global publishers mnalipwa na nani kwa hii kazi?

babukijana

JF-Expert Member
Jul 21, 2009
13,112
16,012
Gazeti pendwa la Amani linakwenda mbele zaidi kwa kueleza mkakati mzima, jinsi kituo hicho cha ngono cha vigogo, kilichopo ndani ya ofisi ya Massage Centre, iliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam ilivyofanyiwa upepelelezi kwa miezi sita kabla ya kufumuliwa rasmi Jumamosi iliyopita (Septemba 26, 2009).

Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi, Machi mwaka huu, kituo hicho cha uchuaji kilibainika kujihusisha na utoaji wa huduma ya ngono kwa siri na katika hilo, tahadhari ya hali ya juu ilichukuliwa.

Vyanzo vya awali vilipasha kwamba huduma ya ngono haikuwa na maelezo mapokezi, badala yake mteja akiwa chumbani anafanyiwa ‘massage’ anaruhusiwa kunong’ona na mhudumu kisha kuongeza hela ili apate huduma ya ‘jumla’.

Ilielezwa pia kwamba kwa wateja wazoefu ambao walikwishawahi kuhudumiwa ngono kituoni hapo, walikuwa na uhuru wa kuulizia ‘kamchezo hako’ hata mapokezi au kwa njia ya simu kwa sababu hawakuwa wakitiliwa shaka yoyote.

Kufuatia hali hiyo, chanzo chetu kilibainisha kwamba kwa mteja mzoefu alipotaka kuhudumiwa ngono, alipofika mapokezi aliulizia ‘full massage’, kauli ambayo ilieleweka vizuri kwa mhudumu.

Aidha, uchunguzi ulibaini kwamba kwa mteja wa ‘full massage’, alikuwa akipewa upendeleo zaidi kwa kuwa fedha anazolipa ni nyingi ambazo zinakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya mhudumu wakati kwa huduma ya massage, kiasi kikubwa ni cha mmiliki.

Kutokana na ‘data’ hizo, Machi mwaka huu, kitengo cha waandishi wa habari za uchunguzi kwenye Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, kilituma mtu ndani ya kituo hicho na kuambulia majibu hasi.

Mchunguzi huyo wa Global ambayo inachapisha magazeti ya Amani, Uwazi, Ijumaa, Risasi, Ijumaa Wikienda na Championi, alipofika kituoni hapo aliulizia huduma ya ‘full massage’ lakini wahudumu ‘walimtolea nje’ kwamba hakuna biashara ya ngono wanayoifanya.

Kutokana na majibu hayo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kilituma watu wengine watatu kwa nyakati tofauti ambao waliingia kwenye kituo hicho na kugundua kuwa, biashara hiyo ilikuwa inafanyika ndani kwa ndani, pengine bila hata mmiliki kujua.

Katika ripoti ya wachunguzi hao ndani ya kituo hicho, ilibainika kuwa watu ambao huingia kwenye jengo hilo la massage na kupata huduma ya ngono wengi wao ni vigogo kwa sababu ndiyo wanaoweza kumudu gharama.

Ilibainika pia kwamba watumishi wenye hadhi kubwa serikalini, wafanyakazi kwenye taasisi zinazolipa mishahara mikubwa na wafanyabiashara wakubwa au mapedeshee ndiyo ambao huingia kwa kificho kwenye kituo hicho na kupata huduma ya full massage.

Kutokana na kukusanya vielelezo hivyo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kiliwasiliana na Jeshi la Polisi Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam na kuandaa mikakati ya kukifumua kituo hicho cha ngono cha vigogo.

Katika mkakati wa pamoja kati ya Polisi Oysterbay na kitengo cha habari za uchunguzi cha Kampuni ya Global, alipangwa mtu kuingia ndani ya kituo hicho kama mhudumiwa wa full massage ambaye alitakiwa ‘kubip’ simu ya kiongozi wa msafara pale mambo yatakapoiva.

Sanjari na ‘infoma’ huyo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kilipandikiza mtu ndani ya kituo hicho ambaye alikuwa akivijisha taarifa za hali ya mambo yanayoendelea hatua kwa hatu.

Kwa kawaida, kituo hicho hufunguliwa asubuhi na kufanyakazi mpaka saa 2 jioni na katika siku hiyo ya ‘oparesheni’, ilipofika saa 1:57 jioni, ‘infoma’ aliingia ndani na kuomba huduma ya fulla massage.

