Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Status
Not open for further replies.
Mkuu Ontaria, nimeusoma uzi huu mwanzo mwisho, umetisha. Nahitaji kuwa miongoni mwa watu hao 300 kwani nimesoma Master Degree in Finance na FOREX Trading nimesoma theoretically, I want now to do practically because I like it.
BIG UP, usinisahau mkuu.
Hujasoma hadi mwisho,Kama ungekuwa umefanya hivo usinge quote uzi wote,,mwishoni mwa Uzi Kuna angalizo la kutofanya hivo kuepusha usumbufu kwa wanaotumia simu
 
Huu Uzi ni mzuri sana katika kuwafundisha watu juu ya biashara ya FOREX

Binafsi Nina uzoefu wa hii biashara, kwa hiyo napenda kushare machache humu ili watu watambue faida na risk zake..

Kwanza kifupi ni kwamba hii biashara sio rahisi kama wengi wanavyodhani, ina hitaji umakini wa hali ya juu maana unakuwa umekubaliana na mambo mawili. Profit au loss.

Hatua ya kwanza kabisa inabidi uchague broker (hapa pia panahitaji umakini).. Baada ya kuchagua broker inabidi umstudy kwa kina maana kumbuka kwamba wewe unahitaji profit na broker nae anahitaji profit kupitia ku-loose kwako au kuwin (hapa ni brokers wachache)

Kifupi ni kwamba unahitaji kupata uzoefu kidogo kwa kuangalia trend ya biashara kwenye FOREX lakini pia kupitia mtu ambaye ana uzoefu wa kutosha kwenye hii biashara FOREX (hapa itabidi upate mkweli)

Jambo lingine LA msingi ni kufahamu risk ambazo utakumbana nazo katika hii biashara, tambua kwamba kila mtu anahitaji faida kupitia hii biashara, kwa hiyo kupata kwako loss ndio faida kwa mwingine (kwa lugha nyingine naweza kusema ni struggle for the fittest)

Nirudi kwa mtoa mada, kwanza nimpongeze kwa kujaribu kuelezea kwa ufupi uhalisia wa biashara hii lakini kuna Vitu ametazamia kwa lengo la yeye kujiongezea kipato (japokua kihalali) kutoka wa watu watakao kuwa tayari kuianza biashara hii..

Nafafanua kidogo:-
1. Mtoa mada amesema ana mpango wa kufungua office na kutoa train kwa watu 300 bure kwa kushirikiana na brokers alioingia nao ubia (ni wazo zuri)
Naamini train hiyo itakuwa inamzungumia broker (aliyeingia nae ubia) jinsi anavyofanya kazi, offer zake na faida kwa mtu atakayejiunga kupitia huyo broker...
Kwahiyo baada ya train hao watu 300 watajiunga na kuwaambia wengine kujiunga kupitia broker aliyewapa train (na hapa ndipo anapopata faida kupitia watu wanaomtumia broker aliyeingia nae ubia.. Kwahiyo hapo wewe pamoja na broker your fighting for profit... kwahiyo mmoja aki-lose ndio faida ya Mwingine).. Ndio maana nasema hapa inahitaji umakini mkubwa sana.

2. Kama lengo LA mtoa mada ni kugain profit kupitia ubia wake na broker na watu watakaojiunga. Basi naamini katika training atajikita zaidi kuelezea benefits zaid kuliko risks maana target yake ni kuku-win wewe, kwa mantiki hiyo hawezi kujikita zaidi katika risk maana anajua utaogopa atakukosa.

Ndio maana Jambo la msingi unapaswa kujiuliza ni kwanini mtoa mada amekubali kuingia gharama zote hizo kuleta mentors?? (Usifikiri in positive ways pekee yake, check on both side +ve & -ve)

Pili kwanini sahivi anataka kufungua office?? Kwanini asingetengeneza Whatsapp group akatoa elimu bila kusubiri apate office ili atoe fursa kwa watu wa mikoani??

Maana me naamini kumpatia mtu juu ya hii elimu haihitaji uwe na ofisi wala uwe nae ana kwa ana (me niliipata hii elimu kupitia internet pamoja na kusoma vitabu, lakini sahivi nafanya vizuri)

Mwisho nawashauri ni vizuri mkawa makini sana na kujiridhisha kwa kina kabla ya kufanya maamuzi.

NB: hayo ni mawazo yangu kulingana na uelewa wangu na uzoefu wangu juu ya biashara ya FOREX, sijatoa kwa lengo LA kum-criticise mtu bali kwa lengo la kuelimisha zaid.

shkamoo JAJCOM...

Hiki ndicho alichopaswa kueleza.......

Badala ya kuleta kitu kama tangazo la pombe, linaloonyesha mtu anapokunywa bia moja anavyokuwa na furaha na mtanashati....hawaonyeshagi anapokuwa amepiga bia 8 huku amejikojolea, amejinyea, amebakwa, ameanguka na kupata ajali
 
Ndiyo maana kuna kampuni nyingi za clearing and forwarding(C&F) zilizofilisika. Inabidi kabla kukurupuka kwa ushauri inabidi ujue kama hiyo kampuni hiko recognised, reliable na inafanya kazi ethically. Makampuni mengi ya C&F yalikuwa ya wizi mtupu bongo, mengi sasahivi ni mufilis tangu Magufuli aliposhugulikia bandarini. Kuhusu, kuagiza gari Japan wala sihitaji C&F company...naweza agiza mwenyewe direct from Japan.

