mzee wa bwaksi
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 2,231
- 3,888
Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara Young Africans jioni ya leo majira ya saa 10.00 watashuka katika dimba la Benjamin Mkapa kumenyana na Kinondoni Municipal Football Club ( KMC ) katika mwendelezo wa ligi kuu ya Nbc
Ikumbukwe kuwa Yanga imepata ushindi katika mechi 9 mfululizo za ligi ya Nbc huku KMC wakipoteza mechi zao mbili zilizopita za ligi.
Yanga itaingia uwanjani kusaka ushindi wa 10 mfululizo kwenye ligi ya Nbc huku ikiwa na hamasa kubwa baada ya jumapili iliyopita kupata ushindi mchezo wake wa kimataifa dhidi ya Tp Mazembe ya DR Congo, hivyo KMC watakuwa na kazi ngumu ya kuhakikisha wanawazuia Yanga ambao wako kwenye kiwango Bora zaidi.
Usiwe mbali na Uzi huu kwani utakipata kile kitachojili uwanjani
Timu zote tayari zimeshaingia uwanjani na kinachosubiriwa ni Kipyenga cha mwamuzi Isihaka kuashiria kuanza kwa mpambano huu
.........................................
00" Kipyenga kimepulizwa na Kmc waanza mpira
10" Bado milango ni migumu kwa pande zote huku kila timu ikimsoma mpinzani wake
20" Kmc wameanza kufika langoni mwa Yanga ila Shambulizi halikuzaa matunda
32" Yanga wanapata faulo eneo zuri anapiga Aziz Ki ila shuti lake linadakwa na golikipa wa Kmc
38" Gooooal . Yanga wanapata bao la kwanza kupitia Clement Mzize kufuatia mpira wa kona uliopigwa na Aziz K.
45" Clement Mzize anapiga shuti Kali linagonga nguzo na kurudi uwanjan. Ilikuwa ni Shambulizi la hatari langoni mwa kmc.
HT. Dakika 45 za kipindi cha kwanza zimekamilika huku Yanga wakiongoza kwa bao 1-0. Tukutane kipindi cha pili
Kipindi cha pili kimeanza
65" Clement Mzize anapoteza nafasi ya kuiandikia Yanga goli la pili
84" Mayeeeeeeeeeeee...... Shuti lake Kali linagonga nguzo na kurudi uwanjani
90" Dak 3 Zimeongezwa hapa na mwamuzi.
Naam mpira umekwisha Yanga wakiondoka na ushindi wa bao Moja Kwa bila na kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kwa kufikisha alama 62 na kuwaacha wapinzani wake Simba wenye alama zao 54.
Tukutane wakati mwingine. Jioni njema
Ikumbukwe kuwa Yanga imepata ushindi katika mechi 9 mfululizo za ligi ya Nbc huku KMC wakipoteza mechi zao mbili zilizopita za ligi.
Yanga itaingia uwanjani kusaka ushindi wa 10 mfululizo kwenye ligi ya Nbc huku ikiwa na hamasa kubwa baada ya jumapili iliyopita kupata ushindi mchezo wake wa kimataifa dhidi ya Tp Mazembe ya DR Congo, hivyo KMC watakuwa na kazi ngumu ya kuhakikisha wanawazuia Yanga ambao wako kwenye kiwango Bora zaidi.
Usiwe mbali na Uzi huu kwani utakipata kile kitachojili uwanjani
Timu zote tayari zimeshaingia uwanjani na kinachosubiriwa ni Kipyenga cha mwamuzi Isihaka kuashiria kuanza kwa mpambano huu
.........................................
00" Kipyenga kimepulizwa na Kmc waanza mpira
10" Bado milango ni migumu kwa pande zote huku kila timu ikimsoma mpinzani wake
20" Kmc wameanza kufika langoni mwa Yanga ila Shambulizi halikuzaa matunda
32" Yanga wanapata faulo eneo zuri anapiga Aziz Ki ila shuti lake linadakwa na golikipa wa Kmc
38" Gooooal . Yanga wanapata bao la kwanza kupitia Clement Mzize kufuatia mpira wa kona uliopigwa na Aziz K.
45" Clement Mzize anapiga shuti Kali linagonga nguzo na kurudi uwanjan. Ilikuwa ni Shambulizi la hatari langoni mwa kmc.
HT. Dakika 45 za kipindi cha kwanza zimekamilika huku Yanga wakiongoza kwa bao 1-0. Tukutane kipindi cha pili
Kipindi cha pili kimeanza
65" Clement Mzize anapoteza nafasi ya kuiandikia Yanga goli la pili
84" Mayeeeeeeeeeeee...... Shuti lake Kali linagonga nguzo na kurudi uwanjani
90" Dak 3 Zimeongezwa hapa na mwamuzi.
Naam mpira umekwisha Yanga wakiondoka na ushindi wa bao Moja Kwa bila na kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kwa kufikisha alama 62 na kuwaacha wapinzani wake Simba wenye alama zao 54.
Tukutane wakati mwingine. Jioni njema