Gharama za kwenda Serengeti na Ngorongoro kwa mapumziko ni kiasi gani?

frozen

Senior Member
Aug 12, 2010
135
32
Habari wanajamii,
naitaji kufahamu gharama za mtu mmoja kwenda na kurudi serengeti na ngorongoro...kuanzia gharama za usafiri, malazi, chakula na gharama za matembezi ukiwa katika sehemu hizi za utalii
mwenye taarifa ntashukuru akinijuza hapa.
Asante sana
 
Kuna option mbili ya kwanza kama unakwenda ngorongoro crater panda basi hadi arusha ukifika arusha panda noha hadi karatu , ukifika karatu unatafuta guest house nzuri ya ukweli ni kama 10,000/= hadi 15,000/= (nauli ya noha ni 6000/= hadi 8000/= arusha karatu) halafu unakodi gari ya kukupeleka ngorongoro tdi au mkonga nje ni kati ya 80000/= hadi 150000/= unazungushawa siku nzima crater, ukiwa tayari nina watu nawafahamu wanaweza kukupokeya karatu na kukusadiya katika swala hilo
 
Hutapata majibu kwenye hii thread, inaelekea watu wengi hawana utamaduni wa kwenda vacation. Hata mimi nilijaribu kutafuta info za vacation humu sikupata wachangiaji
 
OPOTION YA PILI UNAKODI GARI LA TOURS TOKA ARUSHA WANAKUPA FULL PACKAGE YA AMBAYO INAJUMUISHA GHARAMA ZA USAFIRI MALAZI NA CHAKULA KWA SIKU UTAKAZO TAKA HOTEL UTAPELEKWA HOTEL ZA KIZUNGU NA ZA WAKUBWA aka wanene. NA UTALIPA DOLLARS
 
Kuna option mbili ya kwanza kama unakwenda ngorongoro crater panda basi hadi arusha ukifika arusha panda noha hadi karatu , ukifika karatu unatafuta guest house nzuri ya ukweli ni kama 10,000/= hadi 15,000/= (nauli ya noha ni 6000/= hadi 8000/= arusha karatu) halafu unakodi gari ya kukupeleka ngorongoro tdi au mkonga nje ni kati ya 80000/= hadi 150000/= unazungushawa siku nzima crater, ukiwa tayari nina watu nawafahamu wanaweza kukupokeya karatu na kukusadiya katika swala hilo

Huu ni ushauri mzuri na wa bei rahisi. Niliwahi kupita Ngorongoro nikiwa nasafiri kutoka DAR kwenda Mwanza na gari la binafsi na tulilala Karatu gesti nzuri bei ilikuwa 8000 mwaka 2006. Ila usiku ule majira ya saa 2 kulikuwa na milio ya bunduki, kumbe ni majambazi walivamia duka moja hapo mjini. Ni vizuri akalala Hotelini kwenye usalama zaidi. Na kisha akodi gari la tours kama ulivyomshauri kwa siku na bei ni hiyo around 150K.

OPOTION YA PILI UNAKODI GARI LA TOURS TOKA ARUSHA WANAKUPA FULL PACKAGE YA AMBAYO INAJUMUISHA GHARAMA ZA USAFIRI MALAZI NA CHAKULA KWA SIKU UTAKAZO TAKA HOTEL UTAPELEKWA HOTEL ZA KIZUNGU NA ZA WAKUBWA aka wanene. NA UTALIPA DOLLARS

Hii option ni ghali sana ila inategemea na kamba yake. Kama ni ndefu basi afanye hivyo. It is more safe and comfortable
 
mtu mmoja ni ghali zaidi hasa huduma ambazo ni sharable kama gari.
 
Kama naenda na wife na mtoto kwa mfano halafu mimi najifikisha hapo Karatu nachukua Hoteli gharama za kunipeleka huko Mbugani na kurudi inakuwa how much?
 
