bbc
JF-Expert Member
- Jan 18, 2016
- 3,841
- 4,145
Enzi za chai maharagwe (daladala) mzee mmoja aliletewa chupi 4 toka ng'ambo na mtoto wake. Siku moja alikurupuka asubuhi kuwahi chai maharagwe hata akasahau kuvaa chupi. Alikaa kwa kujiachia akidhani kavaa chupi mojawapo kumbe kasahau. Abiria wa upande wa pili wakaanza kumshangaa lakini yeye alidhani wanaishangaa chupi. Akawaambia "mnaishangaa hii moja, ninazo 3 kama hizi nyumbani"!!!!mkuu mtaani kwetu, kuna nyumba iliwaka usiku, baba mwenye nyumba alitoka na koti afu chini malighafi zote wazi, aliporudiwa na akili alisema yeye alikurupuka akiwa na msuli, so hajui koti kalitoa wapi?