Saa 2:09 jioni, eneo lote la Stendi ya Makumbusho lilikuwa chini ya askari wa kutosha, waliovaa kijeshi na wengine kiraia na ilipofika saa 2:21, infoma alibipu hivyo kuonesha kwamba chumbani mambo yalikuwa yamekwishaiva.

Ilipofika saa 2:30, kituo chote kilikuwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi ambapo wahudumu wawili walikutwa wakiwa uchi kama walivyozaliwa vyumbani, hali iliyotoa picha ya wazi kuwa, walikuwa wakitoa huduma ya full massage kwa wateja.

Katika uvamizi huo, mbali na infoma aliyepandikizwa na kitengo cha habari za uchunguzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi, alikutwa mteja mwingine halisi aliyenaswa chumbani na mhudumu, wote wakiwa watupu kama walivyozaliwa.

Baada ya kamata kamata, iliyochukua dakika kadhaa, polisi waliwakamata wahudumu waliokutwa uchi vyumbani wakiwa kwenye taswira ya kutoa huduma ya ngono kwa wateja wao. Habari kutoka Oysterbay Dar es Salaam juzi, zilisema kuwa wahudumu waliokutwa uchi vyumbani tayari wamepelekwa kwenye Mahakama ya Jiji kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

KUTOKA KWA MHARIRI Lengo la Kampuni ya magazeti ya Global kufuatilia uovu unaofanyika kwenye massage centre jijini Dar ni kuhakikisha jamii inaishi kwa maadili mema na kuepuka maambukizi ya gonjwa hatari la Ukimwi.

Aidha, Global inalipongeza jeshi la polisi nchini, mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Kamanda wa mkoa huo, Mark Karunguyeye, OC-CID, Damas Nyanda, Inspekta Peter Ng’eni na wengine wote kwa kutoa ushirikiano wa hali ya juu katika kufanikisha zoezi hilo na mengine yaliyotangulia.
 
Last edited:
Gazeti pendwa la Amani linakwenda mbele zaidi kwa kueleza mkakati mzima, jinsi kituo hicho cha ngono cha vigogo, kilichopo ndani ya ofisi ya Massage Centre, iliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam ilivyofanyiwa upepelelezi kwa miezi sita kabla ya kufumuliwa rasmi Jumamosi iliyopita (Septemba 26, 2009).

Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi, Machi mwaka huu, kituo hicho cha uchuaji kilibainika kujihusisha na utoaji wa huduma ya ngono kwa siri na katika hilo, tahadhari ya hali ya juu ilichukuliwa.

Vyanzo vya awali vilipasha kwamba huduma ya ngono haikuwa na maelezo mapokezi, badala yake mteja akiwa chumbani anafanyiwa ‘massage' anaruhusiwa kunong'ona na mhudumu kisha kuongeza hela ili apate huduma ya ‘jumla'.

Ilielezwa pia kwamba kwa wateja wazoefu ambao walikwishawahi kuhudumiwa ngono kituoni hapo, walikuwa na uhuru wa kuulizia ‘kamchezo hako' hata mapokezi au kwa njia ya simu kwa sababu hawakuwa wakitiliwa shaka yoyote.

Kufuatia hali hiyo, chanzo chetu kilibainisha kwamba kwa mteja mzoefu alipotaka kuhudumiwa ngono, alipofika mapokezi aliulizia ‘full massage', kauli ambayo ilieleweka vizuri kwa mhudumu.

Aidha, uchunguzi ulibaini kwamba kwa mteja wa ‘full massage', alikuwa akipewa upendeleo zaidi kwa kuwa fedha anazolipa ni nyingi ambazo zinakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya mhudumu wakati kwa huduma ya massage, kiasi kikubwa ni cha mmiliki.

Kutokana na ‘data' hizo, Machi mwaka huu, kitengo cha waandishi wa habari za uchunguzi kwenye Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, kilituma mtu ndani ya kituo hicho na kuambulia majibu hasi.

Mchunguzi huyo wa Global ambayo inachapisha magazeti ya Amani, Uwazi, Ijumaa, Risasi, Ijumaa Wikienda na Championi, alipofika kituoni hapo aliulizia huduma ya ‘full massage' lakini wahudumu ‘walimtolea nje' kwamba hakuna biashara ya ngono wanayoifanya.

