Gambia's public sector to have 4-day working week!

Yes naona kuna logic. Kwa kufanya kazi kwa siku 4 kwa wiki tangu saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni Nisawa na tunaofanya siku 5 kwa wiki tangu saa 2 hadi saa 9.30. Masaa ni yaleyale. Nothing strange
 
Mleta uzi ningekuona wa maana kama ungeongelea umasikini wetu na jinsi CCM ilivyochangia kwa sababu Chadema hajawahi kuwa madarakani na habari za kusherehekea ushindi siku tatu ni mpaka washinde. Lkn miaka 50 Tanzania bado tunatembeza bakuli kuomba, kiwango cha elimu kinashuka kila mwaka, deni la taifa limekuwa kubwa, mtanzania anakula kwa kubahatisha, huduma ya afya imekua mbovu sana bado tunasema chadema. Hizi siasa nadhani zinatupa upofu saa nyingine au na sisi ni sehem ya wachache wanaofaidi
 
........

Kweli wazo zima la uchumi bado halijaeleweka kwetu sisi Waafrika, nafikiri hata hatujui ni nini maana ya uzalishaji!


Gambian President Yahya Jammeh has decreed a four-day working week for public officials, making Friday a day of rest to allow residents in the small West African state more time for prayer and agriculture.
....


I don't get it! Does Agriculture not falling into Economic activities ?
 
[/FONT]
I don't get it! Does Agriculture not falling into Economic activities ?
[/SIZE]

kama lengo lingekuwa ni kuongeza uzalishaji basi angepaswa kuongeza masaa ya kufanya kazi na sio kupunguza!
 
Hili wazo kwa nchi masikini sijui sana kama lina tija kwani kwa umasikini tulokuwa nao unahitaji kufanya kazi kwa bidii sana. Majuzi nimesikia kuna kundi moja limedai hata sisi tuwe na siku ya ijumaa ya mapumziko, sijaelewa kama twaweza kujenga uchumi ulio bora sana katika ulimwengu wa leo.

Kikubwa kilichopo na ninachokiona kwa walio wengi wetu wanaendekeza swala zima la starehe zaidi kuliko kuwaza jinsi ya kutoka. Uchumi unahitaji kujituma sana na si vinginevyo.

Tusiwahukumu Wagambia kwa kudhani sisi tunajua zaidi ya kwao. Inawezekana kabisa wanafanyakazi wanajihusisha na ujasiria mali na hivyo kupewa siku tatu za kufanya shughuli zao. Hapa kwetu wanafanya kazi siku tano mshahara kiduchu na wafanyakazi wanaishia kufanya ufisadi tu. Kama wafanyakazi watazitumia siku tatu za mapumziko kwa kilimo kwa mfano, nchi ikapata mazao mengi ya chakula na biashara, huo umasikini unaweza kupungua sana.
 
Tusiwahukumu Wagambia kwa kudhani sisi tunajua zaidi ya kwao. Inawezekana kabisa wanafanyakazi wanajihusisha na ujasiria mali na hivyo kupewa siku tatu za kufanya shughuli zao. Hapa kwetu wanafanya kazi siku tano mshahara kiduchu na wafanyakazi wanaishia kufanya ufisadi tu. Kama wafanyakazi watazitumia siku tatu za mapumziko kwa kilimo kwa mfano, nchi ikapata mazao mengi ya chakula na biashara, huo umasikini unaweza kupungua sana.

Ndio maana nikasema somo la Uchumi na Uzalishaji bado halijaeleweka kwetu Waafrika na ndio maana hauoni tatizo lilipo, hauwezi kupunguza Umaskini kwenye maskini kama hiyo kwa kupunguza masaa ya kufanya kazi, unapunguza kwa kuongeza masaa ya kufanya kazi tu basi!
 
Yes naona kuna logic. Kwa kufanya kazi kwa siku 4 kwa wiki tangu saa 2 asubuhi hadi saa 12 jioni Nisawa na tunaofanya siku 5 kwa wiki tangu saa 2 hadi saa 9.30. Masaa ni yaleyale. Nothing strange
hivi unafahamu saa 2 hadi saa 9:30 maana yake effectively ni masaa mangapi?
 
mbona wazo zuri tu hili, si kasema ili watu wapate muda wa ibada na kilimo sasa kuna tatizo gani hapa, au ubank teller ndio kazi pekee siku hizi.
 
Sasa hapo CDM imeingiaje???mbona hiki chama kinawakosesha amani mioyoni mwenu
 
Si kila jambo ruksa kuiga,mengine hayana manufaa.Kama tunafanya kazi kwa siku 5 na bado tunaburuza mkia kwenye maendeleo,ikiwa siku nne itakuwaje?Tuache ushabiki,tusilazimishane uvivu!
 
