Fedha za Radar Kurudishwa: Mgogoro kati ya BAE, TZ na UK

Tangu asubuhi TBC imekuwa ikitangaza ya kwamba ujumbe wa Tanzania upo Uingereza kufuatia fidia ya malipo ya rada.

Kwa kumbu kumbu zangu hii si mara ya kwanza kwa waziri Membe kutuma ujumbe wa aina hiyo huko uigereza kwaajili ya malipo husika. Suala la kujiuliza ni kwamba kama Membe mwenyewe alikwisha wasilisha suala hilo kwa serikali ya uingereza kwa kupitia waziri wa nje mwenzake wa nchi hiyo, anawezaje tena kuanzisha mazungumzo ya moja kwa moja na kampuni husika!

Diplomasia ya aina hiyo aliiona wapi?

Swali lingine kwanini wakati habari zilipoanza kuvuja ya kwamba Tanzania iliuziwa rada kwa bei mbaya, mbona hakuwa anajishugulisha kutoa ushirikiano wake katika kutafuta ukweli wa tuhuma hizo, iweje sasa wakati mambo yamekamilika awe mwepesi kutaka kuvuna asikopanda.

Katika hali halisi kukaa kimya kwa serikali ya Tanzania wakati suala hili linafanyiwa uchunguzi kumeiondolea uhalali wowote wa kudai tuzo iliyotolewa kwa suala hilo. Hivyo wahusika wana haki ya kuunda chombo chao kitakachobuni njia muafaka wa kufikisha tuzo hiyo kwa walengwa ambao ni watanzania.

Katika hali hiyo ni matumizi mabaya ya fedha za umma kuendelea kuingia gharama za mara kwa mara kwaajili ya kwenda uingereza eti kufuatilia malipo hayo wakati tuna ubalozi huko.

===================
KATIKA PICHA:

wabunge1.jpg

Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb.) akiongea na Naibu Spika wa Bunge la uingereza, Mhe. Nigel Evans (Mb) katikati ni Mhe. Job Ndugai, Naibu Spika wa Bunge la Tanzania. Ujumbe wa Wabunge wanne wa Tanzania unaongozwa na Naibu spika. (Picha Assah Mwambene)
wabunge2.jpg

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Job Ndugai akiteta jambo na Spika wa Bunge la Kenya walipokutana katika Bunge la Uingereza jana. Waheshimiwa Wabunge wako nchini Uingereza kufuatilia malipo ya zaidi ya paundi milioni 29 kutoka BAE System baada ya Mahakama nchini hapa kuiamuru kampuni hiyo kuilipa Tanzania baada ya kugumdulika kwamba kampuni hiyo iliongeza bei ya ununuzi wa Radar.

wabgunge3.jpg

Balozi wa Tanzania Uingereza, Mheheshimiwa Peter Kallaghe akiteta jambo na Waheshimiwa Wabunge wa Tanzania, Jobu Ndugai (Naibu Spika), Mussa Azzan Zungu (Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na Mhe. Angela Kairuki
 
Jun21/2011
Written by haki | By Ayob Mzee - London



IMG_7512.JPG

IMG_7519.JPG



Today a group of Tanzania all party parliamentarians visited Britain as a part of a fact find mission on how the people of Tanzania will get their money as a result of a ruling in a case where the Arms company BAE Systems which pleaded guilty at a Cfrown Court in London to minor charges of false accounting relating to its controversial sale of military radar equipment to Tanzania in 1999.

This group led by the Deputy speaker Hon Job Ndugai Mp comprised of Hon. Mussa Zungu MP Angelah Kairuki MP, John Cheyo MP, Ms Justina Shauri from the Parliament of Tanzania ,Grace Shangali ,assistant Director of Europe and A
merica Department , Assah Mambene , Head of information -Foreign Affairs and Olivia Maboko ,desk officer (UK) at the Department of Europe and America The sale has been surrounded by allegations of corruption.

During the court ruling it was stated that that British Aerospace Defense Systems Limited failed:

"to keep accounting records which were sufficient to show and explain payments made pursuant to (a) a contract between Red Diamond Trading Limited and Envers Trading Corporation, (b) a further contract between British Aerospace (Operations) Limited and Merlin International Limited."

Under the settlement, BAE pleaded guilty to not accounting accurately for $12.4m of payments made between 1999 and 2005 to a Tanzania-based businessman, Shailesh Vithlani, for his work as a marketing agent in helping to secure a £28 million radar contract from the Government of Tanzania in 1999.


Mr Justice Bean said he accepted "there is no evidence that BAE was party to an agreement to corrupt". But pointed out that they "did not need to be" because the company had deliberately structured the payments to the agent via an offshore company controlled by BAE to another Panama-based company controlled by Mr Vithlani so that they were placed "at two or three removes from any shady activity".

Moreover, in the basis of the plea accompanying the agreement, BAE admitted the following:

"Although it is not alleged that BAE plc was party to an agreement to corrupt, there was a high probablility that part of the $12.4 million [paid to the Tanzania agent] would be used in the negotiation process to favour British Aerospace Defence Systems Ltd."

As Mr Justice Bean said of this high probability:

"indeed there was. Otherwise it is inexplicable . . . why the payments . . . exceeded $12m; and even more inexplicable why 97% of that money should have been channelled via . . . an offshore company controlled by BAE, and paid to . . . another offshore company controlled by Mr Vithlani."