Mimi nakubali kwamba hii FX trading ni nzuri na it can be a lucrative way to make money. Lakini wabongo wengi nimegundua tuna pupa na hatuulizi the right questions badala yake tunafwata mkumbo (following the crowd)

Huyu ndugu Ontaria ametoa maelezo mengi ambayo ni mazuri tu, lakini hajatuambia alitumia website gani ya Forex Trading kutengeneza hizo pesa. Badala yake, ameongelea mambo ya kufungua ofisi, training and so on ili apate wateja kutengeneza pesa.

Sisi tunataka atueleze kwa ufupi kwamba alitumia website hipi, account au bank card ya namna gani kuendesha hiyo FX Trading na atupatie statement inayo onyesha earning zake katika trading. Pia ikiwezekana, siyo lazima, atupatie ka background kake kadogo with evidence.
Wahenga wakidhungu wanasema "when a wise man points at the moon, a fool looks at the finger". Nimetumia C&F kama mfano, ila wewe kwa ujinga ukauchukulia kama ujumbe husika ktk haya majadiliano.

Ontario wewe piga kazi...uzuri wa huu uzi upo labda Jamiiforum ife, watakuja kushuhudia humu ukweli wako.

Hatusemi mtu atapata hela au utajiri kirahisi, lakini ni fursa nyepesi kuifanya pindipo unapokuwa umeiva kwenye elimu yake.Uzuri tunaotoa ushuhuda humu wote tunasema tumeshapata hasara...sasa kama yupo ambaye hataki hiyo hasara basi haimfai hii biashara na ofcoz yeyote ile.
 
Natumai na Mimi sijachelewa hata kama nimechekewa ila naomba nafasi mkuu niwepo kwa ajili ya kujifunza zaidi natanguliza shukrani pia hope kila kitu kitaenda sawa
 
Asante sana kwa kuweka wazi fursa hii adhimu kwetu watanzania. Ubarikiwe sana Ontario, tupe sasa utaratibu wako wa kutusajili kwenye Hilo kundi la 300 au zaidi ili tuanze sasa kuwa pamoja badala ya kusubiri uendelee kuumia mwenyewe wakati kuna uwezekano hata wa kukusaidia japo Kama sio kifedha basi hata kufuatilia kazi zingine ili kupunguza muda wa kuweka mambo yote sawa.
 
Huu Uzi ni mzuri sana katika kuwafundisha watu juu ya biashara ya FOREX

Binafsi Nina uzoefu wa hii biashara, kwa hiyo napenda kushare machache humu ili watu watambue faida na risk zake..

Kwanza kifupi ni kwamba hii biashara sio rahisi kama wengi wanavyodhani, ina hitaji umakini wa hali ya juu maana unakuwa umekubaliana na mambo mawili. Profit au loss.

Hatua ya kwanza kabisa inabidi uchague broker (hapa pia panahitaji umakini).. Baada ya kuchagua broker inabidi umstudy kwa kina maana kumbuka kwamba wewe unahitaji profit na broker nae anahitaji profit kupitia ku-loose kwako au kuwin (hapa ni brokers wachache)

Kifupi ni kwamba unahitaji kupata uzoefu kidogo kwa kuangalia trend ya biashara kwenye FOREX lakini pia kupitia mtu ambaye ana uzoefu wa kutosha kwenye hii biashara FOREX (hapa itabidi upate mkweli)

Jambo lingine LA msingi ni kufahamu risk ambazo utakumbana nazo katika hii biashara, tambua kwamba kila mtu anahitaji faida kupitia hii biashara, kwa hiyo kupata kwako loss ndio faida kwa mwingine (kwa lugha nyingine naweza kusema ni struggle for the fittest)

Nirudi kwa mtoa mada, kwanza nimpongeze kwa kujaribu kuelezea kwa ufupi uhalisia wa biashara hii lakini kuna Vitu ametazamia kwa lengo la yeye kujiongezea kipato (japokua kihalali) kutoka wa watu watakao kuwa tayari kuianza biashara hii..

Nafafanua kidogo:-
1. Mtoa mada amesema ana mpango wa kufungua office na kutoa train kwa watu 300 bure kwa kushirikiana na brokers alioingia nao ubia (ni wazo zuri)
Naamini train hiyo itakuwa inamzungumia broker (aliyeingia nae ubia) jinsi anavyofanya kazi, offer zake na faida kwa mtu atakayejiunga kupitia huyo broker...
Kwahiyo baada ya train hao watu 300 watajiunga na kuwaambia wengine kujiunga kupitia broker aliyewapa train (na hapa ndipo anapopata faida kupitia watu wanaomtumia broker aliyeingia nae ubia.. Kwahiyo hapo wewe pamoja na broker your fighting for profit... kwahiyo mmoja aki-lose ndio faida ya Mwingine).. Ndio maana nasema hapa inahitaji umakini mkubwa sana.

2. Kama lengo LA mtoa mada ni kugain profit kupitia ubia wake na broker na watu watakaojiunga. Basi naamini katika training atajikita zaidi kuelezea benefits zaid kuliko risks maana target yake ni kuku-win wewe, kwa mantiki hiyo hawezi kujikita zaidi katika risk maana anajua utaogopa atakukosa.

Ndio maana Jambo la msingi unapaswa kujiuliza ni kwanini mtoa mada amekubali kuingia gharama zote hizo kuleta mentors?? (Usifikiri in positive ways pekee yake, check on both side +ve & -ve)

Pili kwanini sahivi anataka kufungua office?? Kwanini asingetengeneza Whatsapp group akatoa elimu bila kusubiri apate office ili atoe fursa kwa watu wa mikoani??

Maana me naamini kumpatia mtu juu ya hii elimu haihitaji uwe na ofisi wala uwe nae ana kwa ana (me niliipata hii elimu kupitia internet pamoja na kusoma vitabu, lakini sahivi nafanya vizuri)

Mwisho nawashauri ni vizuri mkawa makini sana na kujiridhisha kwa kina kabla ya kufanya maamuzi.

