<br />Hongera CDM. Angalienei suala la arusha (umeya) kuna mkono wa nani pale? Tuyamalize tuanza mapya, Lema pls play your part, tumechoka sasa. Moja ya sifa za chama bora ni kuwa na uwezo wa kutatua matatizo kwa wakati.
Mwenyekiti wenu wa magamba mbona kila siku anaandikiwa hotuba lakini haziwi na mvuto hata kidogo? Anayoibuni mwenyewe utaijua tu, kama vile ya "kujigeuza mawingu akanyeeshe mtera"!!!Lema hana akili ya kuandaa hotuba anachojua ni vurugu.
Nipo hapa Arusha mjini vijana wamekusanyika kwenye vikundi vikundi wakijadili hotuba ya Mhe. G. Lema aliyoitoa leo bungeni. Wengi wanashauriana kuandaa maandamano kumpokea mbunge wao mara baada ya bunge kumalizika, sababu wanazotoa ni kwamba kaonyesha ujasiri kwa kuiambia serikali bila woga hali halisi ya maisha ya vijana na wananchi kwa ujumla hasa suala la polisi kuwabambikia kesi na mauaji ya raia wasio na hatia. Wanasema hawajashtushwa na Lema kutolewa nje maana wanajua kazi ya kuwasemea waliyomtuma siyo rahisi kama wengine wanavyofikiri. Nauliza ikiwa Chadema Arusha iko tayari kuwaunga mkono vijana hawa, kwangu naona ni suala la heri wanaJF mna mawazo gani.
<br /><br />asante babaMi nafikiri haina maana ya kujikusanya na kwenda kumpokea.......labda tu kwasbabu hatuna kazi za kufanya.........hayo ni mambo anayotakiwa kuyasema mara kwa mara na kuikosoa serikali na kuwakosowa wenzake pale wanapokosea ................NO BIG DEAL
Kwa maneno yako umeikubali hotuba yake hata kama yeye binafsi humkubali ilkuwa creative na real inayogusa hisia za wananchi.Hotuba ya kuandikiwa Lema anaitoa wapi akili hiyo ya kuandika hotuba! Bogus yule kaandikiwa tu
Jamani hamuamini kuwa kaiandaa yeye, hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa hotuba ya upinzani si hotuba za kusifia na kupaka mafuta serikari ukiona serikali inalalamika jua imeguswa penyewe. Natamani sana kuwa mwana Arusha kwa sababu wakati wa uchaguzi walijua nini wanatakiwa kufanya hongera sana Lema na hasa wana Arusha wote.Hivi ile hotuba nani kaiandaa?