Mkuu kwa Mtanzania wa kawaida ambaye si Fisadi kwenda Polini kutalii kwa kutumia magari ya Watalii ni ghali sana na ndo maana TANAPA WANAJARIBU KUHAMASISHA KWA WATU KWENDA KWA KUTUMIA USAFIRI WA TANAPA ILA NI KWA BAADHI YA HIFADHI AMBAZO SI ZA KULALA HUKO MFANO
1. ARUSHA NATIONAL PARK

2. TARANGIRE

3. LAKE MANYARA

KWA UPANDE WA NGORONGORO WAO HAWANA HUO UTARATIBU NA UKIZINGATIA KWAMBA TANAPA NA NGORONGORO CONSERVATION AREA NI VITU VIWILI TOFAUTI,

ILA KAMA JAMAA ALIVYO SEMA HAPO UNAWEZA TUMIA OPTIONAL HIZO, ILA KWA KUONGEZEA

1. KWA HIFADHI ZA TARANGIRE, MANAYARA NA ARUSHA NATIONLA PARK HAKUNA SHIDA KABISA MAKE SEHEMU YA KULALA INAPATIKANA

TARANGIRE- Hapa unaweza kwenda na gari lako au la kukodi na ukarudi kulala either Arusha town, Babati town, Mto wa mbu au Karatu

2. MANYARA NATIONAL PARK- Hapa unaweza kwenda kwa usafiri wako au wa kukodi na ukarudi kulala Mto wa mbu, Karatu au Arusha Town

3. ARUSHA NATIONAL PARK- Hii ndi hifadhi cheap kwan unaweza hata kwenda na mark II yako na ukarudi kulala A town

4. NGORONGORO- Hii unaweza tumia usafiri wako au wa kukodi, ila kama ni usafiri wako hakikisha ni gari la 4WD vinginevyo hutaruhusiwa kushuka creter, na hata kama wewe ndo Dreva na gari ni la 4WD ni lazima uwe na mtu mzoefu akuendeshe zile barabara ni noma hukawii kupiga chini na gari lako, na MADREVA wageni wengi wanaopita hizo njia kwenda hata MUSOMA HUWA WENGI WANAPATA MISUKOSUKO SANA

KULALA- Hapa kama umekodi gari ni lazima uwe na pesa ya kutosha na isiwe ya mawazo hapo unaweza lala hoteli kama SERENA, CRETER LODGE, NGORONGORO WILDLIFE LODGE, SOPA LODGE NA KAZALIKA HAPA UKITAKA BEI ZAO WEWE google tu zipo na huitaji kusimiliwa, ILA NI GHALI SANA TENA SANA WAPO HATA WAZUNGU WANAOSHINDWA HIZO BEI ZA KULALA
KULALA- Au unaweza lala sehemu inaitwa KIMBA kwa wamasai ni gest house ila haiko freshi, au urudi kulala KARATU

5, SERENGETI- Hii ndo hifadhi Ngumu kuriko zote na hapa ni lazima ujipange vya kutosha make kule hakuna UJANJA NI LAZIMA ULALE TU INGAWA KUNA OPTIONAL KIBAO
- Hapa ni lazima ukodo gari za tours au utumie la kwako wewe na familia yako na ni lazima liwe 4WD kwa sabau barabara za kule zina vumbi na mchanga wa kufa mtu so hukawii kukwama na ni lazima uwe na Mzoefu wa kukuendasha kwani SERENGETI NDO HIFADHI YENYE AJARI NYINGI SANA, KAMA WEWE HUNA UELEWA WA ZILE BARABARA KUPIGA CHINI SI KITU CHA KUSHANGAZA KABISA

KULALA- Hoteli za kitalii, SERENA, SERENA KILAWIRA. LOBO WILDLIFE LODGE, SERONERA WILDLIFE LODGE, SOPA LODGE, SERENGETI KEMPISK HOTEL- Hizi hoteli ni ghali sana kwa PESA ZA MAWAZO HUWEZI LALA HUMO

KULALA- Camp KAMA MKO WENGI MNAWEZA NENDA NA MAHEMA YENU AU YA KUKODI NA MKAPIGA CAMP SEHEMU ZIPO ILA NI LAZIMA KULIUPIA MAKE MNAPEWA NA ASKARI WA KUWALINDA MWENYE BUNDUKI MSIJE KUVAMIWA NA TEMBO AU MAJANGIRI

- HOSTEL YA TANAPA- Hii ndo sehemu ya kulala iliyo cheap kuliko zote ila booking inahitajika mapema sana make zinatumiwa sana na wanafunzi na hata wazungu wasio kuwa na uwezo wa kwenda kwenye hoteli kubwa, ILA NI SAFI NA ZINA VIWANGO

- MUGUMU SERENGETI- Hapa manweza maliza kuzunguka makenda kulala KWENYE MJI WA MUGUMU ni kama kilomita 70 kutoka Seronera

SO Mkuu ghalama kubwa ya kwenda kwenye hizo hifadhi mbili iko kwenye kulala na chakula na wala si usafiri magari ya kukodi ya bei che yako mengi sana, ishu ni kulala na chakula, na hata chakula mnaweza beba je kulala?