NB: hayo ni mawazo yangu kulingana na uelewa wangu na uzoefu wangu juu ya biashara ya FOREX, sijatoa kwa lengo LA kum-criticise mtu bali kwa lengo la kuelimisha zaid.

At least wewe unaongea kama professional ama mtu mwenye uelewa, sio km baadhi ya watu wanatema mashudu hata hawaelewi nini wanasema.

Umetukumbusha tena kitu ambacho nimekizungumza hapa mara kadhaa, kua forex inahitaji dedication sana sana sana.

Nirudi kwenye hoja zako ulizozinumber.

1. Kwanza naomba usipindishe maneno, sielewi kama umekosea ama umekusudia. Hii ni continuous thing ambayo itarun kwa decades za kutosha, unaposema nafungua office ya kutrain wa2 300 bure unakua umenimisquote. Nimesema natoa special offer kwajili ya member 300 kutoka JF, wapate training then nitakua nao benet kuhakikisha wanamake profitable trades. Baada ya hapo programme itaanza rasmi - tutaingiza wanafunzi wa kutosha tu, na sitawapa free trainings. Nitawacharge kitu kidogo ambacho tutaona inafaa kwao na kwetu pia.

Mimi kumleta broker ni kurahisisha mambo. Huwezi ukamtrain mtu hasa mbongo ambae uelewa wake ni mdogo afu kisha unamwambia broker yupo UK au USA. Hapo ni ngumu , mimi kumleta broker ni katika kufanya vitu kiuhalisia, kwa openness na transparency. Naona unazungumzia mambo ya mimi kuwa IB, cjui nani kasema, na hata kama ni hivyo iko wapi shida?!

Pia kama umesoma vzr post yangu nimegusia kdg type ya broker ambae ninadeal nae. Sijui kama uliona hiyo ama hukuelewa.

2. Boss hii point yako ya 2 imekaa kama kuna kitu you want to prove... yani kuna negativities ambazo hazina logic unaraise.
Mtu mwenye akili timamu hawezi akahoji faida ya Office, mtu anakuchallenge kisa unafungua office afu hapo hapo anasema forex inahitaji knowledge kubwa afu kisha anashauri hiyo knowledge itolewe WhatsApp. Tusiwe na roho ya kwanini - wewe umepata knowledge usichukie uonapo mwenzio nae anatolewa usingizini??

Mimi hii si biashara yng ya kwanza. Hata biashara ya kuku, inabidi uingie gharama ya kujenga mabanda na kuandaa kila kitu ndio uanze kufuga kuku. Wewe umepata hiyo elimu kwa njia zako unazozijua wewe, haimaanishi njia zingine ni za kipvmbavu. Yani unanishauri nichukue watu 300 then niwafundishe forex kwa group la WhatsApp na si kufungua office afu niwadirect kwa broker ambae hata hawajui alipo au anaoperate vipi.

Biashara yoyote lazima ugharamie, mimi kupanga office space, kuleta mentors nk ni 1 ya vitu ambavyo nilividraft ili kuhakikisha natengeneza consistent profitable traders na gharama zote nilizipiga. Naweza nisitengeneze pesa leo ama kesho but baada ya mwaka nikiwa nimeestablish mizizi, nina watu TZ wananizungumzia naweza kutengeneza pesa.

If you have any doubts about me, naomba nianze hii kitu ili nikuprove wrong. Nafungua ofisi, natafuta vibali vyote, naleta broker, natrain mamia kwa mamia, nitajitahidi mimi na team yangu tutengeneze traders ambao wataina matunda ya forex, na through the whole process nitatengeneza faida yangu na watu watakua na freedom ya uchumi kuliko leo graduate anagombania remote na mdg wake wa primary.

Mimi kama mimi Ontario nilianza biashara nikiwa bado mdg sana, nilianza na kuku 50 wa broilers, watu walinicheka, wengine wakawa wananidiscourage even my own parents. Leo hii hiyo biashara inakuwa featured Forbes, CNN, BBC World Service, SABC, DW nk. Hata hii nayo siwezi kuishia kati, afe kipa afe beki. Ipo siku watu wote wanaoleta senseless negativities nitawaprove wrong. Nipe miaka miwili tu, yani miezi 24 tu since nikianza.
I will leave a living legacy ya hii biashara kwa hapa TZ - nitakumbukwa si kwa utajiri bali kwa namna nitakavyowafungua watu macho na fikra ktk Global businesses. That alone kwangu ni ushindi mkubwa
 
Wazo la nne
Si hata wazo la msingi sana, hahaa. Sijui niandike nini, lkn nachotaka kumaanisha ni usiwe mchoyo, kama kuna rafiki yako wa faida unahisi inabidi aone huu uzi usisite kumtag.

Ni bora tukaepuka kuQuote huu uzi, ni mrefu sana sana, yani ukiquote unatusumbua sana ambao tunatumia simu na gadgets zingine ndogo ndogo.

Karibuni kwaaliji ya ku discuss.

Updates

Moja ya ombi la msingi ambalo nimeona watu wengi wanaulizia ni - "Ontario ni kitabu gani naweza kuanza nacho?"

Kila mtu ambae yupo interested atafute kitabu kinaitwa Currency trading for Dummies: Kimeandikwa na Brian Dolan 2nd Ed ndio poa zaidi. Cover yake ni kama changano then kuna dunia hivi inaramani za nchi mbali mbali.

mkuu hii ni kama binary option sometime wanakua matapeli tu
 
Nashukuru sana kwa elimu nzuri sana. Naomba niwemo kwenye list yako ya watu 300. Dola 100 mpaka 300 za kuanzia zipo. Naomba tupate mawasiliano yako ili tukupate kiurahisi.
 
