EWURA yawakamata walanguzi wa mafuta ya Petroli Loliondo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Snapinsta.app_364202848_298751659232099_7142656237262631_n_1080.jpg

Timu ya Wakaguzi EWURA ikishirikiana na vyombo vingine vya Usalama imewakamata walanguzi wa mafuta ya petroli wakihifadhi na kuuza mafuta hayo kwenye madumu ya lita 20 na 200. Aidha waliokomatwa kwa kukutwa wakiuza mafuta Loliondo ni:

1. Wilson Bussein Balagiswa
Lita:411

2. John Emanuel Nanyaro
Lita:120

3. Resty Mushi
Lita:12

Watu hawa waliokutwa wakiuza mafuta hayo wanashikiliwa mahabusu ya Loliondo kwa upelelezi zaidi..
Vile vile wenye vituo ambavyo viliwauzia mafuta hayo nao wametiwa nguvuni kwa ajili ya upelelezi zaidi. EWURA inawaonya wamekatazwa wafanyabiashara wenye vituo vya mafuta kuacha mara moja kuuzia watu mafuta kwenye madumu isipokuwa kwenye vyombo vya moto kwani ni kinyume na taratibu za leseni zao.

Wenye vituo wanaoshikiliwa ni wa vituo vya Vituo ni Abdi Pemba Petrol Station na Ally Joseph Karanjay Petrol Station.
Snapinsta.app_363523938_1010368603324798_5770449052216251583_n_1080.jpg
 
Kiki nyingine za kijinga sana wanaacha kudili na walio ficha maelfu ya liters kwenye visima vya masheli wao wanadili na madumu mawili jinga kabisa hii mijitu
 
Back
Top Bottom