Working hours from 08:00 am to 06: 00 pm Compensate the fifth day dropped. Ni sawa. Nice calculations, Ustadh Yahaya Jumanne.
 
unaweza kuonekana ni uamuzi mbaya kwa nje, lakini na sisi wenyewe tukiutumia mpango huo tunaweza kujiwezesha, kama alivyo sema kutumia muda huo kwenye kilimo, na tukitilia maanani kwamba chakula ni aghali kuanzia mihogo , unga na mboga mboga hivyo muda huo tunaweza kuweka kibustani cha mboga na chumi zetu bado zipo kwenye kilimo, hivyo hata nafasi za kazi ni haba na pia kujenga maana ujenzi wetu ni wa kibinafsi sio makandarasi
 
Since Africans are by nature lazy people, idea of 4-day working week would be very popular not just in Gambia but throughout the continent. You have to remember, before Europeans or other foreigners set foot in Africa, there was no concept of work. People waited for fruits to fall from trees, killed an animal and voila you have food. No hassles. So this politician is on to something with his idea of a 4-day working week.
 
kama lengo lingekuwa ni kuongeza uzalishaji basi angepaswa kuongeza masaa ya kufanya kazi na sio kupunguza!

hivi kuongeza muda wa kufanya kazi ina maana kuongeza uzalishaji?
mimi nadhani muhimu ni kutafuta njia za kuongeza ufanisi katika kazi.

tatizo nilionalo kwa alhadji, prof. dr. gen. jammeh ni kwamba anawalimisha wafanyakazi wa serikali
kwenye mashamba yake. sasa huenda hayo mabadiliko ni kuwapa wafanyakazi kuhudumia mashamba
yao na pia kwenda hudumia mashamba ya rais. (kweli afrika ina kila aina ya watawala)
 
unaweza kuonekana ni uamuzi mbaya kwa nje, lakini na sisi wenyewe tukiutumia mpango huo tunaweza kujiwezesha, kama alivyo sema kutumia muda huo kwenye kilimo, na tukitilia maanani kwamba chakula ni aghali kuanzia mihogo , unga na mboga mboga hivyo muda huo tunaweza kuweka kibustani cha mboga na chumi zetu bado zipo kwenye kilimo, hivyo hata nafasi za kazi ni haba na pia kujenga maana ujenzi wetu ni wa kibinafsi sio makandarasi

Ndio maana nikasema somo la Uchumi au misingi ya Uchumi ambao Dunia nzima inaufuata bado haujaeleweka kwetu Afrika na ndio maana wewe pamoja na Waafrika wengi hawaoni tatizo katika huo uamuzi wa Raisi wa Gambia, lakini kama uamuzi kama huo ungechukuliwa na kiongozi mwingine yoyote nje ya Afrika hata Afrika ya Kaskazini tu ungeona huo moto wake wa watu kulalamika na kusababisha huyu kiongozi kupoteza kazi yake!

Hivyo inaonyesha na kudhihirisha kwamba sisi bado sana!
 
hivi kuongeza muda wa kufanya kazi ina maana kuongeza uzalishaji?
mimi nadhani muhimu ni kutafuta njia za kuongeza ufanisi katika kazi.

tatizo nilionalo kwa alhadji, prof. dr. gen. jammeh ni kwamba anawalimisha wafanyakazi wa serikali
kwenye mashamba yake. sasa huenda hayo mabadiliko ni kuwapa wafanyakazi kuhudumia mashamba
yao na pia kwenda hudumia mashamba ya rais. (kweli afrika ina kila aina ya watawala)

Hilo unaloliongelea wewe ni hatua ya pili ya maendeleo (yaani ufanisi), ambayo sisi hatujafikia bado, kwa hiyo katika ngazi ya chini ya maendeleo kama yetu ambapo ufanisi hauna nafasi au una nafasi ndogo sana ni kufanya kazi tu kwa masaa mengi ndio suluhisho na sio kupunguza!

Ngoja nikupe mfano chukulia Kiwanda cha chuma kama M.M steel, wafanyakazi wake wengi ni vibarua ambao hawana ujuzi (watu wa kupakia na kushusha mizigo, n.k), hivyo kazi zao ni za mikono na ngumu, kwa hiyo namna ya kuongeza uzalishazi M.M Steel ni kwa kuamua wafanyakazi wafanye kazi masaa mengi tu zaidi, unaweza ukapunguza tu masaa ya kufanya kazi kama watu wako wanaofanya kazi wana ujuzi wa kutosha, nikimaanisha kwa upande wa MmM steel kuna metallurgist wa kutosha, wakemia wa kutosha, watu wa kuendesha mashine wenye ujuzi wa kutosha, sasa hapo ndipo unaweza kuingiza hoja ya ufanisi na flexibility kwa maana kazi ile ile ambayo ingefanywa na watu 15 sasa anafanya mtu mmoja, hivyo hauhitaji tena vibarua, lakini ktk nchi ambazo hata mapinduzi ya viwanda hazijaanza bado kama za Afrika huo ufanisi haupo, hivyo kilichopo KWA SASA ni nguvu kazi tu na misuli ya watu, hivyo unavyoamua kupunguza masaa ya kazi inamaana unapunguza uzalishaji na matokeo yake hata wale wachache walioajiriwa kama vibarua pia wanapoteza kidogo walicho nacho!