The problem is that BAE has decline to pay the people of Tanzania the said sum citing corruption. Intead it has set up A panel of advisory board on Tanzania which will be chaired by Lord Cairns. Philippa Foster Back, OBE will serve as Deputy Chair. .This panel will advise them on how to pay Tanzania
 
Haya ni marudio ya hoja ambayo imejadiliwa sana. Ukweli unabaki pale pale kwamba kama wewe umeibiwa lakini kwa sababu yoyote ile ukashindwa kumfuatilia mwizi wako, au ukashindwa kujua kwamba umeibiwa, akitokea whistle blower akakuambia na hata akafanikisha kurudishiwa mali yako, msamaria mwema huyo hajinyakulii haki ya umiliki wa mali hiyo.

Anaweza tu akaomba kushukuriwa lakini siyo kukupangia matumizi ya recoveries zako. Uingereza walifuatilia issue hii kwa sababu kampuni ya BAE ambayo ilihusika na wizi huu na yenyewe ilikuwa ina-face credibility problems kama serikali isingeingilia kati. Haikuwa favour kwa Tanzania japo Tanzania ilikuwa ni beneficiary ya ufuatiliaji huo.


Hakuna justification yoyote ya fedha hizi kutorejeshwa kwa aliyeibiwa na msimamo wa Membe na serikali ndiyo utashi sahihi na wanaoshangaa wanaendekeza ukoloni ambao hauna nafasi katika hili. Membe endelea kudai mpaka kieleweke!

 
kieleweke nini wakati Membe hana sauti mbele ya weupe? Wewe hujamsoma kisaikolojia kwamba anataka aje afanye hoja ya kutafutia uraisi 2015. Shenz taipuuu!
 
kieleweke nini wakati Membe hana sauti mbele ya weupe? Wewe hujamsoma kisaikolojia kwamba anataka aje afanye hoja ya kutafutia uraisi 2015. Shenz taipuuu!

Kumbe sasa nakuelewa vizuri wewe na wapingaji wenzio. Kumbe hapa kuna hofu ya political mileage na siyo umuhimu wa Tanzania kupata haki yake. Kweli mbumbumbu nchi wamesheheni. Yaani tunaangalia kila kitu kwa jicho la urais wa 2015 na tunapinga kwa sababu hiyo. Angelisemea Shibuda ingekuwa ok kwa vile hagombei urais siyo! Sasa naelewa lile tusi pale kwenye red linastahili kukurudia mkuu!
 
This is a waste of public funds; why send such a big delegation of parliamentarians who have not even bothered up to now, to require the government to take legal action to the perpetrators of that onerous crime.
 
Bahati mbaya tulishalisemea sana jambo hili, na kwa uhakika haliwezi kumwongezea kitu chochote kwenye hizo mbio!
Anazidi kujidhalilisha, na kuonyesha kuwa Wakubwa wetu ni wavivu wa kufikiri na kutenda!
 
This is a waste of public funds; why send such a big delegation of parliamentarians who have not even bothered up to now, to require the government to take legal action to the perpetrators of that onerous crime.

That is a subject for another day. The size of the delegation underlines the importance of the matter. Let them pursue our course to the conclusive determination.
 
huu ni uzuzu,yani pesa yenye haijafika wameanza matanuzi!mbona MEMBE hajatoa shukurani kwa bi clear shot kulivalia njuga suala lile na kujiuzulu?
 
Ukisikia umburu kenge ndio huo. Wamejikusanya kuja kufuja pesa zaidi za walipa kodi. Waliofanikisha zoezi zima ni UK Government iweje leo wanadandia umaarufu wa kurejeshwa pesa wakati serikali ya Wezi akina JK na kundi lake la mafisadi wanawazuia Takukuru kuwashitaki.
 
Kujidhalilisha!
Ni makondoo gani hao wameenda huko bila kuhoji?
Natamani wagomewe kabisa wasipewe hata mia ili siku nyingine wachanganye na zao!
 
Kwa mujibu wa TBC news ya leo saa mbili usiku BAE system imekataa ushawishi wa wabunge kutoka Tanzania ukiongozwa na Membe na naibu spika wa kutaka chenchi isilipwe kwa NGOs bali ilipwe kwa serikali ya TZ
 
Kumbe sasa nakuelewa vizuri wewe na wapingaji wenzio. Kumbe hapa kuna hofu ya political mileage na siyo umuhimu wa Tanzania kupata haki yake. Kweli mbumbumbu nchi wamesheheni. Yaani tunaangalia kila kitu kwa jicho la urais wa 2015 na tunapinga kwa sababu hiyo. Angelisemea Shibuda ingekuwa ok kwa vile hagombei urais siyo! Sasa naelewa lile tusi pale kwenye red linastahili kukurudia mkuu!
.Mmeshindwa kuchukua za Chenge alizozipata kutokana na deal hilo hilo la rada, japo mlitafuniwa mpaka account namba alikozificha sasa mnalilia za waingereza wanaotuonea huruma. Tunazihitaji pamoja na zile za Chenge na wale wengine wote wasiotajwa lakini sii kupitia kwa mikono michafu na ya wanyanganyi wa serikali ya ccm.NO NO NO P/SE!!
 
Huu ni ujinga uliopitiliza kiwango. Kuonyesha kweli hizo fedha inabidi zirudi, Tanzania ilipaswa kufanya uchunguzi wake wa nani alifaidika na rusha/wizi huo, na watu hao wakiwa tayari kwenye mikono ya sheria, hapo ndipo kungekuwa na legitimacy ya kudai malipo hayo, bila hivyo ni aibu kabisa!!
 
Back
Top Bottom