Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
Nimesikitishwa sana na habari iliyochapishwa na gazeti la Ijumaa wikienda (Global publishers) inayohusu watotot walioenda mahakamani kumlilia mtoto wao ambaye ni mtuhumiwa wa biashara ya ukahaba. Kitendo cha kuwapiga picha, kuwataja majina na wanapoishi na kusoma si dhani kama ni sahihi. Watoto hawa leo wataanza kuitwa watoto wa changudoa mitaani na shule. I can imagine mateso ya kisaikolojia watakayoyapata na naweza kufikiria madhara ya muda mrefu yatakayoombatana na kadhia hii. Habari hii ingeweza kukamilika na kueleweka pasipo kuweka majina na picha za watoto hawa. Tumeshuhudia mara kadhaa mkiandika habari za maneno kama "kigogo fulani", jina kapuni nk...kwa nini haikuwa hivi kwa watoto hawa. Kwa nature ya kazi yangu nimekutana na watu wengi ambao leo wanaishi maisha ya tabu kwa kuwa waliacha shule.....na moja ya savavu kubwa ni kunyanyaswa kwa namna moja au nyingine. halii hii hupeleka mtu kukua huku amekosa "kujiamini" (self esteem). hali hii ina madhara makubwa sana katika maisha yetu ya kila siku...tabia zetu, uwezo wa kufanya maamuzi, uongozi nk hujengwa katika kipindi mtoto anakua. Nawasikitikia sana hawa watoto.....habari hii iko hapa