 
Duuuuuuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!! inaonekana kuweka uzi bila kuitaja CDM hainogi?
 
Ndio maana nikasema somo la Uchumi au misingi ya Uchumi ambao Dunia nzima inaufuata bado haujaeleweka kwetu Afrika na ndio maana wewe pamoja na Waafrika wengi hawaoni tatizo katika huo uamuzi wa Raisi wa Gambia, lakini kama uamuzi kama huo ungechukuliwa na kiongozi mwingine yoyote nje ya Afrika hata Afrika ya Kaskazini tu ungeona huo moto wake wa watu kulalamika na kusababisha huyu kiongozi kupoteza kazi yake!

Hivyo inaonyesha na kudhihirisha kwamba sisi bado sana!
kuna njia nyingi za kujenga uchumi, inategemea na mode ya production yako ikoje na products, sasa sisi hatuko industrialised, hivyo opportunity bado ni kidogo, kwenye service industry pia bado tuko nyuma, na utumiaji wa nyenzo ili kuongeza ufanisi bado tuko nyuma matokea yake tija ipo chini na creativity ya watu pia ipo nyuma , matokeo yake serikali au wenye viwanda wana kulipa mshahara wa mlo moja, sasa wewe unaweza kuendelea kufanya kazi zaidi ukapata ziada au huo muda wa ziada ukajilimia mchicha wako nk utakuwa ume save shs ngapi? au umejiongezea kiasi gani kwenye pato lako kwa kulima?

Pili vyombo vyetu vya kutoa mikopo bado viko nyuma, na hata wakikupa pato lako na makato , inakuwa shida saana ku qualify for housing loan nk, sasa ukitumia nafasi hiyo kwenda ku supervise ujenzi wa chumba/nyumba yako utakuwa ume save kiasi gani? badala ya kumpatia mjenzi/contractor? hilo sio pato la ziada?

kuna mtu alikuwa ana jenga nyumba mikocheni ya tpdc, nyumba zao hizo zenye sebule tatu, lakini alikuwa ana supervise mwenyewe. na huko ndiko tuna hesabu ndio waliokuwa nazo wanajenga.

au wewe kilimo umeona hakilipi? au kula mboga za majani ni umasikini.

au kuweka mifugo iwe kuku, ngombe mpaka kitimoto, baada ya hapo ndio mtu anaweza ku-build creativity ya kuboresha kilimo chake , packaging, na hata akienda kazini kashiba basi uzalishaji wake waweza kuwa una tija zaidi.
 
Hilo unaloliongelea wewe ni hatua ya pili ya maendeleo (yaani ufanisi), ambayo sisi hatujafikia bado, kwa hiyo katika ngazi ya chini ya maendeleo kama yetu ambapo ufanisi hauna nafasi au una nafasi ndogo sana ni kufanya kazi tu kwa masaa mengi ndio suluhisho na sio kupunguza!

Ngoja nikupe mfano chukulia Kiwanda cha chuma kama M.M steel, wafanyakazi wake wengi ni vibarua ambao hawana ujuzi (watu wa kupakia na kushusha mizigo, n.k), hivyo kazi zao ni za mikono na ngumu, kwa hiyo namna ya kuongeza uzalishazi M.M Steel ni kwa kuamua wafanyakazi wafanye kazi masaa mengi tu zaidi, unaweza ukapunguza tu masaa ya kufanya kazi kama watu wako wanaofanya kazi wana ujuzi wa kutosha, nikimaanisha kwa upande wa MmM steel kuna metallurgist wa kutosha, wakemia wa kutosha, watu wa kuendesha mashine wenye ujuzi wa kutosha, sasa hapo ndipo unaweza kuingiza hoja ya ufanisi na flexibility kwa maana kazi ile ile ambayo ingefanywa na watu 15 sasa anafanya mtu mmoja, hivyo hauhitaji tena vibarua, lakini ktk nchi ambazo hata mapinduzi ya viwanda hazijaanza bado kama za Afrika huo ufanisi haupo, hivyo kilichopo KWA SASA ni nguvu kazi tu na misuli ya watu, hivyo unavyoamua kupunguza masaa ya kazi inamaana unapunguza uzalishaji na matokeo yake hata wale wachache walioajiriwa kama vibarua pia wanapoteza kidogo walicho nacho!


nadhani hii hoja nabidi kutazamwa kwa mapana zaidi. kwani kutumia nguvukazi bila kuongeza ufanisi ni sawa na kubeba
maji kwenye tenga. natumaini humaanishi kuongeza mitulinga ndio jawabu la maendeleo kwa nchi kama zetu.
kama mapumziko yanalengo la kuhuisha nguvukazi ili nguvukazi hiyo iweze kuzalisha kwa ufanisi zaidi basi mkakati huo utafaa tu.
 
Back
Top Bottom