HOTELI HIZI
SERONERA, LOBO WILDLIFE LODGE, NGORONGORO WILDLIFE LODGE NA MANYARA wakati zikiwa za Serikali kabla ya kuuzwa walikuwa na bei nzuri kwa ajiri ya Watanzania, ila baada ya kuuzwa nazani wamiliki wake hawana huo utaratibu tena
 
OPOTION YA PILI UNAKODI GARI LA TOURS TOKA ARUSHA WANAKUPA FULL PACKAGE YA AMBAYO INAJUMUISHA GHARAMA ZA USAFIRI MALAZI NA CHAKULA KWA SIKU UTAKAZO TAKA HOTEL UTAPELEKWA HOTEL ZA KIZUNGU NA ZA WAKUBWA aka wanene. NA UTALIPA DOLLARS

Hakuna usafiri wa moja kwa moja kutoka Dar...kwa mfano ndege au helikopta?
 
Hakuna usafiri wa moja kwa moja kutoka Dar...kwa mfano ndege au helikopta?

Mkuu ni pesa yako tu,

1. Magari- Unaweza book na wakakufuata Dar ila ni wewe na na hizo kampuni za tours tu

2. Ndege- Unaweza Panda ndege Ndogo lakini zinazo fanya safari kati ya Seronera, Manyara, Arusha, Zanzibar, Dar na kwingineko,

It means Ukipanda hizo ndege hadi seronera utapokelewa na Kampuni ambayo mtakuwa mmesia kubalina nayo na unaweza maliza kutalii ukapanda ndege huko huko Ukarudi Dar

Ila ni lazima ujipange make hapo hakuna cha bei za watanzania wala wageni, waote ni sawa
 
Mkuu ni pesa yako tu,

1. Magari- Unaweza book na wakakufuata Dar ila ni wewe na na hizo kampuni za tours tu

2. Ndege- Unaweza Panda ndege Ndogo lakini zinazo fanya safari kati ya Seronera, Manyara, Arusha, Zanzibar, Dar na kwingineko,

It means Ukipanda hizo ndege hadi seronera utapokelewa na Kampuni ambayo mtakuwa mmesia kubalina nayo na unaweza maliza kutalii ukapanda ndege huko huko Ukarudi Dar

Ila ni lazima ujipange make hapo hakuna cha bei za watanzania wala wageni, waote ni sawa

Asante sana, umekuwa wa msaada mkubwa.

Ningepata mtu wa kunipa makadirio ya hiyo safari kwa ndege ningeshukuru mno pia
 
Mkuu kwa Mtanzania wa kawaida ambaye si Fisadi kwenda Polini kutalii kwa kutumia magari ya Watalii ni ghali sana na ndo maana TANAPA WANAJARIBU KUHAMASISHA KWA WATU KWENDA KWA KUTUMIA USAFIRI WA TANAPA ILA NI KWA BAADHI YA HIFADHI AMBAZO SI ZA KULALA HUKO MFANO
1. ARUSHA NATIONAL PARK

2. TARANGIRE

3. LAKE MANYARA

KWA UPANDE WA NGORONGORO WAO HAWANA HUO UTARATIBU NA UKIZINGATIA KWAMBA TANAPA NA NGORONGORO CONSERVATION AREA NI VITU VIWILI TOFAUTI,

ILA KAMA JAMAA ALIVYO SEMA HAPO UNAWEZA TUMIA OPTIONAL HIZO, ILA KWA KUONGEZEA

1. KWA HIFADHI ZA TARANGIRE, MANAYARA NA ARUSHA NATIONLA PARK HAKUNA SHIDA KABISA MAKE SEHEMU YA KULALA INAPATIKANA

TARANGIRE- Hapa unaweza kwenda na gari lako au la kukodi na ukarudi kulala either Arusha town, Babati town, Mto wa mbu au Karatu

2. MANYARA NATIONAL PARK- Hapa unaweza kwenda kwa usafiri wako au wa kukodi na ukarudi kulala Mto wa mbu, Karatu au Arusha Town