Salute bosses

Utangulizi

Wengi mmesikia sikia sana kuhusu Forex trading, mmepata kujua taarifa kadhaa kuhusu hii biashara lakini mmeshindwa kufahamu nini kinaendelea. This is the perfect thread, tutaelewa kila kitu hapa na hakuna atakayebaki na swali kichwani - we have to leave this thing completely naked. Nakuhakikishia (mimi Ontario) kupitia hii thread sitamwacha mtu yeyote nyuma. Naomba twende pa1, tufahamu, tujifunze, tuelimike, tuhamasike na tujichallenge.

Kwanza nitoe shout out na credits kwa member mmoja hapa JF anaitwa Davion Delmonte Jr. Aliwahi kupost uzi educative sana kuhusu forex, ni moja ya uzi wa forex uliopata hamasa kubwa hapa JF ndio maana nikauchagua kama sample -lkn kuna nyuzi zingine nyingu tu, nakushauri unaweza kuupitia kidogo Fahamu utajiri kwenye biashara ya fedha za kigeni (FOREX TRADING)

Tuendelee
Katika tembea tembea zangu, mwaka 2016 mwanzoni nilikuwa Durban, nikakutana na dogo mmoja anaitwa Mike Lungu, ye mwenyewe anajiita MLU. Kukutana kwetu kulikuwa very coincidentally, mimi nilikua naishi Garden Court hotel, asubuhi muda wa breakfast tukajikuta tumekaa meza moja. Baada ya Kusalimiana tukajikuta story haziishi, nikazungumza mengi sana kwa upande wangu, baadae nikataka kujua na yeye upande wake.

Mike akanieleza kuwa alidrop out of college akiwa mwaka wa kwanza, na kwa kile kipindi alisafiri kutoka kwao Mpumalanga sasa amekuja Durban kukutana na mentor wake. Nikataka kujua zaidi kuhusu hiyo mentorship inayomfanya atoke Mpumalanga (ambapo ni mbali sana na Durban). Mike akaniambia kwamba ni Forex.

Kipindi hiko nilikua sielewi chochote kuhusu forex, yani sina clue kabisa. Mike Akaanza kuniambia kuhusu watu waliofanikiwa sana ktk forex, akanitajia kijana mmoja ambae siku kama 3 zilizopita nilimuona anafanya interview kwa TV lkn nikashindwa kabisa kumwelewa anachokisema. Huyo dogo aliyenitajia ni celeb wa forex SA na anaitwa Sandile Shezi, ni dogo mwenye utajiri mkubwa sana kupitia forex, nae aliacha chuo mwanzoni kbs mwa masomo.
6784542861cf86e42eed93dd8361df54.jpg
Sandile Shezi anaemiliki Global Forex Institute.

Kama ilivyo kawaida ya wabongo wengi, nikambishia sana Mike, nikamwambia hiyo kitu ni utapeli na wizi ambao hauwezi ukamtajirisha mtu wa kawaida. Nilikua sina knowledge kbs lakini nilikomaa kusema kua forex nayo ni kama forever living (networking marketing). Hata nilivyosoma kwenye mitandao, bado nilimbishia sana Mike kuhusu hiyo forex nikidai kuwa kamwe siwezi poteza muda wangu na pesa katika huo upvmbavu, nikafika hatua ya kumDiss kua anapoteza mufa wake bure.

Basi, tukawa tunapiga story zingine, namweleza kuhusu Bongo nk. Yani tulitokea kuwa marafiki ndani ya muda mfupi sana, nilikaa pale kwa siku 8 nikaondoka kurudi Bongo. Lakini Tuliendelea kuwa in touch, hasa kupitia WhatsApp, tunajuliana hali na maendeleo kimaisha. Mimi nampa updates za kilimo na ufugaji na yeye ananipa updates za Forex kwa upande wake.

Sept 2016 nikaendaga USA, basi nikawa namsumbua sana MLU kwamba kilimo ni kitamu sana bora aache hizo forex yake afanye kilimo. MLU akanambia sasa Octario kwenda US unaona ni mafanikio makubwa? Tukabishana mwishoni akasema nimpe mwezi mmoja anishangaze - mimi nikawa namcheka, na kumwambia kua yupo ndotoni.

Mara ghafla siku 1 October 2016, Mike akanitumia text, hey Ontario nimevuta BMW mpya 0 km. Wabongo kwenye situation kama hizi hua ni wabishi sana, nami kama kawa nikabishana nae Asubuhi, mchana na usiku (kama dozi ya mseto). Jamaa akanambia subiri nikikamilisha paper works nakutumia picha. Ndani ya siku 4 tu, Mike akanitumia hii picha.
6ccbe86153d474187c32b8a2c8f65d68.jpg


Hapa nikawa mpole - ukweli ambao hakuna binadamu atakubali ni kuwa "Kila binadamu hapa duniani ana chembe chembe ndogo za wivu endapo mtu baki akifanikiwa kumzidi". Huu ni ukweli mchungu, ambao mimi nimeuprove katika situation kadhaa. Lakini watu wanaoweza 'kudeal' na hizo chembe chembe za wivu positively ni rahisi na wao kufanikiwa.

Kama hauwezi kupambana nao ungana nao
Baada ya hile hali nikawa motivated mno. Nikajipiga juu chini Nov 2016 nikarudi SA, nia ni kuonana na Mike. Nafahamu kabisa huyu jamaa hakuna kitu anachofanya hapa duniani zaidi ya hii Forex, leo kanunua gari KALI kupitia hiyo forex, lazima nami niingie humo. Nikajipa moyo kua I am never late.