Kutokana na majibu hayo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kilituma watu wengine watatu kwa nyakati tofauti ambao waliingia kwenye kituo hicho na kugundua kuwa, biashara hiyo ilikuwa inafanyika ndani kwa ndani, pengine bila hata mmiliki kujua.

Katika ripoti ya wachunguzi hao ndani ya kituo hicho, ilibainika kuwa watu ambao huingia kwenye jengo hilo la massage na kupata huduma ya ngono wengi wao ni vigogo kwa sababu ndiyo wanaoweza kumudu gharama.

Ilibainika pia kwamba watumishi wenye hadhi kubwa serikalini, wafanyakazi kwenye taasisi zinazolipa mishahara mikubwa na wafanyabiashara wakubwa au mapedeshee ndiyo ambao huingia kwa kificho kwenye kituo hicho na kupata huduma ya full massage.

Kutokana na kukusanya vielelezo hivyo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kiliwasiliana na Jeshi la Polisi Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam na kuandaa mikakati ya kukifumua kituo hicho cha ngono cha vigogo.

Katika mkakati wa pamoja kati ya Polisi Oysterbay na kitengo cha habari za uchunguzi cha Kampuni ya Global, alipangwa mtu kuingia ndani ya kituo hicho kama mhudumiwa wa full massage ambaye alitakiwa ‘kubip' simu ya kiongozi wa msafara pale mambo yatakapoiva.

Sanjari na ‘infoma' huyo, kitengo hicho cha habari za uchunguzi kilipandikiza mtu ndani ya kituo hicho ambaye alikuwa akivijisha taarifa za hali ya mambo yanayoendelea hatua kwa hatu.

Kwa kawaida, kituo hicho hufunguliwa asubuhi na kufanyakazi mpaka saa 2 jioni na katika siku hiyo ya ‘oparesheni', ilipofika saa 1:57 jioni, ‘infoma' aliingia ndani na kuomba huduma ya fulla massage.

Saa 2:09 jioni, eneo lote la Stendi ya Makumbusho lilikuwa chini ya askari wa kutosha, waliovaa kijeshi na wengine kiraia na ilipofika saa 2:21, infoma alibipu hivyo kuonesha kwamba chumbani mambo yalikuwa yamekwishaiva.

Ilipofika saa 2:30, kituo chote kilikuwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi ambapo wahudumu wawili walikutwa wakiwa uchi kama walivyozaliwa vyumbani, hali iliyotoa picha ya wazi kuwa, walikuwa wakitoa huduma ya full massage kwa wateja.

Katika uvamizi huo, mbali na infoma aliyepandikizwa na kitengo cha habari za uchunguzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi, alikutwa mteja mwingine halisi aliyenaswa chumbani na mhudumu, wote wakiwa watupu kama walivyozaliwa.

Baada ya kamata kamata, iliyochukua dakika kadhaa, polisi waliwakamata wahudumu waliokutwa uchi vyumbani wakiwa kwenye taswira ya kutoa huduma ya ngono kwa wateja wao. Habari kutoka Oysterbay Dar es Salaam juzi, zilisema kuwa wahudumu waliokutwa uchi vyumbani tayari wamepelekwa kwenye Mahakama ya Jiji kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

KUTOKA KWA MHARIRI Lengo la Kampuni ya magazeti ya Global kufuatilia uovu unaofanyika kwenye massage centre jijini Dar ni kuhakikisha jamii inaishi kwa maadili mema na kuepuka maambukizi ya gonjwa hatari la Ukimwi.