3. ARUSHA NATIONAL PARK- Hii ndi hifadhi cheap kwan unaweza hata kwenda na mark II yako na ukarudi kulala A town

4. NGORONGORO- Hii unaweza tumia usafiri wako au wa kukodi, ila kama ni usafiri wako hakikisha ni gari la 4WD vinginevyo hutaruhusiwa kushuka creter, na hata kama wewe ndo Dreva na gari ni la 4WD ni lazima uwe na mtu mzoefu akuendeshe zile barabara ni noma hukawii kupiga chini na gari lako, na MADREVA wageni wengi wanaopita hizo njia kwenda hata MUSOMA HUWA WENGI WANAPATA MISUKOSUKO SANA

KULALA- Hapa kama umekodi gari ni lazima uwe na pesa ya kutosha na isiwe ya mawazo hapo unaweza lala hoteli kama SERENA, CRETER LODGE, NGORONGORO WILDLIFE LODGE, SOPA LODGE NA KAZALIKA HAPA UKITAKA BEI ZAO WEWE google tu zipo na huitaji kusimiliwa, ILA NI GHALI SANA TENA SANA WAPO HATA WAZUNGU WANAOSHINDWA HIZO BEI ZA KULALA
KULALA- Au unaweza lala sehemu inaitwa KIMBA kwa wamasai ni gest house ila haiko freshi, au urudi kulala KARATU

5, SERENGETI- Hii ndo hifadhi Ngumu kuriko zote na hapa ni lazima ujipange vya kutosha make kule hakuna UJANJA NI LAZIMA ULALE TU INGAWA KUNA OPTIONAL KIBAO
- Hapa ni lazima ukodo gari za tours au utumie la kwako wewe na familia yako na ni lazima liwe 4WD kwa sabau barabara za kule zina vumbi na mchanga wa kufa mtu so hukawii kukwama na ni lazima uwe na Mzoefu wa kukuendasha kwani SERENGETI NDO HIFADHI YENYE AJARI NYINGI SANA, KAMA WEWE HUNA UELEWA WA ZILE BARABARA KUPIGA CHINI SI KITU CHA KUSHANGAZA KABISA

KULALA- Hoteli za kitalii, SERENA, SERENA KILAWIRA. LOBO WILDLIFE LODGE, SERONERA WILDLIFE LODGE, SOPA LODGE, SERENGETI KEMPISK HOTEL- Hizi hoteli ni ghali sana kwa PESA ZA MAWAZO HUWEZI LALA HUMO

KULALA- Camp KAMA MKO WENGI MNAWEZA NENDA NA MAHEMA YENU AU YA KUKODI NA MKAPIGA CAMP SEHEMU ZIPO ILA NI LAZIMA KULIUPIA MAKE MNAPEWA NA ASKARI WA KUWALINDA MWENYE BUNDUKI MSIJE KUVAMIWA NA TEMBO AU MAJANGIRI

- HOSTEL YA TANAPA- Hii ndo sehemu ya kulala iliyo cheap kuliko zote ila booking inahitajika mapema sana make zinatumiwa sana na wanafunzi na hata wazungu wasio kuwa na uwezo wa kwenda kwenye hoteli kubwa, ILA NI SAFI NA ZINA VIWANGO

- MUGUMU SERENGETI- Hapa manweza maliza kuzunguka makenda kulala KWENYE MJI WA MUGUMU ni kama kilomita 70 kutoka Seronera

SO Mkuu ghalama kubwa ya kwenda kwenye hizo hifadhi mbili iko kwenye kulala na chakula na wala si usafiri magari ya kukodi ya bei che yako mengi sana, ishu ni kulala na chakula, na hata chakula mnaweza beba je kulala?

HOTELI HIZI
SERONERA, LOBO WILDLIFE LODGE, NGORONGORO WILDLIFE LODGE NA MANYARA wakati zikiwa za Serikali kabla ya kuuzwa walikuwa na bei nzuri kwa ajiri ya Watanzania, ila baada ya kuuzwa nazani wamiliki wake hawana huo utaratibu tena

ASANTE SANA MKUU,JAPO ULITOA USHAURI SIKU NYINGI LAKINI BADO UNAISHI!!!!
 
Habari wanajamii,
naitaji kufahamu gharama za mtu mmoja kwenda na kurudi serengeti na ngorongoro...kuanzia gharama za usafiri, malazi, chakula na gharama za matembezi ukiwa katika sehemu hizi za utalii
mwenye taarifa ntashukuru akinijuza hapa.
Asante sana
Frozen asante kwa uzi huu walau na mm nimejifunza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
gharama kamili ni bei gani?kama unataka kwenda kutalii kupanda mlima kilimanjaro?
 
Back
Top Bottom