeba box? au upo likizo?!
 
Watumbuliwe tuu. Hakuna namna nyingine.

Tunahitaji kurudisha heshima ya utumishi wa umma. Haiwezekani mtu unakuwa public servant na una-expect uwe tajiri. Kama unataka kuwa tajiri nenda sekta binafsi. Kelele nyingi zitapigwa..ohh..ni visasi..na mengineyo. Lakini ukweli unabaki pale pale. Wengi tulijisahau. Na kama wasemavyo waswahili..hakuna marefu yasiyo na mwisho. Ngoja akina Kitilya waanze kubebwa kwenye karandinga ndo mtajua watumishi wetu walikuwa wamekubuhu kwa ujangili wa mali ya umma. Go Magufuli ...goooo...
 
Anachofanya hakikwepeki. Hatuwezi kupata maendeleo kama tunafanyamambo tulivyozoea kufanya. Tumepoteza mabilion ya shilling sababu za ufujaji na kulinda wabadhilifu. Hii jamii itashindwa kwenda mbele pamoja kama wizi utaendelea kulelewa kwa maneno na misemo mbalimbali.
Tunamuombea kila la kheri
 
Ni kweli itauma, ni kweli tutashangaa "duh" na wakati mwingine tunaweza hat akuhisi "eeh mbona anamgusa na huyu" lakini kama nilivyosema wakati ule "tengua tengua" bado ipo,, inakuja na hadi hivi sasa sidhani kama hata robo ya uchafu ulioharibu taifa letu umeshughulikiwa. Litagusa hata watu tunaowaheshimu au kuwapenda lakini tuliposhangilia aliposema "atatumbua majipu" tukumbuke hakusema majipu ya wengine tu! Au majipu ya maadui zetu tu. Yakianza kutumbuliwa ya nyumbani mwetu, marafiki zetu, jamaa zetu kama nilivyosema wakati ule tugune tu lakini ndiyo hivyo; "hakuna namna nyingine".

MMM

Ni mtazamo mzuri kuwa na matumaini mema (optimism). Lakini tunahitaji pia mkakati wa kuondoa saratani ambayo imesambaa katika jamii ya Watz ile ya mtazamo kuwa rushwa, ufisadi (wa mapapa na vidagaa), pamoja na mawazo ya kupata vya haraka haraka kwa njia yoyote ile hasa zisizo halali - safari ni ndefu!
 
Fisadi Lowasa hakwepi huu mzunguko ni lazima utamfikia ni swala la muda tu!
Mimi nilishasema hii nchi inahitaji maridhiano, makubaliano na kusameheana watu waanze upya.

Utatumbuaje jipu na wewe mwenyewe jipu. Haki ikitendeka huyo mtumbuaji jipu naye atapona?

Tumekuwa taifa la miamuma iliokubuhu . Yani wewe jipu halaf unatumbua majipu mengine. Unamkomoa nani sasa?
 
Hhahahahaha....Na sisi ndicho tunachotaka...Mafisadi wote wafungwe...safi sana Magufuli...Hatutaki Porojo za mitandaoni...Oooh fisadi oooh nini...Kama ni fisadi afungwe
na yeye pia ajifunge. Mnaendekeza sanaa
 
Ni mtazamo mzuri kuwa na matumaini mema (optimism). Lakini tunahitaji pia mkakati wa kuondoa saratani ambayo imesambaa katika jamii ya Watz ile ya mtazamo kuwa rushwa, ufisadi (wa mapapa na vidagaa), pamoja na mawazo ya kupata vya haraka haraka kwa njia yoyote ile hasa zisizo halali - safari ni ndefu!
Kamwe haitawezekana chini ya CCM labda CCM ya Nyerere ingerudi
 
MM unajua kabisa hapa wale wazee wa kuzungusha umewachokonoa, subiri waje .
 
Nampongeza ndg. Rais kwa kuendelea na kazi nzito ya kushughulika na majipu. Ili mfumo uwe sawa, na sisi wa chini huku ambao tunamwelewa ndg. Rais tumsaidie japo kwa kupambana na vipele. Kama ukiona kipele au kichunusi kwenye maeneo yako ya kazi na unakimudu, haraka sana kitumbue tuu kabla hakijawa jipu. Ukiona jipu haraka sana mtaarifu mtumbua majipu.
 
Mwanzoni kabisa baada ya kuchaguliwa kwa Magufuli na kazi ilipoanza nilisema kitu ambacho sidhani kama watu wengi walielewa au walidhani nasema tu kwa sababu ya ushabiki. Nchi yetu ilipokuwa imefikia kiongozi yeyote ambaye alikuwa anakuja kuupokea uongozi uliopita jukumu lake la kwanza kabisa lilikuwa ni kusafisha; kuleta nidhamu na kubwa zaidi kupambana na ufisadi kama simba mbele swala. Sidhani kama watu walitegemea shock and awe ambayo inaendelea sasa nchini na labda inakwaza watu wengi.

.....
Ni kweli itauma, ni kweli tutashangaa "duh" na wakati mwingine tunaweza hat akuhisi "eeh mbona anamgusa na huyu" lakini kama nilivyosema wakati ule "tengua tengua" bado ipo,, inakuja na hadi hivi sasa sidhani kama hata robo ya uchafu ulioharibu taifa letu umeshughulikiwa. ... "hakuna namna nyingine".

MMM

Tengua tengua ya zile nyumba za serikali walizozininii vipi? Inakuja pia?
Mkapa alienda ikulu kuomba kibarua cha kufanya, unafikiri Magu atampatia Mkapa kibarua cha kuhakikisha zile nyumba zinarudi tena serikalini?

Maumivu yakizidi, lima kwa meno!
 
Back
Top Bottom