Aidha, Global inalipongeza jeshi la polisi nchini, mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Kamanda wa mkoa huo, Mark Karunguyeye, OC-CID, Damas Nyanda, Inspekta Peter Ng'eni na wengine wote kwa kutoa ushirikiano wa hali ya juu katika kufanikisha zoezi hilo na mengine yaliyotangulia.
kilamara nimekua nikiangalia hawa waandishi wa magazeti ya udaku na kusoma habari za wao kufuatilia haya mambo ya ngono kwenye massage parlour na naishia kushangaa tu,nashindwa kuelewa ni kukosa kazi ama nini maana hii ni too much na kwa akili yangu mimi hii ni kuingilia uhuru wa watu sasa,hii imetokea wiki hii,kuna ingine waliwafanyia wachina na nyingine msasani sijui sasa nashindwa kuelewa hawa waandishi lengo lao hasa ni nini?halafu kinachonishangaza zaidi ni namna wanavyofanya uchunguzi wao then ndio wawataarifu Polisi halafu polisi wakikamata watuhumiwa huwa hatuoni kilichoendelea zaidi ya kuja kushtuka pale wanapofanya mpango mwingine kama huo,maswali yanakuja pale polisi wanaoshirikiana katika hiyo kazi yao ni walewale na kituo ni kilekile hapa lazima kuna namna.hizo kesi mbona huwa hamripoti ilnavyoendelea hadi kuisha?maana sasa hii ni kuingilia uhuru wa raia watu washindwe kufanya shughuli zao kwaajili ya hawa waandishi,nadhani hapo bongo kila mtu ana uhuru wa kufanya anachohitaji almradi asivunje sheria na wanafanya mambo yao kifichoni na kwa makubaliano yao wenyewe na mteja hakuna anayemlazimisha mwenzie sasa ya nini kuwaingilia?hii si haki kabisa na ni unyanyasaji wa raia wenzenu pasipo kuwa na mantiki yoyote ya kufanya hivyo,kama ni uovu hapo global pamejaa uozo wa kila aina ni basi tu watu wanakaa kimya.BADILIKENI MNAKERA SANAAAA
 
Walisema 'uvamizi' sidhani hata kulikuwa na search warrant hapo,ni kiasi cha wamiliki kuwachukulia hatua za kisheria kama palikuwa hamna warrant,Global publishers wameharibu maisha ya watu wengi,mbona hawavamii massage parlours za muheshimiwa mmoja wa kike zilizopo Regent na Namanga?
 
Global publishers kufuatilia mambo ya ndani ya massage parlours ni upuuzi, kwani wote wanaofanyakazi humo na wanaokwenda kupata huduma ni watu wazima na wana uhuru na haki ya kufanya mambo yao bila bughuza. Acheni kufuatilia mambo binafsi ya watu nendeni Kigoma na Kagera kule msituni magari yanakovamiwa kila siku chunguzeni hao watu na toeni taarifa polisi wawashughulikie
 
nadhani hao waandishi cheap alionao huyu jamaa ndio wanaomuangusha,na ukikutana nao wanajiona ni kama wale paparazi walimsababishia kifo queen diana,yaani hapo global jamaa ni wakuja kuanzia mkurugenzi mpaka mfagia ofisi,mi imeniuzi sana,sishiriki wala sipo TZ lakini issue hizi ni mbaya sana watu wangapi wameachwa na wachumba wao kwa ajili ya story zao hizi za kilevi,waandishi nadhani wanalazimishwa kutafuta story na mkurugenzi almradi gazeti liuze,lakini sio kihivyo,mi mmojawapo wa waathirika wa haya magazeti ya huyu jamaa,siwezi kusema nini kilitokea lakini hawa waandishi wanatakiwa waangalie kwamba kuna kesho,huwezi ukamuandika mtu kwa story ya kashfa kisha unamuwahi nyumbani kabla gazeti halijatoka umpe hongo ili akiona story kesho yake asishangae
 
Actually magazeti yenyewe ni vizuri kuyasoma online sababu ni bure, otherwise siwezi kuspend few shs zangu. Pia naona huyu jamaa anawatuma waandishi wake wafanye hayo mambo. OR kuna issue personal maana kuna msomaji amesema ile ya Regent haifuatilii. Hapo hakuna kesi kwani hawajavunja sheria, wamefanya falagha, hakuna aliyebakwa, yaani ni ushamba tu wa hao waandishi na Mkurugenzi wao.
Mteja.
 
Wa kulaumiwa ni Serikali kuruhusu magazeti ya aina hiyo. Shigongo anaandika kitu kinachoshabikiwa na wengi. Ingawa sina takwimu lakini magazeti yake yanasomwa na Watanzania wengi tu. Tena si ajabu kuliko magazeti mengine. Kama ni pesa anazipata kwa uongo na ukweli wa magazeti yake. Hata Mengi amewahi kuyaanzisha yakamshinda (Kasheshe).
 
Back
Top Bottom