Safari hii nilivyokutana nae sikuishi hotel, Mike alinifata Airport tukaenda kwake. Nyumba ambayo alikua anaishi ni sawa ama zaidi ya hizi ambazo mawaziri hapa Bongo wanazitumia. I was over shocked. Nikasema afe simba afe mmasai lazima hii kitu niijue. Hapa ndipo Mike alipoanza kunizingua, utani mwingi wa kunicheka kua mimi najifanya mjanja kumbe ni mshamba tu, akawa anasema hawezi kunielekeza hadi nipige magoti nimshike miguu nimuome msamaa. Haha haha!!

Akanipa tips zote kuhusu forex, akafungua book store yake akanipa vitabu 6 nivisome kwa makini sana. Nikavisoma haraka haraka kwa pupa, ili mradi nivimalize then Mike anipe mbinu nami nianze kupiga hela. Nilivyomaliza kusoma ki1 nikamtaarifu Mike, akanichapa swali 1 nikajibu pumba na mashudu. Jamaa akaniambia nisome upya letter by letter. Nikapunguza jazba, nikaweka concentrate ya kutosha, nikaanza kuelewa.

Sikukaa muda mrefu sana nikarudi Bongo. Nikawa naendelea kusoma vitabu alivyonipa kwa umakini sana na akawa ananiuliza maswali ya hapa na pale.

Nilivyoanza Forex trading

Mpaka hapa bado wengi hamuelewi nini maana ya Forex, bado hamfahamu hata nazungumzia nini, usiwe na pupa na jazba kama nilivyokuwa nazo. Twendeni pole pole, mpk hii thread inaisha hakuna atakayetoka mtupu.

Wiki kadhaa baada ya mwaka mpya 2017 nikaanza forex rasmi. Mike alinipa mwongozo wa awali akaniomba nifungue 'demo account'. hii ni account ambayo imewekwa virtual money, unaitumia kwa ajili ya kujifunza kutrade. Ukijiona umeiva unahamia kwenye real account ambayo unaweka pesa yako na kuanza kutrade kiuhalisia.

Nikapiga hii demo account, kwa kuwa sikua na msimamizi (mentor) karibu yangu ikanichukua mwezi mzima kumaster hii trading. Nikaanza kuona mwanga, nagonga profits, naelewa nini kinaendelea, nikaanza kujua basics za market analysis - fundamental na analytical. Baadae nikapata picha kubwa zaidi kuhusu hii kitu. Kwakweli nikajidharau sana sana kwanini nilikua namcheka Mike hapo awali, nikajiona Baxhite wa kiwango cha standard gauge.

Nikajiridhisha kuwa I am good to go. Na Mike rafiki yangu wa faida akanipa go ahead. Nikaanza kwanza na $700, nikakimbiza kimbiza nikaona nagonga profits za ajabu mpk nikawa naanza kuogopa. Kuna ile kasumba fulani wabongo tunayo kama unahisi unatapeliwa hivi, nami nikaanza kua na hiyo feeling. Nikawa kama vile nachallenge ubongo wangu, kusema hii haiwezi ikawa real, yani capital ndogo na bado napiga profits za ajabu hivi.

Nikakimbiza hadi kufika $2000 ndani ya wiki 2, nikasema nijaribu kuichomoa ile pesa kidogo nione kama ni real. Nikawithdraw $500, kudadeki kitu kikakubali, nikaenda CRDB nikavuta kamilioni kangu na tuchenji kadhaa. Sasa nikasema hapa ni kupiga pesa mpk mnikome. Mambo yakawa matamu sana, nikipata shida kwenye kuku na mashamba yangu nachomoa pesa kutoka kwenye trading account ndani ya siku 2 au 3 ninayo mkononi nafanya mambo mengine. Na kadri nilivyozidi kuchomoa pesa na kuwa nayo mkononi ndio nilikua napata morali ya kufanya forex.

Siku nikachomoa $1500 kwaajili ya mdogo wangu ambae ndio alikua anaenda kuanza form 1 huko Moshi. Hapa account yangu ilikua imefika kama $11,000. Nikasema hii pesa ($1500) niliyoichomoa lazima niirudishe ndani ya siku ile ile ili kubalance mahesabu.

Kuna kitu kinaitwa Psychology of trading and Over Trading. Hivi vitu nilikua naviona tu kwenye vitabu lkn naviruka kwa kuvipuuza, hii siku wakati nipo aggressive kurudisha pesa niliyochomoa ndio nikavunja hizo kanuni. Aisee nikaingia kwenye trades, nikawa nimeovertrade, nikaacha trades zinarun usingizi ukanipitia. Sikukumbuka kuweka stop loss (SL) wala take profit (TP) [hivi vitu tutavielewa baadae], aisee kumbe hiyo siku kulikuwa na economic news release. Baada ya kushtuka kutoka usingizini nilichokiona sikuamini macho yangu.

Nasema kama ile siku sijafa kwa presha siwezi tena kufa kwa presha siku za usoni. Yani nilikuta account yangu yote imepukutika kama mvuke. Sikuamini, nilipoteza karibia pesa zote zote ndani ya muda mfupi, sisi tunaita kuBlow ama kuchoma/kuunguza account. Kuna feeling fulani ukipoteza kitu cha thamani unaipata, yani unahisi kama unajikojolea. Sijui kama mnanielewa. Yani sielewi kilichonitokea, ni km nilipigwa ganzi ya ubongo

Nikamshtua Mike kuhusu msala wangu, akacheka sana sana akaniambia, nilijua tu lazima uunguze account, speed yangu ilikua ya mwanga wa radi. Zaidi sana anakambia kuchoma account ndio kukomaa na kuwa mtaalamu ama guru wa trading. Nikapiga moyo konde, nikajipa muda wa kupumzika na kusikilizia machungu yaishe.

