EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Ikiwa imebakia mwaka mmoja hivi kabla ya Fainali za Kombe za Dunia kuanza, macho ya wapenzi wengi wa soka duniani yataelekezwa huko Brazili kwa ajili ya FIFA Confederations Cup 2013 inayoanza tarehe 15/06/2013.
Jumla ya nchi nane zinashiriki katika mashinadano hayo na zitajumuisha baadhi ya wachezaji mashuhuri duniani katika ya mechi zaidi ya 16 zitakazochezwa kwenye viwanja sita tofauti. Nchi zinazoshiriki ni Brazil, Japan, Mexico, Italy, Spain, Uruguay, Tahiti na Nigeria.
Baadhi ya mambo ambayo tutapata fursa ya kuyaona ni kama yafuatayo. Kwanza, tutaona jinsi Brazil ilivyojiandaa kuendesha Fainali za Kombe la Dunia zijazo. Pili, tutawaona mabingwa wa sasa wa Dunia (Spain).
Tatu, goal-line technology itatumika kwa mara ya pili kwenye mashindano ya FIFA. Goal-line technology ilitumika kwa mara ya kwanza mwaka jana katika mashindano ya vilabu bingwa vya mabara nchini Japani.
GoalControl iliyotengenezwa Ujerumani itatumika kwenye Confederations Cup na itaendelea kutumika kwenye Fainali za Kombe la Dunia 2014, kulingana na mafanikio yake kwenye haya mashindano. GoalControl, ambayo ina kamera 14 zenye high speed zinazozunguka kiwanja na kulengeshwa kwenye magoli yote mawili, inatumia kamera kuamua kama mpira umevuka mstari wa goli. Kwa hiyo yale maswali ya "Did the ball cross the line?" yatapungua.
Nne, Tahiti ni underdogs na walifanikiwa kuingia kwenye mashindano hayo baada ya kuifunga New Caledonia bao 1-0 na kuwa nchi ya kwanza kushinda Fainali za Nchi za Bara la Oceania mwaka 2012 tokea yalipoanza kwama 1975. Kabla ya hapo Australia na New Zealand ndiyo walikuwa wanashinda mashindano hayo. Tahiti ina watu 12,000 tuu. Watacheza na Nigeria, kabla ya kukichapa na mabingwa wa dunia, Spain. What an occasion!
Kikosi cha Tahiti ni amateurs, wakiwemo wafanyakazi wa maofisini, wabeba mizigo, walimu, na wafanya biashara. Kuna professional footballer mmoja tuu; mshambuliaji Marama Vahirua mwenye umri wa miaka 33, though namsikia pia Steevy Chong Hue. Marama alikuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa ya vijana wenye umri chini ya miaka 21 na bado hajaichezea Tahiti katika mechi yoyote ya kimataifa.
Wachezaji wa kuangalia
Steevy Chong Hue: Alifunga goli pekee na kuifanya nchi yake kushinda kombe ya Fainali za Bara la Oceanea 2012.
[video=youtube_share;myF44FsME80]http://youtu.be/myF44FsME80[/video]