EXCLUSIVE: Download Rasimu ya Kwanza ya Katiba Mpya hapa na toa maoni

wana JF kama mjuavyo tuko ktk wakati mzuri wa kuijenga nchi yetu hasa kupitia katkba mpya, so yeyote mwenyenayo naomba ili niipitie.thanx
 
Habari za leo wanajamii?

Nina masuali mawili yanayohusu rasimu ya katiba ya Tanzania nayo ni:

1. Jee kuna tovuti (website) ambayo kamati husika imeweka rasimu hiyo ili wananchi waweze kusoma? kama ipo, naomba kujua anuani ya tovuti hiyo.

2. Mbali ya suali la serikali tatu ambalo ndio limechukua kipa umbele katika mijadala, ni masuali gani mengine ambayo rasimu hiyo imependekeza?

shukrani
 
Uhuru wa
imani ya dini
31.-(1) Kila mtu anao uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi
katika mambo ya imani ya dini na anao uhuru pia wa kubadilisha dini,
imani yake au kutokuwa na imani na dini.
(2) Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa
ni huru na jambo la hiari kwa mtu binafsi ili mradi asivunje sheria za nchi.
(3) Shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini itakuwa nje ya
shughuli za mamlaka ya Serikali.
(4) Hifadhi ya haki zilizotajwa katika Ibara hii itakuwa chini ya
taratibu zilizowekwa na sheria ambazo ni muhimu katika jamii ya
kidemokrasia kwa ajili ya usalama, amani, maadili na umoja wa jamii na
wa kitaifa na vitasimamiwa kwa utaratibu ulioainishwa kwenye sheria za
nchi.
(5) Ni marufuku kwa mtu, kikundi au taasisi ya dini kutumia uhuru
wa kutangaza dini kwa kukashifu imani na dini nyingine, kujenga chuki au
kuchochea vurugu na ghasia kwa madai ya kutetea imani au dini.
(6) Dini na imani ya dini haitatumika kwa namna yoyote
itakayowagawa wananchi, kuleta uhasama au kuharibu amani miongoni
mwa wananchi.
(7) Neno “dini” kama lilivyotumika katika Ibara hii litatafsiriwa
kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno
mengine yanayofanana au kuambatana na neno hilo nayo yatatafsiriwa
kwa maana hiyo.
 
Salaam sana.Rasimu iweke wazi kuwepo au kutokuwepo kwa muungano.Tusifiche ukweli,baadae ikasimamisha Katiba kigugumizi.
 
Salaam sana.Rasimu iweke wazi kuwepo au kutokuwepo kwa muungano.Tusifiche ukweli,baadae ikasimamisha Katiba kigugumizi.
 
Uwezo tunao wenyewe wa kuwa na katiba isiyomkandamiza mwananchi aliyehuru lkn yatupasa kutetea haki na maslahi kupitia marekebisho hayo bila kusita.
 
Mamlaka ya Rais yanahitaji ufafanuzi zaidi kwenye RASIMU ya katiba; kuna justification gani kwa Rais kuteua wabunge wakati kuna wabunge wanaowakilisha wananchi?

Hii inawapa mwanya viongozi dhaifu kuteua vimada wao na kuwahonga vyeo at the expense of the country's development.
 
Mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya hivi vyeo hatuvitaki kwenye katiba mpya.
 
nijambo la busara sana kuona nchi inayojitawala yenyew3 kuwa na rasimu ya katiba mpya na ni vizuri sana coz tunataka katiba yetu we are tanzania ni hayo 2 cjui ninyi mnasemaje wadau wangu
 
Back
Top Bottom