Baada ya muda kama week 1 nikaanza upya kama kawa. Nikaweka $3000 nikaanza kukimbiza upya. Mambo yakawa matamu, yani nashukuru baada ya kupoteza ile pesa akili ikawa imenikaa vzr sana ktk kitu kimoja tunaita trading risk management. Nikawa makini kuliko kiasi, nikawa ninatrade pale tu ninapoona kuna opportunity, nikawa very strategic huku nikiamini kuwa bado mimi ni mwanafunzi na nahitaji kujifunza zaidi na zaidi kuhusu financial markets. Mpaka sasa ninavyoongea najiamini ktk trades zng vibaya mno kuliko kipindi chochote kile.

--Sasa twende kwenye maana ya Forex trading.

Forex trading ni nini hasa?

Waliosoma uchumi na masomo ya business chuoni najua tangu naanza uzi wanaelewa nini naongelea kijuu juu. Lkn wenzangu na mimi tuliosoma Sciences, technology, engineering na humanities hatuelewi hata punje.

Forex ama wengine hufupisha kwa kusema FX ni kufupi cha maneno Foreign Currency Exchange. Basically Ni biashara inayosisha kuuza na kununua fedha za kigeni. (Najua wengi hapa akili imegonga kwenye bureau exchange). Yes! Ni kitu kile kile lkn sasa hii Forex ni baba lao, tuwashukuru sana (wazungu) walioleta technology ya computer na Internet. Sasa kiuhalisia tukizungumzia Forex trading ni kubadilisha fedha za kigeni electronically and at real time. (Sijui kama unanielewa?). Ni wewe na computer ama smartphone yako pamoja na bundle lako.

Kinachotokea ni kwamba unaspeculate utendaji ama tuseme performance ya fedha fulani labda Dollar ama Yen ama Pound kisha ukifahamu uelekeo wake either utainunua ama kuiuza, kupitia huo mzunguko utatengemeza pesa kubwa sana ama kama ukijichanganya unapoteza vile vile. Hapa unahitaji uwe na uelewa mpana sana wa kufanya analysis ya soko la dunia (global currency market).

Hii ndio biashara yenye utajiri mkubwa kuliko biashara yoyote ile hapa duniani. Huwezi kuamini kwa siku katika forex trading kuna mzunguko wa $5 trillion (dola trillion tano), naomba hapa tusiiweke in Tsh maana tutaishia kuongea herufi za ajabu mara hexa trillion mara hepta trillion, lkn ni mkwanja mrefu sana. Kiasi kwamba itaihitaji New York Stock Exchange ifanye biashara siku 30 ili kupata pesa za siku 1 zilizopo kwenye forex market. Ndio maana sisi traders hua tunasema "kudownload pesa" yani kwenye forex ni kupakua tu pesa, kama vile upo uTorrent

Central banks zote zinafanya forex trading, financial institutions karibia zote duniani zinafanya forex, wafanyabiashara wakubwa karibu wote wanafanya forex (tena huyu bilionea wetu ambae alibahatika kufanya kazi Wall street atakua ni trader mzuri sana wa forex na stock), Donald Trump ndio hata usimzungumzie - huyu kashindikana, leo hii trump anasukuma tweets ambazo zinabadilisha upepo wa dollar katika soko ili yeye na team yake wagonge pesa, mpk anatoka madarakani atakua kazidisha utajiri wake hata mara 5.

Ukweli uliofichwa kuhusu forex

Sijui nisemaje, lkn ukweli ni kwamba kuna nguvu kubwa sana sana sana inatumika na mabenki kuwafanya watu wasiitambue forex. Wenzetu Ulaya na Marekani walishtuka mapema sana, kwao forex si kitu kipya sana japo bado kuna wingu kubwa hapo kati. Huku Afrika ndio usiseme, wenzetu SA kidogo wamewahi kushtuka kutokana na muingiliano mkubwa kati yao na mataifa ya Magharibi.

Utamu upo hivi - Leo hii ukichukua mil 10 na kuiweka benki katika fixed account, utapewa interest ya 7-10% kwa mwaka, hiyo miezi yote 12 unasubiria milioni 1. Lakini kwa forex ukiwa unajitambua ukaweka mil10 ukatrade, kama ww ni average trader ndani ya siku 2 utakua umepiga faida ya milioni 1. Sasa hapa benki zinapambana juu chini ili watu wasitambue forex ili wasije kupoteza wateja wa fixed accounts. Na ukweli ni kwamba pesa zinazowekwa fixed account bank hua wanazitumia kufanya forex trading, hii kuwapa watu mikopo hua ni kiini macho tu.

1 ya changamoto niliyokumbana nayo ni hii ya bank. Wakati nachomoa pesa ndogo ndogo ilikua ni faster tu, ndani ya siku 3 pesa iko mkononi. Lkn siku niliyojaribu kuchomoa pesa ndefu ndipo nilipoelewa nguvu inayotumika na mabenki. Sitataja jina la benki niliyokuwa natumia, ni bank ya kibongo (local bank), lkn kiukweli walinizungusha sana, wamenisumbua vibaya mno, wananisainisha makaratasi kila siku, kila siku naambiwa nikutane na XX, mara wananiambia nithibitishe kua ile pesa si "money laundering" "kutakatisha pesa". Hii yote ilikua ni mbinu ya kunidiscourage nisiendelee na forex, kumbe hawajui mtu wanaeshindana nae. Hayo yote nilikua nishayasoma kwenye vitabu siku nyiiingi, ni kama nilikua nina theory sasa nimeeingia kwenye practical. Mwishoe wakanipa changu!!

