Kichuchunge
JF-Expert Member
- Dec 2, 2020
- 338
- 891
Nilikuwa kwenye mahusiano na mdada hivi mtu mzima, kwa miaka kama mitatu. Alikuwa anafanya biashara ya kuuza vilevi. Hiyo biashara ni ya kwake binafsi. Sasa katika mahusiano yetu japo kuna wakati alini cheat nikamgundua, lakini aliniomba msamaha sana yakaisha. Akawa kama amejirudi flani hivi hadi nikaanza kushawishika kama vile kutaka kumpa sapoti kwenye wa biashara yake.
Nikaanza kumuongezea mtaji kidogo kidogo kisha nikaanza kumnunulia vitu vya kuboresha ile sehemu ya biashara yake ili papendeze zaidi (decorations). Palivyoanza kuvutia, wateja wakaanza kujaa kumbe miongongoni mwao mmoja akamshawishi, wakaingia kwenye mahusiano kimya kimya bila mimi kujua kwa kuwa mara nyingi nilikuwa bize sana. Siku nilipokuja kugundua akaingiwa na hofu sana, akadhani nitakuja kumdhuru hivyo akaomba ili awe salama, uhusiano wetu uishie hapo.
Sikuwa na kinyongo, nilimkubalia ila tu nikampa sharti moja tu kwamba anipe vitu vyangu vyote (decorations na viti na meza mpya nilizokuwa nimemnunulia pale kwenye biashara) vilivyokuwa vimechangia kupaboresha pale sehemu ili akibaki, abaki kama nilivyokuwa nimemkuta. Na huyo mtu wake mpya aliyekuwa amempata aweze kumboreshea kama anampenda. Kwa kweli nilivichukua, kasoro pesa ya mtaji niliyokuwa nimemuongezea ndio sikuidai tu, ila cha ajabu huyo mdada akawaka sana, akamsimulia kila mtu kwamba mimi ni mshamba, iweje nimfanyie kitu halafu nimnyang'anye? Binafsi ningeweza kumuachia, isipokuwa roho ikaniuma sana na kunifanya nijiulize kwamba uboreshaji wangu wa pale sehemu kwa pesa zangu mwenyewe ndio umesababisha hayo yote kwa hiyo niondoke tu hivi hivi na kumuachia aendelee kutanua huku mimi nikikung'uta makalio na yeye akiendelea kupigwa 'pipe' na mtu mwingine? Kosa langu hapo ni nini? Kuchukua mali zangu?
Nikaanza kumuongezea mtaji kidogo kidogo kisha nikaanza kumnunulia vitu vya kuboresha ile sehemu ya biashara yake ili papendeze zaidi (decorations). Palivyoanza kuvutia, wateja wakaanza kujaa kumbe miongongoni mwao mmoja akamshawishi, wakaingia kwenye mahusiano kimya kimya bila mimi kujua kwa kuwa mara nyingi nilikuwa bize sana. Siku nilipokuja kugundua akaingiwa na hofu sana, akadhani nitakuja kumdhuru hivyo akaomba ili awe salama, uhusiano wetu uishie hapo.
Sikuwa na kinyongo, nilimkubalia ila tu nikampa sharti moja tu kwamba anipe vitu vyangu vyote (decorations na viti na meza mpya nilizokuwa nimemnunulia pale kwenye biashara) vilivyokuwa vimechangia kupaboresha pale sehemu ili akibaki, abaki kama nilivyokuwa nimemkuta. Na huyo mtu wake mpya aliyekuwa amempata aweze kumboreshea kama anampenda. Kwa kweli nilivichukua, kasoro pesa ya mtaji niliyokuwa nimemuongezea ndio sikuidai tu, ila cha ajabu huyo mdada akawaka sana, akamsimulia kila mtu kwamba mimi ni mshamba, iweje nimfanyie kitu halafu nimnyang'anye? Binafsi ningeweza kumuachia, isipokuwa roho ikaniuma sana na kunifanya nijiulize kwamba uboreshaji wangu wa pale sehemu kwa pesa zangu mwenyewe ndio umesababisha hayo yote kwa hiyo niondoke tu hivi hivi na kumuachia aendelee kutanua huku mimi nikikung'uta makalio na yeye akiendelea kupigwa 'pipe' na mtu mwingine? Kosa langu hapo ni nini? Kuchukua mali zangu?