Hakuna bank yoyote ingependa ujue kuhusu forex, yani hata humo kwenye mabenki wafanyakazi wa humo humo benki hawatambui kabisa kuhusu forex. Ni wajanja tu ndio wanaweza wakaelewa nini kinaendelea huko duniani. Nguvu inayotumika si ya nchi hii.

Hata juzi nilimpa jukumu member m1 hapa JF ambae alinisaidia kusajili kampuni yangu mwanzo kbs, nilimuomba afatilie ishu ya forex BRELA, wizara ya fedha na BOT. Yani kuna blah blah vibaya mno, watu hawataki kufunguka kabisa. Lakini tutafika tu, dunia haiwezi ikatuacha just kwasababu ya manufaa ya wachache, sio fair.

Way forward

9899c7dad05c1ace817ac027eb891b45.jpg
Hii picha niliichukua kwa bahati mbaya nikiwa mile 60,000 angani lkn hapa iko relevant.
Hivi nazungumza sina muda mrefu tangu nitoke Afrika Kusini, na nilichokifuata naweza kusema kwa asilimia 99% kimefanikiwa. Nimetumia gharama nyingi sana kufanikisha dhumuni langu but it's worth it. Naamini hivyo.

Naangalia fedheha na dhihaka tunayopata wasomi, it's too much. (Nikisema wasomi simaanishi kama unavyodhani bana hahahaaa, no disrespect hata mwenye form 4 nae ni msomi). Jamii imekua na expectation kubwa mtu akifika form 4, form 6, degree namasters, watu wanategemea uwe mtu fulani hivi, mwenye maisha fulani hivi. Lkn kwa system ya nchi zetu hizi , inakua tofauti, inafika kipindi huwezi kumtofautisha graduate na mtu kama msaga sumu ama man Fongo.

Kwa experience niliyonayo nikaona Forex is the BEST way forward kuepuka hizi fedheha za ajabu. Unakuta mtu hata wazazi wako wanajilaumu kwanini walitumia nguvu kukupeleka shule, walikua wanategemea a lot kutoka kwako, lkn hadi leo unakuta graduate ana miaka 26 anagombania kipande cha nyama na mdogo wake. Lol.

Iko hivi wakuuu:-

●●Nimefanikiwa kuAttract mentors watatu akiwemo mentor wng binafsi, kuja Bongo kwaajili ya kutoa training, coaching na mentorship kuhusu forex. Nimeona niwatumie waafrika kusini kutokana na uzoefu mpana walionao na uwelewa katika forex kwa hapa Afrika.

●●kwa usumbufu wa Local banks nimeweza kuongea na FNB bank, hii ni bank makini na maarufu sana SA ambao wana experience kubwa ktk kudeal na transactions za forex. Wamekubali partnership na uzuri Bongo wana branches kadhaa so ni rahisi zaidi.

●●Nimeweza kuAttract forex broker kuja Bongo. Hapa kidogo nikupe uelewa - Broker ni financial institute inayokuwezesha wewe kuingia global market na kufanya trades zako. Wanakupa platform ya wewe kuweza kutrade katika soko la kimataifa. Fedha zote sasa zinapitia kwa broker wako, ukitaka kupokea pesa zako zinapita kwa broker, huwezi ukatrade bila kua na broker.
Sasa kwenye forex kuna aina 2 ya brokers, niseme kuna aina nyingi lkn hizi mbili ndio common zaidi.

1. Market makers: hawa ni broker wanaeshindana na wewe retail trader. Hawa ni hatari sana kwa afya yako. Huyu broker yupo against na wewe, yeye anapambana wewe upoteze pesa, na hiyo unayopoteza inakua faida yake. Anaweza kufanya hujuma za kila aina ili upoteze pesa yako kwa kutrade, yeye ndio apate faida.

2. ECN forex broker: Huyu ndie broker safi kwaajili ya afya yako. Huyu atahakikisha kufa kupona wewe uwe unapiga faida, anataka wewe milele daima uendelee kupiga pesa kupitia forex, muda wote yupo na wewe benet ili usianguke. Why?! Huyu ni broker ambae anapata commission ndogo sana kwa kila unapoexecute trade, sasa ili yeye apate faida inabidi wewe trader uwe unaweza kutrade zaidi na zaidi, na ili wewe uweze kutrade zaidi inabidi uwe unawin ili uzidi kuwa na account kubwa ya ww kuendelea kutrade zaidi.

Sasa broker ninayemtumia mimi ni huyu ECN, nimefanya juhudi kubwa sana kuweza kumshawishi aje afungue branch Bongo. Na as planned amekubali, uzuri ni kua vibali vyake vinamruhusu aingie nchi yoyote ile Duniani. Na kwasasa tayari wana branch kwa jirani zetu hapo Kenya. na hivi naongea tayari wameshafungua account ya FNB Tanzania ili kusudi kutuwezesha kuweza kufanya one day deposit/withdraw. Yani ukitaka kuchomoa pesa yako kutoka trading account zoezi hilo litakamilika ndani ya siku 1 tu.

Na tayari nimewapa ushauri ambao wanaufanyia kazi - waweze kuleta broker visa card. Yani kunakuwepo na card ambayo itatuwezesha kuchomoa pesa 1 kwa 1 kupitia ATM yoyote ile duniani.
Kitu kama hiki:-
8a8a1308766b3617cf78b85a6bdffc57.jpg


Nini tutegemee

Mpaka sasa ninavyozungumza team yangu tunafanya kazi, kazi kweli kweli kuhakikisha haya yote ninayoyazungumza hayaishii kwenye papers ama JF. I want to get this thing done, come rain or shine, ije jua ama inyeshe mvua.

Hapa naandika huu uzi nahisi nakula muda wangu - but it's worth it. Napambana kupata papers zote, ili operations ziwe legalised kwa sheria na utaratibu wa nchi. It's hard but it will be done.

Jana nimetoka kucheki office na nitailipia soon. Tumependezwa sana na Jangid plaza ipo pale mataa karibu na Dar Free Market. Nimeshaonana na mmiliki, badp kukamilisha paper works tu.
c7d5df684fb732908483b161556f0399.jpg
44dea36bd9ac6e051cd9403b75aa76c9.jpg


Let's get started

Any time niko tayari kuanza, soon indeed!! Tunataka watu wawe financial independent, watu waweze kucontrol uchumi wao pasipo kuinyenyekea/kuililia serikali. We must move forward with the rest of the world, same time same speed bado hatujachelewa.

Am young but very motivated. Sijui niseme nini, but hivi naongea nimereject mwaliko kutoka World Bank ambapo nimealikwa kushiriki ktk Global Youth Symposium for SDGs, nimewaambia nimebanwa. Just nipate muda na space ya kupush hii kitu ianze. Na itaanza tu inshaallah.

Tutatoa kila kitu unachohitaji ili uwe profitable forex trader. Kadri tunavyokuwa ndivyo tutazidi kupanuka, kuwafikia watu wa mikoani mpk hii kitu ieleweke. Najua it's not easy, but it's possible.

Only Special for JF
Since day 1 JF is my family, tunakutana majukwaa mbali mbali tunataniana, kukwaruzana, kupishana mitazamo, lkn sisi ni ndugu. Thanks kwa team nzima kupambana effortlessly kuhakikisha hii kitu (JamiiForums) inadumu, najua wanapitia mengi ili JF iwe shut down lkn wameendelea kuwa strong forever. Na Alaaniwe hayawani yule anayetaka kuizima JF, na mwingine anataka kuzima mtandao. Shame!! - no politics am real.

Mimi nikikwambia nimelipa Rand 14,000 (ni kama mil 2.5) kwaajili ya 1 to 1 mentorship huwezi kuamini. But wanaoelewa forex wanajua nini namaanisha. Vijana makini sana ambao pia nina malengo ya kumeet nao mwakani wanaitwa AstroFX wana charge $7500 kwaajili ya 1 week training na 6 months guidance ktk forex.

Mimi nimekaa na kuwaza sana, nimefikiria nitoe offer ya watu wa mwanzo kabisa kutoka JF. It's gonna be FREE! namaanisha 100% FREE. Watu 300 wa mwanzo nitakaoanza nao hii safari nitatoa learning materials, trainings, mentorship, na 3 months guidance for free. I am blessed to bless others - Don't misquote me.

Kwanini nafanya free?! Bado forex haijulikani TZ, na ni ngumu sana kubadili mind set ya watanzania wengi - ambao mara nyingi hua hawapendi kujifunza. So, natoa hii kitu for free kwa watu wa mwanzo, ili wapige pesa na wabadili financial status zao. Then hawa watu watakua ambassadors wangu, namaanisha hawa ndio watatutangaza pande zote za TZ. Watu wakimake consistent profits, wakaelewa how it works basi kama watu hawa si wachoyo wa mafanikio wataenda kuwashtua wenzao - ndugu, jamaa na marafiki. Hapo tutaanza na reasonable fees mpk tutakapoona ni muda sasa wa sisi nasi kula jasho letu, ndio tutaanza kuweka bei za faida.

Again I salute all you bosses

ONTARIO.
Endelea kutoa" up date" mkuu
 
Asante kwa kunipanua mawazo, kwa hiyo hata mie ambaye sijasomea masomo ya biashara kabiisaa yaani naweza kufanya hii kitu ndugu?
 
Dah mimi hapa nabaki msomaji tu. Kwanza nahisi hii biashara inataka mtu smart zaidi kichwani. Japo watanzania wengi huwa tunakuwa wakurupukaji sana huku tukifikiria kupiga hela tu bila kupenda tujifunze kwanza kitu na kukielewa vyema. kesho tunaanza kulia. Sijui niko sahihi?
 
Biashara zote dunian zinasimama kwenye kanuni moja: 'supply and demand', weka akili yako hapo na utafakari what are supplying to fulfill the certain demand? Alichosema ONTARIO si kipya na kadadvua vizuri, ila mimi nikasema kwa sasa hapa Tz hakiwezekani labda kizazi kijacho. Nikirudi kwenye kanuni ya 'supply and demand' kwa kuangalia biashara ya forex ninajiridhisha pasi na shaka kwamba ni NDOTO kufanikiwa kwa sasa hapa Tz with the trending political economies surrounded with people whose blogged minds are like yours.

The law of supply and demand is the theory explaining the interaction between the supply of a resource (forex in this case) and the demand for that resource. The law of supply and demand defines the effect the availability of a particular product and the desire (or demand) for that product has on price. Generally, a low supply and a high demand increases price, and in contrast, the greater the supply and the lower the demand, the lower the price tends to fall.
Hujui unachobishania. Mimi nimesoma uchumi nakuelewa vizuri, nimesoma pia finance n.k. Hii kitu huwezi kuifahamu kwa kutegemea elimu hiyo tu. Ndo maana umeambiwa kuna watumishi wa benki baadhi hawajui nini kinaendelea duniani. Hebu amua kujifunza kwanza.
 
Mkuu ONTARIO, ninaomba kuwa mmoja wa wanafunzi wa hii knowledge pindi utakapokamilisha masuala yako ya uratibu wa mafunzo.
 
Hata mimi niwemo katika hao 300. Ila Mr. Ontario utatujuaje wakati ID za humu "upepo sio?"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom